You are on page 1of 5

OFISI YA RAIS

TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA

MKOA WA KIGOMA

MTIHANI WA UTAMILIFU MKOA DARASA LA VI, NOVEMBA 2023

MUDA: SAA 1:30 ________________ SOMO: MAARIFA YA JAMII


Maelekezo
1. Karatasi hii ina sehemu A na B zenye maswali arobaini na tano (45).
2. Jibu maswali yote katika kila sehemu.
SEHEMU A: Chagua jibu sahihi
1. Mtaalamu wa mazingira aliwashauri wanakijiji wa Mpapa mkoa wa Ruvma, kuacha uharibifu na
uchafuzni wa hewa Je, shughuli zipi za kibinadamu walizoshauriwa kuacha?
A. Ufugaji wa wanyama B. Uchomaji wa vichaka na misitu kwa ajili ya kilimo
C. Kufukuza watu D. Upandaji wa mazao E. Kusafisha mazingira
2. Kuna aina taofauti za upepo katika uso wa dunia unaovuma kutoka baharini kwenda nchi kavu au
kutoka nchi kavu kwenda baharini Je ni aina ipi upepo huleta upepo mwanana wan chi kavu?
A. Upepo uvumao kutoka baharini kwenda nchi kavu B. Upepo uvumao kutoka kaskazini kelekea
kusini C. Upepo uvumao kutoka magharibi kuelekea mashauriki D. Upepo uvumao kutoka
kusini kwenda kaskazini E. Upepo uvumao kutoka nchi kavu kwenda baharini
3. Tanzania ni nchi yenye lugha moja Kiswahili na inayozungumzwa nchi nzima. Lugha hii imeunganisha
makabila yote nchini. Ni taasisi ipi inayo husika na usimamizi na ukuaji wa lugha hiyo?
A. BASATA B. TUKI C. BAKWATA D. Bakita E. BMT
4. Tanganyika ilikuwa nchi ya kwanza kupata uhuru katika ukanda wa Afrika mashariki.Ilipata uhuru
wake tar. 9.12.1961. Je ni karne gani hili tukio lilitokea?
A. Karne ya 21 B. Karne ya 19 C. Karne ya 18 D. Karne ya 17 E. Karne ya 20
5. Tunaweza kupata taarifa za kihistoria kutoka vyanzo mbalimbali ni vyanzo taarifa isipokuwa
_________ A. Masimulizi ya mdomo B. Maeneo ya kihistoria C. Maandiko D.
Makumbusho E. Mabadiliko ya binadamu
6. Mtu anayeshughulikia na kufuata ardhini kutafuta mabaki ya kale ya binadamu , majengo na zana
zilizotumika enzi za kale huitwa________
A. Akiolojia B. Makumbusho C. Jumla ya makumbusho D. Mwana kiolojia E. Maeneo ya
kihistoria
7. Ukataji miti, uchomaji vichaka na ulimaji ovyo ni moja ya ____ mazingira.
A. Kurekebisha B. Kuharibu C. Kuifadhi mazingira D. Shughuli za kiuchumi E. Kilimo
8. Kwa nini ardhi huchukuliwa kama chanzo cha rasilimali zote?______
A. Huweza shughuli za kilimo B. Nguzo za rasilimali zote C. Makazi ya viumbe wanaoishi majini
D. Hutumika katika usafirishaji E. Huvutia watalii
9. Tanzania ni nchi iliyobarikiwa kuwa na vyanzo vingi vya maji kama vile maziwa, mito na bahari.Je ni
ziwa lipi kubwa zaidi Tanzania? A. Nyasa B. Victoria C. Rukwa D. Tanganyika E.
Natroni.
10. Mtaalamu wa mazingira alikuwa akitoa elimu kwa wanakijiji juu ya utunzaji wa mto Mgulwi ambao ni
chanzo kikuu cha maji kijijini hapo. Je, ni jambo gani aliwasisitiza wanakijiji hao kulifanya?
A. kufyeka vichaka B. kufulia pembezoni C. kupanda miti pembezoni
D. kufuga pembezoni E. kulima pembezoni
11. Ni kwa namna gani misitu husaidia kupungua kwa joto katika uso wa dunia?
A. hupunguza hewa ya ukaa na kuakisi mwanga wa jua B. hupunguza gesi ya oksijeni
C. huzalisha gesi ya methani D. hutoa kuni E. hupunguza mvua
12. Kupungua kwa kiwango cha theluji katika milima mirefu na kuongezeka kwa kina cha bahari ni
matokeo ya kitu gani?
A. mvua kubwa B. ongezeko la joto duniani C. upepo mkali
D. tetemeko la ardhi E. uwepo wa misitu mikubwa
13. Watanzania huadhimisha sikukuu mbalimbali kila mwaka zikiwemo za kisiasa na za kidini. Kati ya
matukio yafuatayo ni lipi huanza kuadhimishwa kila mwaka?
A. kifo cha baba wa taifa Mwalimu J. K. Nyerere B. muungano wa Tanganyika na Zanzibar
C. Uhuru wa Tanganyika D. Krismasi E. Mapinduzi ya Zanzibar
14. Vita vya kagera ni moja kati ya matukio ambayo hayatasahaulika hapa nchini. Je, vita hivyo
vilipiganwa lini? A. 1905 – 1907 B. 1945 – 1947 C. 1960 – 1961
D. 1914 – 1918 E. 1978 – 1979
15. Mwalimu na wanafunzi walikuwa wakijadiliana kuhusu vipengele vya hali ya hewa. Ni kipengele kipi
cha hali ya hewa ambacho hupimwa katika vizio vya mililita za ujazo?
A. mwanga wa jua B. halijoto C. mgandamizo wa hewa D. upepo E. mvua
16. Kila mwaka tunashuhudia majira mbalimbali na ndani ya majira hayo hutokea tofauti ya urefu kati ya
usiku na mchana. Je, hayo ni matokeo ya tukio gani?
A dunia kujizungusha kwenye mhimili wake B. dunia kulizunguka jua C. kupatwa kwa jua
D. kupatwa kwa mwezi E. kupwa na kujaa kwa maji
17. Ukiwa kama mtaalamu wa maswala ya mazingira ni njia gani hautawashauri wakulima kufanya ili
kukabiliana na ukame?
A. Kilimo cha umwagiliaji B. Kupanda mazao yanayostahamili ukame
C. kuhamasisha wakulima kuacha kilimo D. Kupanda mazao yanayokomaa kwa muda mfupi
E. matumizi ya samadi
18. Hewa iliyo katika mwendo ni moja kati ya vipengele vya hali ya hewa. Je, hewa hiyo inaitwaje?
A. mgandamizo wa hewa B. unyevuanga C. mwanga wa jua D. upepo E. mvua
19. Bwana Malingona alijaribu kulima zao la kahawa katika mkoa wa Pwani. Licha ya mvua za kutosha
zinazonyesha katika mkoa huo lakini zao hilo halikustawi. Unafikiri ni kwanini?
A. uwepo wa baridi kali B. uwepo wa joto kali C. uwepo wa rutuba nyingi
D. ukosefu wa mvua E. ukosefu wa viuwatilifu
20. Tunapoongelea utamaduni hatuwezi kuacha kuzungumzia ngoma za asili. Ipi kati ya zifuatazo ni
ngoma ya asili ya wangoni?
A. mganda B. kuhoda C. mdundiko D. lizombe E. beta
21. Umoja wa mataifa umetuma ndege mbili nchini Kongo DRC ili kupeleka shehena ya chakula na dawa
za binadamu kuwanusuru wahanga wa vita vinavyoendeshwa na kikundi cha M23. Je, ndege hizo
zipo chini ya shirika lipi la umoja wa mataifa?
A. ILO B. UNICEF C. UNESCO D. IMF E. UNHCR
22. Tanzania ni mwanachama wa Jumuiya mbalimbali za kimataifa ikiwemo Jumuiya ya maendeleo ya
nchi za kusini mwa Afrika (Southern Africa Development community - SADC). Je, jumuiya hii
ilianzishwa mwaka gani?
A. 1992. B. 2012 C. 2016. D.2000 E. 2002
23. Richard Burton, John Hanning Speke na Dr. Livingstone walifika Pwani ya Afrika Mashariki kwa
malengo gani? A. Kueneza dini ya kikristo B. kutafuta ardhi kwaajili ya kilimo
cha mazao ya biashara na maeneo yenye hali ya hewa nzuri kwaajili ya makazi C. kueneza dini
ya Kiislamu D. kufanya biashara E. kuchukua pembe za ndovu
24. Sir Donald Kameroon, Sir Horace Byatt, Sir Edward Twining na Julius Von Soden walikuwa ni
viongozi katika utawala wa wajerumani na waingereza hapa Tanganyika. Je, walijulikana kwa jina
gani? A. liwali B. mtwana C. akida D. kansela E. gavana
25. Uvamizi wa wakoloni katika bara la Afrika ulianza miaka ya 1870. Hii ni karne ya ngapi?
A. karne ya 18 B. karne ya 19 C. karne ya 187 D. karne ya 1870 E karne ya 21
26. Mfumo wa kwanza wa kiuchumi na kiutawala ambapo watu waliishi na kushirikiana pamoja uliitwaje?
A. Ujima B. Ujamaa C. Ubepari D. Ukabaila E. Utumwa

27. Mganga aliyewaaminisha Watanganyika katika vita vya Maji maji kuwa risasi za wajerumani
zitabadilika kuwa maji alikuwa nani?
A. Kinjekitile Ngwale B. Chifu Mangungo C. Kibanga D. Karl Peters
28. Mkutano wa Berlin ni mkutano uliojumuisha mataifa ya kibeberu kwa lengo la kugawana makoloni
barani Afrika. Mkutano huu uliitishwa na nani?
A. Karl Peters B. Vasco Da Gama C. Kansela Otto von Bismark D. umoja wa mataifa E.
Barthomeo Diaz
29. Mkataba uliofanyika mwaka 1890 kati ya serikali ya Uingereza na Ujerumani wenye madhumini ya
kurekebisha mipaka ya mwaka 1886 ulijulikana kama:
A. mkataba wa Hamaton B. mkataba wa freire C. mkataba wa Berlin
D. mkataba wa Heligoland E. mkataba wa Vienna
30. Uchaguzi wa kwanza hapa nchini uliohusisha vyama vingi vya siasa ulifanyika mwaka 1995. Je, ni
Rais yupi alichaguliwa?
A. Julius K. Nyerere B. Benjamin Mkapa C. Kikwete D. Magufuli E. A. H. Mwinyi
31. Ardhi ni rasilimali muhimu sana ambayo hubeba rasilimali nyingine. Ipi kati ya zifuatazo si rasilimali
inayopatikana ardhini?
A. gesi asilia B. mazao ya chakula C. maji D. madini E. watu

32. Bahari ya Hindi ni moja ya rasilimali zilizopo Tanzania je, ni aina gani ya rasilimali?
A. rasilimali ya kutengenezwa B. rasilimali ya Afrika C. rasilimali ya asili
D. rasilimali maalumu E. rasilimali kuu
33. Reli ya kati inayoanzia Dar es Salaam hadi Kigoma nchini Tanzania ilianza kujengwa mwaka 1905
kwa lengo la kusafirisha malighafi wakati wa ukoloni. Je, ni wakoloni wa taifa gani waliijenga reli
hiyo? A. Waingereza B. Wajerumani C. Wachina D. Wareno
E.Waitaliano
34. Wanafunzi wa shule ya msingi Mzinga walipewa kazimradi na mwalimu wao kuchora ramani ya dunia
kuonesha milima mirefu. Ni aina ipi ya kipimio cha ramani wataitumia kuchora ramani hiyo?
A. kipimio kikubwa B. kipimio cha kati C. kipimio kidogo D. njia ya mstari E. njia ya
uwiano
35. Kama utateuliwa kumuongoza Bi. Marion ambaye ni mtalii kutoka Austria anayetaka kupanda mlima
Kilimanjaro mkitokea Dar Es Salaam kwa ndege ya Dream Liner, ndege ya shirika la ndege la
Tanzania mtatua katika kiwanja gani?
A. Uwanja wa ndege wa Chunya B. Uwanja wa ndege wa Bukoba C. Uwanja wa ndege wa
Kilimanjaro D. Uwanja wa ndege wa Mwanza E. Uwanja wa ndege wa Mtwara
36. Makumbusho ni sehemu ambayo kumbukumbu za kihistoria huifadhiwa .Je mtu anayefanya kazi
katikati makumbusho huitwa______
A. Mwanakiolojia B. Mwanamakumbusho C. Mwangalizi wa makumbusho
D. Mtaalamu wa historia kuhusu utamaduni na maisha ya binadamu E. Mwanamziki
37. Ni tukio lipi kati ya haya yafuatayo lilitangulia kutokea hapa Tanzania ?_______
A.Kifo cha Abeid A. Karume B. Mapinduzi ya Zanzibar C. Kifo cha chifu Mkwawa D. Vita
vya Kagera E. Mfumo wa vyama vingi vya siasa.
38. Sensa ya watu na makazi ilianyika mara ya mwisho mwaka 2022 na ilisaidia kutambua idadi watu
katika nchi. Je ni lini Tanzania itafanya sensa nyingine?
A. 2024 B. 2032 C. 2030 D. 2025 E. 2027
39. Ndani ya familia nani anayestahili kuafanya majukumu yafuatayo maji, kukusanya kuni, safi wa
nyumbani na kupika?
A. Mama na baba B. Wanafamilia wenye uwezo wa kufanya kazi C. Mama na Binti yake
D.Mama, watoto, binti na kijana wa kazi E. Baba
40. Familia ya bwana Sangana inaishi sehemu ya bondeni ni janga gani linaweza kuikumba hiyo familia?
A. Mafuriko B. Moto C. Ukame D. Suunami E. Njaa
SEHEMU B: ANDIKA JIBU SAHIHI KWENYE KARATASI YAKO YA KUJIBIA

41. Jumuiya ya madola ni jumuiya inayoundwa na nchi zilizotawaliwa na nchi gani?................................


42. Mwanafunzi wa darasa la sita alichora ramani ya Tanzania lakini mwalimu wa somo la maarifa ya
jamii alipokuwa anasahihisha madaftari hakuweza kutambua ramani ilikuwa inahusu nini .Je unafikiri
ni kitu gani muhimu kulikosekana?_______________
43. Taja madhara mawili yanayosababishwa na mkataji mti ovyo
(a)________________(b)_________________
44. Dunia ina mizunguko miwili ambayo ni dunia kujizungusha kwenye muhimili na
____________________
45. Mfumo wa kwanza wa kiuchumi katika hatua na mabadiliko ya maendeleo ya binadamu ni
_________________
MAJIBU MAARIFA YA JAMII

1. B II. MMOMONYOKO WA UDONGO


2. A 44. DUNIA KULIZUNGUKA JUA
3. D 45. UJIMA
4. E
5. E
6. D
7. B
8. B
9. B
10. C
11. A
12. B
13. E
14. E
15. E
16. B
17. C
18. D
19. B
20. D
21. E
22. A
23. A
24. E
25. B
26. A
27. A
28. C
29. D
30. B
31. E
32. C
33. B
34. C
35. C
36. D
37. C
38. B
39. B
40. A
41. UINGEREZA
42. KICHWA CHA RAMANI
43.
I. UKAME

You might also like