Professional Documents
Culture Documents
Kupungua uzito kunategemea na kiwango cha mafuta cha mtu mwilini (body fat), uzito wa mtu,
calories anazohitaji kwa siku, BMI yake pamoja na lengo la mtu la kupungua uzito. Je vyakula
ninavyokula hunipa nguvu (calories) na uwezo wa kumudu majukumu yangu ya kila siku? Nahitaji
kupunguza kiwango cha mafuta mwilini kwa kiasi gani? Kwa wengine wanahitaji kupunguza
asilimia 10, 20 au 25 ya kiwango cha mafuta mwilini.
Kwa maana hiyo, si kila diet plan humfaa kila mtu, inaweza ikakufaa wewe lakini isimfae mtu
mwingine.
Cha kuzingatia ili kupungua uzito ni kufuata ushauri wa wataalamu wa lishe (nutritionists),
daktari, wataalamu wa mazoezi na nk. Kama utafuatilia diet plan hii, utaona kila siku unahitaji
kunywa kikombe kimoja cha kahawa, ni vizuri kubadilisha unywaji wa kahawa kwa chai, yaani
kama leo utakunywa kahawa kesho kunywa chai na kadhalika. Kwa wale wenye ugonjwa wa
shinikizo la damu (hypertension), anxiety disorders na nk, wanashauriwa kuepuka kahawa kabisa
na hivyo wanywe chai. Wagonjwa wa kisukari wanaweza kunywa chai au kahawa kwa kukamulia
ndimu au limao ndani yake na hivyo kuongeza ladha.
Tembea kwa muda wa dakika 30 asubuhi au jioni kabla ya kula chakula chochote. Kwa wale
wenye mashine ya tredmill basi pia tembea kwa muda wa dakika 30 kwa kuanza na spidi ndogo
(kama namba 5 na kuongeza hadi spidi namba 8). Unaweza pia kukimbia kwa muda wa nusu saa
au kukimbia kwenye mashine ya tredmill kwa muda wa nusu saa. Anza kukimbia kwa spidi ndogo
(kwenye tredmill) halafu ongeza spidi yako, au unaweza kukimbia kwa spidi ya juu kama spidi 8
kwa muda wa dakika 5 na kisha kupunguza hadi spidi 5, hii inaitwa interval training, lengo ni
kukupa uwezo wa kufikisha dakika 30, kuchoma mafuta mwilini, kupunguza mapigo ya moyo
yarudi kwenye kiwango cha kawaida kwani wakati unafanya mazoezi mapigo ya moyo
huongezeka sana, kuupa uwezo moyo wako wa kufanya kazi vizuri.
Wale wenye matatizo ya kiafya ya mapigo ya moyo au wale ambao walishawahi kuugua hapo
awali matatizo haya kama atrial fibrillation, ventricular tarchycardia na nk, wagonjwa wa pumu,
ni vizuri kufanya mazoezi chini ya uangalizi wa wataalamu wa mazoezi (sports therapist) pamoja
na kushauriana na daktari.
Fanya mazoezi ya tumbo (sit-ups) kati ya 15-20. Ukiona ni ngumu sana unaweza kuanza hata na
sit-ups 10 na utakuwa unaongeza kadri siku zinavyoenda na kadri utavyokuwa unazoea maumivu
ya nyama za mbavu na tumbo.
Unaweza kutumia bench au kulala sakafuni. Ukimaliza kutembea na kufanya sit-ups kunywa maji
ya uvuguvugu glass 4. Siyo lazima unywe yote kwa wakati mmoja. Unaweza kuwa unakunywa
huku unaendelea na mambo mengine mpaka glasi 4 ziishe. Ili kuongezea ladha unaweza
kukamulia ndimu au limao katika maji hayo ya uvuguvugu. Limao na ndimu siyo tu huongeza
ladha bali pia vinasaidia kupunguza mafuta mwilini.
Jioni:
Tembea au kimbia tena kwa muda wa nusu saa (dakika 30) pamoja na kufanya sit-ups wakati
unasubiri chakula cha usiku.
Tembea kwa nusu saa asubuhi (dakika 30) na fanya sit-ups 15-30. Baada ya mazoezi kunywa maji
ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni:
Tembea au kimbia tena kwa muda wa nusu saa (dakika 30) na baada ya hapo fanya sit-ups 15-20
kisha kunywa maji ya uvuguvugu glasi 4. Epuka juisi aina yoyote ile iwe fresh au za kwenye boksi
kwani mara nyingi watu wanahadaiwa na juisi za kwenye boksi zinazosema ni fresh na hazina
kemikali yoyote, ukweli ni kwamba kampuni zinazotengeneza juisi hizi huwapa tenda kampuni za
kutengeneza manukato ambazo ndizo hutengeneza maboksi haya na kuweka syrup na harufu
kulingana na harufu ya tunda linalohitajika, mfano kama kampuni ya kutengeneza juisi inahitaji
boksi la harufu ya embe basi watawatengenezea boksi hilo kwa kutumia syrup ya embe na harufu
ya embe.
Pia juisi za kwenye boksi, wakati wa kutengenezwa huhifadhiwa kwa muda mrefu na kupitia
mlolongo mrefu wa utengenezaji hivyo kuondoa virutubisho asilia muhimu pamoja na fibre
ambazo ni muhimu sana kiafya.
Mazoezi kama kawaida. Kimbia au tembea kwa dakika 30, kisha fanya sit-ups 20-30. Kunywa maji
ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni:
Tembea au kimbia kwa muda wa nusu saa. Fanya sit-ups 20-30. Kunywa maji ya uvuguvugu glasi
4 baada ya kufanya mazoezi. Unaweza kula matunda wakati unasubiria chakula cha usiku.
Tembea au kimbia kwa muda wa nusu saa, kisha fanya sit-ups 20-30. Kunywa maji ya uvuguvugu
glasi 4.
Jioni:
Mazoezi kama kawaida.
Kimbia kwa dakika 30, kama utatembea, tembea kwa dakika 45. Fanya sit-ups 20-30. Kunywa
maji ya uvuguvugu galsi 4.
Jioni:
Kimbia kwa dakika 30 au tembea kwa dakika 45. Fanya sit-ups 20-30. Kunywa maji ya uvuguvugu
glasi 4.
Chakula cha usiku (Dinner):
Kula mboga mboga aina yoyote ile pamoja na matunda kwa wingi.
Tembea kwa dakika 45 au kimbia kwa muda wa nusu saa. Fanya sit-ups 20-30. Kunywa maji ya
uvuguvugu glasi 4.
Jioni:
Mazoezi kama kawaida.
Tembea kwa dakika 30-45, kama unakimbia basi kimbia kwa muda wa nusu saa. Fanya sit-ups 20-
30 kisha kunywa maji ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni:
Mazoezi kama kawaida
Chakula cha usiku (Dinner):
Nusu kuku au beef sausage, pamoja na wali maharage na salad au kachumbari ya aina yoyote ile
ya kutosha lakini isiwe na mayonnaise, cheese au butter.
Unaruhusiwa kunywa glasi 2 za white wine baada au wakati unakula kama ni kuku. Au glasi 2 za
red wine baada au wakati unakula kama ni beef sausage. Ila kama ni kuku iwe kuku, kama ni beef
sausage iwe hiyo na siyo vyote viwili.
SEHEMU YA PILI:
Katika muendelezo wa makala ya jinsi ya kupunguza uzito wako sehemu ya pili, leo tutaangalia
namna ya kufanya mazoezi na kula kwa mpangilio kuanzia siku ya nane (8) hadi ya kumi na nne
(14).
Vidokezo Muhimu
Kama ulifuatilia sehemu ya kwanza, muda wa kufanya mazoezi umeongezeka ukilinganisha na
zile siku saba za mwanzo, na pia siku hizi hakuna tena mazoezi ya kutembea ni kukimbia tu.
Unatakiwa kukimbia polepole kwa muda wa nusu saa. Ongeza spidi kwa dakika tano, punguza
dakika tano zinazofuata, ongeza spidi tena kwa dakika moja, punguza kwa dakika moja, ongeza
tena kwa dakika 1 au 2, punguza tena kwa dakika 1(Wale wenye mashine ya kukimbilia yaani
tredmill, kimbia kwa muda wa nusu saa kwa spidi 8, ongeza spidi hadi 9 kwa muda wa dakika 5,
punguza hadi spidi 8 kwa muda wa dakika 5 zinazofuata, ongeza spidi hadi 10 kwa muda wa
dakika 1, ongeza tena kwa dakika moja hadi spidi 11, punguza spidi hadi 10 kwa dakika 1
inayofuata, ongeza spidi hadi 12 kwa dakika 2 za mwisho. Tembea kwa dakika 3-4 kwa spidi ndogo
sana yaani kuanzia 5 kushuka chini mpaka utakapoona mapigo yako ya moyo kwenye mashine
yamerudi katika hali yake ya kawaida au chini ya 80.). Jumla utakuwa umekimbia kwa dakika 45.
Hii husaidia kupunguza mafuta mwilini hasa yale yanayozunguka viungo muhimu pamoja na yale
yaliyo kwenye mishipa ya damu, husaidia moyo kufanya kazi vizuri na huongeza muscle strength.
Kwa wale ambao inawawia vigumu kujizuia kula baada ya kupata chakula cha usiku, basi piga
mswaki nusu saa baada ya kula, hii itasaidia kukuondolea hamu ya kutaka kula tena. Mazoezi ya
sit-ups utaongeza kwa kadri unavyojisikia lakini isiwe chini ya sit-ups 50.
Jioni:
Kimbia tena kwa dakika 45, fanya sit-ups 50. Kunywa maji ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni:
Kimbia kwa dakika 45. Fanya sit-ups 50. Maji ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni:
Mazoezi kama kawaida kisha kunywa maji ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni:
Mazoezi kama kawaida
Jioni:
Mazoezi kama kawaida.
Jioni:
Mazoezi kama kawaida
Kuanzia siku ya 15 hadi ya 23, muda wa mazoezi umeongezeka na sit-ups pia zimeongezeka. Kama
ulifuatilia kwa makini, basi nadhani umeshaanza kuona mabadiliko katika mwili wako. Wale
wenye mashine ya tredmill, tembea au kimbia kwa spidi ileile kama ya siku zilizopita. Usikate
tamaa, fanya ratiba hii kuwa sehemu ya maisha yako ya kila siku.
Jioni
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja. Fanya sit-ups 50-60. Maji ya uvuguvugu
glasi 4.
Asubuhi
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja. Fanya sit-ups 50-60. Kunywa maji ya
uvuguvugu glasi 4.
Jioni
Mazoezi kama kawaida.
Asubuhi
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja. Fanya sit-ups 60-65. Maji ya uvuguvugu
glasi 4.
Jioni
Mazoezi kama kawaida
Asubuhi
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja. Fanya sit-ups 60-65. Maji ya uvuguvugu
glasi 4.
Mlo wa Asubuhi (Breakfast)
Kikombe kimoja cha chai au kahawa. Slice moja ya mkate ya kuoka (toasted bread). Yai 1 la
kuchemsha, usile kiini chake (yellow part). Sausage moja ya kuchemsha ya nyama ya aina yoyote
isipokuwa nyama ya nguruwe. Matunda aina yoyote.
Jioni
Mazoezi kama kawaida
Jioni
Mazoezi kama kawaida
Jioni
Kimbia au tembea kwa haraka kwa saa moja, ruka kamba kwa muda wa robo saa (15 minutes).
Fanya sit-ups 70-75. Maji ya uvuguvugu glasi 4.
Asubuhi
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja, ruka kamba kwa dakika 15. Fanya sit-ups
70-75. Maji ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja, ruka kamba kwa dakika 15, fanya sit-ups
70-75.
Asubuhi
Ruka kamba kwa dakika 20, fanya sit-ups 100. Leo sio lazima ukimbie. Maji ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni
Ruka kamba kwa dakika 20, fanya sit-ups 100. Maji ya uvuguvugu glasi 4.
Asubuhi
Kimbia au tembea kwa muda wa saa moja, ruka kamba kwa dakika 20, fanya sit-ups 100. Maji ya
uvuguvugu glasi 4.
Jioni
Kimbia au tembea kwa muda wa saa moja, ruka kamba kwa dakika 20, fanya sit-ups 100.
Jioni
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja, ruka kamba kwa dakika 30.
Asubuhi
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja, ruka kamba kwa dakika 30, fanya sit-ups
100, maji ya uvuguvugu glasi 4.
Asubuhi
Kimbia au tembea kwa haraka kwa muda wa saa moja, ruka kamba kwa dakika 30 (au unaweza
kufanya aerobics kwa dakika 30), fanya sit-ups 100. Maji ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni
Mazoezi kama kawaida
Jioni
Pumzika, usifanye mazoezi yoyote.
Chakula cha Usiku (Dinner)
Supu ya samaki wa aina yoyote yule, slice 2 za mkate (toasted brown bread), glasi moja ya juisi
ya aina yoyote (fresh). Maji ya uvuguvugu glasi 4.
Jioni
Pumzika, usifanye mazoezi yoyote.
Jioni
Pumzika, usifanye mazoezi yoyote.
Jioni
Pumzika, usifanye mazoezi yoyote.