You are on page 1of 36

MATHAYO

Utangulizi
Mathayo alikuwa mtoza ushuru ambaye Bwana Yesu alimwita awe mwanafunzi wake mwanzoni kabisa wa
huduma yake ya hadharani. Kwa hiyo mambo mengi anayoyaelezea aliyashuhudia kwa macho yake mwenyewe.
Anaanza kwa kueleza kwa kirefu kuhusu kuzaliwa kwa Yesu na Bikira Maria, kubatizwa kwake na kujaribiwa
kwake nyikani. Yesu alikuja akihubiri juu ya Ufalme wa Mungu ambao ni wa kila mtu anayetaka kupata uzima wa
milele. Mtu anaingia katika Ufalme huu kwa kutubu dhambi na kumwamini Yesu. Mathayo ameyagawa
mafundisho ya Yesu katika sehemu kubwa tano: Maadili, Kueneza Habari Njema, Mifano, Ushirika na kuja kwa
Ufalme wa Mungu. Sehemu ya Mwisho ya Injili ya Mathayo inaeleza juu ya kufa na kufufuka kwa Yesu, na agizo
alilotoa kwa wote wanaomwamini kueneza Habari Njema ulimwenguni kote.

Wazo Kuu
Shabaha kuu ya Mathayo katika kuandika Injili hii, ilikuwa ni kuonyesha kwamba Bwana Yesu anakamilisha
ahadi aliyoitoa Mungu katika Agano la Kale. Kwa sababu hii, Bwana Yesu anatambulishwa kuwa ni mwana wa
Mfalme Daudi na pia mzao wa Abrahamu (1:1). Kadhalika Mathayo anatumia mifano mingi kutoka katika unabii
uliotolewa na manabii wa Agano la Kale, kueleza maisha ya Bwana Yesu ambaye alikuja kuwa Mwokozi wa
Wayahudi (1:21), wa watu Mataifa mengine (4:13-16) na hatimaye Mwokozi wa ulimwengu wote (28:19). Maadili
yawapasayo watu wanaoingia katika Ufalme wa Mungu yanaelezwa katika Mahubiri ya Mlimani (Sura 5-7),
ambapo wana wa Mungu wanaagizwa kukataa kufuata maadili ya dunia hii na kutafuta kwanza Ufalme wa
Mungu na haki yake, ndipo hayo mengineyo watakapozidishiwa. (6:33).

Mgawanyo
1 Maisha na huduma ya Bwana Yesu (1:1-4:25)
2 Mahubiri ya Mlimani (5:1-7:29)
3 Mafundisho, Mifano na Mazungumzo (8:1-18:35)
4 Safari ya kwenda Yerusalemu na maonyo ya mwisho (19:1-23:39)
5 Unabii kuhusu mambo yajayo (24:1-25:46)
6 Kufa na kufufuka kwa Bwana Yesu (26:1-28:20).

1
MATHAYO
Ukoo Wa Yesu Kristo 16Yakobo akamzaa Yosefu ambaye alikuwa
1 Habari za ukoo wa Yesu Kristo mwana wa
Daudi, mwana wa Abrahamu:
mumewe Maria,
mama yake Yesu, aitwaye Kristo b .
2Abrahamu akamzaa Isaki,

Isaki akamzaa Yakobo, 17Hivyo,


kulikuwapo na jumla ya vizazi kumi
Yakobo akamzaa Yuda na ndugu zake. na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi
3Yuda akamzaa Peresi na Zera kumi na vinne tangu Daudi hadi wakati wa
ambao mama yao alikuwa Tamari. uhamisho wa Babeli na vizazi kumi na vinne
Peresi akamzaa Esroni, tangu wakati wa uhamisho wa Babeli hadi
Esroni akamzaa Aramu, Kristo.
4Aramu akamzaa Aminadabu,

Aminadabu akamzaa Nashoni, Kuzaliwa Kwa Yesu Kristo


Nashoni akamzaa Salmoni, 18Basi Kuzaliwa kwake Yesu Kristo kulikuwa
5Salmoni akamzaa Boazi hivi: Maria mama yake alikuwa ameposwa na
na mama yake Salmoni alikuwa Yosefu, lakini kabla hawajakutana kimwili, Maria
Rahabu. alionekana ana mimba kwa uweza wa Roho
Boazi akamzaa Obedi, Mtakatifu. 19Kwa kuwa Yosefu, mwanaume
ambaye mama yake alikuwa Ruthi. aliyekuwa amemposa alikuwa mtu mwadilifu,
Obedi akamzaa Yese, hakutaka kumwaibisha Maria hadharani,
6Yese akamzaa Daudi ambaye aliazimu kumwacha kwa siri.
alikuwa mfalme. 20Lakini mara alipoazimu kufanya jambo hili,

malaika wa Bwana akamtokea katika ndoto na


Daudi akamzaa Solomoni ambaye kusema., “Yosefu mwana wa Daudi, usiogope
mama yake ni yule aliyekuwa mke wa kumchukua Maria awe mke wako, kwa maana
Uria. mimba aliyo nayo ni kwa uweza wa Roho
7Solomoni akamzaa Rehoboamu, Mtakatifu. 21Naye atamzaa mwana , nawe
Rehoboamu akamzaa Abiya, utamwita jina lake Yesu, kwa maana yeye ndiye
Abiya akamzaa Asa, atakayewaokoa watu wake kutoka katika
8Asa akamzaa Yehoshafati, dhambi zao.”
Yehoshafati akamzaa Yoramu a , 22Haya yote yametukia ili kutimiza lile

Yoramu akamzaa Uzia, Bwana alilokuwa amenena kupitia nabii,


9Uzia akamzaa Yothamu, akisema: 23“Tazama, bikira atachukua mimba,
Yothamu akamzaa Ahazi, naye atamzaa mwana, nao watamwita jina lake
Ahazi akamzaa Hezekia, Imanueli,’’ maana yake, “Mungu pamoja nasi.’’
10Hezekia akamzaa Manase, 24Yosefu alipoamka kutoka usingizini,
Manase akamzaa Amoni, akafanya kama vile alivyoagizwa na malaika wa
Amoni akamzaa Yosia, Bwana, akamchukua Maria kuwa mke wake
11wakati wa uhamisho wa Babeli, Yosia 25Lakini hawakukutana kimwili mpaka Maria

alimzaa Yekonia na ndugu zake. alipojifungua mwanawe kifungua mimba


akamwita jina lake Yesu.
12Na baada ya uhamisho wa Babeli,
Yekonia alimzaa Shealtieli, Wataalamu Wa Nyota Wafika Kumwona
Shealtieli akamzaa Zerubabeli, Mtoto Yesu

2
13Zerubabeli akamzaa Abiudi, Baada ya Yesu kuzaliwa katika mji wa
Abiudi akamzaa Eliakimu, Bethlehemu huko Uyahudi, wakati wa
Eliakimu akamzaa Azori, utawala wa mfalme Herode, wataalamu wa
14Azori akamzaa Zadoki, mambo ya nyota kutoka Mashariki walifika
Zadoki akamzaa Akimu, Yerusalemu 2wakiuliza, “Yuko wapi huyo
Akimu akamzaa Eliudi, aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana
15Eliudi akamzaa Eliezari, tumeona nyota yake ikitokea mashariki, nasi
Eliezari akamzaa Matani, tumekuja kumwabudu.’’
Matani akamzaa Yakobo,

a8 Yoramu ndiye Yehoramu b16 Kristo maana yake Masiya, yaani, Mpakwa (aliyetiwa)Mafuta
2
MATHAYO
3Mfalme Herode aliposikia jambo hili wataalamu wa nyota wamemshinda kwa akili,
aliingiwa na hofu sana pamoja na watu wote wa alikasirika sana, naye akatoa amri ya kuwaua
Yerusalemu. 4Herode akawaita pamoja watoto wote wa kiume wenye umri wa miaka
makuhani wakuu na waandishi wa watu, miwili kurudi chini katika mji wa Bethlehemu na
akawauliza ni mahali gani ambapo Kristo sehemu zote za jirani, kufuatana na ule muda
angezaliwa. 5Nao wakamwambia, “Katika alioambiwa na wale wataalamu wa nyota.
Uyahudi, kwa maana hivyo ndivyo ilivyoandikwa 17Ndipo lile lililonenwa na nabii Yeremia

na nabii: lilipotimia.

6 ‘ ‘‘Nawe, Bethlehemu, katika nchi ya Yuda, 18 “Sauti


ilisikika huko Rama,
wewe si mdogo miongoni mwa kilio cha huzuni na maombolezo makuu,
watawala wa Yuda, Raheli akilia kwa ajili ya wanawe,
kwa maana kutoka kwako atakuja mtawala akikataa kufarijiwa,
atakayekuwa mchungaji wa watu kwa sababu hawako tena.’’
wangu Israeli.’ ’’
Kurudi Kutoka Misri
7Ndipo Herode akawaita wale wataalamu 19Baada ya Herode kufa, malaika wa Bwana

wa nyota kwa siri na kutaka kujua kutoka kwao akamtokea Yosefu katika ndoto huko Misri 20na
uhakika kamili wa wakati ile nyota ilipoonekana. kusema, “Ondoka, mchukue mtoto na mama
8Kisha akawatuma waende Bethlehemu mwende, mrudi katika nchi ya Israeli kwa
akiwaambia, “Nendeni mkamtafute kwa bidii sababu wale waliokuwa wanatafuta uhai wa
huyo mtoto. Nanyi mara mumwonapo, mniletee mtoto wamekufa.
habari ili na mimi niweze kwenda kumwabudu.’’ 21Basi Yosefu, akaondoka akamchukua
9Baada ya kumsikia mfalme, wale mtoto na mama yake wakaenda mpaka nchi ya
wataalamu wa nyota wakaenda zao, nayo ile Israeli. 22Lakini aliposikia kwamba Arkelao
nyota waliyoiona mashariki ikawatangulia, nao alikuwa anatawala huko Uyahudi mahali pa
wakaifuata mpaka iliposimama mahali pale Herode baba yake, aliogopa kwenda huko.
alipokuwa mtoto. 10Walipoiona ile nyota Naye akiisha kuonywa katika ndoto, akaenda
wakajawa na furaha kubwa mno. 11Walipoingia zake sehemu za Galilaya, 23akaenda, akaishi
ndani ya ile nyumba, wakamwona mtoto pamoja katika mji ulioitwa Nazareti, hivyo likawa
na Maria mama yake, wakamsujudu na limetimia lile lililonenwa na manabii, “Ataitwa
kumwabudu yule mtoto Yesu. Ndipo Mnazarayo.”
wakafungua hazina zao, wakamtolea zawadi za
dhahabu, uvumba na manemane. 12Nao Yohana Mbatizaji Atayarisha Njia
wakiisha kuonywa katika ndoto wasirudi kwa
Herode, wakarudi kwenda katika nchi yao kwa 3 Siku hizo Yohana Mbatizaji alikuja akihubiri
katika nyika ya Uyahudi, akisema,
njia nyingine. 2“Tubuni, kwa maana Ufalme wa Mbinguni u

karibu.” 3Huyu ndiye yule aliyenenwa habari


Yosefu, Maria Na Mtoto Yesu Wakimbilia zake na nabii Isaya aliposema,
Misri
13Walipokwisha kwenda zao, malaika wa ‘‘Sauti ya mtu yule aliaye huko nyikani,
Bwana akamtokea Yosefu katika ndoto ‘Tayarisheni njia kwa ajili ya Bwana,
akamwambia, “Ondoka, mchukue mtoto na yanyosheni mapito yake.’ ’’
mama yake mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka 4Basi Yohana alivaa vazi lililotengenezwa

nitakapowaambia, kwa maana Herode anataka kwa singa za ngamia akiwa na mkanda wa
kumtafuta huyu mtoto ili amwue.’’ ngozi kiunoni mwake, chakula chake kilikuwa
14Kisha Yosefu akaondoka, akamchukua nzige na asali ya mwitu. 5Watu walimwendea
mtoto na mama wakati wa usiku, nao wakaenda kutoka Yerusalemu, Uyahudi yote na nchi zote
Misri 15ambako walikaa mpaka Herode za kando kando ya mto Yordani. 6Nao
alipokufa. Hili lilikuwa, ili litimie lile lililonenwa na wakaziungama dhambi zao, akawabatiza katika
Bwana kwa kinywa cha nabii kusema, “Kutoka Mto Yordani.
Misri nilimwita mwanangu” 7Lakini alipowaona Mafarisayo na
16Herode alipong’amua kwamba wale

3
MATHAYO
Masadukayo wengi wakija ili kubatizwa, 6akamwambia, “Kama Wewe ndiye Mwana wa
aliwaambia, ‘‘Ninyi watoto wa nyoka! Ni nani Mungu jitupe chini, kwa kuwa imeandikwa,
aliyewaonya kuikimbia ghadhabu inayokuja?
8Basi zaeni matunda yastahiliyo toba. 9Wala ‘ “Atakuagizia malaika zake,
msijidhanie mnaweza kujiambia, ‘Sisi tunaye nao watakuchukua mikononi mwao
Abrahamu, baba yetu, kwa maana nawaambia ili usije ukajikwaa mguu wako kwenye
kuwa Mungu anaweza kumuinulia Abrahamu jiwe.’ ’’
watoto kutoka katika mawe haya. 10Hata sasa
shoka limekwisha kuwekwa tayari kwenye mizizi 7Yesu akamjibu, “Pia imeandikwa:
ya mti. Kila mti usiozaa matunda mazuri, ‘Usimjaribu Bwana Mungu wako.’ ’’
hukatwa na kutupwa motoni. 8Kwa mara nyingine, ibilisi akamchukua
11“Mimi nawabatiza kwa maji kwa ajili ya Yesu mpaka kwenye kilele cha mlima mrefu na
toba. Lakini nyuma yangu anakuja Yeye aliye na kumwonyesha falme zote za dunia na fahari
uwezo kuliko mimi, ambaye sistahili hata zake, 9kisha akamwambia, “Nitakupa hivi vyote
kuchukua viatu vyake. Yeye atawabatiza kwa a kama ukinisujudia na kuniabudu.’’
Roho Mtakatifu na kwa moto. 12Chombo chake 10Yesu akamwambia, “Ondoka mbele
cha kupuria kiko mkononi mwake, naye yangu, Shetani! Kwa maana imeandikwa,
atasafisha sakafu yake ya kupuria, akiikusanya ‘Utamwabudu Bwana Mungu wako, nawe
ngano yake ghalani na kuyachoma makapi kwa utamtumikia Yeye peke yake.’ ’’
moto usiozimika.” 11Ndipo ibilisi akamwacha, nao malaika

wakaja na kumtumikia.
Yesu Abatizwa
13Kisha Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yesu Aanza Kuhubiri
mto Yordani ili Yohana ambatize. 14Lakini 12Yesu aliposikia kwamba Yohana Mbatizaji

Yohana akajitahidi kumzuia, akimwambia, “Mimi alikuwa ametiwa gerezani, alirudi Galilaya.
ninahitaji kubatizwa na Wewe, nawe waja 13Akaondoka Nazareti akaenda kuishi
kwangu nikubatize?’’ Kapernaumu ulioko karibu na bahari, katika
15Lakini Yesu akamjibu, “Kubali hivi sasa, mipaka ya nchi ya Zabuloni na ya Naftali, 14ili
kwa maana ndivyo itupasavyo kwa njia hii kutimiza unabii wa nabii Isaya, kama
kuitimiza haki yote.’’ Hivyo Yohana akakubali. alivyosema:
16Naye Yesu alipokwisha kubatizwa, mara

alipotoka ndani ya maji, ghafula mbingu 15“Nchiya Zabuloni na nchi ya Naftali,


zikamfungukia, akamwona Roho wa Mungu kwenye njia ya kuelekea baharini, ng'ambo
akishuka kama hua na kutulia juu yake. 17Nayo ya Yordani,
sauti kutoka mbinguni ikasema, “Huyu ni Galilaya ya watu Mataifa,
Mwanangu mpendwa, ambaye ninapendezwa 16watu wale waliokaa gizani

sana naye.’’ wameona nuru kuu


nao wale waliokaa katika nchi ya uvuli wa
Kujaribiwa Kwa Yesu mauti,

4 Kisha Yesu akaongozwa na Roho


Mtakatifu kuingia nyikani ili akajaribiwe na
nuru imewazukia.’’

Ibilisi. 2Baada ya kufunga siku arobaini mchana 17Tanguwakati huo, Yesu alianza kuhubiri
na usiku, hatimaye akaona njaa. 3Mjaribu akisema: “Tubuni, kwa maana Ufalme wa
akamjia na kumwambia, “Kama Wewe ndiye Mbinguni umekaribia.’’
Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yawe
mikate.’’ Yesu Awaita Wanafunzi Wake wa Kwanza
4Lakini Yesu akajibu, “Imeandikwa, ‘Mtu 18Wakati Yesu alipokuwa anatembea kando

haishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo ya bahari ya Galilaya aliwaona ndugu wawili,
katika kinywa cha Mungu.’ ’’ Simoni aitwaye Petro na Andrea ndugu yake.
5Ndipo ibilisi akamchukua Yesu mpaka mji Walikuwa wakizitupa nyavu zao baharini kwa
mtakatifu wa Yerusalemu na kumweka juu ya maana wao walikuwa wavuvi. 19Yesu
mnara mrefu mwembamba wa hekalu, akawaambia, “Njooni, nifuateni, nami
nitawafanya muwe wavuvi wa watu.’’ Mara
20
a11 “Kwa” hapa ina maana “ndani ya, katika
4
MATHAYO
wakaziacha nyavu zao, wakamfuata. 13‘‘Ninyi ni chumvi ya ulimwengu. Lakini
21Alipoendelea mbele kutoka pale, chumvi ikipoteza ladha yake, yawezaje
akawaona ndugu wengine wawili, Yakobo kurudishiwa ladha yake tena ? Haifai tena kwa
mwana wa Zebedayo na Yohana nduguye, kitu cho chote, ila kutupwa nje ikanyagwe na
wakiwa wamekaa kwenye mashua pamoja na watu.
baba yao Zebedayo wakiziandaa nyavu zao. 14‘‘Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji

Yesu akawaita. 22Nao mara wakaziacha nyavu uliojengwa kilimani hauwezi kufichika. 15Wala
zao, pamoja na baba yao, wakamfuata. watu hawawashi taa na kuifunika kwa bakuli.
Badala yake, huiweka kwenye kinara chake,
Yesu Ahubiri Na Kuponya Wagonjwa nayo hutoa mwanga kwa kila mtu aliyemo ndani
23Yesu akapita katika Galilaya yote, ya ile nyumba. 16Vivyo hivyo, nuru yenu iangaze
akifundisha katika masinagogi yao, akihubiri mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu
Habari Njema za Ufalme wa Mungu, akiponya mema wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.
kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni
mwa watu.. 24Kwa hiyo sifa zake zikaenea Kutimiza Sheria
sehemu zote za Shamu, nao watu wakamletea 17“Msidhani kwamba nimekuja kuondoa

wote waliokuwa na magonjwa mbalimbali na Torati au Manabii, sikuja kuondoa bali kutimiza.
maumivu, waliopagawa na pepo, wenye kifafa 18Kwa maana,amin, nawaambia, mpaka mbingu

na waliopooza, naye akawaponya. 25Makutano na dunia zitakapopita, hakuna hata herufi moja
makubwa ya watu yakawa yanamjia kutoka ndogo wala nukta itakayopotea kwa namna yo
Galilaya, Dekapoli, Yerusalemu, Uyahudi na yote kutoka kwenye Torati mpaka kila kitu kiwe
kutoka ng'ambo ya Mto Yordani. kimetimia. 19Kwa hiyo, ye yote atakayevunja
mojawapo ya amri ndogo kuliko zote ya amri
Sifa za Aliyebariki hizi, naye akawafundisha wengine kufanya

5 Basi Yesu alipoona makutano, alipanda


mlimani akaketi chini, nao wanafunzi
hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika Ufalme wa
Mbinguni, lakini ye yote azitendaye na
wake wakamjia. 2Ndipo akaanza kuwafundisha, kuzifundisha hizi amri ataitwa mkuu katika
akisema: Ufalme ya Mbinguni. 20Kwa maana nawaambia,
haki yenu isipozidi haki ya waandishi wa sheria
3 “Wana heri walio masikini wa roho, na Mafarisayo, kamwe hamtaingia katika
maana hao Ufalme wa Mbinguni ni wao. Ufalme wa Mbinguni.
4Wana heri wale wanaohuzunika,

maana hao watafarijiwa. Kuhusu Hasira


5Wana heri walio wapole, 21“Mmesikia walivyoambiwa watu wa
maana hao watairithi nchi. zamani kwamba, ‘Usiue, ye yote atakayeua
6Wana heri wenye njaa na kiu ya haki, atapasiwa hukumu.’ 22Lakini mimi nawaambia
maana hao watatoshelezwa. kwamba, ye yote atakayemkasirikia ndugu yake
7Wana heri wenye huruma, wa kiume au wa kike, atapasiwa hukumu. Tena,
maana hao watapata rehema. ye yote atakayemwambia ndugu yake wa kiume
8Wana heri walio na moyo safi, au wa kike, ‘Raca’ a , yaani kumdharau na
maana hao watamwona Mungu. kumdhihaki, atapasiwa kufanyiwa baraza. Lakini
9Wana heri walio wapatanishi, ye yote atakayesema ‘We mpumbavu ulaaniwe!’
maana hao wataitwa wana wa Mungu. Atapasiwa hukumu ya moto wa jehanam.
10Wana heri wanaoteswa kwa sababu ya haki, 23“Kwa hiyo, kama unatoa sadaka yako

maana hao Ufalme wa Mbinguni ni wao. madhabahuni, ukakumbuka kuwa ndugu yako
ana kitu dhidi yako, 24iache sadaka yako hapo
11Mna heri ninyi watu watakapowashutumu hapo, mbele ya madhabahu, uende kwanza
na kuwatesa na kunena dhidi yenu mabaya ya
aina zote kwa uongo kwa ajili yangu. 12Furahini
na kushangilia kwa maana thawabu yenu ni
kuu.
a22 ‘Raca’ ni neno la Kiaramu ambalo maana yake ni dharau
Chumvi na Nuru na dhihaka ya hali ya juu.

5
MATHAYO
ukapatane na ndugu yako wa kiume au wa kike, kuchukua shati lako, mwachie achukue na koti
kisha urudi na ukatoe sadaka yako. pia. 41Kama mtu akikulazimisha kwenda
25“Patana na mshtaki wako upesi wakati kilometa moja, nenda naye kilometa mbili.
uwapo njiani pamoja naye kwenda 42Mpe yeye akuombaye, wala usimgeuzie

mahakamani, ili mshtaki wako asije akakutia kisogo yeye atakaye kukukopa.’’
mikononi mwa hakimu, naye hakimu akakutia
mikononi mwa walinzi, nawe ukatupwa Upendo Kwa Adui
gerezani. 26Amin, nakuambia, hutatoka humo 43‘‘Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Mpende

mpaka umelipa hadi senti ya mwisho” jirani yako na umchukie adui yako.’ 44Lakini
mimi ninawaambia : Wapendeni adui zenu na
Kuhusu Uzinzi waombeeni wanaowatesa ninyi, 45ili mpate
27“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Usizini'. kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa
28Lakini mimi nawaambia: kwamba ye yote maana Yeye huwaangazia jua lake watu waovu
amtazamaye mwanamke kwa kumtamani, na watu wema, naye huwanyeshea mvua
amekwisha kuzini naye moyoni mwake. 29Jicho wenye haki na wasio haki. 46Kama mkiwapenda
lako la kuume likikufanya utende dhambi, ling'oe wale wanaowapenda tu, mtapata thawabu gani?
ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza Je, hata watoza ushuru hawafanyi hivyo?
kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako 47Nanyi kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, je,

mzima utupwe jehanam. 30Kama mkono wako mnafanya nini zaidi ya wengine? Je, hata watu
wa kuume ukikufanya utende dhambi, ukate wasiomjua Mungu, hawafanyi hivyo? 48Kwa hiyo
uutupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza iweni wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni
kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako alivyo mkamilifu.’’
mzima utupwe jehanam.
Kuwapa Wahitaji
Kuhusu Talaka
31‘‘Pia ilinenwa kwamba, ‘Mtu ye yote 6 ‘‘Angalieni msitende wema wenu mbele ya
watu ili wawaone. Kwa maana mkifanya
amwachaye mkewe na ampe hati ya talaka.’ hivyo, hamna thawabu kutoka kwa Baba yenu
32Lakini mimi nawaambia, ye yote amwachaye aliye mbinguni.
mkewe isipokuwa kwa kosa la uasherati, 2‘‘Hivyo mnapowapa wahitaji, msipige
amfanya mkewe kuwa mzinzi. Na ye yote panda mbele yenu kama wafanyavyo wanafiki
amwoaye yule mwanamke aliyeachwa azini.’’ katika masinagogi na mitaani, ili wasifiwe na
watu. Amin, amin nawaambia wao wamekwisha
Kuhusu Kuapa kupokea thawabu yao. 3Lakini ninyi mtoapo
33“Tena mmesikia walivyoambiwa watu wa sadaka, fanyeni kwa siri, hata mkono wako wa
zamani kwamba, ‘Usiape kwa uongo, bali kushoto usijue mkono wako wa kuume
timizeni, nadhiri zile ulizofanya kwa Bwana’ unachofanya, 4ili sadaka yako iwe ni siri. Ndipo
34Lakini mimi nawaambia,’’Msiape kabisa, ama Baba yako wa mbinguni, Yeye aonaye sirini
kwa mbingu, kwa kuwa ni kiti cha enzi cha atakupa thawabu kwa wazi.
Mungu, 35au kwa nchi, kwa kuwa ndipo mahali
pake pa kuwekea miguu, au kwa Yerusalemu, Kuhusu Maombi
kwa kuwa ndio mji wa Mfalme Mkuu. 36Nanyi 5“Nanyi msalipo, msiwe kama wanafiki,

msiape kwa vichwa vyenu kwa kuwa hamwezi maana wao hupenda kusali wakiwa
kuufanya hata unywele mmoja kuwa mweupe wamesimama katika masinagogi na kando ya
au mweusi. 37‘Ndiyo,’ yenu iwe ‘Ndiyo’ na barabara ili waonekane na watu. Amin, amin
‘Hapana’, yenu iwe ‘Hapana.’ Lo lote zaidi ya hili nawaambieni, wao wamekwisha kupata
latoka kwa yule mwovu.’’ thawabu yao. 6Lakini wewe unaposali, ingia
chumbani mwako, funga mlango na umwombe
Kuhusu Kulipiza Kisasi Baba yako aliye sirini. Naye Baba yako aonaye
38“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Jicho kwa sirini atakupa thawabu yako. 7“Nanyi mnaposali
jicho na jino kwa jino.’ 39Lakini mimi nawaambia, msiseme maneno kama wafanyavyo watu
msishindane na mtu mwovu. Lakini kama mtu wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani
akikupiga kwenye shavu la kuume, mgeuzie na kwamba watasikiwa kwa sababu ya wingi wa
la pili pia, 40Kama mtu akitaka kukushtaki na maneno yao. 8Msiwe kama wao, kwa sababu

6
MATHAYO
Baba yenu anajua kile mnachohitaji kabla namna gani ! ”
hamjamwomba.’’
9‘‘Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba : Mungu Na Mali
24‘‘Hakuna mtu ye yote awezaye
“Baba yetu uliye mbinguni, kuwatumikia mabwana wawili, kwa kuwa ama
Jina lako litukuzwe. atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine,
10Ufalme wako uje. au atashikamana sana na huyu na kumdharau
Mapenzi yako yafanyike hapa duniani huyu mwingine. Ninyi hamwezi kumtumikia
kama huko mbinguni. Mungu na mali a .’’
11Utupatie leo riziki zetu za kila siku.
12Utusamehe deni zetu, Msiwe Na Wasiwasi
kama sisi nasi tulivyokwisha 25‘‘Kwa hiyo nawaambia, msiwe na
kuwasamehe wadeni wetu. wasiwasi kuhusu maisha yenu: mtakula nini au
13 Usitutie majaribuni, mtakunywa nini, au kuhusu miili yenu, mtavaa
bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu, nini. Je, maisha si zaidi ya chakula na mwili
kwa kuwa Ufalme ni Wako na nguvu zaidi ya mavazi? 26Waangalieni ndege wa
na utukufu hata milele. Amen.” angani, wao hawapandi wala hawavuni au
kuweka ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni
14Kwa kuwa kama mkiwasamehe watu wengine huwalisha hao. Je, ninyi si wa thamani zaidi
wanapowakosea, Baba yenu wa mbinguni kuliko hao ndege? 27Ni nani miongoni mwenu
atawasamehe pia na ninyi. 15Lakini ambaye kwa kujitaabisha kwake aweza
msipowasamehe watu wengine makosa yao, kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha
wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa yake au kuongeza dhiraa moja b kwenye kimo
yenu. chake ?
28‘‘Nanyi kwa nini kujitaabisha kwa ajili ya

Kuhusu Kufunga mavazi? Fikirini maua ya shambani yameavyo.


16“Mnapofunga, msiwe wenye huzuni kama Hayafanyi kazi wala hayafumi. 29Lakini
wafanyavyo wanafiki. Maana wao hukunja nawaambia, hata mfalme Solomoni katika fahari
nyuso zao ili kuwaonyesha wengine kwamba yake yote hakuvikwa kama mojawapo ya hayo
wamefunga. Amin, amin nawaambia wao maua. 30Lakini ikiwa Mungu anayavika hivi
wamekwisha kupata thawabu yao kamilifu. majani ya shambani, ambayo leo yapo na kesho
17Lakini mnapofunga, jipakeni mafuta kichwani yanatupwa motoni, je, hatawavika ninyi vizuri
na kunawa nyuso zenu 18ili kufunga kwenu zaidi, enyi wa imani haba? 31Kwa hiyo msiwe na
kusionekane na watu wengine ila Baba yenu wasiwasi, mkisema, ‘Tutakula nini?’ Au
aliye sirini, naye Baba yenu aonaye sirini ‘Tutakunywa nini?’ Au ‘Tutavaa nini?’ 32Kwa
atawapa thawabu yenu kwa wazi.” maana watu wasiomjua Mungu ndio
wanaoshindania hayo, lakini Baba yenu wa
Akiba Ya Mbinguni mbinguni anafahamu kwamba mnahitaji hayo
19“Msijiwekee hazina duniani, mahali yote. 33Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa
ambapo nondo na kutu huharibu, nao wevi Mungu na haki yake na haya yote
huvunja na kuiba. 20Lakini jiwekeeni hazina mtaongezewa. 34Kwa hiyo msiwe na wasi wasi
mbinguni, mahali ambapo nondo na kutu kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajitaabikia
haviharibu, wala wevi hawavunji na kuiba. yenyewe. Yatosha kwa siku masumbufu yake.’’
21Kwa sababu mahali akiba yako ilipo, hapo

ndipo pia moyo wako utakapokuwa.’’ Kuwahukumu Wengine


“Usihukumu ili usije ukahukumiwa. 2Kwa
7 maana kwa jinsi ile unavyowahukumu
Jicho Ni Taa Ya Mwili wengine, ndivyo utakavyohukumiwa na kwa
22‘‘Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni kipimo kile utakachotoa ndicho utakachopokea.
nyofu, mwili wako wote utakuwa na nuru.
23Lakini kama jicho lako ni ovu, mwili wako wote
a24 Mali hapa ina maana ya ‘Mammon,’ ambalo ni neno la
utajawa na giza. Kwa hiyo basi, kama nuru Kiaramu
iliyomo ndani yako ikiwa giza, hilo ni giza kuu au kwa Kiyunani ‘‘Mamona’’ maana yake mali, utajiri
b27 Dhiraa moja ni sawa na sentimita 45
7
MATHAYO
3‘‘Kwa nini unatazama kibanzi kidogo
kilichomo kwenye jicho la ndugu yako na wala Mwanafunzi Wa Kweli
huoni boriti iliyoko kwenye jicho lako? 4Au 21“Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’

unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni bali ni
kibanzi kwenye jicho lako wakati kuna boriti yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye
kwenye jicho lako mwenyewe ?’ 5Ewe mnafiki, mbinguni. 22Wengi wataniambia siku ile,
toa kwanza boriti kwenye jicho lako mwenyewe, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako
nawe ndipo utakapoona wazi ili kuondoa kibanzi na kwa jina lako kutoa pepo na kufanya miujiza
kilichoko kwenye jicho la ndugu yako. mingi? 23Ndipo nitakapowaambia wazi,
6‘‘Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu, wala `’Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi
msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya watenda maovu!’
hivyo, watazikanyaga kanyaga na kisha
watawageukia na kuwararua vipande vipande. ” Msikiaji Na Mtendaji
24‘‘Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya

Omba, Tafuta, Bisha maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu


7“Ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mwenye busara aliyejenga nyumba yake
mtapata, bisheni nanyi mtafunguliwa mlango. kwenye mwamba. 25Mvua ikanyesha, mafuriko
8Kwa maana kila aombaye hupewa, naye yakaja na upepo ukavuma ukaipiga hiyo
atafutaye huona, naye abishaye hufunguliwa nyumba, lakini haikuanguka kwa sababu msingi
mlango. wake ulikuwa kwenye mwamba. 26Naye kila
9‘‘Au ni nani miongoni mwenu ambaye anayesikia haya maneno yangu wala
mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe? asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga
10Au mwanawe akimwomba samaki atampa nyumba yake kwenye mchanga. 27Mvua
nyoka? 11Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo
jinsi ya kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo
sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu ikaanguka kwa kishindo kikubwa.’’
vizuri wale wamwombao ? 12Kwa hiyo cho chote
ambacho mngetaka mtendewe na watu, ninyi 28Yesualipomaliza kusema maneno haya,
nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii makutano ya watu wakashangazwa sana na
ndiyo Torati na Manabii.’’ mafundisho yake, 29kwa sababu alifundisha
kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama
Njia Nyembamba Na Njia Pana walimu wao wa sheria.
13‘‘Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba,

kwa maana lango ni pana na njia ni pana Yesu Amtakasa Mwenye Ukoma
ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa
kupitia lango hilo. 14Lakini mlango ni 8 Yesu aliposhuka kutoka mlimani,
makutano makubwa ya watu yakamfuata.
mwembamba na njia ni finyo ielekayo kwenye 2Mtu mmoja mwenye ukoma akaja na kupiga

uzima, nao ni wachache tu waionao.’’ magoti mbele yake akasema, “Bwana, kama
ukitaka, unaweza kunitakasa.’’
Mti na Tunda lake 3Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa,
15“Jihadharini na manabii wa uongo, akamwambia, “Nataka, takasika!’’ Mara yule
wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya mtu akatakasika ukoma wake. 4Kisha Yesu
kondoo, lakini ndani wao ni mbwa mwitu akamwambia, “Hakikisha humwambii mtu ye
wakali.16Mtawatambua kwa matunda yao. Je, yote. Lakini nenda, ukajionyeshe kwa kuhani na
watu huchuma zabibu kwenye miiba au tini utoe sadaka aliyoamuru Mose, iwe ushuhuda
kwenye michongoma? 17Vivyo hivyo, mti kwao kwamba umepona.’’
mwema huzaa matunda mazuri na mti mbaya
huzaa matunda mabaya. 18Mti mwema hauwezi Yesu Amponya Mtumishi Wa Jemadari
kuzaa matunda mabaya wala mti mbaya 5Yesu alipoingia Kapernaumu, jemadari

hauwezi kuzaa matunda mazuri. 19Kila mti mmoja alimjia, kumwomba msaada, 6akisema,
usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa “Bwana, mtumishi wangu amelala nyumbani
motoni. 20Hivyo, kwa matunda yao, amepooza, tena ana maumivu makali ya
mtawatambua.’’ kutisha.’’

8
MATHAYO
7Yesu akamwambia, “Nitakuja na 22Lakini
Yesu akamwambia, “Nifuate, nawe
kumponya.’’ waache wafu wazike wafu wao.’’
8Lakini yule jemadari akamwambia, “Bwana,

mimi sistahili Wewe uingie chini ya dari yangu. Yesu Atuliza Dhoruba
lakini sema neno tu, naye mtumishi wangu 23Naye alipoingia kwenye chombo,
atapona. 9Kwa kuwa mimi nami niko chini ya wanafunzi wake wakamfuata. 24Ghafula
mamlaka, nikiwa na askari chini yangu. kukainuka dhoruba kali baharini hata chombo
Nikimwambia huyu ‘Nenda,’ naye huenda, na kikaanza kufunikwa na mawimbi, lakini Yesu
mwingine nikimwambia, ‘Njoo’, huja. Nami alikuwa amelala usingizi. 25Wanafunzi wake
nikimwambia mtumishi wangu, ‘Fanya hivi,’ wakamwendea na kumwamsha, wakisema,
hufanya.’’ “Bwana, tuokoe! Tunazama!’’
10Yesu aliposikia maneno haya, 26Naye Yesu akawaambia, ‘Kwa nini

akashangaa, akawaambia wale waliomfuata, mnaogopa, enyi wa imani haba?’ Kisha


“Amin, amin nawaambia, hata katika Israeli akaondoka na kukemea dhoroba na mawimbi,
sijaona imani kubwa namna hii. 11Ninawaambia nako kukawa shwari kuu.
kwamba wengi watatoka mashariki na 27Wale watu wakashangaa, wakisema, “Ni

magharibi nao wataketi karamuni pamoja na mtu wa namna gani huyu? Hata upepo na
Abrahamu, Isaki na Yakobo katika Ufalme wa mawimbi vinamtii!.
Mbinguni. 12Lakini warithi wa ufalme watatupwa
katika giza la nje, ambako kutakuwa na kulia na Wawili Wenye Pepo Waponywa
kusaga meno.’’ 28Walipofika ng'ambo katika nchi ya
13Kisha Yesu akamwambia yule jemadari, Wagerasi, watu wawili waliopagawa na pepo
“Nenda na iwe kwako sawasawa na imani wakitoka makaburini walikutana naye. Watu
yako.” Naye yule mtumishi akapona saa ile ile. hawa walikuwa wakali mno kiasi kwamba
hakuna mtu aliyeweza kupita njia ile.
Yesu Aponya Wengi 29Wakapiga kelele, “Una nini nasi, Mwana wa
14Yesu alipoingia nyumbani kwa Petro, Mungu? Umekuja hapa kututesa kabla ya
alimkuta mama mkwe wake Petro amelala wakati ulioamuriwa?’’
kitandani akiwa ana homa. 15Akamgusa mkono 30Mbali kidogo kutoka pale walipokuwa,

wake na homa ikamtoka, naye akainuka na kulikuwa na kundi kubwa la nguruwe wakilisha.
kuanza kumhudumia. 16Jioni ile, wakamletea 31Wale pepo wakamsihi Yesu, “Ukitutoa humu,

watu wengi waliopagawa na pepo, naye turuhusu tuende kwenye lile kundi la nguruwe.’’
akawatoa wale pepo kwa neno lake, na 32Akawaambia, “Nendeni!’’ Hivyo wakatoka

kuponya wagonjwa wote. 17Haya yalifanyika ili na kuwaingia wale nguruwe, nalo kundi lote
litimie lile lililonenwa kwa kinywa cha nabii Isaya likatelemka mbio gengeni, likaingia bahari na
kwamba: kufa ndani ya maji. 33Wale waliokuwa
wakiwachunga hao nguruwe wakakimbia
“Mwenyewe alitwaa udhaifu wetu wakaingia mjini, wakaeleza yote kuhusu yale
na alichukua magonjwa yetu.’’ yaliyowatokea wale waliokuwa wamepagawa na
pepo. 34Kisha watu wote wa mji huo wakatoka
Gharama ya Kumfuata Yesu kwenda kukutana na Yesu. Nao walipomwona
18Yesu alipoona makutano mengi wakamsihi aondoke kwenye nchi yao.
wamemzunguka, aliwaamuru wanafunzi wake
wavuke mpaka ng'ambo. 19Kisha mwalimu Yesu Amponya Mtu Aliyepooza
mmoja wa sheria akamjia Yesu na kumwambia,
“Mwalimu, mimi nitakufuata po pote uendako.’’
20Naye Yesu akamwambia, “Mbweha wana
9 Yesu akaingia kwenye chombo, akavuka
na kufika katika mji wa kwao. 2Wakati huo
huo wakamletea mtu aliyepooza, akiwa
mashimo, nao ndege wa angani wana viota amelazwa kwenye kitanda. Yesu alipoona imani
vyao, lakini Mwana wa Adamu hana mahali pa yao, alimwambia yule mtu aliyepooza,
kulaza kichwa chake.’’ ‘‘Mwanangu, jipe moyo mkuu, dhambi zako
21Mwanafunzi mwingine akamwambia, zimesamehewa.’’
“Bwana, niruhusu kwanza nikamzike baba 3Kwa ajili ya jambo hili, baadhi ya walimu

yangu.”

9
MATHAYO
wa sheria wakasema mioyoni mwao, ‘‘Huyu mtu Navyo viriba vitaharibika, lakini divai mpya
anakufuru!’’ huwekwa kwenye viriba vipya na hivyo divai na
4Lakini Yesu akiyafahamu mawazo yao, viriba huwa salama.’’
akawaambia, ‘‘Kwa nini mnawaza maovu
mioyoni mwenu? 5Kwa kuwa ni lipi lililo rahisi: Msichana Afufuliwa Na Mwanamke Aponywa
kusema, ‘Dhambi zako zimesamehewa,’ au 18Wakati Yesu akiwa anawaambia mambo

kusema, ‘Simama, utembee?’ 6Lakini, ili mpate haya, mara akaingia kiongozi wa sinagogi
kujua kwamba Mwana wa Adamu anayo akapiga magoti mbele yake, akimwambia, ‘‘Binti
mamlaka duniani kusamehe dhambi,'' Ndipo yangu amekufa sasa hivi, lakini uje uweke
akamwambia yule aliyepooza, “Simama, chukua mkono wako juu yake naye atakuwa hai.’’
kitanda chako na uende nyumbani kwako.’’ 19Yesu akaondoka akafuatana naye, wanafunzi
7Yule mtu akasimama, akaenda nyumbani wake pia wakaandamana naye.
kwake. 8Makutano walipoyaona haya, wakajawa 20Wakati huo huo mwanamke mmoja

na hofu ya Mungu, wakamtukuza Mungu ambaye alikuwa na ugonjwa wa kutokwa damu


ambaye alikuwa ametoa mamlaka kama hii kwa kwa muda wa miaka kumi na miwili, akaja
wanadamu. nyuma ya Yesu akagusa upindo wa vazi lake,
21kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama

Kuitwa Kwa Mathayo nikigusa tu vazi lake, nitaponywa.’’


9Yesu alipokuwa akienda kutoka huko, 22Yesu akageuka, naye alipomwona
alimwona mtu mmoja jina lake Mathayo akiwa akamwambia, “Binti, jipe moyo mkuu, imani
ameketi forodhani mahali pa kutozea ushuru. yako imekuponya.’’ Naye yule mwanamke
Yesu akamwambia, “Nifuate.’’ Mathayo akapona kuanzia saa ile ile.
akaondoka, akamfuata.
10Wakati Yesu alipokuwa ameketi chakulani Yesu Amfufua Binti Wa Kiongozi Wa
ndani ya nyumba, watoza ushuru wengi na Sinagogi.
wenye dhambi wakaja kula pamoja naye na 23Yesu alipofika nyumbani kwa yule
wanafunzi wake.11Mafarisayo walipoona mambo kiongozi wa sinagogi na kuwaona waombolezaji
haya, wakawauliza wanafunzi Wake, “Kwa nini wakipiga filimbi za maombolezo na watu wengi
Mwalimu wenu anakula na watoza ushuru na wakipiga kelele, 24akawaambia, “Ondokeni! Kwa
‘wenye dhambi’?’’ maana binti huyu hakufa, bali amelala.’’
12Lakini Yesu aliposikia hayo, akawaambia, Wakamcheka kwa dhihaka. 25Lakini watu
“Watu wenye afya hawahitaji tabibu, lakini wale walipokwisha kutolewa nje, akaingia mle ndani
walio wagonjwa ndio wanaohitaji tabibu. na kumshika yule binti mkono, naye akaamka.
13Nendeni mkajifunze maana ya maneno haya, 26Habari hizi zikaenea katika maeneo yale yote.

‘Nataka rehema, wala si dhabihu.’ Kwa maana


sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.’’ Yesu Awaponya Vipofu
27Yesu alipokuwa akiondoka mahali pale,

Yesu Aulizwa Kuhusu Kufunga vipofu wawili wakamfuata, wakipiga kelele kwa
14Wanafunzi wa Yohana Mbatizaji wakaja nguvu na kusema, “Mwana wa Daudi,
na kumwuliza Yesu, “Imekuwaje kwamba sisi na tuhurumie!’’
Mafarisayo tunafunga, lakini wanafunzi wako 28Alipoingia mle nyumbani wale vipofu

hawafungi?’’ wakamjia. Akawauliza, “Mnaamini kwamba


15Yesu akawajibu, “Je, wageni wa bwana – ninaweza kufanya jambo hili?”
arusi waweza kuomboleza wakati angali pamoja Wakamjibu, “Ndio Bwana.’’
nao? Wakati utafika ambapo bwana arusi 29Ndipo Yesu akagusa macho yao na

ataondolewa kwao, hapo ndipo watakapofunga. kusema, “Iwe kwenu sawasawa na


16“Hakuna mtu anayeshonea kiraka kipya mnavyoamini.’’ 30Macho yao yakafunguka. Yesu
kwenye nguo kuukuu, kwa maana kile kiraka akawaonya vikali, akisema, “Angalieni mtu ye
kitachanika kutoka kwenye hiyo nguo na yote asijue kuhusu jambo hili.’’ 31Lakini wao
kuchanika kwake kutakuwa kubaya zaidi ya wakaenda na kueneza habari zake katika eneo
hapo mwanzo. 17Wala watu hawaweki divai lile lote.
mpya kwenye viriba vikuukuu. Kama wakifanya
hivyo, viriba vitapasuka na divai itamwagika. Yesu Amponya Mtu Bubu

10
MATHAYO
32Walipokuwa wanatoka, mtu mmoja mtakachoingia, tafuteni humo mtu anayestahili,
aliyekuwa amepagawa na pepo na ambaye nanyi kaeni kwake mpaka mtakapoondoka.
hakuweza kuongea aliletwa kwa Yesu. 33Yule 12Mkiingia kwenye nyumba, itakieni amani.

pepo alipotolewa, yule mtu aliyekuwa bubu 13Kama nyumba hiyo inastahili, amani yenu na

akaongea. Ule umati wa watu ukastaajabu na iwe juu yake, la sivyo, amani yenu na iwarudie
kusema, “Jambo kama hili kamwe halijapata ninyi. 14Kama mtu ye yote hatawakaribisha
kuonekana katika Israeli.” ninyi, wala kusikiliza maneno yenu, kungu’uteni
34Lakini Mafarisayo wakasema, “Huyo mavumbi kutoka kwenye miguu yenu
anatoa pepo kwa uwezo wa mkuu wa pepo.’’ mtakapokuwa mnatoka kwenye nyumba hiyo au
mji huo. 15Amin, amin nawaambia, itavumilika
Watenda Kazi Ni Wachache zaidi miji ya Sodoma na Gomora katika hukumu
35Yesu akazunguka katika miji yote na vijiji kuliko mji huo.
vyote, akifundisha katika masinagogi yao ,
akihubiri Habari Njema za Ufalme na kuponya Mateso Yanayokuja
kila ugonjwa na kila aina ya maradhi miongoni 16“Tazama, ninawatuma kama kondoo

mwa watu. 36Alipoona makutano aliwahurumia katikati ya mbwa mwitu. Kwa hiyo mwe werevu
kwa sababu walikuwa wanasumbuka na bila kama nyoka na wapole kama hua.
msaada, kama kondoo wasio na mchungaji. 17“Jihadharini na wanadamu, kwa maana
37Ndipo akawaambia wanafunzi wake, “Mavuno watawapeleka katika mabaraza yao na
ni mengi lakini watenda kazi ni wachache, kuwapiga kwenye masinagogi yao, 18nanyi
38Kwa hiyo mwombeni Bwana wa mavuno, ili mtaburutwa mbele ya watawala na
apeleke watenda kazi katika shamba lake la wafalme kwa ajili Yangu, ili kuwa ushuhuda
mavuno.’’ kwao na mbele ya watu Mataifa. 19Lakini
watakapowapeleka humo, msisumbuke
Yesu Awatuma Wale Kumi Na Wawili kufikirifikiri mtakalosema, kwa maana mtapewa
10 Ndipo Yesu akawaita wanafunzi wake
kumi na wawili, akawapa mamlaka juu
la kusema wakati huo. 20Kwa sababu si ninyi
mtakaokuwa mkinena, bali ni Roho wa Baba
ya pepo wachafu kuwatoa na kuponya kila yenu atakayekuwa akinena kupitia kwenu.
ugonjwa na maradhi ya kila aina. 21“Ndugu atamsaliti ndugu yake ili auawe na
2Haya ndiyo majina ya hao wanafunzi kumi baba atamsaliti mtoto wake, watoto wataasi
na wawili: 3wa kwanza, Simon, aitwaye Petro na dhidi ya wazazi wao na kuwafanya wauawe.
Andrea nduguye, Yakobo mwana wa Zebedayo 22Nanyi mtachukiwa na watu wote kwa ajili ya

na Yohana nduguye, Filipo na Bartholomayo, Jina langu. Lakini yeye atakayevumilia hadi
Tomaso na Mathayo mtoza ushuru, Yakobo mwisho ataokoka. 23Wakiwatesa katika mji
mwana wa Alfayo na Thadayo, 4Simoni mmoja, kimbilieni mji mwingine.Amin, amin
Mkananayo na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu. nawaambia, hamtamaliza miji yote ya Israeli
kabla Mwana wa Adamu hajaja.
Kutumwa Kwa Wale Kumi Na Wawili 24“Mwanafunzi hawezi kumzidi mwalimu
5Hawa kumi na wawili, Yesu aliwatuma wake wala mtumishi hamzidi bwana wake.
akawaagiza, “Msiende miongoni mwa watu 25Yatosha mwanafunzi kuwa kama mwalimu

Mataifa wala msiingie mji wo wote wa wake na mtumishi kuwa kama bwana wake.
Wasamaria. 6Lakini afadhali mshike njia Ikiwa mkuu wa nyumba ameitwa Beelzebuli a , je,
kuwaendea kondoo wa nyumba ya Israeli si zaidi sana wale wa nyumbani mwake
waliopotea. 7Wakati mnapokwenda, hubirini mwenyewe!
mkisema, ‘Ufalme wa Mbinguni umekaribia.’
8Ponyeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni Anayestahili Kuogopwa
wenye ukoma, toeni pepo wachafu. Mmepata 26“Kwa hiyo msiwaogope hao, kwa maana

bure, toeni bure. 9Msichukue dhahabu, wala hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa,
fedha, wala shaba kwenye vifuko vyenu. wala hakuna siri ambayo haitajulikana.
10Msichukue mkoba wa safari, wala kanzu mbili, 27Ninalowaambia gizani, ninyi lisemeni mchana

wala jozi ya pili ya viatu, wala fimbo, kwa maana peupe na lile mnalosikia likinong'onwa,
mtenda kazi anastahili posho yake.
11“Mji wo wote au kijiji cho chote
a25 ‘‘Beelizebubu’’ au kwa Kiyunani Beezebub au Beelzebub
yaani, Beelzebuli maana yake mkuu wa pepo
11
MATHAYO
masikioni mwenu, lihubirini kwenye paa la
nyumba. 28Msiwaogope wale wauao mwili lakini 11 Baada ya Yesu kumaliza kutoa maagizo
kwa wale wanafunzi wake kumi na
hawawezi kuua roho afadhali mwogopeni yeye wawili, aliondoka hapo akaenda kufundisha na
awezaye kuiangamiza roho na mwili katika kuhubiri katika miji yao.
jehanam b . 29Je, shomoro wawili hawauzwi kwa 2Yohana Mbatizaji aliposikia akiwa gerezani

senti mbili tu? Lakini hakuna hata mmoja wao mambo ambayo Kristo a alikuwa akiyafanya,
atakayeanguka pasipo Baba yenu kujua.. 30Hata aliwatuma wanafunzi wake 3ili wakamwulize,
nywele za vichwa vyenu zote zimehesabiwa. “Wewe ndiye yule aliyekuwa aje, au tumngojee
31Hivyo msiogope, kwa maana ninyi ni wa mwingine?’’
thamani kubwa zaidi kuliko shomoro wengi. 4Yesu akajibu, “Rudini mkamwarifu Yohana
32“Kila mtu atakayenikiri mbele ya watu, yale mnayosikia na kuyaona: 5Vipofu wanapata
mimi nami nitamkiri yeye mbele za Baba yangu kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma
aliye mbinguni. 33Lakini ye yote atakayenikana wanatakaswa, viziwi wanasikia, wafu
mimi mbele ya watu, mimi nami nitamkana wanafufuliwa na maskini wanahubiriwa habari
mbele ya Baba yangu aliye mbinguni.’’ njema. 6Ana heri mtu yule asiyechukizwa kwa
ajili yangu”
Sikuleta Amani, Bali Upanga 7Wale wanafunzi wa Yohana walipokuwa
34“Msidhani kwamba nimekuja kuleta amani wanaondoka, Yesu akaanza kusema na
duniani. Sikuja kuleta amani bali upanga. makutano kuhusu Yohana Mbatizaji.
35Kwa maana nimekuja kumfitini Akawauliza, “Mlipokwenda kule nyikani,
mtu na babaye, mlikwenda kuona nini? Unyasi ukiyumbishwa na
binti na mamaye, upepo? 8Kama sivyo, mlitoka kwenda kuona nini
mkwe na mama mkwe wake. basi? Mtu aliyevaa mavazi mazuri.? Hasha,
36Nao adui za mtu watakuwa ni wale watu wa wale wanaovaa nguo nzuri wako katika
nyumbani kwake. majumba ya wafalme. 9Basi mlitoka kwenda
kuona nini? Je, ni kumwona nabii? Naam,
37‘‘Yeyote ampendaye baba yake au mama nawaambia, yeye ni zaidi ya nabii. 10Huyo ndiye
yake kuliko anavyonipenda mimi, hastahili kuwa ambaye habari zake zimeandikwa:
wangu. Ye yote ampendaye mwanawe au binti
yake kuliko anavyonipenda Mimi, hastahili kuwa ‘‘ ‘Tazama namtuma mjumbe mbele yako,
wangu. 38Tena ye yote asiyeuchukua msalaba atakayetengeneza njia mbele yako.’
wake na kunifuata, hastahili kuwa Wangu.
39Ayang’ang’aniaye maisha yake atayapoteza, 11Amin, nawaambia, miongoni mwa watu
lakini yeye atakayeyatoa maisha yake kwa ajili waliozaliwa na wanawake, hajatokea mtu aliye
yangu atayaona.” mkuu zaidi ya Yohana Mbatizaji, lakini aliye
mdogo kabisa katika Ufalme wa Mbinguni, ni
Watakaopokea Thawabu mkuu kuliko Yohana. 12Tangu siku za Yohana
40“Mtu ye yote atakayewapokea ninyi Mbatizaji hadi sasa, Ufalme wa Mungu
atakuwa amenipokea mimi na ye yote hupatikana kwa nguvu, nao wenye nguvu
atakayenipokea mimi atakuwa amempokea wauteka. 13Kwa maana manabii wote na Torati
Yeye aliyenituma. 41Mtu ye yote anayempokea vilitabiri mpaka wakati wa Yohana. 14Kama mko
nabii kwa kuwa ni nabii, atapokea thawabu ya tayari kukubali hilo, yeye Yohana ndiye yule
nabii na mtu anayempokea mwenye haki kwa Eliya ambaye manabii walikuwa wamesema
kuwa ni mwenye haki, atapokea thawabu ya angekuja. 15Yeye aliye na sikio na
mwenye haki. 42Kama ye yote akimpa hata asikie.16“Lakini kizazi hiki nikifananishe na nini?’’
kikombe cha maji mmoja wa hawa wadogo kwa Kinafanana na watoto waliokaa sokoni
kuwa ni mwanafunzi wangu, amin, wakiwaita wenzao na kuwaambia,
ninawaambia, hataikosa thawabu yake.’’
17 “ ‘Tuliwapigia filimbi,
Yesu na Yohana Mbatizaji lakini hamkucheza,
tuliwaimbia nyimbo za msiba
b28 Jehanum au Kiyunani’’ ‘‘Gehena’’ maana yake kuzimu,
yaani, motoni a2 Kristo yaani Masiya maana yake Mpakwa (Aliyetiwa) Mafuta.

12
MATHAYO
lakini hamkuomboleza.’ Bwana Wa Sabato
Wakati huo Yesu alipitia kwenye
18Kwa maana Yohana Mbatizaji alikuja hali wala 12 mashamba ya ngano siku ya sabato.
hanywi, nao wanasema, ‘Yeye ana pepo.’ Wanafunzi wake walikuwa na njaa, wakaanza
19Mwana wa Adamu alikuja akila na kunywa, kuvunja masuke ya ngano na kuyala. 2Lakini
nao wanasema, ‘Tazama, mlafi na mlevi, rafiki Mafarisayo walipoona jambo hili,
wa watoza ushuru na wenye dhambi!’ Lakini wakamwambia, “Tazama! Wanafunzi wako
hekima huthibitishwa kwa haki ya matendo wanafanya jambo lisilo halali siku ya Sabato.’’
yake.’’ 3Yesu akawajibu, “Je, hamjasoma
alichofanya Daudi na wenzake walipokuwa na
Ole Wa Miji Isiyotubu njaa? 4Aliingia katika nyumba ya Mungu akala
20Ndipo Yesu akaanza kuilaumu miji mikate iliyowekwa wakfu, yeye na wenzake,
ambamo alifanya miujiza yake mingi kuliko jambo ambalo halikuwa halali kwao kufanya,
kwingine, kwa maana watu wake hawakutubu. isipokuwa makuhani peke yao. 5Au hamjasoma
21 “Ole wako, Korazini! Ole wako Bethsaida! katika Torati kwamba siku ya Sabato makuhani
Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, huvunja sheria ya Sabato Hekaluni lakini
ingelifanyika Tiro na Sidoni, miji hiyo ingekuwa hawahesabiwi kuwa na hatia? 6Nawaambia
imetubu tangu zamani kwa kuvaa magunia na wazi kwamba, Yeye aliye mkuu kuliko Hekalu
kujipaka majivu. 22Lakini nawaambia, itavumilika yupo hapa. 7Kama mngelikuwa mmejua maana
zaidi kwa Tiro na Sidoni katika siku ya hukumu, ya maneno haya, ‘Ninataka rehema, wala si
kuliko kwenu, 23Nawe Kapernaumu,je, dhabihu,’ msingeliwalaumu watu wasio na hatia,
utainuliwa hadi mbinguni? La hasha, 8kwa maana Mwana wa Adamu ndiye Bwana

utashushwa pande za chini sana b . Miujiza wa Sabato.’’


iliyofanyika kwako ingefanyika huko Sodoma,
mji huo ungalikuwapo hadi leo. 24Lakini Yesu Anamponya Mtu Aliyepooza Mkono
nakuambia kwamba, itavumilika zaidi kwa 9Yesu akaondoka mahali hapo, akaingia

Sodoma katika siku ile ya hukumu kuliko wewe. katika sinagogi lao, 10huko alikuwepo mtu
aliyepooza mkono. Wakitafuta sababu ya
Hakuna Amjuaye Baba Ila Mwana kumshtaki Yesu, wakamwuliza, “Je, ni halali
25Wakati huo Yesu alisema, “Ninakuhimidi kuponya siku ya
Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa Sabato?’’
umewaficha mambo haya wenye hekima na 11Yesu akawaambia, “Ni nani miongoni

wenye elimu, nawe ukawafunulia watoto mwenu, mwenye kondoo wake ambaye huyo
wachanga. 26Naam, Baba, kwa kuwa hivyo kondoo akitumbukia shimoni siku ya Sabato
ndivyo ilivyokupendeza. hatamtoa? 12Mtu ana thamani kubwa kiasi
27“Nimekabidhiwa vitu vyote na Baba yangu: kuliko kondoo. Kwa hiyo ni halali kutenda mema
hakuna mtu amjuaye Mwana ila Baba, wala siku ya Sabato.’’
hakuna amjuaye Baba ila Mwana na ye yote 13Ndipo akamwambia yule mtu, ‘‘Nyoosha

ambaye Mwana anapenda kumdhihirisha Baba mkono wako.’’ Akaunyoosha, nao ukaponywa
kwake.’’ ukawa mzima kama ule mwingine. 14Lakini
Mafarisayo wakatoka nje wakafanya shauri
Yesu Awaita Waliolemewa Na Mizigo baya juu yake jinsi watakavyoweza kumwua
28“Njooni kwangu, ninyi nyote mnaotaabika Yesu.
na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.
29Jifungeni nira yangu, mjifunze kutoka kwangu, Mtumishi Aliyechaguliwa Na Mungu
kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa 15Lakini Yesu alipoyatambua mawazo yao,

moyo, nanyi mtapata raha nafsini mwenu. 30Kwa akaondoka mahali hapo. Watu wengi
maana nira yangu ni laini na mzigo wangu ni wakamfuata, naye akawaponya wote,
mwepesi.’’ 16akiwakataza wasiseme yeye ni nani. 17Hii

ilikuwa ili litimie lile neno lililonenwa kwa kinywa


cha nabii Isaya, kusema :
b23 Pande za chini sana hapa ina maana ya neno la Kiyunani
Hades au kwa Kiyahudi Sheol, yaani, Kuzimu.

13
MATHAYO
18‘‘Tazama mtumishi wangu niliyemchagua, Mwana wa Adamu atasamehewa, lakini ye yote
mpendwa wangu, ninayependezwa anenaye neno dhidi ya Roho Mtakatifu
naye. hatasamehewa, iwe katika ulimwengu huu au
Nitaweka Roho yangu juu yake, katika ulimwengu ujao.’
naye atatangaza haki kwa mataifa.
19Hatagombana wala hatapiga kelele, Mti Na Matunda Yake
wala hakuna atakayesikia sauti yake njiani. 33‘‘Ufanye mti kuwa mzuri nayo matunda
20Mwanzi uliopondeka hatauvunja, yake yatakuwa mazuri, au ufanye mti kuwa
utambi unaofuka moshi hatauzima, mbaya na matunda yake yatakuwa mabaya,
mpaka atakapoifanya haki ishinde. kwa maana mti hutambulikana kwa matunda
21“Katika jina lake mataifa wataweka tumaini yake. 34Enyi uzao wa nyoka! Mnawezaje
lao.’’ kunena mambo mema, wakati ninyi ni waovu?
Kwa maana kinywa cha mtu huyanena yale
Yesu Na Beelzebuli yaliyoujaza moyo wake. 35Mtu mwema hutoa
22Kisha wakamletea mtu aliyekuwa yaliyo mema kutoka katika hazina ya mambo
amepagawa na pepo, naye ni kipofu na bubu, mema yaliyohifadhiwa ndani yake, naye mtu
Yesu akamponya, hata akaweza kusema na mwovu hutoa yaliyo maovu kutoka katika hazina
kuona. 23Watu wote wakashangaa na kusema, ya mambo maovu yaliyohifadhiwa ndani yake.
“Je, yawezekana huyu ndiye Mwana wa 36Lakini nawaambia, katika siku ya hukumu

Daudi?’’ watu watatoa hesabu kuhusu kila neno lisilo


24Lakini Mafarisayo waliposikia jambo hili maana walilonena. 37Kwa maana kwa maneno
wakasema, “Mtu huyu anatoa pepo wachafu yako utahesabiwa haki na kwa maneno yako
kwa uwezo wa Beelzebuli a , mkuu wa pepo utahukumiwa.”
wachafu.’’
25Yesu alijua walichokuwa wakiwaza, Ishara Ya Yona
akawaambia, ‘‘Kila ufalme ukigawanyika dhidi 38Kisha baadhi ya Mafarisayo na walimu wa

yake wenyewe huangamia. Hali kadhalika kila sheria wakamwambia, “Mwalimu, tunataka
mji au watu wa nyumba moja iliyogawanyika kuona ishara kutoka kwako.’’
dhidi yake yenyewe haiwezi kusimama. 26Kama 39Lakini Yeye akawajibu, ‘‘Kizazi kiovu na

Shetani akimtoa Shetani, atakuwa cha uzinzi kinaomba ishara! Lakini hakitapewa
amegawanyika yeye mwenyewe. Basi ufalme ishara yo yote isipokuwa ile ishara ya nabii
wake utawezaje kusimama? 27Nami kama natoa Yona. 40Kwa maana kama vile Yona alivyokuwa
pepo wachafu kwa nguvu za Beelzebuli b , watu ndani ya tumbo la nyangumi c kwa muda wa
wenu je, wao hutoa pepo wachafu kwa uwezo siku tatu mchana na usiku, vivyo hivyo Mwana
wa nani? Hivyo basi, wao ndio wa Adamu atakuwa katika moyo wa nchi siku
watakaowahukumu. 28Lakini kama Mimi ninatoa tatu, mchana na usiku. 41Siku ya hukumu watu
pepo wachafu kwa Roho wa Mungu, basi wa Ninawi watasimama pamoja na kizazi hiki na
Ufalme wa Mungu umekuja juu yenu. kukihukumu, kwa maana wao walitubu katika
29“Au tena, mtu awezaje kuingia katika kuhubiri kwa Yona na tazama hapa yupo yeye
nyumba ya mtu mwenye nguvu na kuteka nyara aliye mkuu kuliko Yona. 42Malkia wa Kusini
mali zake asipomfunga kwanza yule mwenye atasimama wakati wa hukumu na kukihukumu
nguvu? Akiisha mfunga, ndipo hakika anaweza kizazi hiki, kwa kuwa yeye alikuja kutoka miisho
kuteka nyara mali zake. ya dunia ili kuisikiliza hekima ya Solomoni na
30“Mtu asiyekuwa pamoja nami yu kinyume hapa yupo aliye mkuu kuliko Solomoni.’’
nami na mtu ambaye hakusanyi pamoja nami,
hutawanya. 31Kwa hiyo nawaambia, kila dhambi Mafundisho Kuhusu Pepo Mchafu
na kufuru watu watasamehewa, lakini mtu 43“Pepo mchafu amtokapo mtu, hutanga-

atakayemkufuru Roho Mtakatifu hatasamehewa. tanga katika sehemu zisizo na maji akitafuta
32“Mtu ye yote atakayesema neno dhidi ya mahali pa kupumzika, lakini hapati. 44Ndipo
husema, ‘Nitarudi kwenye ile nyumba yangu
nilikotoka,’ Naye arudipo huikuta ile nyumba
a24 Beelizebuli au Beelizebubu maana yake: mkuu wa pepo
wachafu.
ikiwa tupu, imefagiliwa na kupangwa vizuri.
b27 Beelzebul au Beelizebubu maana yake mkuu wa pepo
wachafu. c40 Nyangumi ni samaki mkubwa sana
14
MATHAYO
45Kisha huenda na kuwaleta pepo wachafu atanyang'anywa. 13Hii ndiyo sababu nasema
wengine saba, wabaya zaidi kuliko yeye, nao nao kwa mifano:
huingia na kuishi humo. Nayo hali ya mwisho ya
mtu yule huwa mbaya zaidi kuliko ile ya kwanza. ‘‘Ingawa wanatazama, hawaoni,
Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki cha uovu.’’ wanasikiliza, lakini hawasikii, wala
hawaelewi.
Mama Na Ndugu Zake Yesu
46Wakati alipokuwa akali anazungumza na 14Kwao unatimia ule unabii wa Isaya aliposema:
makutano, mama Yake na ndugu Zake ‘‘ ‘Hakika mtasikiliza lakini hamtaelewa,
walisimama nje wakitaka kuongea naye. 47Ndipo na pia mtatazama lakini hamtaona.
mtu mmoja akamwambia, “Tazama mama Yako 15Kwa maana mioyo ya watu hawa imekuwa

na ndugu Zako wamesimama nje, wanataka mizito,


kuongea na Wewe.’’ hawasikii kwa masikio yao, na wamefumba
48Lakini Yeye akamjibu na kumwambia yule macho yao.
mtu, “Mama yangu ni nani, nao ndugu zangu ni Wasije wakaona kwa macho yao,
nani?’’ 49Akiwanyoshea mkono wanafunzi wakasikia kwa masikio yao,
Wake, akasema, “Hawa hapa ndio mama wakaelewa kwa mioyo yao,
Yangu nao ndugu Zangu! 50Kwa maana ye yote wakageuka, nami nikawaponya.’
afanyaye mapenzi ya Baba Yangu wa mbinguni,
ndiye ndugu Yangu, dada Yangu na mama 16“Lakiniheri macho yenu, kwa sababu yanaona
yangu.’’ na heri masikio yenu kwa sababu yanasikia.
17Amin, nawaambia, manabii wengi na wenye

Mfano Wa Mpanzi haki walitamani kuona yale mnayoyaona, nao

13 Siku iyo hiyo Yesu akatoka nje ya


nyumba akaketi kando ya bahari. 2Umati
hawakuyaona na kusikia yale mnayosikia lakini
hawakuyasikia.’’
mkubwa mno wa watu ukakusanyika
kumzunguka hata ikabidi aingie katika chombo Maelezo Ya Mfano Wa Mbegu
na kuketi humo, nao watu wote wakawa 18“Sikilizeni basi maana ya ule mfano wa

wamesimama ukingoni mwa bahari. 3Ndipo mpanzi: 19Mtu ye yote anaposikia neno la
akawaambia mambo mengi kwa mifano, Ufalme, naye asilielewe, yule mwovu huja na
akisema: “Mpanzi alitoka kwenda kupanda kunyakua kile kilichopandwa moyoni mwake, hii
mbegu zake. 4Alipokuwa akipanda, baadhi ndiyo ile mbegu iliyopandwa kando ya njia.
zikaanguka kando ya njia, ndege wakaja na 20Ile mbegu iliyopandwa kwenye sehemu yenye

kuzila. 5Nyingine zikaanguka sehemu yenye mawe ni mtu yule ambaye hulisikia neno na
mawe, ambapo hapana udongo mwingi. Zikaota mara hulipokea kwa furaha. 21Lakini kwa kuwa
haraka kwa sababu udongo ulikuwa hauna kina. hana mizizi yenye kina ndani yake, lile neno
6Lakini jua lilipozidi, mimea hiyo ilinyauka na hukaa kwa muda mfupi. Inapotokea dhiki au
kukauka kwa sababu mizizi yake haikuwa na mateso kwa ajili ya hilo neno, yeye mara
kina. 7Mbegu nyingine zilianguka katikati ya huchukizwa. 22Ile mbegu iliyopandwa katika
miiba, miiba hiyo ikakua ikazisonga. 8Mbegu miiba ni yule mtu alisikiaye neno, lakini
nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri masumbufu ya dunia na vishawishi vya mali
ambapo zilitoa mazao, nyingine mara mia moja, hulisonga lile neno na kulifanya lisizae matunda.
nyingine mara sitini na nyingine mara thelathini. 23Lakini ile mbegu iliyopandwa kwenye udongo
9Yeye mwenye masikio ya kusikia na asikie.’’ mzuri ni yule mtu ambaye hulisikia neno na
kulielewa. Naye hakika hutoa matunda, akizaa
Sababu Ya Kufundisha Kwa Mifano mara mia, au mara sitini, au mara thelathini ya
10Wanafunzi wake wakamwendea mbegu iliyopandwa.’’
wakamwuliza, “Kwa nini unasema na watu kwa
mifano?’’ 11Akawajibu, “Ninyi mmepewa Mfano Wa Magugu
kuzifahamu siri za Ufalme wa Mbinguni, lakini 24Yesu akawaambia mfano mwingine,
wao sivyo. 12Kwa maana yule aliye na kitu akasema: ‘‘Ufalme wa Mbinguni unaweza
atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele, lakini kufananishwa na mtu aliyepanda mbegu nzuri
yule asiye na kitu, hata kile alichonacho katika shamba lake. 25Lakini wakati kila mtu

15
MATHAYO
alipokuwa amelala, adui yake akaja na kupanda 37Akawaambia, “Aliyepanda mbegu nzuri ni
magugu katikati ya ngano, akaenda zake. Mwana wa Adamu. 38Shamba ni ulimwengu na
26Ngano ilipoota na kutoa masuke, magugu mbegu nzuri ni wana wa Ufalme. Magugu ni
nayo yakatokea. wana wa yule mwovu. 39Yule adui aliyepanda
27“Watumishi wa yule mwenye shamba magugu ni Ibilisi . Mavuno ni mwisho wa dunia,
wakamjia na kumwambia, ‘Bwana, si tulipanda nao wavunaji ni malaika.
mbegu nzuri shambani mwako? Basi, magugu 40‘‘Kama vile magugu yang’olewavyo na

yametoka wapi ? kuchomwa motoni, ndivyo itakavyokuwa wakati


28Akawajibu, ‘Adui ndiye aliyefanya jambo wa mwisho wa dunia. 41Mwana wa Adamu
hili.’ Wale watumishi wakamwuliza, ‘Je, unataka atawatuma malaika zake, nao watakusanya
twende tukayang'oe? ” kutoka katika Ufalme wake kila kitu
29Lakini akasema, ‘Hapana, msiyang'oe, kinachosababisha dhambi na watenda maovu
kwa maana wakati mking’oa magugu mnaweza wote. 42Nao watawatupa katika tanuru la moto
mkang'oa na ngano pamoja nayo. 30Acheni ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
ngano na magugu vikue vyote pamoja mpaka 43Ndipo wenye haki watang'aa kama jua katika

wakati wa mavuno. Wakati huo nitawaambia Ufalme wa Baba yao. Yeye aliye na masikio , na
wavunaji, wayakusanye magugu kwanza, asikie.
wayafunge matita matita ili yachomwe moto,
kisha wakusanye ngano na kuileta ghalani Mfano Wa Hazina Iliyofichwa na Lulu
mwangu.’ ’’ 44‘‘Ufalme wa Mbinguni unafanana na

hazina iliyofichwa shambani, ambayo mtu


Mfano Wa Mbegu ya Haradali mmoja alipoiona akaificha tena. Kisha katika
31Akawaambia mfano mwingine, akasema, furaha yake, akaenda akauza vyote alivyokuwa
“Ufalme wa Mbinguni ni kama punje ya haradali, navyo, akalinunua lile shamba.’’
ambayo mtu aliichukua akaipanda shambani 45‘‘Tena, Ufalme wa Mbinguni unafanana na

mwake. 32Ingawa mbegu hiyo ni ndogo kuliko mfanyi biashara aliyekuwa akitafuta lulu safi.
mbegu zote, lakini inapokua ni mmea mkubwa 46Alipoipata lulu moja ya thamani kubwa,

kuliko yote ya bustanini, nao huwa mti mkubwa, alikwenda akauza vyote alivyokuwa navyo
hata ndege wa angani huja na kutengeneza akainunua.
viota katika matawi yake.’’
Mfano Wa Wavu
Mfano Wa Chachu 47“Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama wavu
33Akawaambia mfano mwingine, ‘‘Ufalme wa kuvulia samaki uliotupwa baharini ukavua
wa Mbinguni unafanana na chachu ambayo samaki wa kila aina. 48Ulipojaa, wavuvi
mwanamke aliichukua akaichanganya katika wakavuta pwani, wakaketi na kukusanya samaki
vipimo vitatu vya unga mpaka wote ukaumuka.’’ wazuri kuwaweka kwenye vyombo safi, lakini
wale samaki wabaya wakawatupa. 49Hivi ndivyo
Sababu Ya Yesu Kutumia Mifano itakavyokuwa wakati wa mwisho wa dunia.
34Yesu alinena mambo haya yote kwa Malaika watakuja na kuwatenganisha watu
makutano kwa mifano. Wala pasipo mfano waovu na watu wenye haki. 50Nao watawatupa
hakuwaambia lo lote. 35Hii ilikuwa ili kutimiza lile hao waovu katika tanuru la moto ambako
lililonenwa kwa vinywa vya manabii kusema: kutakuwa na kilio na kusaga meno.
51Yesu akauliza, ‘‘Je, mmeyaelewa haya

‘‘Nitakifungua kinywa changu niseme nao yote?''


kwa mifano, Wakamjibu, ‘‘Ndiyo.’’
nitahubiri mambo yaliyofichika tangu 52Akawaambia, ‘‘Basi kila mwalimu wa

kuumbwa kwa misingi ya ulimwengu.’’ sheria aliyefundishwa elimu ya Ufalme wa


Mbinguni ni kama mwenye nyumba anayetoa
Ufafanuzi Wa Mfano Wa Magugu kutoka katika ghala yake mali mpya na mali ya
36Kisha Yesu akaagana na makutano, zamani.’’
akaingia nyumbani. Wanafunzi wake wakamjia
wakamwambia, ‘‘Tueleze maana ya ule mfano Yesu Akataliwa Nazareti
wa magugu shambani.’’ 53Yesu alipomaliza kutoa mifano hii,

16
MATHAYO
akaondoka. 54Alipofika mjini kwao, kupitia nchi kavu, kutoka mijini. 14Yesu alipofika
akawafundisha watu katika sinagogi lao. Nao kando ya bahari aliona makutano makubwa ya
wakastaajabu, wakauliza, ‘‘Mtu huyu amepata watu, akawahurumia na akawaponya wagonjwa
wapi hekima hii na uwezo huu wa kufanya wao.
miujiza?” 55‘‘Huyu si yule mwana wa seremala? 15Ilipofika jioni, wanafunzi wake wakamjia

Mama yake si yeye aitwaye Maria, nao ndugu wakamwambia, “Mahali hapa ni nyikani, na
zake ni Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? muda sasa umekwisha, waage makutano ili
56Nao dada zake wote hawako hapa pamoja waende zao vijijini wakajinunulie chakula.’’
nasi? Mtu huyu amepata wapi basi mambo haya 16Yesu akawaambia, “Hakuna sababu ya

yote?’’ 57Wakachukizwa naye. wao kuondoka. Ninyi wapeni chakula.’’


Lakini Yesu akawaambia, “Nabii hakosi 17Wakamjibu, “Tuna mikate mitano na

heshima isipokuwa katika nchi yake na samaki wawili tu.’’


nyumbani kwake.’’ 18Akawaambia, “Nileteeni hivyo vitu hapa.’’
58Naye hakufanya miujiza mingi huko kwa 19Akaagiza makutano wakae chini kwenye

sababu ya kutokuamini kwao. nyasi. Akaichukua ile mikate mitano na wale


samaki wawili, akainua macho yake akatazama
Yohana Mbatizaji Akatwa Kichwa mbinguni, akavibariki na kuimega ile mikate,
Wakati huo, mfalme Herode aliyekuwa kisha akawapa wanafunzi wake hiyo mikate na
14 mtawala alisikia habari kuhusu sifa za hao samaki,wanafunzi wakawagawia makutano.
Yesu, 2akawaambia watumishi wake, “Huyu ni 20Wote wakala, wakatosheka, nao wanafunzi

Yohana Mbatizaji, amefufuka kutoka kwa wafu! wake wakakusanya vipande vilivyosalia,
Hiyo ndiyo sababu nguvu za kutenda miujiza wakajaza vikapu kumi na viwili. 21Idadi ya wale
zinafanya kazi ndani yake.’’ watu waliokula walikuwa wanaume 5,000, bila
3Herode alikuwa amemkamata Yohana kuhesabu wanawake na watoto.
akamfunga na kumweka gerezani kwa sababu
ya Herodia, mke wa Filipo, ndugu yake, 4kwa Yesu Atembea Juu Ya Maji
kuwa Yohana alikuwa amemwambia Herode 22MaraYesu akawaambia wanafunzi wake

kwamba, “Si halali kwako kuwa na huyo waingie kwenye chombo watangulie kwenda
mwanamke.’’ 5Herode alitaka sana kumwua ng'ambo ya pili ya bahari, wakati Yeye
Yohana, lakini akiogopa watu kwa maana anawaaga wale makutano. 23Baada ya
walimtambua kuwa ni nabii. kuwaaga, akaenda zake mlimani peke yake
6Katika siku ya kuadhimisha sikukuu ya kuomba. Jioni ilipofika, Yesu alikuwa huko peke
kuzaliwa kwa Herode, binti wa Herodia alicheza Yake. 24Wakati huo kile chombo kilikuwa
mbele ya watu waliohudhuria akamfurahisha kimeshafika mbali kutoka nchi kavu
sana Herode 7kiasi kwamba aliahidi kwa kiapo kikisukwasukwa na mawimbi kwa sababu upepo
kumpa huyo binti lo lote atakaloomba. 8Yeye ulikuwa wa mbisho.
akiwa amefundishwa na mama yake, huyo binti 25Wakati wa zamu ya nne ya usiku a , Yesu

akasema, “Nipatie kichwa cha Yohana Mbatizaji akawaendea wanafunzi wake akiwa anatembea
kwenye sinia.’’ 9Mfalme akasikitika, lakini kwa juu ya maji. 26Wanafunzi wake walipomwona
ajili ya kile kiapo alichoapa mbele ya wageni, akitembea juu ya maji, waliingiwa na hofu kuu,
akaamuru kwamba apatiwe ombi lake. 10Hivyo wakasema, ‘‘Ni mzimu.’’ Wakapiga yowe kwa
akaagiza Yohana Mbatizaji akatwe kichwa mle kuogopa.
gerezani. 11Kichwa chake kikaletwa kwenye 27Lakini mara Yesu akasema nao,
sinia, akapewa yule binti, naye akampelekea akawaambia, “Jipeni moyo! Ni Mimi, msiogope.’’
mama yake. 12Wanafunzi wa Yohana wakaja na 28Petro akamjibu, ‘‘Bwana, ikiwa ni Wewe,

kuuchukua mwili wake kwenda kuuzika. Kisha niambie nije kwako nikitembea juu ya maji.’’
wakaenda wakamwambia Yesu. 29Yesu akamwambia, “Njoo.’’

Basi Petro akatoka kwenyen chombo,


Yesu Alisha Watu Elfu Tano akatembea juu ya maji kumwelekea Yesu.
13Yesu aliposikia haya yaliyokuwa 30Lakini alipoona upepo mkali aliingiwa na hofu,

yametukia, aliondoka kwa chombo akaenda naye akaanza kuzama, huku akipiga kelele,
mahali pasipo na watu ili awe peke yake. Lakini “Bwana, niokoe!’’
watu walipopata habari, wakamfuata kwa miguu
a25 “Zamu ya nne ya usiku’’ ni kati ya saa 9 na saa 12 alfajiri
17
MATHAYO
31Mara Yesu akanyosha mkono Wake na yangu wa mbinguni hakulipanda, litang'olewa.
kumshika, akamwambia, “Wewe mwenye imani 14Waacheni, wao ni viongozi vipofu,
haba, kwa nini uliona shaka?’’ wanaoongoza vipofu. Kama kipofu
32Nao walipoingia ndani ya chombo, upepo akimwongoza kipofu mwenzake, wote wawili
ukakoma. 33Ndipo wote waliokuwamo ndani ya watatumbukia shimoni.’’
kile chombo wakamwabudu Yesu wakisema, 15Petro akasema, “Tuelezee maana ya huu

“Hakika, Wewe ndiwe Mwana wa Mungu.’’ mfano.’’


16Yesu akawauliza, “Je, bado ninyi
Yesu Awaponya Wagonjwa Genesareti hamfahamu? Je, hamfahamu 17kwamba cho
34Walipokwisha kuvuka, wakafika nchi ya chote kiingiacho kinywani huenda tumboni na
Genesareti. 35Watu wa eneo lile walipomtambua hatimaye hutolewa nje na kuwa uchafu? 18Lakini
Yesu, walipeleka habari sehemu zote za jirani. kitokacho kinywani hutoka moyoni, na hiki
Watu wakawaletea wagonjwa wao wote ndicho kimtiacho mtu unajisi. 19Kwa maana
36wakamsihi awaruhusu wagonjwa waguse tu ndani ya moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji,
pindo la vazi Lake, nao wote waliomgusa, uzinzi, uasherati, wizi, ushahidi wa uongo na
wakaponywa. masingizio. 20Haya ndiyo yamtiayo mtu unajisi,
lakini kula bila kunawa mikono hakumtii mtu
Mapokeo Ya Wazee unajisi.”
Ndipo baadhi ya Mafarisayo na walimu
15 wa sheria wakamjia Yesu kutoka Imani ya Mwanamke Mkananayo
Yerusalemu na kumwuliza, 2“Mbona wanafunzi 21Yesu aliondoka mahali pale akaenda

wako wanakiuka mapokeo ya wazee waliopita? sehemu za Tiro na Sidoni. 22Mwanamke mmoja
Kwa maana wao hawanawi mikono yao kabla Mkananayo aliyeishi jirani na sehemu hizo akaja
ya kula!’’ kwake, akilia, akasema, “Nihurumie,Ee Bwana,
3Yesu akawajibu, “Mbona ninyi mnavunja Mwana wa Daudi, binti yangu amepagawa na
amri ya Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu? pepo na anateseka sana.’’
4Kwa maana Mungu alisema, ‘Waheshimu baba 23Lakini Yesu hakumjibu neno. Hivyo

yako na mama yako’ na ‘Ye yote amtukanaye wanafunzi wake wakamwendea na kumsihi
baba yake au mama yake, na auawe.’ 5Lakini sana, wakisema, “Mwambie aende zake, kwa
ninyi mwafundisha kwamba mtu akimwambia maana anaendelea kutupigia kelele.’’
baba yake au mama yake, ‘Kile ambacho 24Yesu akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya

ningeweza kukusaidia kimewekwa wakfu kwa kondoo wa Israeli waliopotea.’’


Mungu,’ basi hana tena sababu ya kumsaidia 25Lakini yule mwanamke akaja, akapiga

baba yake. 6Basi kwa ajili ya mafundisho yenu magoti mbele ya Yesu, akasema, ‘‘Bwana,
mnavunja amri ya Mungu. 7Ninyi wanafiki! Isaya nisaidie!’’
alikuwa sawa alipotabiri juu yenu kwamba: 26Yesu akajibu, ‘‘Si haki kuchukua chakula

cha watoto na kuwatupia mbwa.’’


8“ ‘Watuhawa huniheshimu kwa midomo yao, 27Yule mwanamke akajibu, “Ndiyo, Bwana,

lakini mioyo yao iko mbali nami. lakini hata mbwa hula makombo yanayoanguka
9Kuniabudu kwao ni bure, kutoka kwenye meza za bwana zao.’’
nayo mafundisho yao ni maagizo ya 28Ndipo Yesu akamwambia, “Mwanamke,

wanadamu tu.’ ’’ imani yako ni kubwa! Iwe kwako kama


unavyotaka.’’Naye binti yake akapona tangu saa
Vitu Vitiavyo Unajisi ile ile.
10Yesu akaita ule umati wa watu
akawaambia, “Sikilizeni na mwelewe: Yesu Aponya Watu Wengi
11kinachomfanya mtu kuwa najisi mbele za 29Yesu akaondoka na kwenda kando ya

Mungu si kile kiingiacho kinywani mwake, bali ni bahari ya Galilaya. Kisha akapanda mlimani,
kile kitokacho kinywani mwake.’’ akaketi huko. 30Umati mkubwa wa watu
12Kisha wanafunzi wake wakamjia na wakamjia, wakiwaleta vilema, vipofu,viwete,
kumwuliza, Je, unajua kwamba Mafarisayo bubu na wengine wengi, wakawaweka miguuni
walichukizwa sana waliposikia yale uliyosema?’’ pake, naye akawaponya.31Hao watu
13Akawajibu, “Kila pando ambalo Baba wakashangaa walipoona bubu wakisema,

18
MATHAYO
vilema wakipona, viwete wakitembea na vipofu mikate. 6Yesu akawaambia, “Jihadharini,
wakiona, wakamtukuza Mungu wa Israeli. jilindeni na chachu ya Mafarisayo na ya
Masadukayo.’’
Yesu Alisha Watu Elfu Nne 7Wakajadiliana wao kwa wao, wakisema,
32Kisha Yesu akawaita wanafunzi wake “Ni kwa sababu hatukuleta mikate.’’
akawaambia, “Ninahurumia huu umati wa watu, 8Yesu, akitambua mazungumzo yao,
kwa sababu sasa wamekuwa pamoja nami kwa akasema, “Enyi wa imani haba! Mbona
muda wa siku tatu na hawana cho chote cha mnajadiliana miongoni mwenu kuhusu kutokuwa
chakula, nami sipendi kuwaaga wakiwa na njaa na mikate? 9Je, bado tu hamwelewi?
wasije wakazimia njiani.” Je,hamkumbuki ile mikate mitano iliyolisha watu
33Wanafunzi wake wakasema, ‘‘Tutapata 5,000 na ni idadi ya vikapu vingapi vya mabaki
wapi mikate ya kutosha kuwalisha umati huu wa mlivyokusanya? 10Au ile mikate saba iliyolisha
watu mkubwa namna hii, nasi tuko nyikani?’’ watu 4,000 na ni idadi ya vikapu vingapi vya
34Yesu akawauliza, “Mnayo mikate mabaki mlivyokusanya? 11Inakuwaje

mingapi?’’ mnashindwa kuelewa kwamba nilikuwa sisemi


Wakamjibu, ‘‘Tunayo mikate saba na nanyi habari za mikate? Jilindeni na chachu ya
visamaki vichache.” Mafarisayo na Masadukayo.” 12Ndipo
35Yesu akawaambia ule umati wa watu wakaelewa kwamba alikuwa hasemi juu ya
waketi chini. 36Kisha akachukua ile mikate saba chachu ya kutengeneza mikate, bali juu ya
na wale samaki, naye akiisha kumshukuru mafundisho ya Mafarisayo na Masadukayo.
Mungu, akavimega na kuwapa wanafunzi wake,
nao wakawapa ule umati wa watu. 37Wote Petro Amkiri Yesu Kuwa Ni Mwana Wa
wakala na kushiba. Baadaye wanafunzi Mungu
wakakusanya vipande vilivyosalia, wakajaza 13Basi Yesu alipofika katika eneo la Kaisaria

vikapu saba. 38Idadi ya watu walikuwa wanaume Filipi, akawauliza wanafunzi wake, “Watu
4,000, bila kuhesabu wanawake na watoto. husema Mwana wa Adamu ni nani?”
39Baada ya kuaga ule umati wa watu, Yesu 14Wakamjibu, “Baadhi ya watu husema ni

aliingia chomboni akaenda sehemu za Yohana Mbatizaji, wengine husema ni Eliya na


Magadani a . bado wengine husema, ni Yeremia au
mmojawapo wa manabii.’’
Mafarisayo Wadai Ishara 15Akawauliza, ‘‘Je, ninyi, mnasema mimi ni

Mafarisayo na Masadukayo wakamjia nani?’’


16 Yesu na kumjaribu kwa kumwomba 16Simoni Petro akamjibu, “Wewe ndiwe

awaonyeshe ishara kutoka mbinguni. Kristo a , Mwana wa Mungu aliye hai.’’


2Akawajibu akawaambia, “Ifikapo jioni, 17Naye Yesu akamwambia, ‘‘Heri wewe,

mnasema, ‘Hali ya hewa itakuwa nzuri, kwa Simoni mwana wa Yona, kwa maana hili
kuwa anga ni nyekundu,’ 3nanyi wakati wa halikufunuliwa kwako na mwanadamu, bali na
asubuhi mnasema, ‘Leo kutakuwa na dhoruba, Baba yangu aliye mbinguni. 18 ‘‘Nami
kwa sababu anga ni nyekundu na mawingu nakuambia, wewe ndiwe Petro na juu ya
yametanda.’ Mnajua jinsi ya kupambanua kule mwamba huu nitalijenga kanisa langu, hata
kuonekana kwa anga, lakini hamwezi malango ya kuzimu hayataweza kulishinda.
kupambanua dalili za nyakati. 4Kizazi cha 19Nitakupa funguo za Ufalme wa Mbinguni na lo

waovu na cha zinaa hutafuta ishara ya majira, lote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa
lakini hakitapewa ishara yo yote isipokuwa Mbinguni, lo lote utakalofungua duniani litakuwa
ishara ya Yona.” Yesu akawaacha, akaenda limefunguliwa mbinguni.’’ 20Kisha akawakataza
zake. wanafunzi wake wasimwambie mtu ye yote
kwamba Yeye ndiye Kristo.
Chachu Ya Mafarisayo Na Masadukayo
5Wanafunzi wake walipofika ng’ambo ya pili Yesu Anatabiri Juu Ya Kifo Chake
ya bahari, walikuwa wamesahau kuchukua
a16 Kristo maana yake Masiya, yaani, Mpakwa
a39 Magadani hapa inamaanisha Magdala. (Aliyetiwa)Mafuta.’’

19
MATHAYO
21Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaeleza macho yao, hawakumwona mtu mwingine ye
wanafunzi wake kwamba hana budi kwenda yote isipokuwa Yesu .
Yerusalemu na kupata mateso mengi kwa 9Walipokuwa wakishuka kutoka mlimani,

mikono ya wazee, wakuu wa makuhani na Yesu akawaagiza, ‘‘Msimwambie mtu ye yote


walimu wa sheria na kwamba itampasa auawe maono haya mpaka Mwana wa Adamu
na siku ya tatu atafufulika. atakapofufuka kutoka kwa wafu.’’
22Petro akamchukua kando akaanza 10Wale wanafunzi wakamwuliza, “Kwa nini

kumkemea, akisema, “Mungu apishie hayo basi walimu wa sheria wanasema kwamba
mbali! Jambo hili kamwe halitakupata!!’’ lazima Eliya aje kwanza?’’
23Lakini Yesu akageuka na kumwambia 11Yesu akawajibu, ‘‘Ni kweli, Eliya lazima

Petro , “Rudi nyuma yangu, Shetani! Wewe ni aje kwanza naye atatengeneza mambo yote.
kikwazo kwangu. Moyo wako hauwazi yaliyo ya 12Lakini nawaambia, Eliya amekwisha kuja, nao

Mungu, bali ya wanadamu.’’ hawakumtambua, bali walimtendea kila kitu


24Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, walichotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu pia
“Mtu ye yote akitaka kunifuata, ni lazima ajikane atateswa mikononi mwao.’ ” 13Ndipo wale
mwenyewe na auchukue msalaba wake, wanafunzi wakaelewa kuwa alikuwa
anifuate. 25Kwa maana ye yote anayetaka anazungumza nao habari za Yohana Mbatizaji.
kuyaokoa maisha yake atayapoteza, lakini ye
yote atakayeyapoteza maisha yake kwa ajili Yesu Amponya Kijana Mwenye Pepo
yangu atayapata. 26Kwa maana itamfaidia nini 14Walipofika penye umati wa watu, mtu

mtu kuupata ulimwengu wote, lakini mmoja akamjia Yesu na kupiga magoti mbele
akayapoteza maisha yake? Au mtu atatoa nini yake, akasema, 15“Bwana, mhurumie
badala ya maisha yake? 27Kwa maana Mwana mwanangu. Yeye ana kifafa na anateseka sana.
wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake Mara kwa mara huanguka kwenye moto au
pamoja na malaika zake, naye ndipo kwenye maji. 16Nilimleta kwa wanafunzi wako
atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo lakini hawakuweza kumponya.’’
yake. 28Nawaambia kweli, baadhi yenu hapa 17Yesu akajibu, “Enyi kizazi kisichoamini na

hawataonja mauti kabla ya kumwona Mwana wa kilichopotoka, nitakaa nanyi hata lini, nami
Adamu akija katika Ufalme wake.’’ nitawavumilia hadi lini? Mleteni kijana hapa
kwangu.’’ 18Yesu akamkemea yule pepo
Yesu Abadilika Sura Mlimani mchafu, akamtoka yule kijana, naye akapona
Siku sita baada ya jambo hili,Yesu saa ile ile
17 akawachukua Petro, Yakobo na 19Kisha wanafunzi wakamwendea Yesu

Yohana ndugu yake Yakobo, na kuwaleta wakati ambapo hakuna watu, wakamwuliza,
mpaka juu ya mlima mrefu mahali pasipo na “Kwa nini sisi hatukuweza kumtoa?”
watu. 2Wakiwa huko, Yesu alibadilika sura 20Akawajibu, ‘‘Kwa sababu ya imani yenu

mbele yao. Uso wake ukang'aa kama jua na ndogo. Ninawaambia kweli, mkiwa na imani
nguo zake zikawa na weupe wa kuumiza kama punje ndogo ya haradali, mtauambia
macho. 3Ghafula wakawatokea mbele yao Mose mlima huu, ‘Ondoka hapa uende pale’ nao
na Eliya, wakizungumza na Yesu. utaondoka. Wala hakutakuwa na jambo
4Ndipo Petro akamwambia Yesu, ‘‘Bwana, lisilowezekana kwenu.’’ 21 ‘‘Lakini hali kama hii
ni vema sisi tukae hapa. Ukitaka, nitafanya haitoki ila kwa kuomba na kufunga.’’
vibanda vitatu: kimoja chako, kingine cha Mose 22Siku moja walipokuwa pamoja huko

na kingine cha Eliya.’’ Galilaya, Yesu akawaambia, “Mwana wa Adamu


5Petro alipokuwa angali ananena, ghafula, anakwenda kutiwa mikononi mwa watu. 23Nao
wingu linalong'aa likawafunika na sauti ikatoka watamwua na siku ya tatu atafufuka.’’
kwenye hilo wingu ikisema, ‘‘Huyu ni mwanangu Wanafunzi wakahuzunika sana.
mpendwa, ninayependezwa naye sana,
msikilizeni Yeye.’’ Yesu Na Petro Watoa Kodi Ya Hekalu
6Wale wanafunzi, waliposikia haya, 24Baada ya Yesu na wanafunzi wake kufika

wakaanguka chini kifudifudi, wakajawa na hofu. Kapernaumu, wakusanyaji wa kodi ya Hekalu


7Lakini Yesu akaja na kuwagusa, akawaambia,

“Inukeni na wala msiogope.’’ 8Walipoinua

20
MATHAYO
wakamjia Petro na kumwuliza, “Je, Mwalimu
wenu halipi kodi ya Hekalu a ?’’ Mfano Wa Kondoo Aliyepotea
25Petro akajibu, “Ndiyo, Yeye hulipa.” Petro 10‘‘Angalia ili usimdharau mmojawapo wa

aliporudi nyumbani, Yesu akawa wa kwanza hawa wadogo, kwa maana nawaambia, malaika
kulizungumzia, akamwuliza, “Unaonaje wao mbinguni daima wanauona uso wa Baba
Simoni?’’ Wafalme wa dunia hupokea ushuru na yangu aliye mbinguni.’’ 11Kwa maana Mwana
kodi kutoka kwa nani? Je, ni kutoka kwa watoto wa Adamu alikuja kuokoa kile kilichopotea.
wao au kutoka kwa watu wengine?” 12“Mwaonaje? Ikiwa mtu anao kondoo mia
26Petro akamjibu, “Kutoka kwa watu moja na mmoja wao akapotea, hatawaacha
wengine.’’ Yesu akamwambia, “Kwa hiyo watoto wale tisini na tisa vilimani na kwenda kumtafuta
wao wamesamehewa. 27Lakini ili tusije huyo mmoja aliyepotea? 13Naye akisha mpata,
tukawaudhi, nenda baharini ukatupe ndoana. amin, nawaambia, hufurahi zaidi kwa ajili ya
Mchukue samaki wa kwanza utakayemvua, huyo kondoo mmoja kuliko wale tisini na tisa
fungua kinywa chake nawe utakuta humo fedha, ambao hawakupotea. 14Vivyo hivyo, Baba yenu
ichukue ukalipe kodi yako na yangu.” wa mbinguni hapendi hata mmojawapo wa
hawa wadogo apotee.’’
Aliye Mkuu Katika Ufalme Wa Mbinguni
Wakati huo, wanafunzi wakamjia Yesu Ndugu Yako Akikukosea
18 na kumwuliza “Je, nani aliye mkuu 15“Kama ndugu yako akikukosea, nenda

kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni?” ukamwonyeshe kosa lake, kati yenu ninyi wawili
2Yesu akamwita mtoto mdogo na peke yenu. Kama akikusikiliza, utakuwa
kumsimamisha katikati yao. 3Naye akasema: umempata tena ndugu yako. 16Lakini kama
‘‘Amin, nawaambia, msipoongoka na kuwa hatakusikiliza, nenda na mtu mwingine mmoja
kama watoto wadogo, kamwe hamtaingia katika au wawili ili kila neno lithibitishwe na ushahidi
Ufalme wa Mbinguni. 4Kwa hiyo mtu yeyote wa mashahidi wawili au watatu. 17Kama
ajinyenyekezaye kama huyu mtoto, ndiye aliye akikataa kuwasikiliza hao, liambie kanisa, naye
mkuu kuliko wote katika Ufalme wa Mbinguni. kama akikataa hata kulisikiliza kanisa, basi
5“Ye yote amkaribishaye mtoto mdogo mtendeeni mtu huyo kama vile ambavyo
kama huyu kwa jina langu, anikaribisha mimi. mngemtendea asiyeamini.
18“Amin, nawaambieni, lo lote
Kujaribiwa Ili Kutenda Dhambi mtakalolifunga duniani litakuwa limefungwa
6Lakini kama mtu ye yote anamsababisha mbinguni na lo lote mtakalolifungua duniani
mmojawapo wa hawa wadogo wanaoniamini litakuwa limefunguliwa mbinguni.
atende dhambi, ingekuwa bora kwake afungiwe 19“Tena nawaambia, ikiwa wawili wenu

jiwe kubwa la kusagia shingoni mwake na watakubaliana duniani kuhusu jambo lo lote
kutoswa katika kilindi cha bahari. watakaloomba, watafanyiwa na Baba yangu
7“Ole wa ulimwengu kwa sababu ya yale aliye mbinguni. 20Kwa kuwa wanapokusanyika
mambo yanayosababisha watu kutenda dhambi! pamoja watu wawili au watatu kwa jina langu,
Mambo hayo lazima yawepo, lakini ole wake mimi niko papo hapo pamoja nao.”
mtu yule ambaye huyasababisha. 8Ikiwa mkono
wako au mguu wako unakusababisha utende Kusamehe
dhambi, ukate na uutupe mbali. Ni afadhali 21Ndipo Petro akamjia Yesu na kumwuliza,

kwako kuingia katika uzima ukiwa huna mkono “Bwana, ndugu yangu anikosee mara ngapi
mmoja au mguu mmoja, kuliko kuwa na mikono nami nimsamehe? Je, hata mara saba?”
miwili au miguu miwili na kutupwa katika moto 22Yesu akamjibu, ‘‘Sikuambii hata mara

wa milele. 9Nalo jicho lako kama saba, bali hata saba mara sabini.’’
linakusababisha utende dhambi ling'oe, ulitupe
mbali. Ni afadhali kwako kuingia katika uzima Mfano Wa Mtumishi Asiyesamehe
ukiwa na jicho moja, kuliko kuwa na macho 23‘‘Kwa hiyo Ufalme wa Mbinguni unaweza

mawili lakini ukatupwa katika moto wa jehanam. kufananishwa na mfalme aliyetaka kufanya
hesabu zake za fedha na watumishi wake.
24Alipoanza kufanya hesabu zake, mtu mmoja
a24 Kodi ya hekalu hapa ilikuwa “didrachmas,’’ yaani drakamu mbili
ambazo ni sawa na nusu shekeli.

21
MATHAYO
aliyekuwa anadaiwa talanta 10,000 a ,
aliletwa 4Akawajibu, “Je, hamkusoma kwamba hapo
kwake. 25Kwa kuwa alikuwa hawezi kulipa deni mwanzo Mwumba aliwaumba mtu mume na mtu
hilo, bwana wake akaamuru kwamba auzwe, mke. 5Naye akasema, ‘Kwa sababu hii mtu
yeye, mkewe, watoto wake na vyote alivyokuwa atamwacha baba yake na mama yake naye
navyo, ili lile deni lipate kulipwa. ataambatana na mkewe na hao wawili
26‘‘Yule mtumishi akampigia magoti, watakuwa mwili mmoja?’ 6Hivyo si wawili tena,
akamsihi yule bwana akisema, `Naomba bali ni mwili mmoja. Kwa hiyo kile
univumilie, nami nitakulipa deni lako lote.’’ alichokiunganisha Mungu, mwanadamu
27Yule bwana wa huyo mtumishi akamwonea asikitenganishe.’’
huruma, akafuta deni lake lote, akamwacha 7Wakamwuliza, “Kwa nini basi Mose

aende zake. aliagiza mtu kumpa mkewe hati ya talaka na


28“Lakini yule mtumishi alipokuwa anatoka kumwacha?’’
nje, akakutana na mtumishi mwenzake 8Yesu akawajibu, “Mose aliwaruhusu
aliyekuwa amemkopesha dinari mia moja b . kuwaacha wake zenu kwa sababu ya ugumu wa
Akamkamata, akamkaba koo akimwambia, mioyo yenu. Lakini tangu mwanzo haikuwa
‘Nilipe kile ninachokudai!’ hivyo. 9Mimi nawaambia, ye yote amwachaye
29“Yule mtumishi mwenzake akapiga magoti mkewe isipokuwa kwa sababu ya uasherati
akamsihi akisema, ‘Naomba univumilie, nami naye akaoa mke mwingine, anazini.” Naye
nitakulipa deni lako lote.’ amwoaye yule mwanamke aliyeachwa pia
30“Lakini akakataa. Badala yake, alienda anazini.”
akamtupa gerezani hata atakapolipa hilo deni. 10Wanafunzi wake wakamwambia, “Kama
31”Watumishi wenzake walipoona haya hali ndiyo hii kati ya mume na mke, ni afadhali
yaliyotukia wakaudhika sana, nao wakaenda na mtu asioe!’’
kumwambia bwana wao kila kitu kilichokuwa 11Yesu akawaambia, ‘‘Si watu wote
kimetukia. wanaoweza kupokea neno hili, isipokuwa wale
32“Yule bwana akamwita yule mtumishi tu waliojaliwa na Mungu 12Kwa maana wengine
akamwambia, ‘Wewe mtumishi mwovu! Mimi ni matoashi kwa sababu wamezaliwa hivyo,
nilikusamehe deni lako lote uliponisihi. 33Je, wengine wamefanywa matoashi na wanadamu
haikukupasa kumhurumia mtumishi mwenzako na wengine wamejifanya matoashi kwa ajili ya
kama mimi nilivyokuhurumia wewe?’ 34Kwa Ufalme wa Mbinguni. Yeye awezaye kulipokea
hasira yule bwana wake akamtia yule mtumishi neno hili na alipokee.’’
mikononi mwa askari wa gereza ili ateswe
mpaka atakapolipa yote aliyokuwa anadaiwa. Yesu Awabariki Watoto Wadogo
35“Hivi ndivyo Baba yangu wa mbinguni 13Kisha watoto wadogo wakaletwa kwa

atakavyomfanyia kila mmoja wenu ikiwa Yesu ili aweke mikono yake juu yao na
hatamsamehe kutoka moyoni kila mmoja ndugu awaombee. Lakini wanafunzi wake
yake aliyemkosea.’’ wakawakemea wale waliowaleta.
14Yesu akasema, “Waacheni watoto
Yesu Afundisha Kuhusu Talaka wadogo waje kwangu, wala msiwazuie, kwa

19 Yesu alipomaliza kusema maneno


haya, aliondoka Galilaya, akaenda
maana Ufalme wa Mbinguni ni wa wale walio
kama hawa. 15Naye akaweka mikono yake juu
sehemu za Uyahudi, ng'ambo ya Mto Yordani. yao, akaondoka huko.
2Umati mkubwa wa watu ukamfuata, naye

akawaponya huko. Kijana Tajiri


3Baadhi ya Mafarisayo wakamjia ili 16Mtu mmoja akamjia Yesu na kumwuliza,,

kumjaribu wakamwuliza, “Ni halali mtu “Mwalimu mwema, nifanye jambo gani jema ili
kumwacha mke wake kwa sababu yo yote?’’ nipate uzima wa milele?”
17Yesu akamjibu, “Mbona unaniita mimi

mwema? Hakuna aliye mwema ila Mmoja tu,


a24 Talanta moja ilikuwa sawa na mshahara wa kibarua wa miaka ndiye Mungu: Lakini ukitaka kuingia uzimani,
kumi na mitano. zitii amri.”
b28 Dinari moja ilikuwa kama mshahara wa kibarua wa siku moja.

22
MATHAYO
18Yule mtu akamwuliza,’’Amri zipi?’’ ujira wa dinari moja a kwa siku, akawapeleka
Yesu akamjibu, ‘‘Usiue, usizini, usiibe, kwenye shamba lake la mizabibu.
usishuhudie uongo, 19waheshimu baba yako na 3“Mnamo saa tatu akatoka tena, akawakuta

mama yako na umpende jirani yako kama nafsi wengine wamesimama sokoni bila kazi.
yako.’’ 4Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni mkafanye
20Yule kijana akasema, ‘‘Hizi zote kazi katika shamba langu la mizabibu, nami
nimezishika. Je, bado nimepungukiwa na nini?’’ nitawalipa cho chote kilicho haki yenu.’ 5Kwa
21Yesu akamwambia, ‘‘Kama ukitaka kuwa hiyo wakaenda.
mkamilifu, nenda, kauze vitu vyote ulivyo navyo ‘‘Akatoka tena mnamo saa sita na pia saa
na hizo fedha uwape maskini, nawe utakuwa na tisa akafanya vivyo hivyo. 6Mnamo saa kumi na
hazina mbinguni. Kisha njoo, unifuate.’’ moja akatoka tena akawakuta wengine bado
22Yule kijana aliposikia hayo, akaenda zake wamesimama bila kazi. Akawauliza, ‘Kwa nini
kwa huzuni, kwa sababu alikuwa na mali nyingi. mmesimama hapa kutwa nzima pasipo kufanya
kazi?’
Hatari Za Utajiri 7Wakamjibu, ‘Ni kwa sababu hakuna ye
23Ndipo Yesu akawaambia wanafunzi wake, yote aliyetuajiri.’
“Amin, amin nawaambia, itakuwa vigumu kwa Akawaambia, ‘Ninyi nanyi nendeni
mtu tajiri kuingia katika Ufalme wa Mbinguni. mkafanye kazi katika shamba langu la
24Tena nawaambia, ni rahisi zaidi kwa ngamia mizabibu.’
kupita kwenye tundu la sindano kuliko mtu tajiri 8“Ilipofika jioni, yule mwenye shamba la

kuingia katika Ufalme wa Mungu.’’ mizabibu akamwambia msimamizi,‘Waite hao


25Wanafunzi wake waliposikia haya, vibarua na uwalipe ujira wao, ukianzia na wale
walishangaa sana na kuuliza, “Ni nani basi walioajiriwa mwisho na kuishia na wale
awezaye kuokoka?’’ walioajiriwa kwanza.’
26Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, 9Wale vibarua walioajiriwa mnamo saa kumi

“Kwa mwanadamu jambo hili haliwezekani, na moja, wakaja na kila mmoja wao akapokea
lakini kwa Mungu mambo yote yanawezekana.’’ dinari moja. 10Hivyo wale walioajiriwa kwanza
27Ndipo Petro akamjibu, ‘‘Tazama, sisi walipofika, walidhani watalipwa zaidi. Lakini kila
tumeacha kila kitu na kukufuata, tutapata nini mmoja wao pia alipokea dinari moja.
basi?’’ 11Walipoipokea, wakaanza kulalamika dhidi ya
28Yesu akawaambia, “Amin, amin yule mwenye shamba, 12wakisema,‘Hawa watu
nawaambia , wakati wa kufanywa upya vitu walioajiriwa mwisho wamefanya kazi kwa muda
vyote, wakati mwana wa Adamu atakapoketi wa saa moja tu, nawe umewafanya sawa na sisi
kwenye kiti chake cha utukufu cha enzi, ninyi ambao tumestahimili taabu na joto lote la
mliomfuata pia mtaketi katika viti vya enzi kumi mchana kutwa?’
na viwili, mkiyahukumu makabila kumi na mawili 13“Yule mwenye shamba akamjibu mmoja

ya Israeli. 29Kila mmoja aliyeacha nyumba au wao, ‘Rafiki, sijakudhulumu. Je, hukukubaliana
ndugu zake wa kiume au wa kike au baba au nami kwa ujira wa kawaida wa dinari moja?
mama au watoto au mashamba kwa ajili Yangu, 14Chukua ujira wako na uende. Mimi nimeamua

atapokea mara mia zaidi ya hayo na ataurithi kumlipa huyu mtu aliyeajiriwa mwisho kama
uzima wa milele. 30Lakini wengi walio wa nilivyokupa wewe. 15Je, sina haki yangu kufanya
kwanza watakuwa wa mwisho nao walio wa kile nitakacho na mali yangu mwenyewe ? Au
mwisho watakuwa wa kwanza.’’ unaona wivu kwa kuwa nimekuwa mkarimu?’
16‘‘Vivyo hivyo, wa mwisho watakuwa wa

Mfano Wa Wafanyakazi Katika Shamba La kwanza na wa kwanza watakuwa wa mwisho.’’


Mizabibu
“Kwa maana Ufalme wa Mbinguni Yesu Atabiri Tena Kuhusu Kifo Chake
20 unafanana na mtu mwenye shamba 17Basi Yesu alipokuwa anapanda kwenda

aliyetoka alfajiri ili kwenda kuajiri vibarua Yerusalemu, aliwachukua kando wale
kufanya kazi katika shamba lake la mizabibu wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia,
2Baada ya kukubaliana na hao vibarua kuwalipa

a2 Dinari moja ilikuwa mshahara wa kibarua wa siku moja.

23
MATHAYO
18‘‘Tazameni, tunapanda kwenda Yerusalemu, Daudi, uturehemu.’’
naye Mwana wa Adamu atatiwa mikononi mwa 32Yesu akasimama na kuwaita, akawauliza,

viongozi wa makuhani na walimu wa sheria, nao “Mnataka niwafanyie nini?’’


watamhukumu kifo 19na kumtia mikononi mwa 33Wakamjibu, “Bwana, tunataka kuona.’’

watu Mataifa ili wamdhihaki na kumpiga mijeledi 34Yesu akawahurumia na kuwagusa macho

na kumsulibisha msalabani, naye siku ya tatu yao. Mara macho yao yakapata kuona, nao
atafufuka!’’ wakamfuata.

Ombi La Mama Yake Yakobo na Yohana Yesu Anaingia Yerusalemu Kwa Shangwe

21
20Kisha mama yao wana wa Zebedayo Walipokuwa wanakaribia Yerusalemu,
akamjia Yesu pamoja na wanawe, naye akiwa wakafika Bethfage katika Mlima wa
amepiga magoti mbele yake, akamwomba Yesu Mizeituni, ndipo Yesu akawatuma wanafunzi
amfanyie upendeleo. wake wawili, 2akiwaambia, “Ingieni katika kijiji
21Yesu akamwuliza, “Unataka nini?’’ kilichoko mbele yenu, nanyi mtakuta punda
Akajibu, “Tafadhali, wape wanangu hawa, amefungwa na mwanapunda pamoja naye.
mmoja aketi upande wako wa kuume na Wafungueni na mniletee. 3Kama mtu ye yote
mwingine upande wako wa kushoto katika akiwasemesha lo lote, mwambieni, ‘Bwana ana
Ufalme wako.’’ haja nao, naye atawaruhusu mwalete mara.
22Yesu akawaambia, “Ninyi hamjui 4Haya yalitukia ili litimie lile lililonenwa na

mnaloomba. Je,ninyi mnaweza kunywea nabii, akisema:


kikombe nitakachonywea mimi?’’
Wakajibu, “Tunaweza.’’ 5‘‘Mwambieni Binti Sayuni,
23Yesu akawaambia, “Kwa kweli kikombe ‘Tazama, mfalme wako anakuja kwako,
changu mtakinywea, lakini kuketi upande wangu ni mnyenyekevu, naye amepanda punda,
wa kuume au wa kushoto, si langu mimi juu ya mwanapunda, mtoto wa punda.’
kuwapa. Nafasi hizo ni za wale ambao kwa ajili
yao zimeandaliwa na Baba yangu.’’ 6Wale wanafunzi wakaenda, wakafanya
24Wale wanafunzi wengine kumi waliposikia kama vile Yesu alivyokuwa amewaagiza.
haya, waliwakasirikia hao ndugu wawili. 25Lakini 7Wakamleta yule punda na mwanapunda, nao

Yesu akawaita wote pamoja na kuwaambia, wakatandika mavazi yao juu ya hao punda na
“Mnafahamu kuwa watawala wa watu Yesu akaketi juu yake. 8Umati mkubwa wa watu
wasiomjua Mungu huwatawala kwa nguvu, nao wakatandika nguo zao barabarani na wengine
wenye vyeo huonyesha mamlaka yao. 26Isiwe wakakata matawi kutoka kwenye miti
hivyo kwenu. Badala yake, ye yote anayetaka wakayatandika barabarani. 9Ule umati wa watu
kuwa mkuu miongoni mwenu hana budi kuwa uliomtangulia na ule uliomfuata ukapiga kelele
mtumishi wenu, 27Naye anayetaka kuwa wa ukisema,
kwanza miongoni mwenu ni lazima awe
mtumwa wenu, 28 kama vile ambavyo Mwana “Hosana Mwana wa Daudi!’’
wa Adamu hakuja ili kutumikiwa, bali kutumika “Amebarikiwa Yeye ajaye kwa Jina la
na kuutoa uhai wake uwe fidia kwa ajili ya Bwana!’’
wengi’’ “Hosana juu mbinguni!’’

Yesu Awaponya Vipofu Wawili 10Yesu alipoingia Yerusalemu, mji wote


29Wakati Yesu na wanafunzi wake ukataharuki, watu wakauliza, “Huyu ni nani?’’
walipokuwa wakiondoka Yeriko, umati mkubwa 11Ule umati wa watu ukajibu, “Huyu ni Yesu,

wa watu ulimfuata. 30Vipofu wawili walikuwa yule nabii kutoka Nazareti katika Galilaya.’’
wameketi kando ya barabara. Waliposikia
kwamba Yesu alikuwa anapita, wakapiga kelele Yesu Atakasa Hekalu
wakisema, “Bwana, Mwana wa Daudi, 12Yesu akaingia katika eneo la hekalu na

uturehemu!’’ kuwafukuza wote waliokuwa wakinunua na


31Ule umati wa watu ukawakemea na kuuza vitu hekaluni, akazipindua meza za watu
kuwaambia wanyamaze, lakini wao wakazidi waliokuwa wakibadilisha fedha na viti vya wale
kupaza sauti wakisema, “Bwana, Mwana wa waliokuwa wakiuza njiwa. 13Akawaambia,

24
MATHAYO
“Imeandikwa, ‘Nyumba yangu itaitwa nyumba ya ‘Mbona basi hamkumwamini?’ 26Lakini
sala,’ lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la tukisema, ‘Ulitoka kwa wanadamu’,
wanyang'anyi.’’ tunawaogopa hawa watu, maana wote
14Vipofu na vilema wakamwendea kule wanamtambua Yohana kuwa ni nabii.’’
hekaluni, naye akawaponya. 15Lakini viongozi 27Kwa hiyo wakamjibu Yesu, ‘‘Sisi hatujui.’’

wa makuhani na walimu wa sheria walipoona Ndipo akawaambia, ‘‘Wala mimi


mambo ya ajabu aliyofanya na kuwasikia watoto sitawaambia ni kwa mamlaka gani ninatenda
wakishangilia katika eneo la hekalu wakisema, mambo haya.’’
“Hosana Mwana wa Daudi, walikasirika,
wakamwuliza Yesu, Mfano Wa Wana Wawili
16“Je, unasikia hayo hawa wanayosema?’’ 28“Lakini mwaonaje? Mtu mmoja alikuwa na

Akawajibu, wana wawili. Akamwendea yule wa kwanza


“Naam, kwani hamkusoma, akamwambia, ‘Mwanangu, nenda ukafanye kazi
kwenye shamba la mizabibu leo.’
‘‘ ‘Kutoka katika vinywa vya watoto 29“Yule mwanawe akamjibu ‘Mimi
wachanga sitakwenda’, baadaye akabadili mawazo yake
na wale wanaonyonya umeamuru sifa akaenda.
kamili?’ ’’ 30“Kisha yule baba akamwendea yule

mwanawe mwingine akamwambia vile vile.


17Akawaacha, akatoka nje ya mji, akaenda Yeye akajibu, ‘Nitakwenda baba,’ lakini
hadi Bethania, akalala huko. hakwenda.
31“Ni yupi kati yao hao wawili aliyetimiza kile

Mtini Wanyauka alichotaka baba yake?’’


18Asubuhi na mapema, Yesu alipokuwa Wakamjibu, “Ni yule wa kwanza.’’
akirudi mjini, alikuwa na njaa. 19Akiuona mtini Yesu akawaambia, “Amin, amin
kando ya barabara, akaukaribia lakini hakupata nawaambia, watoza ushuru na makahaba
tunda lo lote ila majani. Ndipo akauambia, wanawatangulia kuingia katika Ufalme wa
“Wewe na usizae matunda tena kamwe!” Papo Mungu. 32Kwa maana Yohana alikuja kwenu
hapo ule mtini ukanyauka. kuwaonyesha njia ya haki, lakini hakumsadiki,
20Wanafunzi wake walipoona jambo hili lakini watoza ushuru na makahaba
wakashangaa, wakamwuliza, “Imekuwaje mtini wakamsadiki. Nanyi hata mlipoona hayo,
huu kunyauka ghafula?’’ baadaye hamkutubu na kumsadiki.’’
21Yesu akawajibu, “Amin, amin nawaambia,

kama mkiwa na imani wala msiwe na shaka, si Mfano Wa Wapangaji Waovu


kwamba mtaweza kufanya tu yale yaliyofanyika 33“Sikilizeni mfano mwingine: Kulikuwa na

kwa huu mtini, bali hata mkiuambia huu mlima, mtu mmoja mwenye shamba ambaye alipanda
‘Ng'oka, ukatupwe baharini,’ nalo litafanyika. mizabibu. Akajenga ukuta kulizunguka,
22Lo lote mtakaloomba katika kusali, mkiamini, akatengeneza shinikizo ndani yake na akajenga
mtapokea. mnara wa ulinzi. Kisha akalikodisha hilo shamba
la mizabibu kwa wakulima fulani, naye
Wahoji Kuhusu Mamlaka Ya Yesu akaondoka akasafiri kwenda nchi nyingine.
23Yesu alipoingia hekaluni, viongozi wa 34“Wakati wa mavuno ulipokaribia, akawatuma

makuhani na wazee wa watu wakamjia watumishi wake kwa hao wakulima


alipokuwa anafundisha na kusema, “Unafanya waliopangishwa ili kukusanya matunda yake.
mambo haya kwa mamlaka gani, naye ni nani 35‘‘Wale wapangaji wakawakamata wale

aliyekupa mamlaka hayo?’’ watumishi, wakampiga mmoja, wakamwua


24Yesu akawajibu, “Nami nitawauliza swali mwingine na yule wa tatu wakampiga mawe.
moja. Kama mkinijibu, mimi nitawaambia ni kwa 36Kisha akawatuma kwao watumishi wengine,

mamlaka gani ninafanya mambo haya. wengi kuliko wale wa kwanza, nao wale
25Ubatizo wa Yohana, ulitoka wapi? Je, ulitoka wapangaji wakawatendea vile vile. 37‘‘Mwisho
mbinguni au kwa wanadamu?’’ wa yote, akamtuma mwanawe kwao, akisema,
Wakaanza kuhojiana wao kwa wao na ‘Watamheshimu mwanangu.’
kusema, ‘‘Tukisema ulitoka mbinguni atatuuliza, 38‘‘Lakini wale wapangaji walipomwona

25
MATHAYO
mwanawe, wakaambiana wao kwa wao, ‘Huyu ‘Karamu ya arusi imeshakuwa tayari, lakini wale
ndiye mrithi. Njoni na tumwue ili tuchukue urithi niliowaalika hawakustahili kuja. 9Kwa hiyo
wake.’ 39Hivyo wakamchukua, wakamtupa nje nendeni katika njia panda mkamwalike
ya shamba la mizabibu, wakamwua. karamuni ye yote mtakayemwona’ 10Wale
40“Kwa hiyo, huyo mwenye shamba, watumishi wakaenda barabarani
atakapokuja atawafanyia nini hao wakulima?’’ wakawakusanya watu wote waliowaona, wema
41Wakamjibu, “Kwa huzuni kuu na wabaya. Ukumbi wa arusi ukajaa wageni.
atawaangamiza kabisa hao wadhalimu na 11“Lakini mfalme alipoingia ndani ili
kulipangisha shamba lake kwa wakulima kuwaona wageni, akamwona mle mtu mmoja
wengine ambao watampatia fungu lake la ambaye hakuwa amevaa vazi la arusi. 12Mfalme
matunda wakati wa mavuno.’’ akamwuliza, ‘Rafiki, uliingiaje humu bila vazi la
42Yesu akawaambia, “Je, hamjasoma katika arusi?’ Yule mtu hakuwa na la kusema.
maandiko kwamba: 13Ndipo mfalme akawaambia watumishi

wake, ‘Mfungeni mikono na miguu mkamtupe


“Lile jiwe walilolikataa waashi nje, kwenye giza. Huko kutakuwa na kilio na
limekuwa jiwe kuu la pembeni, kusaga meno.’
Bwana ndiye aliyefanya jambo hili, 14Kwa maana walioitwa ni wengi, lakini

nalo ni la ajabu machoni petu?’ walioteuliwa ni wachache.’’

43‘‘Kwa hiyo ninawaambia, Ufalme wa Kulipa Kodi kwa Kaisari


Mungu utaondolewa kwenu na watapewa watu 15Ndipo Mafarisayo wakatoka nje
wengine wawezao kuzaa matunda yake.’’ wakaandaa mpango wa kumtega Yesu katika
44“Yeye aangukaye kwenye jiwe hili atavunjika maneno yake. 16Wakatuma wanafunzi wao
vipande vipande, lakini yule litakayemwangukia kwake pamoja na Maherode, wakisema,
atasagika sagika kabisa. ‘‘Mwalimu, tunajua kwamba wewe ni mtu
45Viongozi wa Makuhani na Mafarisayo mwadilifu na unafundisha njia ya Mungu katika
waliposikia mifano ya Yesu, walitambua kuwa kweli bila kuonyesha tofauti kwa mtu wala
alikuwa akiwasema wao. 46Wakatafuta njia ya upendeleo. 17Tuambie basi, Wewe unaonaje?
kumkamata lakini wakaogopa ule umati wa watu Ni halali kulipa kodi kwa Kaisari au la?’’
kwa kuwa wao walimwona Yesu kuwa ni nabii. 18Lakini Yesu akijua makusudi yao mabaya

akawaambia, ” Enyi wanafiki, kwa nini mnajaribu


Mfano Wa Karamu Ya Arusi kunitega ? 19Nionyesheni hiyo sarafu
Yesu akasema nao tena kwa mifano, inayotumika kwa kulipia kodi. ” Wakamletea
22 akawaambia, 2“Ufalme wa Mbinguni dinari. 20Naye akawauliza, ”Sura hii na
unaweza kufananishwa na mfalme mmoja maandishi haya ni vya nani ?”
aliyemwandalia mwanawe karamu ya arusi. 21Wakamjibu, ‘‘Ni vya Kaisari.’’
3Akawatuma watumishi wake kuwaita wale Basi Yesu akawaambia, ‘‘Mpeni Kaisari
waliokuwa wamealikwa karamuni, lakini kilicho cha Kaisari, naye Mungu mpeni kilicho
wakakataa kuja. cha Mungu.’’
4‘‘Kisha akawatuma watumishi wengine 22Waliposikia hili, wakashangaa. Hivyo

akisema, ‘Waambieni wale walioalikwa kwamba wakamwacha, wakaenda zao.


karamu iko tayari kwa ajili yenu, nimekwisha
kuchinja mafahali wangu na vinono. Karibuni Ndoa Na Ufufuo
|akaenda shambani mwake, mwingine akaenda 23Siku hiyo hiyo Masadukayo, wale
kwenye biashara yake. wasemao kwamba hakuna ufufuo wa wafu,
5“Lakini hawakuzingatia, wakaenda zao, wakamjia Yesu na kumwuliza swali, wakisema,
huyu shambani mwake na mwingine kwenye 24‘‘Mwalimu, Mose alisema, ‘Kama mtu akifa bila

biashara zake. 6Wengine wao wakawakamata kuwa na watoto, ndugu yake amwoe huyo
wale watumishi wake wakawatenda vibaya na mjane ili ampatie watoto huyo nduguye
kuwaua. 7“Yule mfalme akakasirika sana, aliyekufa. 25Basi palikuwa na ndugu saba
akapeleka jeshi lake likawaangamiza wale miongoni mwetu. Yule wa kwanza akaoa mke,
wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto. naye akafa na kwa kuwa hakuwa na watoto,
8“Kisha akawaambia watumishi wake, akamwachia nduguye yule mjane. 26Ikatokea

26
MATHAYO
vivyo hivyo kwa yule ndugu wa pili na wa tatu, aliyeweza kumjibu Yesu neno. Tena tangu siku
hadi wote saba. 27Hatimaye, yule mwanamke hiyo hakuna aliyethubutu kumwuliza tena
naye akafa. 28Sasa basi, siku ile ya ufufuo, yeye maswali.
atakuwa mke wa nani miongoni mwa wale
ndugu saba, kwa kuwa wote walikuwa Yesu Awashutumu Walimu Wa Sheria Na
wamemwoa huyo mwanamke?” Mafarisayo

23
29Yesu akawajibu, “Mwapotoka kwa sababu Kisha Yesu akauambia ule umati wa
hamjui maandiko wala uweza wa Mungu. watu pamoja na wanafunzi wake:
30Wakati wa ufufuo watu hawataoa wala 2“Walimu wa sheria na Mafarisayo wameketi

kuolewa, bali watakuwa kama malaika wa katika kiti cha Mose, 3hivyo inawapasa kuwatii
Mungu mbinguni. 31Lakini kuhusu ufufuo wa na kufanya kila kitu wanachowaambia. Lakini
wafu, hamjasoma kile Mungu alichowaambia msifuate yale wanayotenda, kwa sababu
kwamba, 32 ‘Mimi ni Mungu wa Abrahamu, hawatendi yale wanayohubiri. 4Wao hufunga
Mungu wa Isaki na Mungu wa Yakobo?’ Yeye si mizigo mikubwa na kuiweka mabegani mwa
Mungu wa wafu bali ni Mungu wa walio hai.’’ watu, lakini wao wenyewe hawako radhi hata
33Ule umati wa watu uliposikia hayo, kuinua kidole ili kuisogeza.
ulishangaa sana kwa mafundisho yake. 5“Wao hufanya mambo yao yote ili

waonekane na watu. Vikasha vya ngozi vyenye


Amri Kuu Kuliko Zote maandiko ya sheria na kurefusha matamvua ya
34Mafarisayo waliposikia kwamba Yesu mavazi yao, 6wanapenda kukaa viti vya sehemu
alikuwa amewanyamazisha Masadukayo, za heshima karamuni na vile viti maalum sana
Mafarisayo wakakusanyika pamoja. 35Mmoja katika masinagogi, 7hupenda kusalimiwa
wao, mtaalam wa sheria, akamwuliza swali ili masokoni kutaka watu wawaite ‘Rabi a ’.
kumjaribu, akisema, 36 “Mwalimu, ni amri ipi 8“Lakini ninyi msiitwe ‘Rabi’ kwa sababu

katika Torati iliyo kuu kuliko zote?’’ mnaye Bwana mmoja na ninyi nyote ni ndugu.
37Yesu akamjibu, “‘Mpende Bwana Mungu 9Nanyi msimwite mtu ye yote ‘Baba’ hapa

wako kwa moyo wako wote na kwa roho yako duniani kwa maana mnaye Baba mmoja, naye
yote na kwa akili zako zote.’ 38Hii ndio amri iliyo yuko mbinguni. 10Wala msiitwe ‘mwalimu’ kwa
kuu, tena ni ya kwanza. 39Nayo ya pili ni kama maana mnaye mwalimu mmoja tu, ndiye Kristo.
hiyo, nayo ni hii: ‘Mpende jirani yako kama nafsi 11Yeye aliye mkuu kuliko ninyi nyote miongoni

yako.’ 40Amri hizi mbili ndizo msingi wa Torati na mwenu atakuwa mtumishi wenu. 12Kwa kuwa ye
manabii.’ ’’ yote anayejikweza atashushwa, na ye yote
anayejinyenyekeza atakwezwa.
Swali Kuhusu Mwana wa Daudi 13“Lakini ole wenu, walimu wa sheria na
41Wakati Mafarisayo wakiwa Mafarisayo, wanafiki! Kwa maana mnawafungia
wamekusanyika pamoja, Yesu akawauliza, watu milango ya Ufalme wa Mbinguni. Ninyi
42“Mnaonaje kuhusu Kristo a ? Yeye ni mwana wenyewe hamuingii humo, nao wale wanaotaka
wa nani?” kuingia mnawazuia. 14 “Ole wenu walimu wa
Wakamjibu, “Yeye ni mwana wa Daudi.’’ sheria na Mafarisayo, enyi wanafiki! Mnakula
43Akawaambia, “Inakuwaje basi kwamba katika nyumba za wajane, nanyi kwa kujifanya
Daudi akinena kwa Roho, anamwita Kristo kuwa wema, mnasali sala ndefu. Kwa hiyo
‘Bwana,’ kwa maana asema, adhabu yenu itakuwa kubwa zaidi.’’
15“Ole wenu walimu wa sheria na
44“ ‘Bwana Mungu alimwambia Bwana wangu: Mafarisayo, wanafiki! Ninyi mnasafiri baharini na
keti wewe mkono wangu wa kuume, nchi kavu ili kumfanya mtu mmoja ageuke na
hadi nitakapowaweka adui zako chini ya kuwafuata ninyi, lakini baada ya kumpata,
miguu yako.’ mnamfanya mwana wa jehanamu mara mbili
kuliko ninyi!
45“Kama basi Daudi anamwita yeye ‘Bwana,’ 16“Ole wenu, viongozi vipofu! Ninyi
awezaje kuwa mwanae?’’ 46Hakuna mtu mwasema, ‘Mtu akiapa kwa hekalu, kiapo hicho
si kitu, lakini mtu akiapa kwa dhahabu ya
a42 Kristo maana yake Masiya ,yaani Mpakwa(Aliyetiwa) Mafuta.’’
a7 Rabi maana yake bwana, mwalimu

27
MATHAYO
hekalu, amefungwa kwa kiapo chake.’ 17Ninyi katika masinagogi yenu na wengine
vipofu wapumbavu! Ni kipi kilicho kikuu zaidi, ile mtawafuatia kutoka mji mmoja hadi mji
dhahabu au lile hekalu ambalo ndilo linaloifanya mwingine. 35Hivyo ile damu ya wenye haki wote
hiyo dhahabu kuwa takatifu? 18Pia mnasema, iliyomwagwa hapa duniani, tangu damu ya
‘Mtu akiapa kwa madhabahu, si kitu, lakini mtu Abeli, ambaye alikuwa hana hatia, hadi damu ya
akiapa kwa sadaka iliyo juu ya madhabahu, Zekaria mwana wa Barakia, mliyemwua kati ya
amefungwa kwa kiapo chake?’ 19Ninyi vipofu! Ni Patakatifu na madhabahu, itawajia juu yenu.
kipi kikuu zaidi, ile sadaka, au ile madhabahu 36Amin, nawaambieni, haya yote yatakuja juu ya

ambayo ndiyo inayoifanya hiyo sadaka kuwa kizazi hiki.’’


takatifu? 20Kwa hiyo, mtu aapaye kwa
madhabahu, huapa kwa hiyo madhabahu na Yesu Aililia Yerusalemu
vitu vyote vilivyo juu yake. 21Naye mtu aapaye 37“Ee Yerusalemu, mnaowaua manabii na

kwa hekalu, huapa kwa hilo hekalu na kwa huyo kuwapiga mawe wale waliotumwa kwenu! Mara
akaaye ndani yake. 22Naye aapaye kwa mbingu, ngapi nimetamani kuwakusanya watoto wako,
huapa kwa kiti cha enzi cha Mungu na kwa kama vile kuku akusanyavyo vifaranga vyake
Yeye aketiye juu ya kiti hicho. chini ya mbawa zake, lakini hukutaka! 38Tazama
23“Ole wenu walimu wa sheria na nyumba yako imeachwa tupu na ukiwa. 39Kwa
Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana mnatoa maana nawaambia, hamtaniona tena mpaka
zaka ya mnanaa, bizari na jira, lakini mmeacha siku ile mtakaposema, ‘Amebarikiwa Yeye ajaye
mambo makuu zaidi ya sheria, yaani, haki, kwa Jina la Bwana.”
huruma na uaminifu. Haya imewapasa
kuyafanya bila kusahau hayo mengine. 24Ninyi Kubomolewa Kwa Hekalu Kwatabiriwa
viongozi vipofu, mnachuja kiroboto lakini
mnameza ngamia!
25“Ole
24 Yesu akatoka hekaluni na alipokuwa
akienda zake, wanafunzi wake
wenu, walimu wa sheria na wakamwendea ili kumwonyesha majengo ya
Mafarisayo, ninyi wanafiki! Kwa maana hekalu. 2Ndipo Yesu akawauliza, “Je, mnayaona
mnasafisha nje ya kikombe na kisahani, lakini haya yote? Amin, amin nawaambia, hakuna
ndani mmejaa unyang’anyi na kutokuwa na hata jiwe moja hapa litakalobaki juu ya jingine,
kiasi. 26Enyi Mafarisayo vipofu! Safisheni kila moja litabomolewa.”
kwanza ndani ya kikombe na sahani, ndipo nje
patakuwa safi. Ishara Za Nyakati Za Mwisho
27“Ole wenu, walimu wa sheria na 3Yesu alipokuwa ameketi kwenye Mlima wa

Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnafanana na Mizeituni, wanafunzi wake wakamjia mahali


makaburi yaliyopakwa chokaa, ambayo pasipo na watu, wakamwuliza, “Tuambie,
yanapendeza kwa nje lakini ndani yamejaa mambo haya yatatukia lini, nayo ni nini dalili za
mifupa ya wafu na kila aina ya uchafu. 28Vivyo kuja kwako na za mwisho wa dunia?
hivyo, kwa nje ninyi mnaonekana kwa watu 4Yesu akawajibu, “Angalieni, mtu
kuwa wenye haki, lakini kwa ndani mmejaa asiwadanganye. 5Kwa maana wengi watakuja
unafiki na uovu. kwa jina langu wakidai, ‘Mimi ndiye Kristo, nao
29“Ole wenu, walimu wa sheria na watawadanganya wengi. 6Mtasikia habari za
Mafarisayo, ninyi wanafiki! Mnajenga makaburi vita na matetesi ya vita,angalieni msitishike, kwa
ya manabii na kuyapamba makaburi ya wenye maana haya hayana budi kutukia, lakini ule
haki. 30Nanyi mwasema, ‘Kama tungaliishi mwisho bado. 7Taifa litainuka dhidi ya taifa na
wakati wa baba zetu, tusingalikuwa tumeshiriki ufalme dhidi ya ufalme. Kutakuwa na njaa na
katika kumwaga damu ya manabii!” 31Hivyo matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali.
mnajishuhudia wenyewe kwamba ninyi ni wana 8Haya yote yatakuwa ndio mwanzo wa utungu.

wa wale waliowaua manabii. 32Haya basi, 9“Ndipo mtasalitiwa, ili mteswe na kuuawa,

kijazeni kipimo cha dhambi ya baba zenu! nanyi mtachukiwa na mataifa yote kwa ajili
33“Ninyi nyoka, ninyi uzao wa nyoka wenye yangu. 10Wakati huo, wengi wataacha imani
sumu! Mtaiepukaje hukumu ya jehanam? 34Kwa yao, nao watasalitiana kila mmoja na mwenzake
sababu hii tazama nawapelekea manabii na na kuchukiana. 11Watatokea manabii wengi wa
wenye hekima na walimu. Baadhi yao mtawaua uongo, nao watawadanganya watu wengi.
na kuwasulibisha, wengine mtawapiga mijeledi 12Kwa sababu ya kuongezeka kwa uovu upendo

28
MATHAYO
wa watu wengi utapoa, 13Lakini yule watawakusanya wateule wake kutoka pande
atakayevumilia hadi mwisho ndiye zote nne za dunia, kutoka mwisho mmoja wa
atakayeokoka. 14Injili ya Ufalme itahubiriwa mbingu hadi mwisho mwingine.
ulimwenguni pote, kuwa ushuhuda kwa mataifa 32‘‘Jifunzeni kutokana na mtini. Matawi yake

yote. Ndipo ule mwisho utakapokuja. yanapoanza kuwa laini na kuchipua majani,
15Hivyo mtakapoona lile ‘Chukizo la fahamuni kwamba kiangazi kimekaribia. 33Hata
Uharibifu’ lililonenwa na nabii Danieli hivyo, mwonapo mambo hayo, jueni kwamba yu
limesimama mahali patakatifu, asomaye na karibu malangoni. 34Amin, amin nawaambia,
afahamu, 16Basi wale walioko Uyahudi kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote
wakimbilie milimani. 17Ye yote aliyeko juu ya yawe yametimia. 35Mbingu na dunia zitapita,
paa la nyumba asishuke ili kuchukua cho chote lakini maneno yangu hayatapita kamwe. ”
kutoka ndani ya nyumba. 18Yeye aliye shambani
na asirudi nyumbani kwenda kuchukua vazi Hakuna Ajuaye Siku Wala Saa
lake. 19Ole wa wenye mimba na wenye watoto 36“Hakuna ajuaye siku wala saa, hata

wachanga siku hizo! 20Ombeni ili kukimbia malaika mbinguni hawajui wala Mwana, ila Baba
kwenu kusiwe wakati wa baridi au siku ya peke yake. 37Kama ilivyokuwa wakati wa Noa,
Sabato. 21Kwa maana wakati huo kutakuwa na ndivyo itakavyokuwa kuja kwake Mwana wa
dhiki kuu ambayo haijapata kuwako tangu Adamu. 38Kwa maana siku zile kabla ya gharika,
mwanzo wa dunia mpaka sasa, wala watu walikuwa wakila na kunywa, wakioa na
haitakuwako tena. 22Kama siku hizo kuolewa, mpaka siku ile Noa alipoingia kwenye
zisingelifupizwa, hakuna hata mtu mmoja safina, 39nao hawakujua lo lote mpaka gharika
ambaye angeliokoka, lakini kwa ajili ya wateule ilipokuja ikawakumba wote. Hivyo ndivyo
siku hizo zitafupizwa. 23Wakati huo kama mtu ye itakavyokuwa atakapokuja Mwana wa Adamu.
yote akiwaambia, ‘Tazama, huyu hapa ni Kristo! 40“Watu wawili watakuwa shambani, mmoja

Au ‘Kristo yuko kule!’ Msisadiki. 24Kwa maana atatwaliwa, mwingine ataachwa. 41Wanawake
watatokea makristo wa uongo na manabii wa wawili watakuwa wanasaga pamoja, mmoja
uongo na kufanya ishara kubwa na miujiza atatwaliwa, mwingine ataachwa.
mingi ili kuwapotosha, hata ikiwezekana wale 42“Kwa hiyo kesheni, kwa maana hamjui ni

wateule hasa. 25Angalieni, nimetangulia siku gani atakapokuja Bwana wenu. 43“Lakini
kuwaambia mapema. fahamuni hili kwamba: Kama mwenye nyumba
26“Kwa hiyo mtu ye yote akiwaambia, ‘Yule angelijua ni wakati gani wa usiku ambao mwivi
kule nyikani,’ msiende huko. Au akisema, ‘Yuko anakuja, angelikesha na asingeliiacha nyumba
kwenye chumba,’ msisadiki. 27Kwa maana kama yake kuvunjwa. 44Kwa hiyo ninyi pia hamna budi
vile umeme utokeavyo mashariki na kuonekana kuwa tayari, kwa sababu Mwana wa Adamu
hata magharibi, ndivyo itakavyokuwa kuja atakuja saa msiyotazamia.”
kwake Mwana wa Adamu. 28Kwa maana po
pote ulipo mzoga, huko ndiko wakusanyikapo Mfano Wa Mtumishi Mwaminifu
tai. 45“Ni nani basi aliye mtumishi mwaminifu na

mwenye busara ambaye bwana wake


Kuja Kwa Mwana Wa Adamu amemweka kusimamia watumishi wengine
29‘‘Mara baada ya dhiki ya siku zile, katika nyumba yake, ili awape chakula chao
kwa wakati muafaka? 46Heri mtumishi yule
jua litatiwa giza, ambaye bwana wake atakapokuja atamkuta
nao mwezi hautatoa nuru yake, akifanya hivyo. 47Amin, amin nawaambia,
nazo nyota zitaanguka kutoka angani atamweka mtumishi huyo kuwa msimamizi wa
na nguvu za anga zitatikisika.’ mali yake yote. 48“Lakini kama huyo mtumishi ni
mwovu naye akasema moyoni mwake, ‘Bwana
30‘‘Ndipo
itakapotokea ishara ya Mwana wa wangu atakawia muda mrefu,’ 49naye kisha
Adamu angani na makabila yote ya dunia akaanza kuwapiga watumishi wenzake na kula
yataomboleza.. Nao watamwona Mwana wa na kunywa pamoja na walevi, 50bwana wa
Adamu akija juu ya mawingu ya angani, katika mtumishi huyo atakuja siku ambayo mtumishi
uwezo na utukufu mkuu. 31Naye atawatuma huyo hamtazamii na saa ile ambayo haijui.
malaika zake kwa sauti kuu ya tarumbeta, nao 51Atamkata huyo mtumishi vipande vipande na

29
MATHAYO
kumweka katika sehemu moja pamoja na aliyepewa talanta mbili akafanya vivyo hivyo,
wanafiki, mahali ambako kutakuwa ni kulia na akapata nyingine mbili zaidi. 18Lakini yule
kusaga meno.” mtumishi aliyekuwa amepokea talanta
moja,alikwenda akachimba shimo ardhini na
Mfano Wa Wanawali Kumi kuificha ile fedha ya bwana wake.
“Wakati huo, Ufalme wa Mbinguni 19“Baada ya muda mrefu yule bwana wa

25 utakuwa kama wanawali kumi wale watumishi akarudi na kufanya hesabu


waliochukua taa zao na kwenda kumlaki bwana nao. 20Yule mtumishi aliyepokea talanta tano
arusi. 2Watano wao walikuwa wapumbavu na akaja,akaleta nyingine tano zaidi. Akasema,
watano walikuwa wenye busara. 3Wale ‘Bwana uliweka kwenye uangalizi wangu talanta
wapumbavu walichukua taa zao lakini tano. Tazama, nimepata faida talanta tano
hawakuchukua mafuta ya akiba, 4lakini wale zaidi.’
wenye busara walichukua taa zao na mafuta ya 21“Bwana wake akamwambia, ‘Umefanya

akiba kwenye vyombo. 5Bwana arusi alipokawia vizuri sana, mtumishi mwema na mwaminifu!
kuja wale wanawali wote wakasinzia na kulala. Umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache,
6“Usiku wa manane pakawa na kelele: nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo
‘Tazameni, huyu hapa bwana arusi! Tokeni nje ushiriki katika furaha ya bwana wako!”
mkamlaki!’ 22“Yule mwenye talanta mbili naye akaja.
7“Ndipo wale wanawali wote wakaamka na Akasema, `Bwana, uliweka kwenye uangalizi
kuzitengeneza taa zao. 8Wale wapumbavu wangu talanta mbili. Tazama nimepata hapa
wakawaambia wale wenye busara, ‘Tupatieni talanta mbili zaidi.’
mafuta yenu kidogo, taa zetu zinazimika.’ 23Bwana wake akajibu, ‘Umefanya vizuri
9“Lakini wale wenye busara wakawajibu, sana, mtumishi mwema na mwaminifu,
‘Sivyo, hayatutoshi sisi na ninyi pia. Afadhali umekuwa mwaminifu kwa vitu vichache,
mwende kwa wauzao mkajinunulie mafuta yenu. nitakuweka kuwa msimamizi wa vitu vingi. Njoo
10“Nao walipokuwa wakienda kununua ushiriki katika furaha ya bwana wako.’
mafuta, bwana arusi akafika. Wale wanawali 24“Kisha yule mtumishi aliyepokea talanta

waliokuwa tayari, wakaingia ndani pamoja naye moja akaja, akasema, ‘Bwana, nilijua kwamba
kwenye karamu ya arusi na mlango ukafungwa. wewe ni mtu mgumu, unayevuna mahali
11“Baadaye wale wanawali wengine nao usipopanda na kukusanya mahali usipotawanya
wakaja, wakaita, ‘Bwana! Bwana! Tufungulie mbegu. 25Kwa hiyo niliogopa, nikaenda,
mlango!’ nikaificha talanta yako ardhini. Tazama, hii hapa
12“Lakini yeye bwana arusi akawajibu, ile iliyo mali yako.’
‘Amin, amin nawaambia, siwajui ninyi!’ 26“Bwana wake akajibu, ‘Wewe mtumishi
13“Kwa hiyo kesheni, kwa sababu hamjui mwovu na mvivu! Ulijua kwamba ninavuna
siku wala saa.’’ mahali nisipopanda na kukusanya mahali
nisipotawanya mbegu. 27Vema basi, ingekupasa
Mfano wa Watumishi Watatu Walioachiwa kuweka fedha yangu kwa watoa riba, nirudipo,
Talanta nichukue ile iliyo yangu na faida yake?
14“Tena, Ufalme wa Mbinguni ni kama mtu 28‘‘ ‘Basi mnyang'anyeni hiyo talanta

anayetaka kusafiri, akawaita watumishi wake na mkampe yule mwenye talanta kumi.’ 29Kwa
kuweka mali yake kwenye uangalizi wao. maana kila mtu mwenye kitu ataongezewa,
15Mmoja akampa talanta tano a mwingine talanta naye atakuwa navyo tele. Lakini kwa mtu yule
mbili b na mwingine talanta moja c , kila mmoja asiye na kitu, hata kile alicho nacho
alipewa kwa kadiri ya uwezo wake. Kisha yeye atanyang'anywa.30“Nanyi mtupeni huyo
akasafiri. 16“Yule aliyepewa talanta tano mtumishi asiyefaa nje, kwenye giza, mahali
akaenda mara moja akafanya nazo biashara ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.’ ’’
akapata talanta nyingine tano zaidi. 17Yule
Kondoo Na Mbuzi
a15 Talanta tano ilikuwa na mshahara wa kibarua wa miaka 75 31“Mwana wa Adamu atakapokuja katika
b15 Talanta mbili ilikuwa sawa na mshahara wa kibarua wa miaka utukufu wake na malaika wote watakatifu
30
c15 Talanta moja ilikuwa zaidi ya mshahara wa kibarua wa miaka pamoja naye, ndipo atakapoketi juu ya kiti cha
kumi na mitano. enzi cha utukufu wake. 32Mataifa yote

30
MATHAYO
watakusanyika mbele zake, naye atawatenga 3Basi viongozi wa makuhani na wazee wa
kama mchungaji anavyotenga kondoo na mbuzi. watu wakakusanyika katika jumba la utawala la
33Atawaweka kondoo upande wake wa kuume kuhani mkuu, jina lake Kayafa. 4Wakafanya
na mbuzi upande wake wa kushoto. shauri ili kumkamata Yesu kwa siri na kumwua.
34“Ndipo Mfalme atawaambia wale walioko 5Lakini wakasema, “Isiwe wakati wa sikukuu, la

upande wake wa kuume, ‘Njoni, ninyi sivyo kutakuwa na ghasia miongoni mwa watu.”
mliobarikiwa na Baba yangu, urithini Ufalme
ulioandaliwa kwa ajili yenu tangu kuumbwa kwa Yesu Anapakwa Mafuta Huko Bethania
ulimwengu. 35Kwa maana nilikuwa na njaa 6Wakati Yesu akiwa Bethania nyumbani

mkanipa chakula, nilikuwa na kiu mwa Simoni aliyekuwa na ukoma, 7mwanamke


mkaninywesha, nilikuwa mgeni mkanikaribisha, mmoja alimjia akiwa na chupa ya marmar yenye
36nilikuwa uchi mkanivika, nilikuwa mgonjwa manukato ya thamani kubwa, akayamimina
mkanitunza, nami nilikuwa kifungoni mkaja kichwani mwa Yesu alipokuwa ameketi mezani
kunitembelea.’ kula chakula.
37“Ndipo wale wenye haki watakapomjibu 8Lakini wanafunzi wake walipoona hayo

wakisema, ‘Bwana, ni lini tulikuona una njaa wakakasirika, wakasema, “Kwa nini ubadhirifu
tukakulisha au ukiwa na kiu tukakunywesha? huu wote? 9Manukato haya yangeliuzwa kwa
38Lini tulikuona ukiwa mgeni tukakukaribisha au bei kubwa na fedha hizo wakapewa maskini.’’
ukiwa uchi tukakuvika? 39Tena ni lini tulikuona 10Yesu akijua jambo hili, akawaambia,

ukiwa mgonjwa tukakutunza au ukiwa kifungoni “Mbona mnamsumbua huyu mwanamke? Yeye
tukakutembelea?’ amenitendea jambo zuri sana. 11Maskini
40“Naye Mfalme atawajibu, ‘Amin, amin mtakuwa nao siku zote, lakini mimi hamtakuwa
ninawaambia, kwa jinsi mlimvyotendea nami siku zote. 12Alipomiminia haya manukato
mmojawapo wa hawa ndugu Zangu walio kwenye mwili amefanya hivyo ili kuniandaa kwa
wadogo, mlinitendea Mimi.’ ajili ya maziko yangu. 13Ninawaambia kweli,
41“Kisha atawaambia wale walio upande mahali po pote habari njema itakapohubiriwa
Wake wa kushoto, ‘Ondokeni kwangu, ninyi ulimwenguni mwote, jambo hili alilofanya
mliolaaniwa, nendeni kwenye moto wa milele litatajwa pia, kwa ukumbusho wake.’’
alioandaliwa kwa ajili ya ibilisi na malaika zake.
42Kwa maana nilikuwa na njaa hamkunipa Yuda Akubali Kumsaliti Yesu
chakula, nilikuwa na kiu hamkuninywesha, 14Kisha mmojawapo wa wale kumi na
43nilikuwa mgeni nanyi hamkunikaribisha, wawili, yeye aitwaye Yuda Iskariote, alikwenda
nilikuwa uchi hamkunivika, nilikuwa mgonjwa kwa viongozi wa makuhani 15na kuuliza,
hamkunitunza na nilikuwa gerezani nanyi “Mtanipa nini nikimtia Yesu mikononi mwenu?
hamkuja kunitembelea.’ Wakamlipa vipande thelathini vya fedha.
44“Ndipo wao pia watajibu, ‘Bwana ni lini 16Tangu wakati huo Yuda akawa anatafuta

tulikuona ukiwa na njaa au kiu, au ukiwa mgeni wasaa mzuri wa kumsaliti Yesu.
au uchi , au ukiwa mgonjwa na kifungoni na
hatukukuhudumia?’ Yesu Ala Pasaka Pamoja Na Wanafunzi
45“Naye atawajibu, ‘Amin, amin nawaambia, 17Siku ya kwanza ya Sikukuu ya Mikate

kwa jinsi ambavyo hamkumtendea mmojawapo Isiyotiwa Chachu wanafunzi walimjia Yesu
wa hawa ndugu zangu walio wadogo, wakamwuliza, ‘‘Unataka tuandae wapi kwa ajili
hamkunitendea mimi.’ yako ili kuila Pasaka?’’
46“Ndipo hawa watakapoingia kwenye 18Akajibu, ‘‘Nendeni kwa mtu fulani huko

adhabu ya milele, lakini wale wenye haki mjini mkamwambie, ‘Mwalimu asema hivi: saa
wataingia katika uzima wa milele.’’ yangu imekaribia, nitaiadhimisha Pasaka
pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba
Shauri Baya La Kumwua Yesu yako.’ ’’ 19Hivyo wanafunzi wakafanya kama vile

26 Yesu alipomaliza kusema hayo yote,


akawaambia wanafunzi wake, 2“Mnajua
Yesu, alivyokuwa amewaelekeza, nao
wakaandaa Pasaka.
kwamba baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, 20Ilipofika jioni, Yesu alikuwa ameketi

naye Mwana wa Adamu atasalitiwa ili mezani pamoja na wale kumi na wawili. 21Nao
asulibiwe.’’ walipokuwa wakila, Yesu akasema, “Amin, amin

31
MATHAYO
nawaambia, mmoja wenu atanisaliti.’’ wake mpaka kwenye bustani iitwayo
22Wakahuzunika sana, wakaanza Gethsemane, akawaambia, “Kaeni hapa wakati
kumwambia mmoja mmoja, ‘‘Je, ni mimi ninakwenda kule kuomba.’’ 37Akamchukua Petro
Bwana?’’ pamoja na wale wana wawili wa Zebedayo,
23Yesu akawaambia, ‘‘Yule aliyechovya naye akaanza kuhuzunika na kufadhaika.
mkono wake katika bakuli pamoja nami, ndiye 38Kisha Yesu akawaambia, “Moyo wangu

atakayenisaliti. 24Mwana wa Adamu yu aenda umejawa na huzuni kiasi cha kufa. Kaeni hapa
kama alivyoandikiwa. Lakini ole wake mtu yule na mkeshe pamoja nami.’’
amsalitie Mwana wa Adamu. Ingeliwakuwa bora 39Akaenda mbele kidogo, akaanguka
kwake kama asingalizaliwa ! ” kifudifudi akaomba, akisema, “Baba yangu,
25Kisha Yuda, yule aliyemsaliti akasema, kama inawezekana, kikombe hiki na kiniepuke,
‘‘Kweli si mimi, Rabi?’’ lakini si kama nitakavyo mimi bali kama
Yesu akajibu, ‘‘Naam, wewe mwenyewe utakavyo Wewe.’’
umesema.’’ 40Kisha akarudi kwa wanafunzi wake na

kuwakuta wamelala. Akamwuliza Petro, “Je,


Kuanzishwa Kwa Meza ya Bwana ninyi wanaume, hamkuweza kukesha pamoja
26Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua nami kwa saa moja? 41‘‘Kesheni na mwombe,
mkate, akashukuru, akaumega, akawapa msije mkaanguka majaribuni. Hakika roho iko
wanafunzi wake akisema, ‘‘Twaeni, mle, huu radhi lakini mwili ni dhaifu.’’
ndio mwili wangu.’’ 42Akaenda tena mara ya pili na kuomba,
27Kisha akachukua kikombe, akashukuru, “Baba yangu, kama ikiwezekani kikombe hiki
akawapa akisema, ‘‘Kunyweni nyote katika kiniepuke nisikinywe, mapenzi yako yafanyike.’’
kikombe hiki. 28Hii ndiyo damu yangu ya agano, 43Aliporudi, akawakuta tena wamelala kwa

ile imwagikayo kwa ajili ya wengi kwa ondoleo la sababu macho yao yalikuwa mazito. 44Hivyo
dhambi. 29Lakini ninawaambia, tangu sasa akawaacha akaenda zake tena mara ya tatu na
sitakunywa tena kutoka katika uzao huu wa kuomba akisema maneno yale yale.
mzabibu, mpaka siku ile nitakapokunywa mpya 45Kisha akarudi kwa wanafunzi wake

pamoja nanyi katika Ufalme wa Baba yangu.’’ akawaambia, ‘‘Bado mmelala na kupumzika?
30Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka Tazameni, saa imefika ambapo Mwana wa
kwenda mlima wa Mizeituni. Adamu hana budi kutiwa mikononi mwa wenye
dhambi. 46Inukeni, twendeni zetu ! Huyu hapa
Yesu Atabiri Petro Kumkana yule anisalitiye! ”
31Kisha Yesu akawaambia, “Usiku wa leo

ninyi nyote mtaniacha, kwa maana imeandikwa: Yesu Akamatwa


47Alipokuwa bado anasema, Yuda,
“ ‘Nitampiga mchungaji, mmojawapo wa wale Kumi na Wawili, akafika,
nao kondoo wa hilo akiwa amefuatana na umati mkubwa wa watu
kundi watatawanyika.’ wenye panga na marungu waliokuwa
wametumwa na viongozi wa makuhani na
32Lakinibaada ya mimi kufufuka, nitawatangulia wazee wa watu. 48Basi msaliti alikuwa amewapa
kwenda Galilaya.’’ hao watu ishara kwamba: ‘‘Yeye nitakayembusu
33Petro akajibu “Hata kama wote ndiye, mkamateni.’’ 49Mara akamjia Yesu na
watakuacha, kamwe mimi sitakuacha.’’ kumsalimu, “Salaam, Rabi!’’ Akambusu.
34Yesu akajibu, “Amin, amin ninakuambia, 50Yesu akamwambia, “Rafiki, fanya kile

usiku huu huu, kabla jogoo hajawika, utanikana ulichokuja kufanya hapa.
mara tatu.’’ Kisha wale watu wakasogea mbele,
35Lakini Petro akasema, ‘‘Hata kama itabidi wakamkamata Yesu. 51Ghafula mmoja wa wale
kufa pamoja na Wewe, kamwe sitakukana.’’ waliokuwa na Yesu alipoona hivyo, akaushika
Nao wanafunzi wengine wote wakasema vivyo upanga wake, akauchomoa na kumpiga
hivyo. mtumishi wa Kuhani Mkuu, akamkata sikio.
52Ndipo Yesu akamwambia, “Rudisha
Yesu Anaomba Gethsemane upanga wako mahali pake, kwa maana wote
36Kisha Yesu akaenda pamoja na wanafunzi watumiao upanga watakufa kwa upanga. 53Je,

32
MATHAYO
unadhani siwezi kumwomba Baba yangu naye Petro Amkana Bwana Yesu
mara moja akaniletea zaidi ya majeshi kumi na 69Wakati huu Petro alikuwa amekaa nje

mawili ya malaika? 54Lakini je, maandiko uani. Mtumishi mmoja wa kike akamjia na
yatatimiaje yale yasemayo kwamba ni lazima kumwambia, “Wewe pia ulikuwa pamoja na
itokee hivi?” Yesu wa Galilaya.’’
55Wakati huo Yesu akawaambia ule umati 70Lakini Petro akakana mbele yao wote

wa watu, “Mmetoka na panga na marungu kuja akisema, “Sijui hilo usemalo.’’


kunikamata kama vile mimi ni mnyang’anyi? 71Alipotoka nje kufika kwenye lango,

Siku kwa siku niliketi hekaluni nikifundisha, mtumishi mwingine wa kike alimwona,
mbona hamkunikamata? 56Lakini haya yote akawaambia watu waliokuwapo, “Huyu mtu
yametukia ili maandiko ya manabii yapate alikuwa pamoja na Yesu Mnazareti.’’
kutimia.” Ndipo wanafunzi wake wote 72Akakana tena kwa kiapo akisema, “Mimi

wakamwacha na kukimbia. simjui huyo!’’


73Baada ya muda mfupi wale waliokuwa

Yesu Mbele Ya Kuhani Mkuu wamesimama pale wakamwendea Petro


57Wale waliokuwa wamemkamata Yesu wakamwambia, “Hakika wewe ni mmoja wao
wakampeleka kwa Kayafa, Kuhani Mkuu, mahali kwa maana ile namna yako ya kusema ni kama
ambapo walimu wa sheria pamoja na wazee yao.”
walikuwa wamekusanyika. 58Lakini Petro 74Ndipo Petro akaanza kujilaani na
akamfuata kwa mbali mpaka uani kwa Kuhani kuwaapia, Mimi simjui mtu huyo!’’
Mkuu. Akaingia ndani akaketi pamoja na walinzi Papo hapo jogoo akawika. 75Ndipo Petro
ili aone litakalotukia. akakumbuka lile neno alilokuwa amesema Yesu
59Basi viongozi wa wazee, makuhani na “Kabla jogoo hajawika utanikana mara tatu.’’
baraza lote wakatafuta ushahidi wa uongo dhidi Akaenda nje, akalia sana.
ya Yesu ili wapate kumua. 60Lakini hawakupata
jambo lo lote, ingawa mashahidi wengi wa Yesu Aletwa Mbele Ya Pilato
uongo walijitokeza.
Hatimaye wakajitokeza mashahidi wawili wa 27 Asubuhi na mapema, viongozi wa
makuhani wote na wazee wa watu
uongo 61na kusema : “Huyu mtu alisema, ‘Nina wakafanya shauri pamoja dhidi ya Yesu ili
weza kulivunja hekalu la Mungu na kulijenga kumwua. 2Wakamfunga, wakampeleka na
tena kwa siku tatu .’ ’’ kumkabidhi kwa Pilato, ambaye alikuwa
62Kisha Kuhani Mkuu akasimama na mtawala.
kumwambia Yesu, “Je, wewe hutajibu? Ni
ushahidi wa namna gani hawa watu wauletao Yuda Ajinyonga
dhidi yako?” 63Lakini Yesu alikuwa kimya. 3Yuda, ambaye ndiye aliyekuwa amemsaliti

Ndipo Kuhani Mkuu akamwambia, Yesu, alipoona kuwa Yesu amehukumiwa,


“Nakuapisha mbele za Mungu aliye hai, tuambie akajuta na akarudisha vile vipande thelathini vya
ikiwa wewe ndiwe Kristo, Mwana wa Mungu.” fedha alivyopewa na viongozi wa makuhani na
64Yesu akajibu, “Wewe umenena. Lakini wazee wa watu. 4Akasema, “Nimetenda
ninawaambia nyote, Tangu sasa mtamwona dhambi, kwa maana nimeisaliti damu isiyo na
Mwana wa Adamu akiwa ameketi mkono wa hatia.”
kuume wa Mungu Mwenye Nguvu na akija juu 5Basi Yuda akavitupa vile vipande vya

ya mawingu ya mbinguni.’’ fedha ndani ya hekalu akaondoka akaenda na


65Ndipo Kuhani Mkuu akararua nguo zake kujinyonga.
na kusema, “Amekufuru! Kwa nini tunahitaji 6Wale makuhani wakuu wakazichukua zile

ushahidi zaidi? Tazama, sasa ninyi mmesikia fedha wakasema, ‘‘Si halali kuchanganya fedha
hayo makufuru. 66 Uamuzi wenu ni nini?” hizi na sadaka kwa sababu hizi ni fedha zenye
Wakajibu, ‘‘Anastahili kufa ” damu.’’ 7Kwa hiyo baada ya kushauriana,
67Kisha wakamtemea mate usoni na waliamua kuvitumia kununulia shamba la
wengine wakampiga ngumi. Wengine walimpiga mfinyanzi, liwe mahali pa kuzikia wageni. 8Hii
makofi 68na kusema, “Tutabirie, wewe Kristo! Ni ndiyo sababu lile shamba likaitwa, ‘Shamba la
nani aliyekupiga?” Damu’ hadi leo. 9Ndipo likatimia lile lililonenwa
na nabii Yeremia kwamba, ‘‘Walichukua vile

33
MATHAYO
vipande thelathini vya fedha, thamani
aliyopangiwa na watu wa Israeli, 10wakanunulia Askari Wamdhihaki Yesu
shamba la mfinyanzi, kama vile Bwana 27Kisha askari wa mtawala wakampeleka

alivyoniagiza.’’ Yesu kwenye Praitorio a na wakakusanya kikosi


kizima cha askari kumzunguka. 28Wakamvua
Yesu Mbele Ya Pilato nguo Zake na kumvika vazi la rangi nyekundu,
11Wakati Yesu akiwa amesimama mbele ya kisha 29wakasokota taji ya miiba wakaiweka
mtawala, mtawala akamwuliza, “Wewe ndiye kichwani pake. Wakamwekea fimbo katika
mfalme wa Wayahudi?’’ mkono wake wa kuume, wakapiga magoti
Yesu akasema, “Wewe wasema hivyo.’’ mbele zake na kumdhihaki wakisema “Salaam,
12Lakini viongozi wa makuhani na wazee mfalme wa Wayahudi!’’ 30Wakamtemea mate,
walipomshtaki, hakujibu neno. 13Ndipo Pilato wakachukua ile fimbo wakampiga kichwani tena
akamwuliza, “Je, husikii ni mambo mangapi na tena. 31Baada ya kumdhihaki, wakamvua lile
wanayokushtaki nayo?’’ 14Lakini Yesu vazi , wakamvika tena nguo Zake. Kisha
hakumjibu hata kwa shtaka moja,kiasi kwamba wakampeleka ili kumsulibisha.
mtawala alishangaa sana.
15Basi ilikuwa ni desturi ya mtawala Yesu Asulibishwa
kumfungua mfungwa mmoja atakayechaguliwa 32Walipokuwa wakienda, wakakutana na

na umati wa watu wakati wa sikukuu. 16Wakati mtu mmoja kutoka Kirene, jina lake Simoni, nao
huo alikuwapo mfungwa mmoja mwenye sifa wakamlazimisha kuubeba ule msalaba.
mbaya, aliyeitwa Baraba. 17Hivyo umati wa watu 33Wakafika mahali paitwapo Golgotha, (ambayo

walipokusanyika, Pilato akawauliza, “Mnataka maana yake ni, Mahali pa Fuvu la Kichwa),
niwafungulie nani, Baraba au Yesu Yeye 34wakampa Yesu divai iliyochanganywa na

aitwaye Kristo?’’ 18Kwa kuwa alitambua Yesu nyongo ili anywe, lakini alipoionja, akakataa
alikuwa amekabidhiwa kwake kwa ajili ya wivu. kuinywa. 35Walipokwisha kumsulibisha
19Pilato akiwa ameketi kwenye kiti cha wakagawana mavazi Yake kwa kuyapigia kura,
hukumu, mkewe akampelekea ujumbe huu: ‘‘ ili litimie lile neno lililonenwa na nabii, ‘Waligawa
Usiwe na jambo lo lote juu ya huyu Mtu asiye na nguo zangu miongoni mwao na vazi langu
hatia, kwa kuwa leo nimeteseka sana katika wakalipigia kura. 36Kisha wakaketi,
ndoto kwa sababu Yake.” wakamchunga. Juu ya kichwa chake, kwenye
37
20Lakini viongozi wa makuhani na wazee msalaba, wakaandika shtaka lake: ‘HUYU NI
wakaushawishi ule umati wa watu kwamba YESU, MFALME WA WAYAHUDI.’
waombe Baraba afunguliwe na Yesu auawe. 38Wanyang'anyi wawili walisulibiwa pamoja
21Mtawala akawauliza tena, “Ni yupi kati ya naye, mmoja kuume Kwake na mwingine
hawa wawili mnayetaka niwafungulie?” kushoto Kwake. 39Watu waliokuwa wakipita
Wakajibu, “Baraba’’ njiani wakamvurumishia matukano huku
22Pilato akawaambia, “Basi nifanye nini na wakatikisa vichwa vyao 40na kusema, “Wewe
huyu Yesu aitwaye Kristo?’’ ambaye utalivunja hekalu na kulijenga kwa siku
Wakajibu wote , “Msulibishe!’’ tatu, jiokoe mwenyewe basi! Kama Wewe ni
23Pilato akauliza, “Kwa nini? Amefanya kosa Mwana wa Mungu, shuka kutoka msalabani.’’
gani?’’ 41Vivyo hivyo, viongozi wa , makuhani,

Lakini wao wakazidi kupiga kelele, walimu wa sheria na wazee wakamdhihaki


“Msulibishe.’’ wakisema, 42 “Aliwaokoa wengine, lakini hawezi
24Pilato alipoona kwamba hawezi kufanya lo kujiokoa mwenyewe!. Yeye ni Mfalme wa Israeli!
lote, lakini badala yake ghasia zilikuwa Ashuke sasa kutoka msalabani, tutamwamini.
zinaanza, akachukua maji, akanawa mikono 43Anamwamini Mungu, basi Mungu na
yake mbele ya ule umati wa watu, akasema. amwokoe sasa kama anamtaka, kwa maana
“Sina hatia juu ya damu ya mtu huyu. Hili ni alisema, ‘Mimi ni Mwana wa Mungu.’ ’’ 44Hata
jukumu lenu!”
25Watu wote wakajibu, ‘‘Damu yake na iwe

juu yetu na juu ya watoto wetu!’’ a27Praitoria maana yake makao makuu ya mtawala. Jumba la
26Basi akawafungulia Baraba, na baada ya kifalme lilokuwa linakaliwa na Pontio Pilato huko Yerusalemu,
palipokuwa na kiti cha hukumu
kumchapa Yesu mijeledi, akamtoa ili asulibiwe.

34
MATHAYO
wale wanyang'anyi waliosulibiwa pamoja naye Walinzi Pale Kaburini
wakamtukana vivyo hivyo. 62Kesho yake, yaani siku iliyofuata ile ya

Maandalizi ya Sabato, viongozi wa makuhani na


Kifo Cha Yesu Mafarisayo wakamwendea Pilato 63na kusema,
45Tangu saa sita hadi saa tisa giza lilifunika “Bwana, tumekumbuka kwamba yule
nchi yote. 46Ilipofika saa tisa Yesu akapaza mdanganyifu kabla hajafa alisema, ‘Baada ya
sauti akalia, “Eloi, Eloi lama sabakthani?’’ siku tatu nitafufuka.’ 64Kwa hiyo uamuru kaburi
Maana yake, “Mungu wangu, Mungu wangu, lilindwe kwa uthabiti mpaka baada ya siku tatu.
mbona umeniacha?’’ La sivyo, wanafunzi wake wanaweza kuja
47Baadhi ya wale watu waliokuwa kuuiba mwili wake na kuwaambia watu kwamba
wamesimama pale waliposikia haya, wakasema amefufuka kutoka kwa wafu. Udanganyifu huu
‘‘Anamwita Eliya,’’ wa mwisho utakuwa mbaya kuliko ule wa
48Ghafula mmoja wao akaenda mbio na kwanza.”
kuleta sifongo akaichovya kwenye siki, 65Pilato akawaambia, “Ninyi mnao askari

akaiweka kwenye mwanzi akampa Yesu ili Walinzi. Nendeni, liwekeeni ulinzi kadiri
anywe. 49Wengine wakasema, “Mwacheni na mwezavyo”. 66Kwa hiyo wakaenda na walinzi ili
tuone kama Eliya atakuja kumwokoa.’’ kulilinda kaburi kwa uthabiti, wakatia mhuri
50Yesu alipolia tena kwa sauti kuu, akakata kwenye lile jiwe na kuweka ulinzi.
roho.
51Wakati huo huo pazia la hekalu Yesu Afufuka
likachanika vipande viwili, kuanzia juu hadi
chini. Dunia ikatetemeka na miamba ikapasuka. 28 Baada ya Sabato, alfajiri mapema siku
ya kwanza ya juma, Maria Magdalene
52Makaburi yakafunguka na miili ya watakatifu na yule Maria mwingine walikwenda kulitazama
waliokuwa wamekufa ikafufuka. 53Wakatoka kaburi.
makaburini na baada ya Yesu kufufuka waliingia 2Ghafula pakawa na tetemeko kubwa la

kwenye Mji Mtakatifu na kuwatokea watu wengi. ardhi, kwa sababu malaika wa Bwana alishuka
54Basi yule jemadari na wale waliokuwa kutoka mbinguni akaenda penye kaburi
pamoja naye wakimlinda Yesu walipoona lile akalivingirisha lile jiwe na kulikalia. 3Sura ya
tetemeko na yale yote yaliyokuwa yametukia, huyo malaika ilikuwa kama umeme na mavazi
wakaogopa wakasema, “Hakika huyu alikuwa ni yake yalikuwa meupe kama theluji. 4Wale
Mwana wa Mungu!’’ walinzi wa kaburi walimwogopa sana,
55Walikuwako wanawake huko, wakiangalia wakatetemeka hata wakawa kama wafu.
kwa mbali. Hawa walikuwa wamemfuata Yesu 5Yule malaika akawaambia wale wanawake,

tangu Galilaya ili kushughulika na mahitaji yake. “Msiogope.kwa maana ninajua kuwa
56Miongoni mwao walikuwapo Maria Magdalena, mnamtafuta Yesu aliyesulibiwa. Hayupo hapa,
6

Maria mama yake Yakobo na Yosefu na mama kwa kuwa amefufuka, kama vile alivyosema.
yao wana wa Zebedayo. Njoni mpatazame mahali alipokuwa amelazwa.
7Kisha nendeni upesi mkawaambie wanafunzi

Maziko Ya Yesu Wake kwamba, ‘Amefufuka kutoka kwa wafu,


57Ilipofika jioni, alifika mtu mmoja tajiri naye awatangulia kwenda Galilaya. Huko ndiko
kutoka Arimathea aitwaye Yosefu, ambaye pia mtakakomwona. Sasa nimekwisha kuwaambia.”
alikuwa mwanafunzi wa Yesu. 58Akamwendea 8Hivyo wale wanawake wakaondoka pale

Pilato, kumwomba mwili wa Yesu. Pilato kaburini, wakiwa wamejawa na hofu lakini
akaamuru apewe. 59Yosefu akauchukua mwili wenye furaha nyingi, wakaenda mbio ili
wa Yesu, akauviringishia nguo ya kitani safi kuwaeleza wanafunzi Wake habari hizo.
nyeupe 60na kuuzika kwenye kaburi lake 9Ghafula Yesu akakutana nao, akasema,

mwenyewe jipya alilokuwa amelichonga kwenye “Salaam!” Wale wanawake wakamkaribia


mwamba. 61Maria Magdalene na yule Maria wakaishika miguu Yake, wakamwabudu.
mwingine walikuwapo mahali pale, wakiwa 10Ndipo Yesu akawaambia, “Msiogope. Nendeni

wameketi mkabala na kaburi. Kisha mkawaambie ndugu zangu waende Galilaya,


akavingirisha jiwe kubwa mlangoni mwa kaburi ndiko watakakoniona.’’
na akaenda zake.
Taarifa Ya Walinzi

35
MATHAYO
11Wakati wale wanawake wakiwa njiani
wakienda, baadhi ya wale askari waliokuwa
wakilinda kaburi walienda mjini na kuwaeleza
viongozi wa makuhani kila kitu kilichokuwa
kimetukia. 12Baada ya viongozi wa makuhani
kukutana na wazee na kutunga hila, waliwapa
wale askari kiasi kikubwa cha fedha
13wakiwaambia, “Inawapasa mseme,
‘Wanafunzi Wake walikuja wakati wa usiku na
kumwiba sisi tulipokuwa tumelala.’ 14Kama
habari hizi zikimfikia mtawala, sisi
tutamwondolea mashaka nanyi hamtapata tatizo
lo lote. 15Kwa hiyo wale askari wakazipokea hizo
fedha nao wakafanya kama walivyoelekezwa.
Habari hii imeenea miongoni mwa Wayahudi
mpaka leo.

Yesu Awatuma Wanafunzi Wake


16Basi wale wanafunzi kumi na mmoja

wakaenda hadi Galilaya kwenye ule mlima


ambao Yesu alikuwa amewaagiza.
17Walipomwona, wakamwabudu, lakini baadhi

yao wakaona shaka. 18Yesu akawajia na


kusema, “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na
duniani. 19Kwa sababu hii, enendeni
ulimwenguni mkawafanye mataifa yote kuwa
wanafunzi, mkiwabatiza kwa Jina la Baba na la
Mwana na la Roho Mtakatifu, 20nanyi
wafundisheni kuyashika mambo yote
niliyowaamuru ninyi. Hakika Mimi niko pamoja
nanyi sikuzote, hadi mwisho wa nyakati.’’ Amen.

36

You might also like