Professional Documents
Culture Documents
Kiswahili Vii
Kiswahili Vii
OFISI YA RAIS
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA
Shule ya Awali na Msingi Isaiah Samaritan
“Mchepuo wa Kiingereza”
S.L.P: 2919 MBEYA
isaiahsamaritanschools@gmail.com
SIMU: 0756 994 562, 0713 604 889
Tawi la Mbeya
MTIHANI WA MWISHO WA MWEZI DARASA LA SABA-FEBRUARI 2020
SOMO: KISWAHILI
JINA: TAREHE:
MUDA: SAA 1 DAKIKA 30
MAELEKEZO
Mtihani huu una jumla ya maswali 45
Jibu maswali yote kutokana na maelekezo uliyopewa.
SEHEMU A: SARUFI
Chagua jibu sahihi kutoka kwenye machaguo kisha andika herufi ya jibu hilo kwenye
mabano
1. Ungeliniambia mapema nisingekubali uende. Kipi ni kiambishi cha masharti katika sentensi hii:
A. U B. –nge- C. –ngeli- D. Ungeli- E. –ili- [ ]
2. Kinyonga anatembea polepole. Neno lililokolezwa wino na kupigiwa mstari limetumika kama
aina ipi ya maneno?
A. Kitenzi B. Kiwakilishi C. Kivumishi D. Nomino E. Kielezi [ ]
3. Watoto wanapigana. Neno wanapigana lipo katika kauli ipi?
A. Kutendea B. Kutenda C. KutendanaD. Kutendwa E. Kutendewa[ ]
4. Kisawe cha neno werevu ni:
A. Ujinga B. Wema C. Uovu D.Ujasiri E. Ukatili [ ]
5. Viumbe wafuatao wapo kwenye kundi la ndege, ISIPOKUWA:
A.Bundi B.Mwewe C.Nzige D. Njiwa E.Kanga [ ]
6. Kule anakoishi bibi Mwamvita.
A. Ndimo B. Ndiko C. Ndipo D. Ndio E. Ndiyo [ ]
7. Kifaa kinachotumika kuwekea mishale hujulikana kama:
A. Ala B. Jibini C. Pingili D. Mkebe E. Podo [ ]
8. Umoja wa sentensi hii: “ Maji yamemwagika” ni:
A. Ji limemwagika C. Maji imemwagika E. Maji limemwagika [ ]
B. Mmaji umemwagika D. Maji yamemwagika
9. Laiti kama ningejua nisingekuamini. Hii ni aina gani ya sentensi?
A. Shurutia B. Tegemezi C. Changamano D. Sahili E. Ambatano [ ]
10. Naomba nimeze japo moja tu la maji maana nina kiu sana.
A. Fundo B. Tonge C. Futo D. Funda E. Lepe [ ]
11. Neno lipi la Kiswahili lenye maana linaweza kuundwa kwa kuondoa silabi moja katika
neno “birika”?
A. Kabi B. Kiri C. Rika D. Kari E. Baki [ ]
12.Neno mwanafunzi lina silabi ngapi?
A. Tisa B. Nne C. Tano D. Sita E. Saba [ ]
13. laweza kutokea:
A. Yeyote B. Wowote C.Popote D. Lolote E. Lelote [ ]
14.Wewe u mpole. Katika sentensi hii herufi u imetumika kama:
A. Kiunganishi C. Kihusisishi E. Kiwakilishi kimilikishi [ ]
B. Kitenzi kisaidizi D. Kitenzi kishirikishi
15.Neno gari lipo katika ngeli ipi?
A. U-ZI B. A-WA C. LI-YA D. KI-VI E. I-ZI [ ]
16.Mnyama aliyekufa bila kuchinjwa hujulikana kama:
A. Kibudu B. Mzoga C. Marehemu D. Hayati E. Mfu [ ]
17. Mwenge wa Uhuru umewasili kijijini kwetu. Sentensi hii ipo katika wakati gani?
A. Uliopo B. Ujao C. Timilifu D. Ujao E. Mazoea [ ]
18.Bunge ndicho chombo pekee chenye mamlaka ya kutunga na ku sheria.
A. Teuliwa B. Tegua C. Tumbua D. Tetea E. Tengua [ ]
19.Tunacheza mpira. Sentensi hii ipo katika nafsi ipi?
A. Nafsi ya kwanza umoja C. Nafsi ya pili wingi E. Nafsi ya tatu umoja [ ]
B. Nafsi ya tatu wingi D. Nafsi ya kwanza wingi
20.Neno lipi kati ya maneno yafuatayo ni kisawe cha neno aibu?
A. Furaha B. Faragha C. Shauku D. Soni E. Dharau [ ]
SEHEMU C: USHAIRI:
Soma shairi lifuatalo kisha jibu maswali yanayofuata
Maisha yaliyo bora, maneno yatamkika,
Walitaka zetu kura,kapuni wakatuweka,
Twaishi kama chokora, na siku
zinakatika,
Hakuna maisha bora, haya ni bora maisha.
MASWALI
31. Shairi hili linazungumzia nini?
A. Maisha bora C. Amani E.Maneno yatamkika [ ]
B. Upigaji kura D. Maisha yaa gerezani
32. Kila mshororo katika ubeti wa shairi hili una mizani ngapi?
A. 8 B. 4 C. 5 D. 16 E. 12 [ ]
33. Vina vya kati katika ubeti wa pili ni :
A. u B. no C. ngu D. ra E. angu [ ]
34. Maana ya nahau kuweka kapuni kama ilivyotumika katika shairi hapo juu ni:
A. Kusaidia C. Kusahau E. Kusononeka [ ]
B. Kukumbuka D. Kushughulikia
35. Mstari uliokolezwa wino katika kila ubeti wa shairi hili hujulikana kama:
A. Mzani B. Kina C. Kituo D. Mkarara E. Ubeti [ ]
36. Kwa ujumla shairi hili lina jumla ya beti ngapi?
A. Nne B. Sita C. Mbili D. Nane E. Tatu [ ]
SEHEMU D: UTUNGAJI
Sentensi zifuatazo zimechanganywa. Zipange katika mtiririko mzuri kwa kuzipa
herufi A,B,C na D.
37. Kwa mara ya kwanza ulilipotiwa katika jimbo la Wuhan nchini China. [ ]
38.Ungonjwa wa homa ya mafua kali ni miongoni mwa magonjwa hatari zaidi duniani. [ ]
39. Mpaka sasa takribani nchi 30 duniani zimesharipoti kukumbwa na ugonjwa huu. [ ]
MASWALI
41. Mtoto aliyefariki kwa mujibu wa habari hii anaitwa nani?
43. Maneno La hasha! Katika kifungu cha habari hapo juu yametumika kuonesha hali gani?
44. Neno kitinda mimba kama lilivyotumika katika kifungu cha habari hapo juu lina maana gani?