You are on page 1of 10

Somo la 7 kwa ajili ya Februari 18, 2023

KWA MMOJAWAPO WA HAO WADOGO


“Kisha Mfalme atawaambia
walioko mkono wake wa kuume,
‘Njooni, mliobarikiwa na Baba
yangu, urithini ufalme
mliowekewa tayari tangu
kuumbwa kwa ulimwengu’”
(Matthayo 25:34)
Je ni nani hao ndugu wa Yesu walio wadogo?
Wenye njaa, kiu, wahamiaji, ombaomba, wagonjwa, wafungwa (Mat.
25:37-40). Mafungu mengine ya Biblia hutaja viziwi, vipofu an viwete.
Hebu tujifunze baadhi ya mifano ya Biblia na kuelewa namna ya
kuwahudumia “ndugu walio wadogo.”
Kisha, jiulize: Ninapaswa kufanya nini kuwasaidia ndugu wa Yesu
walio wadogo?

Mungu huwajali walio wahitaji:


Huduma ya Yesu
Sheria za Ubinadamu

Mifano ya Biblia:
Kuwahudumia maskini
Kuwahudumia wahitaji
MUNGU HUWAJALI WAHITAJI
HUDUMA YA YESU
“Ndipo alipojibu, akawaambia, ‘Nendeni mkamweleze Yohana mlioyaona na kuyasikia:
vipofu wanaona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakasika, viziwi wanasikia,
wafu wanafufuliwa, maskini wanahubiriwa habari njema.’” (Luka 7:22)
Yesu alisoma Isaya 61:1-2 kwenye Sinagogi Nazareti. Aya hii inaainisha
maana ya huduma ya Masihi.
Yesu aliwahudumia wahitaji kwa namna ambayo haikuwa ya kawaida siku
zile.
Watu walifikiri kuwa wahitaji walikuwa
wanaumia kutokana na dhambi zao, hivyo
walihudumiwa kama waliolaaniwa na
Mungu. Yesu aliwapenda na kuwaona
kama watu wanaoweza kuwa raia wa
Ufalme wa Mbinguni.
Alijaribu kukidhi mahitaji yao na
kuwapatia tumaini la Injili.
SHERIA ZA UBINADAMU
“Ikiwa kuna mtu maskini miongoni mwa ndugu zenu, katika mji wowote wa nchi hiyo
ambayo Bwana Mungu wenu anawapa, msiwe na moyo mgumu wala usimfumbie
mkono ndugu yako aliye maskini,” (Kumb 15:7)
Umaskini hautaondolewa kamwe (Kumb. 15:11; Mar. 14:7). Kwa
hiyo Mungu, aliwapa Israeli sheria za kuwalinda wahitaji

Kutoka 23:10-11 Walawi 19:14 Walawi 23:22

Mungu aliahidi mibaraka kwa


msaada wao waliowasaidia
wahitaji
Mashamba Ilikatazwa Sehemu ya (Zab. 41:1; Mit. 28:27).
hayakupandwa kila kuwalaani mavuno Upendo wa Mungu kwa wahitaji
mwaka wa Saba, viziwi au iliachwa nyuma ni mwongozo uliovuviwa kwetu.
masikini waliweza
kula mazao yao
kumwangusha kwa ajili ya Tunawezaje kutowapenda na
kiwete wahitaji kutowajali wahitaji?
MIFANO YA BIBLIA
KUWAHUDUMIA MASKINI
“[…] Uza vyote ulivyonavyo na uwagawie maskini […] Nusu ya mali
yangu nawagawia maskini;” (Luka 18:22; 19:8)
Kuna kufanana kati ya kisa cha mtawala kijana Tajiri (Mat. 19:16-22; Mar. 10:17-22; Luk.
18:18-23) na Zakayo’ (Luk. 19:1-10). Jinsi walivyo wahudumia maskini viliakisi mioyo yao na
uhusiano wao na Yesu
MIFANANO
Wote walikuwa tajiri KIJANA TAJIRI ZAKAYO
Wote walihitaji Yesu alimwambia awape Kwa hiari yake alijitolea
kukutana na Yesu maskini kuwapa maskini
Wote walihitaji Alihitaji kutoa nusu ya
TOFAUTI

uzima wa milele Alihitaji kutoa kila kitu


mali yake
Alimkataa Yesu Alimkubali Yesu
Yesu alihuzunishwa kwa sababu Yesu alifurahi kwa sababu
ya tamaa yake ya fedha alipokea wokovu
KUWAHUDUMIA WAHITAJI
“Kisha BWANA akamwuliza Shetani, ‘Je, umemwangalia huyo mtumishi wangu Ayubu? Kwa kuwa hapana mmoja aliye
kama yeye duniani, mtu mkamilifu na mwelekevu, mwenye kumcha Mungu na kuepukana na uovu?’” (Ayub 1:8)

Kwa nini Ayubu “hakuwa na lawama”? Ayub 29:12-16.


Nilimwokoa maskini aliyenililia (12a)
Yatima na yule asiyekuwa na mtu wa kumsaidia (12b)
Yule aliyekuwa anakufa alinibariki (13a)
Nikaufanya moyo wa mjane kuimba kwa furaha (13b)
Nilijivika haki ikanifunika (14)
Nilikuwa macho kwa vipofu (15a)
Nilijisikia kama mlemavu (15b)
Hebu tujifunze kutoka kwa Ayubu.
Nalikuwa baba kwa mhitaji (16a) Alikuwa makini kwa kuainisha mahitaji
katika mazingira yaliyomzunguka na
Na daawa ya mtu nisiyemjua naliichunguza (16b)
kutenda ilivyostahili.
“Kuna wengi ambao maisha ni mapambano ya
maumivu; wanaona mapungufu yao na hawana
furaha wala imani; wanafikiri hawana cha
kushukuru. Maneno ya upole, muonekano wa
huruma, shukrani vinaweza kuwa kama
kikombe cha maji ya baridi kwa nafsi zenye kiu
za watu wengi wanaopambana na walio
wapweke. Neno la huruma, tendo la wema,
vitanyanyua mizigo ambayo imelemea mabega
yaliyochoka. Na kila neno au tendo lisilokuwa na
ubinafsi la upole ni uwakilishi wa upendo wa
Kristo kwa wanadamu waliopotea.”
E. G. W. (Thoughts From the Mount of Blessing, cp. 2, p. 23)

You might also like