You are on page 1of 101

YALIYOMO

JARIBIO LA 1 ........................................................................................................ 1
JARIBIO LA 2 ........................................................................................................ 4
JARIBIO LA 3 ........................................................................................................ 8
JAIBIO LA 4 ......................................................................................................... 11
JARIBIO LA 5. ..................................................................................................... 14
JARIBIO LA 6 ...................................................................................................... 17
JARIBIO LA 7 ...................................................................................................... 20
JARIBIO LA 8 ...................................................................................................... 24
JARIBIO LA 9 ...................................................................................................... 27
JARIBIO LA 10 .................................................................................................... 29
JARIBIO LA 11 .................................................................................................... 33
JARIBIO LA 12 .................................................................................................... 35
JARIBIO LA 13 .................................................................................................... 39
JARIBIO LA 14 .................................................................................................... 42
JARIBIO LA 15 .................................................................................................... 45
JARIBIO LA 16 .................................................................................................... 49
JARIBIO LA 17 .................................................................................................... 52
JARIBIO LA 18 .................................................................................................... 55
JARIBIO LA 19 .................................................................................................... 57
JARIBIO LA 20 .................................................................................................... 60
JARIBIO LA 21 .................................................................................................... 65
JARIBIO LA 22 ................................................................................................... 68
JARIBIO LA 23 .................................................................................................... 72
JARIBIO LA 24 .................................................................................................... 75
JARIBIO LA 25 .................................................................................................... 77
JARIBIO LA 26 .................................................................................................... 81
JARIOBIO LA 27.................................................................................................. 84
JARIOBIO LA 28.................................................................................................. 87
JARIBIO LA 29 .................................................................................................... 90
JARIBIO LA 30 .................................................................................................... 93
JARIBIO LA 31 .................................................................................................... 96
UHUSIANO ULIOPO KATI YA SEHEMU ZA JICHO NA KAMERA .................. 99
MAJIBU ............................................................................................................. 100

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma i
JARIBIO LA 1
1. Alama ipi kati ya zifuatazo ni alama ya onyo au tahadhari?

(A) (B) (C) (D) (E)


2. Ni sehemu gani ya kiumbe huyo hufanya kazi sawa na ngozi kwa binadamu?

3. ...ni vishipa vidogovidogo ambavyo hupeleka damu kwenye kila seli ya mwili.
(A) aota (B) vena ya mapafu (C) kapilari (D) ateri ya palmonari
4. Moja ya mimea ifuatayo hutunza chakula kwenye majani.
(A) mhindi (B) kitunguu (C) mhogo (D) maharage
5. CO2 + H2O = C6H12O6 + O2. Hii ni fomula ya tendo gani? ______
(A) fotosynthesisi (B) chuma kupata kutu (C) haidrotropizimui
(D) phototropizimu
6. Nyukliasi ya atomi inaundwa na chembechembe zifuatazo:(A) protoni na
nyutroni (B) elektroni na nyutroni (C) elektroni na protoni
(D) elektroni, protoni na nyutroni
7. Volcano hai hutoa kimiminika kizito katika uso wa dunia kiitwacho:
(A) magma (B) lava (C) kreta (D) volcano
8. Moyo umeundwa kwa misuli aina ya ________________________________
(A) misulimsisima (B) misulikunje (C) misulimilia (D) misuliridhia

Koili sekondari koili primary

9. Hii ni transifoma ya aina gani? (A) pozo (B) chocheo (C) ya redio
(D) mkondo geu
10. Mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye figo kwenda kwenye kibofu unaitwa:
(A) aota (B) renali (C) urethra (D) ureta

Sanduku

11. Ni kitendo gani cha ukuaji kilichoonyeshwa na huo mmea ndani ya sanduku?
(A) fotosinthesis (B) haidrotropizimu (C) fototropizimu
(D) jiotrotizimu
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 1
12. Kupiga chafya ni moja kati ya matendo: (A) ya kutoa taka mwili
(B) yasio ya hiari (C) ya hiari (D) ya ugonjwa
13. Myeyuko wa ............................. Hutumika kutambua chakula cha wanga.
(A) ayodini (B) mafuta (C) tindikali (D) nyongo
14. Seli kavu hutoa umeme mkondo ..... (A) mnyoofu (B) geu (C) wima (D) ulalo
15. ................... ni sehemu ya ua ambayo ikikomaa huwa mbegu.
(A) ovari (B) ovuli (C) stigima (D) pistil
16. Kitendo cha chakula kuvunjikavunjika katika mfumo wa mmeng’enyo wa
chakula huiutwa: (A) respiresheni (B) transipioresheni (C) transilokesheni
(D) usanisi nuru
17. Neva inayochukua taarifa kutoka mfumo wa fahamu wa kati na kuzipeleka
kwenye misuli inaitwa neva ............. (A) sensori (B) optiko
(C) mota (D) akustika
18. Ni sehemu ipi ya ua hufanya kazi sawa na uke kwa mnyama?
(A) ovari (B) ovuli (C) stigima (D) kichavulio
19. Unyafuzi ni ugonjwa unaosababishwa na ukosefu wa: (A) mlo kamili
(B) protini (C) vitamini (D) madini
20. Kemikali zinazotengenezwa na chembesahani hufanya kazi sawa kabisa na
vitamin ipi kati ya zifuatazo? (A) vitamin A (B) vitamin B (C) vitamin K
(D) vitamin D
21. Nini kinatokea wakati mtu anapovuta hewa ndani?
(A) daiframu na mbavu hupanda juu (B) daiframu hushuka chini na mbavu
hupanda juu (C) daiframu na mbavu hushuka chini (D daiframu hupanda juu
na mbavu hushuka chini
22. Kundi lipi la vyakula hujenga na kukarabati mwili? (A) chipsi, wali na pilau
(B) pilau, mihogo na ugali (C) maharage, maziwa na samaki (D)
vyakula vyote vya wanga
23. Saidi alifanya jaribio la kutumbukiza kijiti ndani ya glasi yenye maji na
matokeo yakawa kama inavyoonekana katika kielelezo hicho hapo chini.

Unafikiri kitendo cha kijiti hicho kuonekana kama kimepinda ndani ya maji
kinadhihirisha tabia ipi ya mwanga? (A) kusharabiwa (B) kutawanyika katika
rangi saba (C) kuakisiwa (D) kupinda unapotoka midia moja na kuingia
midia nyingine
24. Kiumbe yuipi kati ya wafuatao urutubisho wa mayai hufanyika nje ya mwili?
(A)binadamu (B) ndege (C) panya (D) chura
25. Ipi kati ya zifuatazo ni simboli ya Potasiamu? (A) K (B) P (C) H (D) O
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 2
26. Tafuta ukinzani wa waya ikiwa mkondo wa umeme kwenye sakiti hiyo ni
0.5A. (A) Ohm1 (B) Ohm 6 (C) Ohm 10 (D) Ohm 5
27. Sifa mojawapo inayomuweka popo kuwa katika kundi la mamalia ni:
(A)kutaga mayai (B) kunyonyesha (C)kuruka angani (D) kuwa na meno
28. Seli nyekundu za damu zikifa hugeuzwa na ini kuwa: (A) chembe za mifupa
(B)ute wa damu (C)pigmenti ya nyongo (D) ute wa mifupa
29. Mimea jamii ya mikunde ina vinundu ambavyo hubadili hewa ya naitrojeni
kuwa _________ (A) Naitreti (B) Amoniamu (C) salfeti (D) urea
30. Virusi vya UKIMWI vinapoingia mwilini hushambulia ________________
(A) seli nyekundu za damu (B) seli nyeupe za damu (C) misuli ya mwili
(D) ute wa damu
31. Ni sehemu gani ya mfumo huo hapo chini inatengeneza asidi ya haidrokloriki
kwaajili ya kuua wadudu wanaoingia na chakula wakati wa kula?
(A) B (B) A (C) D (D) C

32. Lipi kati ya mabadiliko yafuatayo ni badiliko la kiuombo? A. Maji kuwa mvuke
B. Maziwa kuchacha C. Kuchoma karatasi D. Pambano la asidi na besi
33. Ni kifaa gani ambacho kinaweza kutawanya miale ya mwanga katika rangi
saba? (A) darubini (B) tochi (C) glasi ya prizimu (D) mche glasi
34. John alichoma kipande cha chuma jikoni na baada ya muda alipoenda
kukishika tena alikuta chuma chote kimepata joto hata upande ule ambao
haupo jikoni. Unafikiri joto la moto lilisafiri kutoka kwenye ncha iliopo motoni
hadi kufika ncha ya pili ambayo haipo kwenye moto kwa njia gani?
(A) mpitisho (B) msafara (C) mnururisho (D) msuguano
35. Magonjwa yafuatayo husababishwa na virusi isipokuwa ………………..
(A) pepopunda (B) surua (C) tetekuwanga (D) polio
36. Nani anapaswa kutoa huduma ya kwanza? (A) daktari (B) mtu yeyote (C)nesi
(D)mwalimu

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 3
37. Kielelezo kifuatacho kinawakilisha vitu gani? (A) visakuzi vya mtandao (B) vitumi vya
mtandao (C) aina za mtandao (D) injini pekuzi

38. Zifuatazo ni mashine rahisi isipokuwa _______________


(A) Koleo (b) Mkasi (c) Shoka (d) Roda (e) baiskeli
39. Watoto na wazee wanapaswa kula zaidi vyakula vya …………… (A) wanga
(B) vitamini (C) fati (D) protini
40. Ateri zote hubeba damu safi kutoka kwenye moyo na kuipeleka sehemu
mbalimbali za mwili isipokuwa ateri ya ............... (A) palmonari (B) aota
(C) renali (D) kapilari

JAZA NAFASI ZA WAZI PAMOJA NA KUKOKOTOA KWA KUONYESHA NJIA


41. (a) kazi ni nini? Eleza. .......................................................................................
(b) Rehema alitumia kani ya Nyutoni 30 kusogeza jiwe lenye uzito wa Kg 5
umbali wa meta 10. Tafuta kazi aliyofanya
42. Badili 900C kuwa nyuzi za farenheiti. …………………………………………….
43. Wanyama wenye uti wa mgongo wamegawanyika katika makundi mawili
kutokana na joto la miili yao, yataje ……………………….… na ……..…………
44. Tafuta thamani ya X katika kielelezo hicho.

0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 10

KG X
30

45. Mkondo wa umeme wenye ampia 0.8 umepita katika waya wenye ukinzani wa
ohm 30. Tafuta volteji yake.

JARIBIO LA 2
1. Gesi ipi hubadili maji ya chokaa kuwa rangi ya maziwa? A) kabonidayoksaidi
B) naitrojeni C) oksijeni D) haidrojeni E) heliamu
2. Fomula ya kikemikali ya chumvi ya mezani ni: A) H2O B) HCl C) Nacl
D) Co2 E) O2
3. Vitu vyote visivyoonekana vina sifa ya: A) kupitisha mwanga B) kuakisi
mwanga C) kusharabu mwanga D) kupindisha miale ya mwanga
E) kutawanya mwanga
4. Kuna aina mbili za umeme ambazo ni: A) mkondo mnyoofu na umeme tuli
B) sakiti na mkondo geu C) umeme tuli na umeme mwendo D) sola na
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 4
TANESCO E) transifoma na jenereta
5. Ogani zifuatazo huhusika na utoaji taka mwilini: A) mapafu, ngozi, ini na
pua B) ngozi, figo, na mdomo C) pua, mdomo, kibofu na ini D) figo, ngozi,
ini na mapafu E) pua, mdomo, figo na macho
6. Nyota ni tofauti na sayari kwa sababu nyota ______ A) huzunguka jua
B) zipo katika hali ya gesi C) zipo katika hali ya kimiminika
D) huzungukwa na mwezi au miezi E) huakisi mwanga wa jua
7. Matokeo ya mwisho ya myeyuko wa protini ni: A) sukari laini B) glukosi
C) asidi za fati na gliserini D) asidi za amino E) asidi za haidrokloriki
8. Seti yenye mimea ambayo mbegu zake hujisambaza zenyewe ni ipi? A) embe,
mchicha, karoti B) sufi, pamba na chikichi C) kunde, mbaazi na maharage
D) nyanya, mapera na mapapai E) pamba na mhogo
9. Kazi inayofanywa na adapta katika umeme ni: A) kushusha volteji ya umeme
kutoka chanzo hadi umeme unaoruhusiwa na chombo B) kuongeza umeme
C) kukata umeme unapozidi kwenye sakiti D) kuongeza au kupunguza
nguvu ya umeme E) kuhifadhi umeme
10. Kulundikana kwa mafuta ndani ya mishipa husababisha tatizo gani?
A) kiribatumbo B) uchovu na homa C) mwili kukosa nguvu D) damu
kutoganda E) shinikizo la damu
11. Ukitaka kupima mwendokasi wa upepo utatumia kifaa gani?
A) anemometa B) haigrometa C) wind vane D) barometa E) themometa
12. Binadamu anapotembea hatelezi na kuanguka kwa urahisi kwa sababu ya
kani ya: A) mvutano B) umeme C) joto D) msuguano E) mpitisho
13. Kipimajoto kinapoonesha 320F hii hujulikana kama: A) kiwango cha
kuchemka maji B) kiwango cha kuganda maji C) kiwango cha kuyeyusha
barafu D) sentigredi E) haidromita
14. Chumvi ya mezani hupatikana kutokana na maji ya bahari: A) kuvukizwa
B)kutoneshwa C) kuchujwa D) kukaushwa E) kuchemshwa
15. Kati ya wanyama wafuatao ni yupi hana uti wa mgongo?______
A) kenge B) binadamu C) jongoo D) nyani E) samaki
16. Mojawapo ya njia za asili za kuhifadhi chakula ni: A) kusindika, kutia
sukari B) kuweka kwenye makopo au chupa viwandani
C) kukausha, kufukiza moshi, kutia chumvi D) kuweka kwenye jokofu
E) kuchemsha sana
17. Ukosefu wa madini ya chuma mwilini husababisha ugonjwa wa:
A) peragra B) kuhara C) anaemia D) kiseyeye E) goita
18. Myeyuko wa majivu yaliyotokana na majani ya migomba yaliyounguzwa,
unaweza kutumika kama malighafi ya kutengenezea sabuni kwa kuwa una
kemikali aina ya: A) besi B) yuriki C) chumvi D) asidi E) alkoholi
19. Kukua kwa meno na kujenga mifupa ya mwili ni faida zitokanazo na
vitamini: A) K B) B C) C D) D E) A
20. Katika hatua za ukuaji wa mbu ni hatua ipi unayoweza kuiangamiza kwa
mafuta ya taa. A) yai B) kiluwiluwi (lava) C) buu D) mbu
kamili E) pupa
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 5
21. Chakula kinachotengenezwa katika sehemu zote za mmea zenye umbijani
ni: A) protini B) wanga C) chumvichumvi D) fati E) mafuta
22. Uchachu wa chungwa bichi husababishwa na kuwepo kwa kemikali ipi?
A) tindikali B) alkoholi C) nyongo D) besi E) nikotini
23. Kundi la wanyama wanaovuta hewa kwa kutumia ogani aina mbili ni:
A) amfibia B) ndege C) mamalia D) reptilia E) vetebrata
24. Ni ugonjwa gani unaosababisha matatizo kwenye mfumo wa upumuaji?
A) kansa B) pumu C) kiseyeye D) shinikizo la damu E) nimonia
25. Kipi kati ya vitu vifuatavyo hakiruhusu sauti kupita? A. ombwe B. hewa
C. maji D. ubao E. chuma
26. Aina ipi ya mbolea ikitumika mara nyingi husababisha ardhi kutozalisha
mazao? A) samadi B) mboji C) mbolea ya viwandani D) marejea
E) minjingu
27. Kimiminika fulani kilimwagikia kwenye nguo na nguo hiyo ikatoboka.
Kimiminika hicho kinaweza kuwa ni: A) besi B) zebaki C) asidi
D) alkoholi
28. Katika mfumo wa fahamu neva hufanya kazi gani? A) kuchukua na
kupeleka taarifa kwenye mfumo mkuu na sehemu zote za mwili B) kuhisi
maumivu yanayotokea kichwani C) kuwezesha macho kuona vitu
mbalimbali D) kutofautisha makuzi ya mtoto wa kike na wa kiume
E) kuratibu mijongeo ya mwili
29. Kazi mbalimbali za mwili huratibiwa na mifumo miwili. Mifumo hiyo ni:
A) mfumo wa fahamu na mfumo wa homoni B) mfumo wa damu na wa
fahamu C) mfumo wa chakula na wa upumaji D) mfumo wa homoni na wa
uoni E) mfumo wa ubongo na wa misuli
30. Katika mate kuna kimeng’enyo aina ya ptylini. Kazi yake ni kumeng’enya
chakula aina ya:- A) Mafuta B) Protini C) Kabohaidreti D) Vitamini
E) Chumvi.
31. Kwa kawaida mwili wa binadamu una lita zipatazo….. za damu;
A) Sita B) Tano C) Nne D) Nane E) mbili
32.Vifuatavyo ni vitumi ingizi kwenye tarakilishi isipokuwa: (A) kipaza sauti (B) kiteuzi
(C) maikrofoni (D) kibodi E) kiteuzi na kibodi
33. Wanyama kama vile nguruwe na binadamu huitwa:- A) habirora
B) omnivore C) Walanea D) Kanivora E) skavenja.
34. …………inamaanisha sehemu ya kike ya ua A) Staili, stigma na sepali
B) kikonyo na pistil C) sepali na staili D) staili, stigma na ovari
35. Sayari ipi huzunguka jua kuelekea upande tofauti na sayari nyingine?
A) venus B) Pluto C) dunia D) Neptune E) uranusi
36. Jotoridi la 212°F ni sawa na nyusi ngani za sentigredi?
A) 100° C B) 180° C C) 78 °C D) 150° C E) 120° C
37. Sauti husafiri upesi zaidi katika: A) Ombwe B) Udongo C) Chuma
D) Maji E) Gesi

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 6
38. Vyakula vyenye virutubisho vya priotini husaidia:- A) Kuupa mwili joto
B) kuulinda mwili C) Kujenga mwili D) Kuupa mwili nguvu
E) kurutubisha mwili.
39. Wanyama wenye sifa ya kuzaa na kunyonyesha ni wanyama kundi la:-
A) Reptilia B) Amphibia C) Insekta D) mamalia E) Arachnida.
40. Mwanasayansi ni mtaalamu anayefanya udadisi, uchunguzi na
kukusanya data. Ili aweze kufikia uamuzi Fulani. Ili aweze kufanya hivyo
inampasa A) Atumie mlango yote ya fahamu B) awe msomi wa sekondari
C) aweze kuandika kiingereza D) atumie maikroskopu E) atumie
teleskopu.

SEHEMU B: JAZA NAFASI ZILZOACHWA WAZI


41. Mkokoteni ni nyenzo daraja la ngapi? __________________________________
42. Joto la kawaida la mwili wa binadamu ni nyuzi _____ za Fahrenheiti.
43. Ikiwa jitihada (J) ni kg 100 na manufaa ya kimakanika (MK) ni 1.5,
kokotoa mzigo. ______________________________________________________
44. Kazi kubwa ya
sehemu
iliyoneshwa
kwa haruefi R
ni ___________

45. Katika mchoro huu retina imewakilishwa na herufi gani?_______________

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 7
JARIBIO LA 3
SEHEMU A: KUCHAGUA HERUFI YA JIBU
1. Kipi kati ya vifuatavyo huhakikisha kuwa damu inatiririka kwa uelekeo
mmoja? a. Chembelele b. Vali c. Ateri d. Aorta e. Vena
2. Ipi kati ya sifa zifuatazo sio sifa za taswira kwenye kioo bapa?
a. Ukubwa wa taswira unalingana na kitu chenyewe
b. Umbali wa taswira nyuma ya kioo ni sawa na umbali wa kitu mbele ya kioo bapa
c. Taswira hugeuzwa , upande wa kulia kuwa kushoto
d. Taswira kwenye kioo bapa ni wima
e. Taswira inakuwa ndogo kuliko kitu chenyewe mbele ya kioo bapa
3. Mtu anayeota moto hufikiwa na joto kwa njia ya ____________
a. Mnururisho b. Msafara c. Mvuko d. Mpitisho e. Myeyuko
4. Robo tatu ya mwili wa binadamu ni ___________
a. Mifupa b. Nyama c. Damu d. Maji e. Nywele
5. Ipi kati ya zifuatazo sio badiliko la kiumbo? a. Maji kuwa mvuke
b. Mshumaa kuyeyuka c. Maji kuganda d. Asali kuwa pombe
e. Kuyeyuka kwa chumvi kwenye maji
6. Ni sehemu zipi za ua zinaungana na kuwa pistili? a. Stigma na staili
b. Sepali, petali na stigma c. Ovari, stigma na staili d. Filamenti na
kichavua e.Filamenti , kichavua na stigma
7. Kipepeo huharibu mimea akiwa katika hatua gani ya ukuaji?
a. Yai b. Lava c. Tunutu d. Buu e. Kipepeo
8. Yafuatayo ni magonjwa yanayoweza kuambukizwa isipokuwa_______
a. Pumu b. Surua c. Kifua kikuu d. Kifaduro e. Tetekuwanga
9. Yafuatayo ni makundi ya injini pekuzi kwenye intanet isipokuwa: (A) injini ya gari
(B) injini pekuzi mtambazi (C) injini saraka (D) injini pekuzi mseto
10. Mtu asiyeona mbali hushauriwa kutumia lenzi aina gani?
a. Bapa b. Mbinuko c. Mbonyeo d. Duara e. Prizimu
11. Yapi ni matokeo ya mwisho ya uyeyushaji wa chakula cha wanga?
a. Asidi za amino b. Glukosi c. Asidi za fati d. Maltosi e. Gliserini
12. Mtu asiyekula matunda na mboga za majani huweza kupata matatizo gani?
a. Macho na ngozi kuwa njano b. Kupungua uzito wa mwili
c. Kuugua mara kwa mara d. Kuwa na njaa sana e. Kudumaa
13. Wanyama wenye uti wa mgongo wamegawanyika katika makundi matano
ambayo ni:
a. Samaki , reptilia, mamalia, kondoo na ndege b. Amphibia, reptilia,
ndege, samaki na mbuzi c. Mamalia , mbuzi , samaki , reptilia na
ndege d. Reptilia , mamalia , ndege, popo na samaki e. Mamalia,
ndege, samaki , reptilia na amphibia

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 8
14. Mapacha wanaotumia plasenta moja wakati wa ukuaji wao tumboni ni
mapacha wa aina gani? a. Wanaotokana na gameti mbili za kiume
b. Wanaotokana na mayai ya kike c. Wanaotokana na kugawanyika kwa
yai moja lililorutubishwa d. Wanaotokana na mayai mawili
yaliyorutubishwa e. Wanaotokana na ovari mbili kuungana
15. Mojawapo kati ya yafuatayo husaidia kuhifadhi mazingira nayo ni___
a. Kusafisha mashamba kwa kuchoma moto b. Kufuga ngo’mbe kwa wingi
c. Kukata miti kwa ajili ya kuni d. Kubadili mazao ya kupanda
shambani e. Kufyeka misitu ili iote tena
16. Viumbe hai wamegawanyika katika makundi makuu mawili ambayo ni
____ a. Wanyama na mimea b. Wanyama na watu c. Ndege na mimea
d. Wadudu na mimea e. Binadamu na mimea
17. Gesi ya oksijeni huhitajika mwilini kwa ajili ya ____ a. Kuchuja chumvi
chumvi mwilini b. Kulainisha chakula c. Kusafirisha maji
d. Kuondoa uchafu mwilini e. Kuunguza chakula ili kupata nishati
18. Sauti kutoka kwenye chanzo husafiri katika mfumo gani? ________
a. Mitetemo b. Mawimbi c. Joto d. Atomue. Kelele
19. Vijidudu vya malaria huweza kutambuliwa kwa kutumia kifaa kinachoitwa
_____ a. Darubini b. Miwani c. Hadubini d. Kamera e. Periskopu
20. Ni mmea gani kati ya mimea ifuatayo hauwezi hujitengenezea chakula
chake? a. Karoti b. Muwa c. Kabichi d. Uyoga e. Mparachichi
21. Anthony alivuta gogo lenye uzito wa kg 15 kwa saa 3, licha ya kutoka jasho
sana, Anthony hakuweza kulisogeza hata kidogo , Je alifanya kazi kiasi gani ?
a. O jouli b. 15 jouli c. 30 jouli d. 5 jouli e. 45 jouli
22. Chunguza kwa makini mchoro ufuatao . Hii ni aina gani ya sakiti ?

a. Sambamba na mfuatano b. Mfuatano na mfululizo c. Mfululizo


d. Mfuatano e. Sambamba
23. Ugonjwa ambao huweza kudumu mwilini kwa miaka mingi na hatimaye
kuharibu moyo, ubongo, na hata kusababisha kifo ni___________________
a. Kaswende b. Trikomona c. Trakoma d. Kisonono e. Klamedia
24. Ipi kati ya hizi si elementi? a. Hidrojeni b. Kabonidioksidi
c. Aluminiamu d. Magnesiamu e. Oksijeni
25. Ni mnyama gani hujikinga na maadui kwa kuwa na miiba mwilini?
a. Nguruwe pori b. Kinyonga c. Nungunungu d. Panya e. Tumbili
26. Ventrikali za moyo zinaposinyaa_____________
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 9
a. aurikali hutanuka b. aurikali hufunga c. aurikali pia husinyaa
d. Vena na ateri hufunga e. Hakuna kinachotokea
27. Ni Kundi lipi ni zito kuliko yote? a. Kilo moja ya mawe b. Kilo moja ya
mchanga c. Kilo moja ya manyoya d. Kilo moja ya pamba
e. Hakuna kundi zito kuliko mengine
28. Zifuatazo ni njia za kujikinga na VVU isipokuwa ____ a. Kuepukana na
uasherati b. Kunywa dawa ya kuua hivyo vijidudu c.Kuepuka kuwekewa
damu yenye Virusi vya UKIMWI d. kutochangia sindano , nyembe, na
miswaki e. Mama mwenye UKIMWI kutonyonyesha mtoto
29. Virusi vya UKIMWI hushambulia seli gani mwilini?
a. Nyeupe b. Nyekundu c. Plasma d. Sahani e Zote
30. Hatua ya pili katika uchunguzi wa kisayansi ni ___________
a. kubaini tatizo b. Kuandaa dhanio c. Hitimisho
d. Kukusanya data e. Kufanya jaribio
31. Mwangwi ni sauti __________ (a) Iliyosharabiwa b. Iliyopenya
c. Iliyoakisiwa d. Iliyopinda e. Iliyoruka
32. Takamwili zilizochujwa na figo husafirishwa nje ya mwili kupitia mrija
wa____ a.Urethra b. Ureta c. Fallopia d. Umio e. Bronchioli
33. Ni aina ipi kati ya vitamin zifuatazo ambayo hufanya kazi ya kugandisha
damu kwenye jeraha? a. B b. E c. D d. C e. K
34. Unaweza kumsaidia mtu aliyezirai kwa____ a. Kumtingisha kwa nguvu
b. Kumlaza kifudifudi c. Kumpa hewa safi d. Kumbonyeza tumboni polepole
e. Kumwagia maji ya vuguvugu usoni
35. Mche wa sumaku wenye ncha ya KUS na KAS ukining’inizwa hewani ncha
ya KAS itaelekea upande gani?
a.Kusini mwa dunia b. Mashariki mwa dunia c. Kaskazini mwa dunia
d. Magharibi mwa dunia e. Katikati ya dunia
36. Mashine rahisi zimegawanyika katika aina kuu ngapi?
a. Mbili b. Sita c. Nne d. Saba e. Tatu
37. Homoni ya thairoksini haiwezi kuzalishwa mwilini kama hakuna:-
a. Ayani b. Kalsiamu c. Fosforasi d. Madini joto e. Sodiamu
38. Badili fahrenhaiti 98.6 kuwa sentigredi
a. 40 b. 36 c. 32 d. 36.9 e. 37
39. Nyama , samaki, maziwa na mayai ni vyakula ambavyo: ________________
a. Hujenga mwili b. Hukinga mwili dhidi ya magonjwa c. Huupa mwili nguvu
d. Huupa mwili joto d. Huimarisha mifupa
40. Huduma ya kwanza kwa mtu anayetapika sana ni kumpa maji yenye
mchanganyiko wa sukari na _______ a. Maziwa b.Mayai c. Chumvi
d. Ndimu e. Majivu

SEHEMU B: MAJIBU MAFUPI


41. Wenzo daraja la pili ina uwiano wa mwendo dhahiri 16. Ikiwa manufaa ya
kimakanika ya wenzo hii ni 8 . Tafuta ufanisi wa wenzo _____________________

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 10
42. Katika mchoro ufuatao herifu ipi inawakilisha ogani ambayo hupambana
na sumu mwilini ?

43. Kisio la kisayansi kuhusu jambo fulani huitwa____________________


44. Kitendo cha viumbe hai kutengeneza viumbe vingine huitwa_______
45. Alama hii hapa chini katika sakiti huwakilisha kifaa
gani? ___________________________________________________________

JAIBIO LA 4
1. Kitendo cha mizizi ya mmea kukua kwa kufuata kani mvuto ya dunia
huitwa………[ ] (a) Fototropizimu (b) Haidrotropizimu (c)Jiotropizimu
(d) Kemotropizimu (e) Jianinashani
2. Kimeng’enyo kinachotolewa na kuta za tumbo kwa ajili ya kumeng’enya
protini huitwa . [ ] (a) Pepsini (b) Amilesi (c) Traipsini (d) Lipase (e) Insulini
3. Mshipa unaosafirisha damu chafu kutoka kwenye moyo kwenda kwenye
mapafu huitwa [ ] (a) Vena ya palimonari (b) Ateri ya palimonari (c) Vena kava
(d) Aota (e) Ateri ya Renali
4. Hatua gani ya utafiti inathibitisha dhanio/bunio? [ ] (a) Kubainisha tatizo
(b) Kukusanya (c) Kuchambua (d) Jaribio (e) Hitimisho
5. Kipi kati ya vifaa vifuatavyo hakipatikani katika sanduku la huduma ya
kwanza…… [ ] (a) Pamba (b) Mkasi (c) Gravu (d) Rula (e) Ayodini
6. Sehemu ya mbegu ambayo inalinda sehemu za ndani za mbegu huitwa … [ ]
(a) Ganda (b) Kiinitete (c) Ghala (d) Tundu dogo (e) Kianza shina
7. Bayogesi ni mchanganyiko wa aina kuu mbili za gesi ambazo ni
kabonidayoksaidi na … [ ] (a) Oksijeni (b) Haidrojeni (c) Mitheni (d) Salfa
(e) Naitrojeni
8. Homoni inayodhibiti kasi ya kuingiza gesi ya oksijeni kwenye mfumo wa
upumuaji inaitwa: (a) Adrenali (b) Thairoksini (c) Insulini (d) Parathormoni
(e) Testosteroni
9. Badili 200 0C kuwa nyuzi za Fareinhaiti. [ ]
(a) 580F (b) 720F (c) 640F (d) 480F (e) 680F
10. Katika mchoro ufuatao wa ua, sehemu inayopokea poleni inaoneshwa kwa
herufi gani? (a) B [ (b) C (c) A (d) E (e) D

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 11
11. Mtu huthibitika kuwa ana UKIMWI iwapo kiwango cha seli za CD4 ni
……………………. kwa kila mililita [ ] (a) 200 CD4 (b) 400 CD4 (c) 1,000 CD4
(d) 500 CD4 (e) 1500 CD4
12. Ugonjwa wa Hemofilia husababishwa na upungufu wa …………………. [ ]
(a) Vitamini C (b) Vitamini K (c) Vitamini A (d) Kalisiamu (e) Ayani
13. Sauti iliyoakisiwa huitwa …………………………………………………..…. [ ]
(a) Mwale (b) Mitetemo (c) Mwangwi (d) Kelele (e) Kupinda kwa sauti
14. Chunguza mlinganyo ufuatao, kisha taja jina la zao lililooneshwa kwa herufi
X. CO2 + H2O + Mwanga wa jua + Chanikiwiti Wanga + X. [ ]
(a) Naitrojeni (b) Kabonimonoksaidi (c) Haidrojeni (d) Klorini (e) Oksijeni
15. Moja kati ya madini yafuatayo huhitajika kutengeneza damu …………. [ ]
(a) Ca (b) K (c) Mg (d) Fe (e) Hg
16. Chunguza mchoro ufuatao wa via vya uzazi vya kike. Tendo la urutubisho
hutokea katika sehemu iliyooneshwa kwa herufi ………………………………... [ ]
(a) D (b) A (c) B (d) C (e) E
A B

D E
C
17. Lipi kati ya magonjwa yafuatayo halisababishwi na Bakteria? [ ]
(a) Polio (b) Dondakoo (c) Pepopunda (d) Trakoma (e) Kifua kikuu
18. Kifaa chenye waya mwembamba kinacholinda vifaa vya umeme dhidi ya shoti
ya umemehuitwa ………. [ ]
(a) Waya wa Ethi (b) Kikinga radi (c) Fyuzi (d) Rektifaya (e) Transifoma
46. Meno, patasi, shoka, kisu na kipande cha mti ni baadhi ya mashine rahisi katika kundi la:
(A) kabari (B) roda (C) wenzo (D) mteremko
20. Kipi kati ya vifaa vifuatavyo kinatumia sumaku.? [ ]
(a) Pasi ya umeme (b) Jiko la umeme (c) Taa ya umeme (d) Kengele ya umeme
(e) Gita la umeme
21. Uhusiano uliopo baina ya viumbe hai na mazingira yao huitwa ………… [ ]
(a) Unajimu (b) Fizikia (c) Mahusiano (d) Kutegemeana (e) Ikolojia
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 12
22. Ipi kati ya sifa zifuatazo si sifa ya Insekta? ………………………………... [ ]
(a) Wana jozi tatu za mabawa (b) Wana sehemu kuu tatu za mwili (c) Wana jozi
tatu za miguu (d) Wanataga mayai (e) Wana jozi moja ya vipapasio
23. Mbadilishano wa hewa katika mwili wa binadamu hutokea kwenye …… [ ]
(a) Pua (b) Trakea (c) Alveoli (d) Brokasi (e) Bronchioli
24. Aina ya lenzi ambavyo hutawanya miale ya mwanga huitwa …………… [ ]
(a) Mbinuko (b) Mbonyeo (c) Bapa (d) Prizimu mstatili (e) Prizimu pembetatu
25. Ugonjwa wa kurithi unaosababisha umbo lisilo la kawaida la seli nyekundu
za damu unaitwa ………………….....…… [ ] (a) Albino (b) Pumu (c) Saratani
(d) Selimundu (e) Haemofilia
26. Sepetu ni daraja gani la nyenzo? [ ] (a) Kwanza (b) pili (c)Tatu (d)Nne (e) Tano
27. Neva zinazosafirisha taarifa kutoka kwenye sikio kwenda kwenye ubongo
huitwa…………………………………. [ ] (a) Neva za optiki (b) Neva za sikio
(c) Seli onji (d) Neva ya Renali (e) Neva za Akaustika
28. Tafuta umbali wa uelekeo wa kani ikiwa kazi iliyofanyika ni Joule 48 na kani
iliyotumika ni Kg 0.6 . [ ] (a) sm 8 (b) m 8 (c) m 28.8 (d) m 80 (e) sm 80
29. Upungufu wa gesi ya oksijeni kwenye ubongo husababisha ……………… [ ]
(a) Anemia (b) Haemofilia (c) Pumu (d) Kuzimia (e) Uchizi
30. Ipi kati ya njia zifuatazo sio njia ya kuwasilisha data? [ ] (a) Kikokotoo
(b) Jedwali (c) Grafu kwa mhimili (d) Pai chati (e) Grafu kwa mstari
31. Sehemu gani ya damu ambayo husambaza virutubisho vya chakula kwenye
sehemu mbalimbali za mwili?…………….. [ ] (a) Seli hai nyekundu (b) Seli hai
nyeupe (c) Plazima (d) Seli hai sahani (e) Vila
32. Tabia ya kifaa cha umeme kupinga kutiririka kwa mkondo wa umeme huitwa
…… [ ] (a) Mkondo (b) Volteji (c) Ukinzani (d) Kupinga (e) Kikinza
33. Kuna njia ngapi kuu za uzazi wa mpango? [ ] (a) 2 (b) 3 (c) 4 (d) 1 (e) 5
34. Njia ya uhakika zaidi ya kujikinga dhidi ya V.V.U ni ……………………. [ ]
(a) Kutumia kondomu (b) Kutofanya kabisa ngono (c) Kuvaa gravu
(d) Kutokuchangia vitu vyenye ncha kali (e) Kuacha kunyonyesha
35. Kifuko cha misuli kinachohifadhi mkojo kwa muda huitwa ……….… … [ ]
(a) Figo (b) Kifuko cha nyongo (c) Alveoli (d) Kibofu cha mkojo (e) Tumbo
36. Mlinganyo wa TINDIKALI + NYONGO CHUMVI + MAJI
hujulikana kama….. (a) Mbadilishano (b) Mvujiko (c) Mbatilisho
(d) Usanisinuru (e) Difyusheni
37. Tafuta ukubwa wa pembe akisi katika mchoro ufuatao . [ ]

(a) 740 (b) 640 (c) 470 (d) 270 (e) 370
38. Kuna jumla ya mifupa mingapi katika kiunzik cha binadamu? [ ]
(a) 58 (b) 22 (c) 33 (d) 206 (e) 48
39. Kitendo cha kubadilisha maji kuwa mvuke huitwa …………………….. [ ]
(a) Kugandisha (b) Kutonesha (c) Kuyeyusha (d) Kuvukiza (e) Mpambano
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 13
40. Misuli ya kwenye moyo wa binadamu huitwa ……………….………… [ ]
(a) Misuli ridhia (b) Misuli milia (c) Aota (d) Misuli ya palimonari (e) Ligamenti

SEHEMU B JAZA NAFASI ZA WAZI


41. Umri kamili wa mimba kwa binadamu tangu kutungwa hadi kuzaa ni siku
_____________________________________________________________________
42. Tafuta mkondo wa umeme katika sakiti ifuatayo :-

43. Tafuta ufanisi wa mashine ikiwa manufaa ya kimakenika ni 5 na uwiano wa


mwendo dhahiri ni 10 ______________________________________________________
44. Tafuta thamani ya X katika mchoro huu.

45. Ubongo wa nyuma huitwa_______________________________________________

JARIBIO LA 5.
1. Moja ya sifa zifuatazo humtambulisha Popo kama MAMALIA
(a) Kuruka (b) Kuishi kwenye paa za nyumba (c) Kupaa angani (d) Kunyonyesha ( )
2. Neno la kisayansi linalosimama badala ya kufanya kazi ni (a) Nishati
(b) Nguvu (c) Kani (d) Msukumo ( )
3. Sehemu kubwa ya miili ya wanyama waliopo katika kundi la mamalia ni
(a) Mifupa (b) Nyama (c) Maji (d) Damu ( )
4. Kamera hufanya kazi sawa na kiungo gani katika mwili wa Binadamu?
(a) Figo (b) Ini (c) Moyo (d) Jicho ( )
5. Katika mchoro huu, sehemu “B” hujulikana kama
A
C
B

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 14
(a) Mzigo (b) Egemeo (c) Jitihada (d) Mashine ( )
6. Mchujo wa mkojo hufanyika katika _______ (a) kibofu (b) Urethra
(c) Figo (d) Mrija wa falopia ( )
7. Mifupa ya meno huimarika kwa kula vyakula vyenye madini ya aina ya _
(a) Kalisiamu (b) Sodium (c) Chuma (d) Kloraidi ( )
8. Kipi ni kizio cha uzito? (a) Sm (b) Kg (c) C° (d) Newto ( )
9. Joto husafiri kwenye chuma kwa njia ya ________ (a) Mpitisho
(b) Msafara (c) Mnururisho (d) Mstari ( )
10. katika mbegu kinachoanza kuota ni ______ (a) Tunda (b) Mzizi
(c) Majani (d) Matawi
11. Sauti inayoakisiwa huitwa ____ (a) Mwangwi (b) Trakoma (c) Mtetemo
(d) Kani ( )
12. Mayai ya kike hutengenezwa kwenye (a)Falopia (b) Uterasi (c) Seviksi
(d) Ovari( )
13. Virusi vya UKIMWI (VVU) huharibu kinga ya mwili kwa kushambulia?
(a) Seli nyekundu za damu (b) Ubongo (c) Seli nyeupe za damu (d) Plazima ( )
14. Vitu vifuatavyo hutoa mwanga wa asili (a) Jua na Nyota (b) Umeme na Jua
(c) Umeme na Nyota (d) Mwezi na kimondo ( )
15. Zifuatazo ni aina za utapiamlo isipokuwa (a) Unyafuzi
(b) Kiribatumbo (c) Surua (d) Kwashakoo ( )
16. Hali tatu za maada ni______ (a) Yabisi,Gesi na Kimiminika (b) Maji, Gesi na
Kimiminika (c) Yabisi, Kimiminika na Maji (d) Yabisi,Mafuta na Kimiminika
17. Sehemu zinazohathirika katika mwili kutokana na uvutaji wa sigara ni
_____ (a) Figo (b) Ini (c) Mifupa (d) Mapafu ( )
18. _____ ni misuli inayotenganisha kifua na tumbo (a) Ateri (b) Kiwambo
(c) Mbavu (d)Kapilari ( )
19. Samaki huvuta hewa kwa kutumia ____ (a) pua (b) Matammvua
(c) Mdomo (d) Magamba ( )
20. Chanzo cha nishati zote duniani ni _____(a) Jua (b) Nyota (c) Mwezi
(d) Vimondo
21. Usambazaji wa chakula mwilini hufanywa na (a) Misuli (b) Neva
(c) Damu (d) Maji
22. Matatizo ya kutoona mbali hutatuliwa kwa kuvaa miwani yenye lenzi ya _
(a) Mbonyeo (b) Retina (c) Mbinuko (d) Fokasi( )
23. Sumaku huvuta vitu vyenye asili ya ____(a) Plastiki (b) Mbao
(c) Mfupa (d) Chuma
24. Hatua ya mwisho katika kukua kuelekea utu uzima _____ (a) Balehe
(b) Ujana (c) Hedhi (d) Utukutu ( )
25. Moto huwaka vizuri kama kuna __________________ (a) Nitrojeni (b) Neoni
(c) Kabonodioksaidi (d) Oksijeni ( )
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 15
26. Damu huzunguka kutoka kwenye_______kwenda katika sehemu za
mwili.(a)Mapafu (b)Figo (c)Moyo (d)Utumbo ( )
27. Mzunguko kamili wa umeme unaitwa_______ (a)Waya (b)Sakiti (c)Betri
(d)Soketi
28. Kugomboa chumvi katika maji ni lazima _______ (a)Uyachemshe
(b)Uyagandishe (c)Uyachuje (d)Uyapoze( )
29. Egemeo linapokuwa katikati ya mzigo na jitihada huonyesha nyenzo daraja
la _____ (a)Nne (b)Tatu (c)Pili (d)Kwanza ( )
30. Sehemu za ubongo ambazo ni kitovu cha mapigo ya moyo na pia upumuaji
ni____ (a)Ugwe mgongo (b)Medula Oblangata (c)Ubongo wa kati na mbele
(d)Serebramu.
31. Nyuzi za sentigredi 75° ni sawa na nyuzi ngapi za farenheiti? (a)212°
(b)180° (c)167° (d)77° ( )
32. Ugonjwa upi kati ya haya hauambukizi? (a)Seli mundu (b)Surua (c)Ukoma
(d)kifua kikuu ( )
33. Hatua ya pili ya ukuaji wa panzi huitwa__(a)Buu (b)Insekta kamili (c)Yai
(d)Tunutu

34. Tafuta thamani ya X ________________________ = Kg ………………


Sm 4 Sm 8

Kg 40 Kg x

(a) 60 (b) 80 (c) 20 (d) 2 (e) 12


35. Binadamu hurefuka sana kutokana na wingi wa homoni za tezi_____
(a)Kongosho (b)Thairoidi (c)Adrenali (d)Pituitari( )
36. Kazi ya uterasi ni kutunza _ (a)Homoni (b)Ovari (c)Mimba (d)Manii ( )
37. Badiliko lipi kati ya mabadiliko yafuatayo ni ya kiumbo?____ (a)Chuma
kupata kutu (b)Mshumaa kuyeyuka (c)Mafuta ya taa kuwaka (d)Matunda
kuoza ( )
38. Kitendo cha mmea kujitengenezea chakuli huitwa ______ (a)Usanisi
(b)Stomata (c)Mizizi (d)Uzalishaji chakula ( )
39. Matokeo ya dunia kujizungusha kwenye mhimili wake tunapata _____
(a)Majira ya mwaka (b)Mchana (c)Usiku (d)Usiku na mchana ( )
40. Mwanga ni mkusanyiko wa rangi__ (a) Tatu (b)Nne (c)Saba (d)Mbili ( )

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 16
SEHEMU B: JAZA NAFASI ZILIZO ACHWA WAZI.
41. Ugonjwa unaoshambulia kichwa na kung’oa nywele huitwa______________
42. Taja aina ya roda ambayo thamani ya mzigo ni sawa na thamani ya
jitihada. ______________________________________________________________
43.Ikiwa uwiano wa mwendo dhahiri wa mashine (wenzo) hapa chini ni 5/6, Tafuta ufanisi
wake.

44.Moto unaotokana na hitilafu ya umeme ni moto daraja la ______________________


45.Ni aina gani ya gesi hujazwa kwenye mitungi ya kuzimia moto (fire extingwisher)? ___

JARIBIO LA 6
1. Kitendo cha mizizi kufyonza maji na madini kutoka katika udongo huitwa:
A. uvukizaji B. upumuaji C. osimosisi D. kusharabu E. usanisi nuru
2. Katika mfumo wa mifupa maungio hushikiliwa na:
A. koromeo B. gegedu C. kano D. nyuzi E. neva
3. Ipi kati ya ogani zifuatazo haipatikani katika mfumo wa mmeng’enyo wa
chakula? A. koromeo B. utumbo mwembamba C. kongosho D. Ini E. figo
4. Ugonjwa wa kifua kikuu (TB) huathiri zaidi ogani gani ya mwili?
A. mapafu B. figo C. ngozi D. pua E. utumbo
5. Chakula kinapokuwa mdomoni huchanganyikana na kimeng’enya cha
ptylin ambacho huvunjavunja vyakula vya: A. protini B. wanga C. vitamin
D. mafuta E. chumvi
6. Kuganda kwa damu husababishwa na kipi kati ya vifuatavyo?
A. fibrinojeni B. madini chuma C. plasma D. seli nyeupe za damu
E. haemoglobini
7. Mtu ambaye huweza kupokea damu kutoka katika makundi yote ya damu
ni Yule mwenye damu kundi: A. O B. AB C. B D. A E. A na B
8. Kipimo cha Fareniheiti huanzia namba ngapi? A. O0F B. 860F C. 2120F
D.320F E.120F
9. Vimiminika vyenye uwezo wa kutanuka pindi joto linapoongezeka na
kusinyaa pindi joto linapopungua hutumika katika kutengeneza:
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 17
A. haidromita B. kipima joto(themomita) C. kipima mvua D. haigromita
E. baromita
10. Ni aina ipi ya vijidudu husababisha ugonjwa wa kipindupindu?
A. protozoa B. bacteria C. amoeba D. plasimodiamu E. virusi
11. Kemikali inayotumika kutibu maji ya kunywa huitwa:
A. klorini B. kalisi C. kabonidaiyoksaidi D. florin E. ayodini
12. Ni yapi kati ya maelezo yafuatayo NI KWELI kuhusu mimea jamii ya
kunde? A. ina sehemu kuu mbili B. ni mimea isiyo na maua C. huzaliana
kwa kugawanyika D. huongeza rutuba katika udongo E. mbegu zake
husambazwa na maji
13. Ni sehemu ipi ya damu ambayo haemoglobini hupatikana?
A. fibrinojeni B. chembe sahani C. plazma D. seli hai nyeupe za damu
E. seli hai nyekundu za damu
14. Unaweza kuwatambua wanyama wanaokula nyama kwa kuangalia:
A. meno yao B. macho yao C. masikio yao D. sauti zao E. matumbo yao
15. Mwale wa mwanga unapotua kwenye uso angavu hugonga na kurudi,
kitendo hiki huitwa: A. kusharabu B. kupenya C. kuakisi D. kuvunja
E. kupinda
16. Sehemu ya sikio la binadamu inayokusanya mawimbi ya sauti inaitwa:
A. neva ya sikio B. koklea C. ngoma ya sikio D. mrija E. pina
17. Dalili kuu ya ujauzito kwa binadamu ni:
A. kutapika B. matiti kutanuka C. kulala muda wote D. kukoma hedhi
E.kuhisi kichefuchefu
18. Chakula kwa ajili ya watoto kinatakiwa kiwe na kiwango cha _____ ili
kusaidia kuimarisha meno na mifupa yao. A. protini B. kabohaidreti
C. madini chumvi D. vitamin E. mafuta
19. Ni lenzi gani hutumika kukuza vitu? A. duara B. mbonyeo C. mbinuko
D. bapa E. maalumu
20. Badiliko la maada linalopelekea badiliko la uzito wa maada huitwa:
A. badiliko la kiumbo B. badiliko la muda C. badiliko rejeshi D. badiliko la
haraka E. badiliko la kikemikali
21. Gesi inayotumika kuhifadhia vinywaji kwenye chupa kama soda ni
A. oksijeni B. kabonidaioksaidi C. methane D.haidrojeni E. naitrojeni
22. Sababu ya hewa ya kabonidaiyoksaidi kutumika kuzima moto ni:
A. husaidia vitu kuungua B. haina harufu C. hubadili maji magumu kuwa
kama maziwa D. hairuhusu kuungua E. inaweza kulipuka
23. Wakati wa uchavushaji chavua husafiri kuelekea kwenye:
A. ovari B. antha C. stigma D. staili E. petali
24. Karatasi nyekundu ya litmasi hutumika kutambua:
A. besi B. chumvi C. pigmenti za ini D. sukari E. asidi
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 18
25. Maelezo yapi ni sahihi kuhusu Ampia? A. ni kifaa cha kupimia mkondo
B. ni kizio cha mkondo wa umeme C. ni kifaa cha kipimia ukinzani D. ni
kifaa cha kupima nguvu ya umeme E. hupimwa kwa kutumia voltimita
26. Ugumba kwa binadamu unaweza kusababishwa na:
A. kula kupita kiasi B. utapiamlo C. kukosa vitamin C D. magonjwa ya
zinaa E. UKIMWI
27. Vifuatavyo hupatikana katika seli ya mnyama na seli ya mmea isipokuwa:
A. nyukliasi B. chembe umbijani C. vakuli D. uteseli E. saitoplazimu
28. Mzigo ulipandishwa mita 8 baada ya mkono wa jitihada kuvutwa mita 24
kuelekea chini, uwiano wa mwendo dhahiri ni: A. 8 B. 4 C. 2 D. 10
E. 3
29. Transipiresheni katika mimea ni muhimu ili kusaidia: A. kuupoza mmea
B. kuondoa kiasi cha maji kisichohitajika C. kukua vizuri D. kupunguza
matumizi ya maji E. kubeba cha`kula cha mmea
30. Ni mlango upi wa fahamu utautumia kutofautisha joto na baridi?
A. ngozi B. jicho C. sikio D. pua E. ulimi
31. Usemi upi sio sahihi kuhusu mishipa ya ateri?
A. hutoa damu kutoka kwenye moyo B. ina ukuta mnene
C. ina msukumo mkubwa wa damu D. inachukua damu yenye oksijeni
nyingi E. ateri nyingi zina vali
32. Pembe akisi imeonyeshwa kwa herufi ipi??
G
F E

B C
A D

33. Kuta za majengo ya mikutano na studio zimewekwa vitu laini ili kuweza:
A. kusharabu sauti B. kuakisi sauti C. kupindisha sauti D. kusambaza
sauti E. kuzuia sauti
34. Ni gesi gani huhitajika na mmea ili kuweza kutengeneza chakula?
A. kabonidaiyoksaidi B. oksijeni C. naitrojeni D. haidrojeni E. salfu
35. Njia bora ya kujikinga na virusi vya UKIMWI na UKIMWI ni:
A. kuepuka kuvaliana nguo B. kuepuka ngono isiyo salama C. kuepuka
kuongea na waathirika D. kuhudhuria kliniki E. kula mlo kamili
36. Joto kutoka katika jua huweza kuufikia uso wa dunia kwa njia ya:
A. mpitisho B. mgandamizo C. mvukizo D. mnururisho E. mvutano
37. Kati ya vifuatavyo kipi huathiri rangi ya mkojo?
A. maziwa B. damu C. uzito wa mwili D. msongo wa mawazo E. dawa
38. Faida kuu ya uzazi wa mpango ni:
A. kuongeza idadi ya watoto B. kuwa na uwezo wa kutoa huduma muhimu

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 19
C. kuepuka matatizo D. kuwapa watoto elimu E. kupata uwezo wa
kujenga nyumba ya kisasa
39. Ni sehemu ipi ya ubongo huratibu kuona, kusikia na kunusa?
A. ubongo wa mbele B. uti wa mgongo C. ugwe mgongo D. medulla
oblongata E. neva
40. Makazi ya chura ni: A. majini B. jangwani C. nchi kavu D. majini na nchi
kavu E. baharini
SEHEMU B: JAZA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI
41. Tafuta thamani ya X;

42. Kuta za ndani za themosi zinapakwa rangi ya fedha ili kuzuia kupotea
kwa joto kwa njia ipi? _________________________________________________
43. Retina katika jicho ni sawa na kifaa gani kwenye kamera? _______________
44. Stomata ni muhimu kwa mimea kama ___________ ilivyo muhimu kwa
panzi.
45. _______ ni waya mwembamba wa kulinda chombo cha umeme kisiunguzwe
na umeme.

JARIBIO LA 7
1. Ugonjwa upi kati ya magonjwa yafuatayo si ugonjwa wa ngono? [ ]
(a) Kaswende (b) Trakoma (c) Kisonono (d) V.V.U / UKIMWI (e) Trikomona
2. Ogani inayozalisha kimeny’enya cha fati na mafuta huitwa ……………….. [ ]
(a) ini - (b) figo (c) kongosho (d) ubongo (e) tumbo
3. Mshipa unaosafirisha damu chafu kwenda kwenye mapafu huitwa ……… [ ]
(a) ateri (b) vena kava (c) vena (d) ateri ya polimonari (e) vena ya polimonari
4. Upi ni mpangilio sahihi wa uandishi wa ripoti ya Jaribio. [ ]
(a) Njia, Vifaa, Kusudi, Matokeao na Hitimisho (b) Njia, Vifaa, Kusudi,
Hitimisho na matokeo (c) Kusudi, Njia, Vifaa, Matokeo na Hitimisho
(d) Kusudi, Vifaa, Njia, Matokeo na Hitimisho
5. Hatua ya kwanza ya kumhudumia majeruhi wa ajari ni [ ]
(a) Kutibia kwenye jeraha (b) Mpeleke majeruhi hospitali (c) Mtoe majeruhi
katika eneo la hatari (d) Kumpatia mchanganyiko wa sukari na chumvi
(e) Kuita gari la wagonjwa
6. Sehemu ipi ya ua inayokuwa na kuwa mbegu baada ya uchavushaji?. [ ]
(a) Ovyuli (b) Ovari (c) Stigma (d) Petali (e) Sepali
7. Gesi gani inayounda bayogesi kwa kiwango kikubwa? [ ]
(a) Kabonidayoksaidi (b) mvuke (c) Naitrojeni (d) Oksijeni (e) Mitheni
8. Homoni inayodhibiti mmeng’enyo wa chakula huitwa………………. [ ]
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 20
(a) Insulini (b) Parathormoni (c) Adrenalini (d) Thairoksini (e) Oksizitesini
9. Joto husafiri kwa njia gani katika maada yenye hali yabisi?. [ ]
(a) Transilokasheni (b) Msafara (c) Mnururisho (d) Mpitisho
(e) Transifomesheni
10. Sehemu inayolinda ua kabla halijachanua huitwa ……………………… [ ]
(a) Petali (b) Sepali (c) ovari (d) staili (e) kikonyoa
11. Kipimio kinachothibitisha kuwa damu ina V.V.U huitwa…… [ ] (a) Kipimio
cha damu (b) Western blot (c) Kipimio cha mkojo (d) Kipimio cha
malaria (e) Kipimio cha haraka
12. Upungufu wa vitamin inayozalishwa katika ngozi kwa msaada wa mwanga
wa jua husababisha ugonjwa wa ……………………. [ ]
(a) Kiseyeye (b) Beriberi (c) Pallagra (d) Matege (e) Ukavu macho
13. Paneli za jua hubadilisha nishati ya mwanga kuwa aina gani ya nishati? [ ]
(a) Umeme (b) Sauti (c) Elektroni (d) Mwanga (e) Joto
14. Kitendo cha kusafirisha chakula kutoka kwenye majani kwenda kuhifadhiwa
huitwa [ ] (a) Respiresheni (b) Transipiresheni (c) Transilokesheni
(d) Fotosinthesisi (e) Kuota kwa mbegu
15. Sehemu ipi katika kielelezo kifuatacho inayohusika katika mfumo wa homoni
na mmeng’enyo wa chakula? [ ] (a) A (b) B (c) C (d) D (e) E

16. Tendo la urutubisho hufanyika katika sehemu gani ya via za uzazi wa


mwanamke? (a) Ovari (b) Uterasi (c) Selviksi (d) Kuta za Uterasi
(e) Mirija ya falopia
17. Haemofilia ni ugonjwa unaosababishwa na upungufu wa ……………… [ ]
(a) Vitamini B1 (b) Vitamini B2 (c) Vitamini K (d) Vitamini C (e) Vitamini B12
18. Kifaa kinachotumika kupima mkondo wa umeme katika sakiti huitwa … [ ]
(a) Voltimita (b) Amita (c) Galvanomita (d) Ohmmita (e) Ampia
19. Sehemu ya seli inayotawala shughuli zote za seli ni ……. [ ] (a) Nyukliasi
(b) Kiwambo cha seli (c) Ukuta wa seli (d) Saitoplazimu (e) Kloroplasti
20. Kuna maumbo mangapi ya sumaku? [ ] (a) 3 (b) 6 (c) 4 (d) 5 (e) 2
21. Moja kati ya shughuli zifuatazo haisaidii kutunza mazingira yetu, nayo ni
…… [ ] (a) Kupanda miti (b) Kujenga uzio (c) Kulima kwa kufuata kontua
(d) Matumizi mrudio wa takataka (e) kukata miti
22. Lava wa kipepeo hujulikana kama……………….. [ ]
(a) Funza (b) Kiluwiluwi (c) Pupa (d) Kiwavi (e) Mdudu kamili
23. Sehemu ya mfumo wa upumuaji ambayo mbadilishano wa gesi hutokea
huitwa? [ ] (a) Trakea au umio wa hewa (b) Pua (c) Viriba hewa
(d) Bronchioli (e) Bronkasi
24. Lenzi inayokusanya miale ya mwanga huitwa … [ ] (a) Lenzi mbinuko
(b) Lenzi mbonyeo (c) Kioo bapa (d) Kioo mbinuko (e) Kioo mbonyeo
25. Ugonjwa unaosababishwa na bakteria aina ya basili huitwa ………….. [ ]
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 21
(a) Kifua kikuu (b) Kichomi (c) Pumu (d) Kansa (e) Kuhara
26. Mkono wa binadamu ni nyenzo daraja la ngapi? [ ]
(a) Kwanza (b) Tatu (c) Nne (d) Pili (e) Tano
27. Sehemu iliyooneshwa kwa herufi K huitwa ……………………..………. [ ]

(a) Aksoni (b) Saitoplazimu (c) Mafuta (d) Dendraiti (e) Nyukliasi
28. Juma alitumia kani ya N.20 kufanya kazi ya joule 50. Tafuta umbali wa
uelekeo wa kani? (a) m 2.5 (b) m 0.25 (c) m 25 (d) m 1000 (e) m 100 [ ]
29. Ipi kati ya yafuatayo si sababu ya kutoa huduma ya kwanza…………... [ ]
(a) Kuokoa maisha (b) Kupata fedha (c) Kupunguza maumivu (d) Kuzuia kutoka
kwa damu (e) Kutoa matumaini
30. Njia ipi inayotumika kuwasilisha data za uchunguzi au utafiti wa kisayansi?
(a) Uchunguzi (b) Wastani (c) Takwimu kwa duara (d) Umbali (e) Asilimia
31. Sehemu ipi katika kielelezo kifuatacho husukuma damu kuelekea sehemu
zote za mwili? (a) A (b) B (c) C (d) D (e) E

32. Alama hii inawakilisha nini katika sakiti ya umeme? [ ]


(a) Kihisi umeme (b) Fyuzi (c) Mkondo geu (d) Mkondo mnyoofu (e) Kikinza
33. Ipi ni njia ya asili ya uzazi wa mpango kati ya zifuatazo. [ ] (a) Kutumia
kondomu (b) Sindano (c) Kuendelea kumnyonyesha mtoto (d) Kutumia vidonge
34. Sehemu ipi ya mwili inayotengeneza seli zinazoshambuliwa na V.V.U [ ]
(a) Uroto mwekundu (b) Moyo (c) Ini (d) Uroto wa njano (e) Mapafu
35. Ogani katika kielelezo kifuatacho hutoa taka mwili gani? [ ]

(a) Urea (b) Jasho (c) Mkojo (d) Kabonidaioksaidi (e) Amonia
36. Muunganiko wa Elementi zisizofanana mbili au Zaidi ya mbili huitwa . [ ]
(a) Molekyuli (b) Valensi (c) Kampaundi (d) Elektroni (e)
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 22
37. Tafuta ukubwa wa pembe akisi (r) [ ]

(a) 350 (b) 550 (c) 450 (d) 1100 (e) 700
38. Ipi kati ya kazi zifuatazo si kazi ya mifupa? [ ] (a) Kutengeneza damu
(b) Kuupa mwili umbo (c) Kusimamisha mwili na kutembea
(d) Kulinda ogani za ndani ya mwili (e) Kupitisha taarifa
39. Badili 143.60F kuwa sentigredi? [ ] (a) 600C (b) 630C (c) 59.40C (d) 760C
(e) 620C
40. Sehemu ya mkekakazi ambayo huingizwa data huitwa: (A) seli amilifu (B) seli
mchakato (C) seli yakinifu (D) seli butu

41. Andika mlinganyo wa alama ya kikemikali inayowakilisha maada ambayo


inauwezo wa kupatikana katika hali kuu tatu za maada……………………..……
42. Tafuta mkondo wa umeme katika sakiti ifuatayo:

43. Mashine ya jitihada ya N250 ilijongea umbali wa meta 16 kuinua mzigo wa


N500 kwa umbali wa meta 4. Tafuta ufanisi wa mashine.
44. Sehemu ya jicho ambayo inafanana na filamu katika kamera huitwa ……….
45. Tafuta thamani ya mzigo X katika mchoro ufuatao:

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 23
JARIBIO LA 8

1. Sehemu maalum katika mwili ambayo hutengeneza homoni ni _____________


A. ubongo B. moyo C. mfupa D. msuli E. tezi
2. Lipi kati ya haya yafuatayo ni badiliko la kikemikali? ________________
A. kuloanisha karatasi B. kuungua kwa mshumaa C. maji kuwa Barafu
D. Kuchanganya maji na sukari E. hakuna jibu
3. Upi ni mpangilio sahihi wa ripoti ya jaribio? ___ A. Kusudi, vifaa, njia, matokeo
na hitimisho B. Kusudi, vifaa, lengo na hitimisho C. Kusudi, vifaa, njia na
lengo. D. Kusudi, lengo, njia na vifaa E. Yote ni majibu sahihi
4. Mojawapo ya mahitaji muhimu katika uotaji wa mbegu ni ___________________
A. joto B. udongo C, matamahuluku D. mbegu iliyokomaa E. mbolea
5. Mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu kwenda nje ya mwili huitwa ______
A. falopia B. ureta C. uterasi D. urethra E. aota
6. Kitendo cha mmea kujitengenezea chakula chake huitwa _____________
A. osmosis B.hamirojo C. respiresheni D. fotosinthesisi E. fototropizimu
7. Joto katika vitu yabisi hupita kwa njia ya _____ A. msafara B. mnururisho
C. mpitisho D. mpitisho na mnururisho E. msafara na mpitisho
8. Mbegu ya mahindi ina ghala ngapi? ______ A. moja B. mbili C. tatu D. nne E. tano
9. Mtu mwenye tatizo au ugonjwa wa kuharisha utamsaidia haraka kwa
kumpatia A. chai B. maji C. mchanganyiko wa chumvi na sukari D. maziwa
E. mchanganyiko wa chumvi na limau
10. Inzi huwa na hatua ____ za ukuaji mpaka kuwa mdudu kamili. A.mbili B. tatu
C. nne D. tano E. moja
11. Ncha mbili za sumaku (Kas – Kas) zikikaribiana __A. huvutana B. hukwepana
C. hutoa cheche D. huzalisha umeme E. huvimba
12. Chembe hai ambayo hufanya kazi ya kushambulia vijidudu vya magonjwa
katika mwili wa binadamu ni _____ A. chembe hai nyekundu
B. chembe hai nyeupe C. chembe hai sahani D. plazima E. chembelele
13. Utatumia kifaa kipi ili kuona vitu vilivyo mbali sana?__ A. kamera B. darubini
C. hadubini D. televisheni E. macho
14. Elimu inayohusu magimba ( vitu vilivyo angani) kama sayari, nyota, mwezi
na viumbe vingine huitwa __ A. Elimu dunia B. Utabiri wa hali ya hewa
C. Uganga D. Unajimu E. Ikolojia

15. Hii ni aina gani ya lenzi? _ A. mbonyeo B. periskopu C. mbinuko D. kibanio

16. Wanyama ambao hula mimea tu huitwa _____ A. hebivora B. kanivora


C. omnivora D. reptilia E. mamalia
17. Chunguza mchoro ufuatao wa sakiti. Je, hii ni aina gani ya sakiti?

A. tuli B. mfuatano C. sambamba D. mstari mnyoofu E. ulalo.


Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 24
18. Zipi kati ya sehemu zifuatazo za uzazi ni za kike tu.
A. urethra B. ovari C. korodani D. kibofu E. stameni
Maziwa, mayai, karanga ni aina ya vyakula ambavyo A. hujenga mwili B. huupa
mwili nguvu C.vyakula vyenye vitamini D.hulinda mwili E. hugandisha damu
20._______ Ni kipimo cha uwezo wa elementi fulani kufanya muungano na elementi
nyingine A. kampaundi B. elementi C. valensi D. tindikali E. metali
21. Ugonjwa wa kisukari husababishwa na upungufu wa homoni ya insulin
inayozalishwa na______ (A) figo (B) moyo (C) wengu (D) ini (E) kongosho
22. Kati ya vyakula hivi chakula cha kujenga mwili ni ___(A) wanga (B) protini
(C) mafuta (D) vitamin (E) maji 23.Kinachosharabu maji katika mmea ni ______
(A) majani (B) mizizi (C) shina (D) stomata (E) matawi
24. Katika seli hai sehemu inayotawala shughuli zote ni ___(A) saitoplazimu
(B) nyukliasi (C) vakyuli (D) tishu (E) uteseli
25. Ogani ya kike ya ua inaitwa stigma,staili na __ (A) stameni (B) pistili (C)ovari
(D) chavuo (E) mbegu
26. Viumbe hai vimeundwa kwa chembe hai ndogo ziitwazo _____(A) seli nyeupe
(B) seli (C) kiini (D) atomi (E) tishu
27. Usambazaji wa chakula kilichomeng’enywa mwilini hufanywa na ____(A) damu
(B) maji (C) hewa (D) oksijeni (E) seli
28. Madini yapi husaidia kuimarisha mifupa mwilini? _____________(A) kalisiamu na
fosiforasi (B) chuma na ayodini (C) fosiforasi na aluminiam (D) magnesiam na
kalisium (E) kalisium na chuma
29. Elimu inayohusika na kutegemeana kwa viumbe hai katika mazingira huitwa
________(A) biolojia (B) saikolojia (C) unajimu (D) ikolojia (E) kemia
30. Upi kati ya magonjwa yafuatayo si ugonjwa wa zinaa? ___________(A) ukimwi
(B) kisonono (C) pepopunda (D) kaswende (E) klamedia
31. Mifupa inayolinda ubongo huitwa ____________(A) vertebra (B) sternum (C) fuvu
(D) mandibo (E) medulla
32. Ipi kati ya sehemu zifuatazo ni sehemu ya kike ya ua? _____ (A) pistil (B) stamen
(C) chamvua (D) stigma (E) petali
33. Ili kujikinga na upungufu wa damu tunashauriwa kula vyakula vyenye
__________(A) wanga (B) mafuta (C) chumvichumvi (D) protini (E) madini ya chuma
34. Mita ya umeme “LUKU” katika nyumba zetu hupima kiasi cha umeme ambao
tunatumia katika ______ (A) kilowats (B) saa (C) volteji (D) kilowatt kwa saa
35. Kizingiti cha mchemko wa maji katika mji wa Iringa wenye jotoridi la 250c ni
1000C . Je kizingiti cha mchemko wa maji kwa mji wa Tanga wenye jotoridi la 300C
ni ______ (A) nyuzi 1000C (B) ndogo kuliko nyuzi 1000 C (C) kubwa zaidi ya nyuzi
1000C (D) nyuzi 10000F (E) nyuzi 2000F
36. Tofauti kubwa kati ya chembe hai za wanyama na mimea ni ________
(A) kiwambo cha seli (B) nyuklia (C) vakuli (D) umbijani (E) saitoplasimu
37. Ni wakati gani maada husinyaa _____________(A) ikipashwa joto (B) ikiwa katika
hali ya kawaida ya joto (C) ikipoozwa (D) ikitawanywa (E) ikiyeyushwa
38. Virusi vya UKIMWI hushambulia seli ________ za damu (A) nyeupe
(B) nyekundu (C) plazima (D) chembe sahani (E) nyeupe na nyekundu
39. Katika uchunguzi wa kisayansi hatua ya kwanza ni ___________ (A)kuchambua
data (B) kutafsiri matokeo (C) kubainisha tatizo (D) kukusanya data
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 25
(E) hitimisho
40. Ni chumvichumvi za aina gani hutengenezwa na mimea jamii ya mikunde? _
(A) fosteti (B) ayodini (C) chuma (D) naitrojeni (E) naitreti

SEHEMU B: JAZA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI


41. Tafuta umbali X katika mchoro huu
Sm4 sm x

Kg 25 Kg 50

42. Chuma + maji + B=kutu.Herufi B inawakilisha____________________

43. Tezi muhimu inayoratibu kazi ya tezi nyingine huitwa ______________

44. Badili 1220F kuwa sentigredi______________________________________

45. Chavua husafiri kutoka kwenye stigima hadi ovari kupitia mrija wa _

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 26
JARIBIO LA 9
1.Chakula kilichomeng’enywa husharabiwa mwilini kwenye A) utumbo
mpana B) utumbo mwembamba C) ini D) figo E) kongosho
2. Urea, chumvichumvi na maji ni taka mwili zinazotolewa na A) ngozi
B) figo C) mapafu D) kongosho E) ini
3. Lipi halihitajiki katika tendo la mmea kusanisi chakula chake? A) oksijeni
B) maji C) umbijani D) mwanga wa jua E) kabondayoksaidi
4. Uyeyushaji wa chakula chenye wanga huanzia kwenye A) utumbo mkubwa
B) tumbo C) mdomoni D) damu E) utumbo mwembamba
5. Mtu mwenye upungufu wa madini joto mwilini hupata A) unyafuzi
B) goita C) utapiamlo D) anaemia E) kiseyeye
6. Maji magumu yanaweza kubadilishwa kuwa maji laini kwa
A) kuyachemsha B) kuyachuja C) kuyagandisha D) kuyapasha moto
E) kuyatonesha
7. Virusi vya ugonjwa wa Ukimwi (VVU) viingiapo mwilini huharibu seli zipi
za damu? A) seli hai nyeupe B) seli hai nyekundu C) plazima
D) haemoglobini E) chembe sahani
8. Sehemu ya sikio inayokusanya mawimbi ya sauti huitwa A) koklea
B) pina C) ngoma D) nyundo E) kikuu
9. Lipi kati ya yafuatayo ni badiliko la kikemikali A) kuyeyusha sukari
B) maji kuganda C) kuyeyuka kwa mshumaa D) kuyeyuka kwa chumvi
kwenye maji E) kupata kutu
10. Shughuli zote katika seli zinatawaliwa na A) nyuklia B) vakuoli
C) kloroplasti D) saitoplazimu E) ukuta wa seli
11. Kumbukumbu za afya ya mtoto chini ya miaka 5 huhifadhiwa katika:
(A) chumba cha wazazi (B) kitabu cha daktari (C) ofisi ya kijiji
(D) ofisi ya mwalimu mkuu (E) kadi ya kliniki
12. Kitendo cha maji katika mimea kusafiri kutoka myeyusho hafifu
kwenda myeyusho mzito huitwa A) respiresheni B) osmosisi C) stomata
D)haidrotropizimu E) translokesheni
13. Eneo maalumu linalokuwa na kani za sumaku huitwa (A) sumaku
B) kani za mvutano (C) uga wa sumaku (D) kani za umeme
14. Ni kiumbe yupi kati ya wafuatao urutubishaji wa mayai hufanyika nje
ya mfumo wa uzazi wa mama? (A) kuku(B) nyoka (C) kunguru (D) chura
(E) binadamu
15. Kipi kati ya yafuatayo siyo muhimu katika uotaji wa mbegu?
A) mwanga B) maji C) hewa D) joto
16. Sehemu ya kike ya ua huitwa A) stameni B) pistili C) stigma D) petali
E) sepali
17. Yafuatayo ni magonjwa ya kuambukiza isipokuwa A) kisukari
B) kifua kikuu C) UKIMWI D) Trakoma E) kipindupindu
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 27
18. Magonjwa yapi yanazuiwa kwa chanjo? A. Surua na kifaduro
B. kichocho na malaria C. kuharisha na dondakoo D. ukimwi na surua
19. Kitendo cha kusafiri kwa chavuo kutoka kichavua hadi kwenye stigma
huitwa A) urutubishaji B) utungisho C) fotosinthesisi D) uchavushaji
20. Matokeo ya mwisho ya kuvunja vunja protini ni _
A. Asidi za amino B. glukosi C. asidi za mafuta D. fati
21. Katika kipande cha chuma joto husafiri kwa njia ya …………….……..
22. Kitendo cha mmea kujitengenezea chakula chake huitwa ……………
23. Jicho lenye kasoro ya kutokuona karibu linaweza kurekebiswa kwa
kuvaa miwani yenye lenzi ………………………………………..……
24. Mrija unaosafirisha mkojo kutoka kwenye figo kwenda kwenye kibofu
cha mkojo unaitwa …………….…………….……………………….……………
25. Barafu ni maji yaliyopo katika hali ya ……………………...……………..
26. Toroli au mkokoteni ni nyenzo daraja la ………………….……………….
27. ……………….. hubadili karatasi ya litimasi bluu kuwa nyekundu.
28. Sehemu ya ubongo ambayo huratibu mijongeo katika mwili na
kuweka mwili katika hali ya msawazo huitwa …………………..………..
29. Ukavu macho ni ugonjwa unaosababishwa na upungufu wa vitamini
…………. Mwilini.
30. Fomula au simboli ya chumvi ya mezani ni ……………..…….……….....

31. Sehemu iliyoonyeshwa kwa herufi C inaitwa …………………………….….


32. Mshipa unaoingiza damu safi kwenye moyo huitwa ……….……………….
33. Hatua za mabadiliko ya ukuaji wa insekta huitwa ……………………..

34. Sayari inayojulikana kwa jina la “nyota ya asubuhi” ni …………… .…

SEHEMU B: JAZA NAFASI AU KOKOTOA


35. Kielelezo kifuatacho huwakilisha tendo la …………………………………

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 28
36. Hili ni jani la mmea uliopo katika kundi la …………………………………..
37. Filamu katika kamera hufanya kazi sawa na ……………..… katika jicho.
38. Myeyuko unaotumiwa kutambua chakula aina ya wanga ni:……….…
39. Umeme unaopita katika sakiti hii ni ampia 5. Kokotoa kiasi cha ukinzani
(R) wa waya kwenye sakiti hii.

40. Badili 800C kuwa Farenheiti


41. Kokotoa uzito wa mzigo K
sm 8
sm 5

Kg 6 K

42. Kutu ni matokeo ya kuungana kwa ayani, ……………na ……..…….….


43. TINDIKALI + NYONGO ………………… + .…………………...
44. Vitamin inayopatikana kwenye mwanga wa jua ni: ………………………
45. Joto la kawaida la mwili wa binadamu ni nyuzi ngapi za sentigredi?…….

JARIBIO LA 10
1. Popo yupo kwenye kundi la ___(A) ndege (B) reptiliya (C) mamalia
(D) wadudu (E) amfibia.

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 29
2. Zifuatazo ni mbegu za ghala moja isipukuwa___(A) mtama (B) mahindi
(C) ngano (D) maharage (E) shayiri.
3. Aina ya chembe hai za damu ambazo hushambuliwa na VVU ni ________
(A) chembesahani (B) seli hai nyekundu (C) seli hai nyeupe
(D) saitoplazimu (E) plasma.
4. Homoni inayothibiti kiwango cha sukari kwenye damu katika mwili wa
binadamu ni ___ (A) amilesi (B) insulin (C) ayodini
(D) glukosi (E) pepsin.
5. Kipi kati ya vifuatavyo huweza kupunguzwa mwilini kwa kushiriki
michezo na mazoezi ya mwili __ (A) mafuta (B) sukari (C) protini
(D) sumu (E) uchafu.
6. Mimea itoayo mbegu huhifadhi chakula chake kwenye ___(A) mizizi
(B) majani (C) shina (D) mbegu (E) tunda.
7. Ni sehemu gani ya ua hubadilika kuwa tunda _____(A) stigma (B) staili
(C) ovari (D) testa (E) manirangi.
8. Kipi kati ya virutubisho vifuatavyo ni muhimu kwa mtoto kupata kwa
wingi ili akue? __(A) vitamin (B) protini (C) mafuta
(D) kabohydrati (E) chumvichumvi za madini.
9. Mojawapo ya zifuatazo siyo sifa ya viumbe hai __(A) kula (B) kuzaliana
(C) kuoza (D) kusogea (E) kukua.
10. Lipi kati ya makundi yafuatayo ni wakala wa uchavushaji? ___
(A) wadudu, maji, upepo (B) joto, maji, wanyama(C) wanyama, udongo,
mvua (D) mwanga, upepo, wadudu (E) maji, wanyama, joto
11. Kazi ya vili zilizopo kwenye kuta za utumbo mwembambani ___
(A) kutengeneza juisi ya gastriki (B) kutoa chakula nje ya mwili
(C) kufyonza chakula kilichomeng’enywa (D) Kumeng’enyachakula
(E) kusafirisha chakula kwenda sehemu mbalimbali za mwili.
12. Yai lililorutubishwa linapogawanyika na kupata watoto zaidi ya
mmoja. Watoto hao huitwa ___(A) mapacha wanaofanana (B) mapacha
wasiofanana (C) mapacha (D) mapacha wasiojiweza
(E) mapacha wakiradikali.
13. Kibofu cha mkojo kikijaa, mkojo hutoka nje ya mwili kupitia kwenye
____(A) figo (B) ateriyarenali (C) urethra (D) ureta (E) mirijayafalopia.
14. Mojawapo ya makundi yafuatayo siyo ya wanyama wenye uti wa
mgongo ___(A) mamalia (B) reptilian (C) amfibia(D) ndege (E) minyoo.
15. Maria alipata jeraha na damu yake ilishindwa kuganda. Hii
inaonesha kuwa Maria alikuwa na ugonjwa wa ___ (A) hemophilia
(B) kiseyeye (C) pepopunda (D) anemia (E) beriberi.
16. Tunapokula matunda kama machungwa, malimao, na machenza
tunapata vitamin: (A) B (B) K (C) E (D) C (E) A
17. Kemikali inayotumika kutambua uwepo wa wanga kwenye chakula
hujulikana kama ____(A) besi (B) tindikali (C)spiriti (D) ayodin (E) alkali
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 30
18. Kati ya magonjwa yafuatayo upi siyo ugonjwa wa kuambukiza?
(A) pumu (B) kisukari (C) kansa (D) homa ya matumbo (E) selimundu
19. Samaki hupumua kwa kutumia_____ (A) mapezi (B) matamvua
(C) matundu ya stomata (D) mapafu (E) spirako
20. Matukio yote yafuatayo yanaonesha mabadiliko ya kiumbo isipokuwa
___(A) kuoza kwa matunda (B) maji kuwa mvuke (C) kuchacha kwa
maziwa (D) chuma kupata kutu (E) kuiva kwa matunda
21. Madini magumu kuliko yote ambayo hutumika pia kukatia vioo ni:
(A) shaba (B)Almasi (C) chuma (D)Tanzanaiti (E) ulanga.
22. Chanzo cha sauti ni ___________________________ (A) redio (B) toni
(C) mwangwi (D) mitetemo (E) kelele
23. Huduma ya kwanza inayofaa kumpa mtu aliyezimia ni ____________
(A) kumwagia maji (B) kumzingira (C) kumfunika blanketi (D) kubana
nguo zake (E) kumpa hewa safi
24. Gesi muhimu wakati wa tendo la usanisi nuru ni____(A) oksijeni
(B) naitojeni (C)hewaukaa (kabonidayoksaidi) (D) haidrojeni (E) agoni
25. Sehemu ya ua inayovutia wadudu huitwa_______________(A) petali
(B) chavua (C) sepali (D) ovary (E) stigma
26. Kiumbe yupi kati ya hawa wafuatao siyo reptilian? ___(A) chura
(B) mjusi (C) mamba (D) kinyonga (E) kobe
27. Katika pambano la kikemia lifuatalo herufi Y inawakilisha nini ____
AYANI + Y+ OKSIJENGE = KUTU (A) asidi (B) besi (C) maji
(D) kabonidayoksaidi (E) mafuta
28. Toroli na kifungua chupa vipo katika nyenzo daraja la ngapi ________
(A) kwanza (B) pili (C) tatu (D) nne (E) tano
29. Kitendo cha mmea kukua kuelekea kwenye mwanga wa jua huitwa _
(A) haidrotropizimu (B)jiotropizimu (C) fototropizimu
(D) themotropizimu (E) kemotropizimu.
30. Njia nzuri ya kujikinga na ugonjwa wa kichocho ni ___(A) kuepuka
kutumia maji yaliyotuama kwa kuoga au kufulia (B) kula mlokamili
(C) kutumia kemikali (D) kuepuka kushirikia na vitu na mgonjwa wa
kichocho (E) kuua konokono wote.
31. Yai zima huzama kwenye maji baridi lakini huelea kwenye maji
chumvi kwa sabab_ (A) maji chumvi hubadili tungamo la yai (B) maji
chumvi yana tungamo kubwa kuliko yai (C) yai lina tungamo kubwa
kuliko maji chumvi (D) maji chumvi ni mepesi kuliko maji baridi
(E) maji chumvi yanatungamo dogo kuliko maji baridi.
32. Mwanga wa mwezi hutokana na ___(A) kupinda kwa mwanga wa
dunia (B) wadudu wanaomulika (C) kimondo (D) kusharabiwa kwa
mwanga toka kwenye dunia (E) kuakisiwa kwa mwanga wa jua.
33. Rula iliyotumbukizwa nusu kwenye maji huonekana kuwa imepinda
.Hii ni kwa sababu ya (A) kutawanywa kwa mwanga (B) kupinda kwa
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 31
miali ya mwanga (C) kuakisiwa kwa miali ya mwanga (D) kuakisiwa
kwa joto (E) kufyonzwa kwa mwanga.
34. Nini kitatokea endapo ncha ya kaskazini na ncha ya kusini ya
sumaku mbili zitakaribiana? ___(A) zitavutana (B) zitashambuliana
(C) zitakwepana (D) hakuna kitakachotokea (E) zitaharibika
35. Kipi kati ya vitu vifuatavyo hakivutwi na sumaku? ___(A) mbao
(B) chuma kigumu (C) nikeli (D) chumalaini (E) bati
36. Vimiminika vinavyotumika kwenye themometa ni __(A) alkoholi na
maji (B) zebaki na alkoholi (C) alkoholi na mafuta ya taa (D) zebaki na
maji (E) maji na mafuta
37. Mchoro ufuatao unaonesha maji yaliyopo kwenye chombo yakiwa
yanachemshwa

Joto linasafiri kutoka pointi X hadi Y kwa njia ya (A) mpitisho na


msafara (B) mpitisho na mnururisho (C) msafaranamnuruisho
(D) msafaranampitisho (E) mpitishotu.
38. Chaji hasi za atomi hujulikana kama ___(A) protoni (B) nyutroni
(C) molekyuli (D) elektroni (E) kiinitete.
39. Matendo yafuatayo yanaonesha kazi imefanyika isipokuwa _____
(A) nguzo kushikilia nyumba (B) mvulana kuviringisha mpira kupitia
getini (C) moto kurusha mpira (D) mwanaume kusukuma mkokoteni
(E) mwanamke kunyanyua ndoo ya maji
40. Katika uchunguzi wa kisayansi ___hutumika kutabiri/kukisia
matokeo ya uchunguzi (A) uchambuzi wa taarifa (B) kutafsiri matokeo
(C) kukusanya taarifa (D) kutambua tatizo (E) bunio
SEHEMU B: JIBU MASWALI YAFUATAYO KAMA ULIVYOULIZWA
41. Chunguza mchoro ufuatao kasha tafuta thamani ya X

42. Sauti iliyoakisiwa na kusikika tena huitwa _____________________


43. Ili mbegu iote inahitaji maji, oksijeni na _______________________
44. __________husababishwa na ukosefu wa vitamin D mwilini
45. Kinga radi na waya wa ethi hutengenezwa kwa madini ya ________

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 32
JARIBIO LA 11
1. Ni kiumbe hai yupi kati ya wafuatao hujitengenezea chakula chake?
A) ng’ombe B) kuku C)binadamu D)mhogo (E) samaki
2. Katika muundo wa atomi elektroni ina chaji ___( A) chanya (B) hasi
(C) za kaboni tu (D) zinazozunguka nje ya atomi.
3. Maada ipi kati ya zifuatazo ni Elementi ? (A) Nacl (B) H20 (C) C02
(D) S04 (E) Ca
4. Lipi ni badiliko la kikemia kati ya haya: (A) mshumaa kuyeyuka
(B) kufanyika kwa mawingu ya mvua (C) kugandisha maji kwa barafu
(D) chuma kupata kutu
5. Unaweza kubadili maji magumu aushi kuwa laini kwa:
(A) kuyachemsha (B) kuyaweka yatulie ili tope lituame chini
(C) kuyatonesha (D) kuweka klorini.
6. Shata katika kamera hufanana na ___ katika jicho la binadamu:
(A) lenzi (B) kope (C) Retina (D) mboni
7. Matendo ya kupata kutu na kuungua hufanana kwa sababu:
(A) Oksijeni hutolewa (B) oksijeni hutumika (C) haidrojeni hutolewa
(D) kabonidayoksaidi hutumika
8. Waya mwembamba wa kulinda chombo cha umeme kisiunguzwe
huitwa: (A) gia boksi (B) fyuzi (C) sakiti (D) zodiaki
9. Mdudu ambaye hupitia hatua tatu za ukuaji kati ya hawa ni: (A) nzige
(B) kipepeo (C) Inzi (D) Nyuki
10. Ni wakati gani katika mabadiliko ya ukuaji homoni huongezeka?
(A) wakati wote (B) wakati wa balehe (C) usiku (D) mchana
11. Ogani iliyo kubwa kuliko zote katika mwili wa binadamu ni:
(A) moyo (B) Figo (C) Ini (D) Kongosho
12. Mifumo mbalimbali ya mwili inayofanya kazi kwa uhusiano mmoja
huunda: (A) seli (B) mifumo (C) kiumbe (D) tishu
13. Kundi la wanyama wanaovuta hewa kwa kutumia ogani mbili ni:
(A) Amfibia (B) Reptilia (C) Mamalia (D) Ndege
14. Mlishano wa simba Swala Nyasi unaweza kuathiriwa
na: (A) upepo (B) moto (C) Mvua (D) joto
15. Damu hupita kwenye mapafu ili: (A) kuchukua oksijeni na kuacha
kabonidayoksaidi (B) kuimarisha mapigo ya moyo (C) mwili uwe na
afya (D) kuchukua kabonidayoksaidi na maji.
16. Kitendo cha matunda kudondoka kutoka juu ya mti hudhihirisha
kuwepo kwa kani: (A) mvutano (B) mburuto (C) msukumo (D) mnyanyuo
17. Kiumbe hai kifuatacho kinachangia kuharibu mazingira kwa kasi:
(A) tembo (B) binadamu (C) ng’ombe (D) Swala
18. Zifuatazo ni sifa zinazomtambulisha kiumbe hai isipokuwa:
(A) kujitengenezea chakula chake (B) kukua (C) kuzaliana (D) kupumua

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 33
19. Sehemu ya mbegu inayohifadhi chakula cha kiinitete ni: (A) ghala
(B) ganda (C) embryo (D) kikonyo
20. Katika uandishi wa ripoti ya jaribio la kisayansi jambo la nne
kuandikwa huwa ni:(A) vifaa (B) matokeo (C) njia (D) hitimisho
21. Asha amepinda miguu, unafikiri ana ukosefu wa madini gani?
(A) kalisiamu (B)magnesiamu (C) chuma (D)sodiamu
22. Moja kati ya hatua zifuatazo huzuia mmomonyoko wa udongo:
(A) kuongeza mifugo (B) kuchoma misitu (C) kupanda miti (D) kukwatua nyasi
23. Kiwavi ni lava wa__.A)mende B)panzi (C)chura (D)kipepeo
24. Chakula kinachoupatia mwili virutubisho vyote katika uwiano sahihi
ni __ (A)mlo wenye protini (B)chakula chenye harufu nzuri (C)mlo kamili
(D)vitamin, fati na madini
25. Mmeng’enyo wa mwisho wa protini ni: (A) glukosi (B) asidi za fati
(C) asidi za amino (D) asidi za glaisero.
26. Hatua za mabadiliko ya ukuaji wa insekta huitwa:
(A) metamofosisi (B) metamofosisi kamili (C)metamofosisi
isiyokamili (D) fototropizimu
27. Kufunga kamba sehemu ya juu ya Jeraha ni huduma ya kwanza kwa
mtu aliye: (A) umwa na nyoka (B) zirai (C) naswa na umeme
(D) aliyevunjika (E) aliyeungua.
28. Faida kuu ya uzazi wa mpango ni: (A) kufanya idadi ya watoto kuwa
kubwa (B) kuwa na uwezo wa kutoa huduma zote muhimu kwa familia
(C) kuepuka matatizo (D) kuwapa watoto elimu.
29. Hemoglobin ni kampaundi iliyo katika chembe ___ za damu.
(A) nyeupe (B) nyekundu (C) sahani (D) zote
30. Haidrojeni + Oksijeni (A) asidi (B) Oksaidi ya Haidrojeni
(C) maji magumu aushi (D) haidroksaidi
31. Atomi moja ya Oksijeni + atomi moja ya Oksijeni unapata:
(A) H2O (B) O (C) CO2 (D) O2
32. Mimea hutengeneza chakula chake kwenye: (A)Kloroplasti
(B) saitoplazimu (C) seli (D) kiwambo
33. Husababisha upungufu wa kinga mwilini;
(A) V.c.d (B) UVC (C) VVU (D) UKIMWI
34. Duodenamu na Iliamu ni sehemu za __ (A) utumbo mpana
(B) utumbo mwembamba (C) seli hai (D)Ini
35. Amina aliyekaa umbali wa mita 3 kutoka egemeo ana uzito wa Kg 60,
kokotoa umbali aliokaa Aida mwenye uzito wa Kg 40. (A) meta 4 ½
(B) meta 3 (C) meta 12 (D) meta 9 ¼

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 34
36. Mchoro huu huwakilisha mguu wa ndege fulani. Kwakuzingatia ulaji
wake, kiumbe huyu yupo katika kundi la A) habivora B) Omnivora
C) Kanivora D)mwewe E)habomkanivora
37. Badili nyuzijoto za Fareinheit 194 kuwa Sentigredi
(A) 900 C (B) 700 C (C) 1420 F (D) 900 F
38. Kokotoa manufaa ya kimakanika iwapo mzigo wa Newton 340
uliinuliwa na jitihada ya Newton 17. (A) 40 (B) 20 (C) 18 ½ 0 F
(D) 142 Newton
39. Mende ni mdudu ambae hupitia hatua __ za ukuaji A)5 B)3 C)4 D)1
40. Katika ua filament huhusika na kubeba ___________________________
A) kichavua B) stigma C) wadudu D) kikonyo

SEHEMU B JIBU KWA KIFUPI


41. Dunia ikikaa katikati ya jua na mwezi hali hiyo huitwa ____________
42. Kukojoa na kiu ya mara kwa mara ya maji, kujisikia mchovu na
dhaifu ni dalili za ugonjwa wa __________________________________
43. Rula ikitumbukizwa ndani ya maji huonekana imepinda hii
husababishwa na ______________________________________________
44. Kifaa kinachotumika kutawanya mwanga katika rangi saba za
spektramu huitwa _____________________________________________
45. Katika via vya uzazi vysa mwanamke mimba hutungwa katika _____

JARIBIO LA 12
1. Zifuatazo ni kazi za damu isipokuwa ____ A: kusafirisha oksijeni
B: kutawanya vichocheo mwilini C: kutengeneza klorofili
D: kusafirisha uchafu E: kusafirisha chakula kilichoyeyushwa
2. Mmea hupata mahitaji yake ya hewa kwa njia ya vitundu vidogo vidogo
vinavyoitwa? A: kloroplasti B: vichomozo C: saitoplazimu
D: stomata E: Vakuoli
3. Kimeng’enya kinachohusika katika kutenganisha maji na maziwa ni ___
A: renini B: pepsin C: peptaidi D: maltosi E: amilesi
4. Kuyeyuka kwa barafu ni badiliko gani la maada? A: kikemikali
B: kiumbo C: kimazingira D: kibaiolojia E: kifiziolojia
5. Mdudu yupi kati ya hawa wafuatao hupitia metamofosisi isiyokamili:-
A: mbu B: kipepeo C: inzi D: nyuki E: mende

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 35
6. Mchoro ufuatao unaonyesha aina gani ya sakiti?

A: sakiti mfuatano B: sakiti sambaba C: sakiti ukinzani D: sakiti


mbadala E: sakiti mkondo
7. Sayari iliyo karibu zaidi na Jua ni? A: Dunia B: Zebaki
C: Uranus D: Zuhura E: Saratani
8. Katika jaribio la Kisayansi ni hatua ipi jibu hupatikana? A: kutambua
tatizo B: kuchunguza kwa muda mrefu C: kuangalia kwa macho
D: kufanya jaribio E: kushuka
9. Seti ipi ya vifaa inaunda sakiti ya umeme iliyokamilika? A: betri, waya,
ubao na msumari B: betri, waya, ubao na glopu C: glopu, waya, betri
na swichi D: glopu, waya, swichi na nguzo
E: swichi, glopu, waya na misumari
10. Nini hutokea iwapo gameti X ya kike itaungana na gameti X ya kiume?
A; mapacha wasiofanana B: mtoto wa kike C: mapacha
walioungana D: mtoto wa kiume E: mapacha wanaofanana
11. Haemoglobini ni kampaundi inayopatikana ndani ya damu katika ____
A: seli nyeupe B: seli hai nyekundu C: ute wa damu D: plazima
E: seli zinazogandisha damu
12. Punje ya mhindi pia ni tunda kwa sababu: A: ina kovu mbili B: ni kubwa
kama zambarau C: inaota D: hupendwa na panya E: ni nzito
13. Sehemu ya kike ya ua iliyo na mbegu ni _____________________________
A: chavua B: pistil C: stameni D: ovuli E: sepali
14. 6CO2 + H20 C6 H12 O6 + 6O2. Ni kitendo gani kimewakilishwa na
mlinganyo huu? A: transipiresheni B: respiresheni
C: fotosinthesisi/ usanisinuru D: oksidesheni E: fototropizimu
15. Chunguza mlishano ufuatao kisha jibu swali linalofuata;-
MIMEA NYATI DUMA. Katika mlishano huo nini kitatokea
ikiwa duma watahama katika mazingira haya? A: mimea itakauka
B: nyati watapungua C: mimea itaongezeka D: nyati watahama
E: mimea itapungua
16. Watu hawawezi kuathiriwa na VVU/UKIMWI kutokana na ____
A: kuumwa na mbu aliyemuuma muathirika B: kujamiiana na
mgonjwa mwenye VVU/UKIMWI C: kuongezewa damu yenye
VVU/UKIMWI D: kuchangia vifaa vya kunyolea na mtu mwenye
VVU/UKIMWI E: kunyonyana ndimi na mtu mwenye VVU/UKIMWI
17. Mshipi na ndoano ya kuvua samaki ni mifano ya nyenzo daraja la ngapi?
A: pili B: kwanza C: tano D: nne E: tatu
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 36
18. Besi + Asidi Y + Maji. Y inawakilisha nini katika mlinganyo huu wa
kemikali? A: chumvi B: asidi C: sukari D: nyongo E: besi
19. Kisonono, kaswende, pangusa na UKIMWI huwekwa kwenye kundi la
magonjwa yanayoenezwa kwa njia ya ____ A: hewa B: zinaa
C: kugusana D: kudungwa E: tohara
20. Mchanganyiko unaotengeneza mboji ni upi? A: udongo, mimea iliyooza
na mchanga B: mchanga, maji na samadi C: udongo, mchanga na
samadi D: samadi, mimea na maji E: mimea iliyooza, mchanga na
samadi
21. Tezi ya pituitari inapotoa homoni nyingi kupita kiasi nini hutokea kwa
binadamu? A: hurefuka sana B: hudumaa sana C: hakuna
madhara D: husababisha kifo E: hunenepa sana na kudumaa
22. Ipi kati ya alama zifuatazo inawakilisha ayani (chuma) ___ A: Ca
B: Fe C: Na D: Hg E: H20
23. Alama husimama badala ya ____ A: kikinza B: omu
C: voltimita D: seli E: ameta
24. Maada inayofanyika kwa muunganiko wa atomi mbili au zaidi tofauti
huitwa A: kiasili B: elementi C: metali D: haidrojeni E: kampaundi
25. Ni kipi kati ya vifuatavyo kimeundwa kwa chembechembe ndogo sana?
A: gesi B: vimiminika C: chembe za damu D: chuma
E: aluminiamu
26. Namanji anaonekana kupinda miguu, unafikiri anakosa madini gani?
A: kalsiam B: sodium C: magnesiam D: chuma E: aluminiam
27. Maji yaliyochanganywa na sukari na chumvi ni huduma ya kwanza kwa
mtu anayesumbuliwa na ___________ A: malaria na kuumwa kichwa
B: kuvunjika mguu au mkono C: kuhara na kutapika D: uti wa
mgongo na homa ya matumbo E: kifua kikuu na mafua
28. Tendo la mmea kukua kuelekea kwenye mwanga huitwa ____
A: haidrotropizimu B: fototropizimu C: kemotropizimu
D: geotropizimu E: tropizimu
29. Ugonjwa wa kifua kikuu husababishwa na bacteria gani?
A: wote walioko hewani B: basili C: plasimodium D: fungi E: amiba
30. Amina aliweka maziwa freshi katika jagi la plastiki, siku ya pili maziwa
yalikuwa yameanza kuganda, nini kilisababisha maziwa kuganda. A:
uchafu wa maziwa B: joto C: bacteria katika hewa
D: ng’ombe alizalisha maziwa ya plastiki
31. Vitu muhimu katika uotaji wa mbegu ni ____ A: udongo, mwanga na
Jua B: hewa, udongo na maji C: joto la kiasi, maji na hewa ya
oksijeni D: joto la kiasi, udongo na mwanga wa Jua, oksijeni E: joto,
udongo na mwanga wa jua
32. Maji yanayochemka na kuwa mvuke huwa yamefikia jotoridi la ________
A: 980C B: 1060F C: 2120F D: 1000F E: 770F
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 37
33. Uchachu wa limao na machungwa mabichi husababishwa na uwepo wa
kemikali iitwayo? A: besi (alkali) B: chumvi C: asidi D: metali
E: alkoholi
34. Unapochemsha maji kwa jiko la mkaa, maji hupata joto kwa njia ya ___
A: mpitisho na msafara B: msafara C: mpitisho na mnururisho
D: msafara na mnururisho E: mnururisho
35. Rovu humpata mtu mwenye upungufu wa madini ya ____ A: kalsiamu
B: oksijeni C: salfa D: ayodini E: chuma
36. Miale ya mwanga wa radi inaonekana kabla ya kusikia mngurumo wa
radi kwa kuwa? A: mwanga unasafiri haraka kuliko sauti B: sauti
husharabiwa kwanza na mawingu C: sauti husafiri haraka kuliko
mwanga D: mwanga huonesha sauti E: mwanga hunyonya maji
37. Sehemu zinazofanya mfumo wa fahamu wa kati ni ____ A: milango ya
fahamu B: neva C: sensori na mota D: ubongo
E: ubongo na ugwe mgongo
38. Kifaa kinachotumika kupima umeme kwenye sakiti kinaitwa __________
A: Anemomita B: volti C: ampia D: omu E: amita
39. Ukifua nguo nyeupe na nyeusi kwa wakati mmoja, nguo nyeusi huwahi
kukauka kwasababu ____ A: kufyonza joto B: kuaksi joto
C: kufyonza unyevu unyevu D: kikinza na upepo E: hukausha maji kiurahisi
40. Mbu aina ya kuleksi husambaza minyoo inayoitwa filaria ambayo
husababisha ugonjwa wa ___ A: pepopunda B: Malaria C: Matende
D: Manjano E: Trakoma

SEHEMU B: ANDIKA JIBU


41. Badili jotoridi 1220F kuwa nyuzi za sentigredi ______________________
42. Musa alitumia nyutoni 10 kusukuma toroli kwa umbali wa mita 5.
Kokotoa kazi iliyofanyika.__________________________________________
43. Iwapo mzigo katika roda huru yenye gurudumu moja una uzito wa kg 30
na jitihada ni kg 5. Tafuta Manufaa ya kimakanika. ________________
44. Waya una ukinzani wa Ohm 15, kiasi cha mkondo wa umeme unaopita
katika waya huo ni ampia 0.3. Tafuta tofauti ya protenshali katika waya
huo _____________________________________________________________
45. Tafuta thamani K katika mchoro huu.

sm 25 sm 15 sm 40

K Gm 20 Gm 15

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 38
JARIBIO LA 13

1. Kifua kikuu na uti wa mgongo ni moja wapo ya magonjwa yanayo


ambukizwa kwa njia ya: A) hewa B) maji C) vyakula
D) mavazi E) inzi
2. Joto husafiri kwenye vitu vyenye asili ya chuma kwa njia ya: A) msafara
B) mpitisho C) mnururisho D) moja kwa moja E) mvukizo
3. Maji huganda katika nyuzi joto ___ A) 100 C au 212 F
0 0 B) 350C au 950F
C) 00C au 320F D) 400C au 1040F E) 00C au 00F
4. Kipi kati ya vifuatavyo ni chanzo kikuu cha nishati? A) jua B) radi
C) nyota D) moto E) mafuta
5. Mahitaji muhimu kwa uhai wa viumbe ni _____ A) maji na hewa
B) chakula na joto C) hewa, maji na chakula D) mwanga na mvua
E) chakual, mavazi na malazi
6. Mwili wa binadamu mtu mzima una jumla ya mifupa ipatayo A) 206
B) 72 C) 300 D) 24 E) 144
7. Samaki huishi majini tu. Hawezi kuishi nchi kavu. Hii ni kwa sababu
hawezi A) kutembea B) kuruka C) kupumua D) kusikia
E) kuogelea
8. Kitendo cha mmea hujitengenezea chakula chake hujulikana kama
A) umbijani B) usanisinuru C) uyeyushaji D) uchavushaji E) osmosisi
9. Baada ya kupukutisha majani mimea kwa kipindi hicho hupumua kwa
kutumia _____ A) stomata B) stomata shina C) vidumazi D) spirako
E) haipumui
10. Maada ipi kati ya zifuatazo inaweza kupatikana katika hali zote tatu za
maada A) mshumaa B) maji C) chuma D) chumvi E) asidi
11. Katika ua mdudu hufuata nini _____________ A) petali B) sepali
C) stigma D) mbochi E) stameni
12. Umuhimu wa mimea aina ya mikunde shambani ni katika kusaidia
kurutubisha udongo kwa kutumia hewa ya: A) naitrojeni B) haidrojeni
C) oksijeni D) kabondioksaidi E) asidi
13. Ili kuondoa chumvi katika maji, tendo lipi kati ya yafuatayo huwa ni lazima
kufanyika? A) kutonesha B) kuchemsha C) kuvukiza
D) kugandisha E) kuyeyusha
14. Vizio vya umeme ni ___ A) waya, betri na ampia B) ohm, volti na ampia
C) joule, betri na amita D) ukinzani, amita na voltimita E) amita,
ampia na betri
15. Katika mmea wa mhindi, punje ya mhindi ni sehemu ya pistili iitwayo:
A) mbegu B) tunda C) stigma D) kikonyo E) staili.
16. Kuungua kwa mshumaa ni badiliko la A) kikemikali B) kiumbo
C) kimakanika D) kisayansi E) kiufundi

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 39
17. Mfupa unaounganisha bega na kidali huitwa ____ A) mvundi B) trauma
C) chafu D) mikano E) mtulinga
18. Upi ni mfululizo sahihi katika ukuaji wa mende? A) mayai, lava, tunutu,
mende B) lava, mayai, mende, tunutu, C) mayai, tunutu, tunutu, mende
D) mende, mayai, lava, tunutu. E) tunutu, mende, mayai, lava.
19. Setlaiti ya ya asili ni ipi kati ya zifuatazo? ____________________________
A) jua B) mwezi C) nyota D sayari)
20. Taasisi inayoelimisha watu kuhusu huduma ya kwanza kwa wagonjwa
ni A) idara ya zimamoto B) ANGAZA C) UMATI D) Msalaba
Mwekundu
21. Ni kiambata gani cha damu ambacho hupambana na magonjwa?
A) chembe nyeupe B) chebe sahani C) plasma D) chembe nyekundu
E) sifongo
22. Baada ya wanafunzi 60 wa darasa la saba shule ya msingi Kibada
kusukuma ukuta kwa dakika 10, walitoka jasho na kuchoka sana, bila
ukuta huo kusogea. Kazi iliyofanyika ilikuwa ni: A) 600W B) 4.5 J
C) 0J D) 600J E) 4.5 J
23. Ukimchunguza bata utaona miguu yake ni tofauti na ya kuku. Miguu ya
bata humwezesha A) kuruka kwa kasi zaidi kuliko kuku B)kutembea
kwa madaha kuliko kuku C) kuparuaparua anapotafuta chakula majini
D) kuogelea majini kuliko kuku E) kusogeza mayai yake pamoja
anapoatamia
24. Jua hupatwa mchana. Tukio hili katika mwanga hudhihirisha ________
A) kupinda kwa mwanga kutoka media moja hadi nyingine B) unyoofu
wa mstari wa mwanga katika safari yake C) mwezi kuwa katikati ya
jua na dunia D) dunia kuwa katikati ya dunia na mwezi E) mwezi ni
mdogo zaidi kuliko jua
25. Takamwili ya kabondayoksaidi hutolewa na; A) pua B) mapafu C) moyo
D) damu E) insulin
26. Kijusi hupata chakula na hewa kikiwa ndani ya tumbo la mama kupitia;
A) plasenta B) uterasi C) mirija ya falopia D) ovari E) kelenge
27. Ni mdudu yupi hupitia hatua za ukuaji za metamofosisi kamili? A) panzi
B) mende C) inzi D) nzige
28. Joto husafiri kwenye hewa kwa njia ya; A) mnunurisho B) msafara
C) mpitisho D) mwendo
29. Nini matokeo ya dunia kulizunguka jua kwa muda wa siku 3651/4?
A) majira mbalimba ya mwaka B) usiku na mchana C) kupatwa kwa
mwezi D) kupwa na kujaa kwa maji baharini
30. Filamu katika kamera ni sawa na __ katika jicho. A) irisi B) pupili C) lenzi
D) retina

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 40
JAZA NAFASI ZA WAZI
31. Eneo linaloathirika na nguvu ya kipande cha sumaku huitwa __________
32. Uwepo wa _________________________ katika aina fulani ya chakula
unaweza kubainishwa kwa kutumia madini ya joto.
33. Neva zinazotoa taarifa kutoka kweye ubongo kupeleka sehemu nyingine
mwilini huitwa ______________
34. Wanyama huvuta hewa ya oksijeni ambayo hutoka kwenye mimea na
mimea hutumia hewa ya _____________ kujitengenezea chakula chake
ambayo hutoka kwa wanyama.
35. Filamu katika kamera inafanya kazi kama ________________ katika jicho
la binadamu.

36. Alama hii huonyesha nini? _______________________


37. Kokotoa kiasi cha ukinzani (R) katika sakiti hii:

20V
0.5A R

38. Katika wenzo ufuatao, tafuta thamani ya X


sm 6 sm 6 sm 3
sm 6

kg x kg 4 kg 8

39. Kamilisha mchakato huu: A inawakilisha nini? ____________________


A + CHUMA + MAJI / UNYEVU = KUTU

40. Kitendo cha kukua kwa mmea kama ilivyooneshwa kwenye kielelezo
hiki hujulikana kama __________________________________________

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 41
TUMIA MCHORO HUU KUJIBU SWALI 41 - 45

41. Sehemu inayowakilishwa na herufi G ni ______________________________


42. Herufi K inawakilisha _____________________________________________
43. Chakula husharabiwa katika sehemu ipi ya herufi _____________________
44. Herufi E ni _____________________________________________________
45. Herufi D inawakilisha ____________________________________________

JARIBIO LA 14
1. …….…… ni kimeng’enya chenye uwezo wa kumeng’enya chakula chenye
asili ya mafuta na kuwa gliseroli na asidi ya mafuta A) lipasi B) amylase
C) taipsini D) peptoni E) amplesi
2. Nini matokeo ya mwisho ya myeyuko wa chakula aina ya protini?
A) Asidi za fati na glaiserini B) Asidi za amino C) Sukari rahisi D) Maltose
E)chumvi
3. Mate huwa na kimenyenyo ambacho hubadilisha ………. kuwa ………..
rahisi. A) Fati, sukari B) Wanga- protini C) Sukari, fati D) Wanga,
sukari E) protini,wanga
4. Wekundu wa damu hupatikana kwenye rangi ya kampoundi iitwayo
A) chembe sahani B) Plazima C) Seli hai nyeupe D) mishipa
E) Haimoglobini
5. Viumbe hai vimeundwa kwa chembechembe ndogo ziitwazo A) Nyukliasi
B) Atomi C) Seli D) seli hai nyekundu E) Saitoplazimu
6. Katika mfumo wa mzunguko wa damu ateri zote hubeba damu yenye
oksijeni isipokuwa A) Vena B) aota C) Palmonari ateli D) Palmonari
vena E) Ateri za Kapilari

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 42
7. Kupatwa kwa jua hutokea wakati ………… upo katikati ya magimba
mawili A) Jua B) Mwezi C) dunia D) sayari E) Jupita
8. Myeyuko wa ……….. hutumika kujaribia uwepo wa wanga katika chakula
A) Zebaki B) Asidi C) Besi D) Ayodini E) insulini
9. Wanyama wanaokula nyama na majani huitwa A) Canivorasi
B) Omnivorasi C) Hebivorasi D) Optivorasi E) Canivorasi na Omnivorasi
10. Ugonjwa wa kiseyeye husababishwa na upungufu wa vitamin
A) C B) D C) A D) E E) K
11. Sehemu ya sikio inayohusika na kukusanya mawimbi ya sauti huitwa?
A) akausitika B) koklea C) miatusi D) pina E) ngoma ya sikio.
12. Ogani ipi kati ya hizi haihusiani na mfumo wa mmeng’enyo wa chakula?
A) figo B) Ini C) Utumbo D) moyo E) kinywa
13. Ni kifaa gani hutumika kukuza taswira ya violwa vidogo sana?
A) periskopu B) prizimu C) lenzi D) darubini E) hadubini
14. Fyuzi hufungwa kwenye vifaa vitumiavyo umeme kama ifungwavyo …..……
kwenye nyumba ili kuepusha hitilafu ya umeme mwingi. A) Sakiti breka
B) waya wa ethi C) volteji D) Ampia E) amita
15. Mtu asiyeona vizuri vitu vilivyopo jirani, anashauriwa kuvaa miwani yenye
lenzi A) mbonyeo B) mbinuko C) bapa D) Prizimu E) Miwani.
16. Mchanga unaopatikana katika firigisi ya kuku husaidia A) kuongeza chakula
B) kusaga chakula C) kuhifadhi nyongo D) kuuwa vijidudu katika vyakula
E) Kukipa kinyesi rangi yake.
17. Kifaa kinachobadilisha mkondo geu wa umeme kuwa mkondo mnyoofu ni
A) Redieta B) Amita C) Transista D) Sakitibreka E)Rektifaya
18. Moja ya matendo yafuatayo hayaharibu usumaku A) Kuchoma moto
B) kugongagonga C) Kutumia umeme mkondo geu D) Kutumia mkondo
mnyoofu wa umeme E)kuweka pamoja na vifaa vya chuma.
19. Kukosekana kwa chanikiwiti katika mmea huweza kusababisha A) Majani ya
mmea kupukutisha B) Majani ya mmea kukauka C) Mmea kukosa madini joto
D) Mmea kushindwa kusanisi chakula E) Mmea kudumaa
20. Kusharabu maji na madini yaliyotokana na mmeng’enyo wa chakula ni moja
ya kazi ya ………. A) utumbo mdogo B) utumbo mpana C) kongosho D) puru
21. Fototropizimu ni kitendo cha mmea kuota kuelekea kwenye A) Maji
B) Kani ya mvutano C) Mwanga D) Kemikali E)Gizani.
22. Sehemu ya chembe hai inayohusika na kutawala shughuli zote za chembe hai
huitwa A) Saitoplazimu B) Vakuoli C) Kloroplasti D) Nyuklias E) Seli
23. Mkondo wa umeme wenye ampia 0.8 umepita kwenye waya wenye ukinzani
wa Omu 24. Je nguvu ya umeme katika sakiti hiyo ni Volti ngapi? A)19.4
B) 192.2 C) 19.2 D) 19.48 E)19.22
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 43
24. Kipi kati ya vifuatavyo hakipitishi mkondo wa umeme?......... A) Zebaki
B) Shaba C) mpira D) chuma E) Waya.
25. Mfumo wa homoni hujulikana pia kama mfumo wa A) endokrini
B) Respiresheni C) Translokation D) Haidrometa E) Transipiresheni
26. Apecha katika kamera hufananishwa na ………… katika jicho A) Retina
B) Irisi C) Konea D) Lenzi E) mboni.
27. Chakula kilichomeng’enywa husharabiwa tumboni kupitia vinyweleo
viitwavyo A) Haidrokloliki asidi B) Vilasi C) Peptoni D) Pepsini
E) vairasi
28. Ni muhimu kuweka kumbukumbu za jaribio lililofanyika kwa sababu
hutumika A) Kama rejea B) Kuchora jedwali la matokeo C) Kurekebisha
taarifa mbalimbali D) Kutangaza umakini wa aliyefanya jaribio
E)Kumtambulisha aliyeandaa jaribio.
29. Data za uchunguzi zilizochambuliwa huweza kuwasilishwa kwa njia ya
A) Ripoti B) Kutafsiri C) Grafu D) Kukokotoa E) Kuchambua.
30. Lipi kati ya yafuatayo siyo badiliko la kikemikali? A) kuungua kwa mkaa
B) kuchacha kwa maziwa C) chuma kupata kutu D) kuoza kwa takataka
E) Hakuna jibu sahihi.
31. Ipi kati ya jozi zifuatazo si sahihi kuhusu lenzi?
A) Lenzi mbonyeo – hurekebisha kutokuona mbali
B) Lenzi mbinuko – hutawanya miale ya mwanga
C) Lenzi mbonyeo- hukusanya miale ya mwanga
D) Lenzi mbinuko – hurekebisha kutoona mbali
E) A,B,C na E ni majibu sahihi
32. Matumizi ya roda katika maisha ya kila siku ni A) kunyanyua vitu vizito
B) kufunga vitu C) kuzibua vizibo vya vyupa D) kurahisisha kukata kuni
E)Kulimia
33. Ni Tezi ipi kati ya zifuatazo huratibu utendaji wa tezi zingine zote katika
mwili wa binadamu? A) Kongosho B) Thairoidi C) Pituitari D) Adrenali E) Ini
34. Joto husafiri kwenye vitu vyenye asili ya chuma kwa njia ya: A) msafara
B) mpitisho C) mnururisho D) moja kwa moja E) mvukizo
35. Seti ipi inaonesha mahitaji muhimu ili kutu iweze kutokea? A) maji,
bika, msumari na kopo B) msumari, mafuta na bika C) maji, msumari,
mafuta na kopo D) hewa, msumali na bika E) msumari hewa na maji
36. Kuungua kwa mshumaa ni badiliko la A) kikemikali B) kiumbo
C) kimakanika D) A na B E) hakuna jibu.
37. Ni kiambata gani cha damu ambacho hupambana na magonjwa?
A) chembe nyeupe B) chebe sahani C) plasma D) chembe nyekundu
E) sifongo
38. Wajenzi wa reli wanaacha nafasi au uwazi kati ya vyuma viwili vya reli.
Hii ni kwaajili ya A) kupunguza idadi ya vyuma B) kupunguza kelele

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 44
za msuguano C) kuzuia kupinda kwa vyuma wakati wa joto D) kuzuia
vyuma kusinyaa wakati wa baridi E) kuweka nafasi kwa ajili ya hewa kupita
39. Dainamo ni kifaa ambacho hufua umeme kwa nishati ya ________________
A) Kimakanika B) Kikemikali C) Jua D) kibaiolojia E) kikemia
40. Tendo la mmea kusafirisha maji kutoka kwenye mizizi hadi kwenye majani
huitwa A) Difyusheni B) Respiresheni C) Transilokesheni D) Osmosisi
E) Transpleshen

JAZA NAFASI AU KOKOTOA


41. Mbolea ya kupandia aina ya NPK ina viasili vitatu, kiasili kinachowakilishwa
na herufi K ni _______________________________________________________
42. Kani ya mvutano kati ya mwezi na dunia matokeo yake ni _______________
43. Mzigo wa kg 4.5 ulinyanyuliwa na kusogezwa umbali wa meta 5. Kokotoa kiasi
cha kazi iliyofanyika.__________________________
44. Chunguza mchoro huu.

Glopu katika sakiti hii haiwaki. Unafikiri ni kwa nini? _________________


45. Tazama mchoro huu.
Ni mnyama gani amewekwa hapo kwa makosa? _______________________

WASIO NA UTI WA MNGONGO

ng’e kaa jongoo mjusi konokono

JARIBIO LA 15
1. Msingi wa uhai wa kiumbehai ni ……………………… (a) misuli
(b) seli (c) damu (d) tishu (e) mifupa
2. Ateri zote husafirisha damu yenye Oksijeni isipokuwa mshipa wa
(a) Ateri mapafu au ateri ya palmonari (b) vena mapafu
(c) Aorta (d) kapilari (e) mishipa yote ya damu
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 45
3. Mavazi hutengenezwa kutokana na …………. (a) pamba na hewa
(b) Rangi na maji (c) ngozi na karatasi (d) mimea, wanyama na
kemikali (e) nyuzi,gundi na karatasi
4. Muunganiko wa kikemikali kati ya elementi mbili au zaidi huunda ….
(a) Valensi (b) Kompaundi (c) Molekyuli (d) Atomu (e) Radikali
5. Ni muhimu kuzingatia kanuni za Afya ili ………………………………..
(a) Tusipatwe na magonjwa (b) Tuishi kwa miaka mingi zaidi ya Mia
moja (c) Tupate kula chakula kwa muda mrefu (d) Tuwe na uzito
Mkubwa kupita kiasi (e) Tuwe na ngozi laini sana
6. Chanzo kikuu cha nishati ya mwanga na joto duniani ni ………….…
(a) mwezi (b) Vimondo (c) moto (d) satelaiti (e) Jua
7. Sauti hutokana na ……………..…. ya maada mbalimbali. (a)Mitetemo
(b) Mitanuko (c) Mivutano (d) Misukumano (e) Mizunguko
8. Uwezo wa kufanyakazi hujulikana kama ……….. (a) nguvu (b) kani
(c) Nishati (d) Mwangwi (e) Msuguano
9. Yupi kati ya wanyama wafuatao hana uti wa mgongo? (a) Nyoka
(b) samaki (c)Chura (d) Simba (e) konokono
10. Ili kujibu swali hili chunguza kielelezo kifuatacho

D C

KIMIMINIKA GESI
YABISI

A B
Herufi ipi huwakilisha tendo la kuyeyuka katika mchoro unaowakilisha
maada hapo juu?.............................................................................................
11. Lipi kati ya mabadilliko yafuatayo ni badiliko la kikemikali?...................
(a) maji kuwa barafu (b) kuyeyuka kwa barafu (c) kuchacha kwa maziwa
(d) maji kuwa mvuke (e) mvuke kuwa maji
12. Kipimo cha uwezo wa elementi Fulani kufanya muungano na elementi
nyingine huitwa ……………….. (a) Radikali (b) kompaundi (c) molekyuli
(d) valensi (e) Ato
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 46
13. Aluminiumu ina valensi ngapi? (a)3 (b)2 (c)1 (d)4 (e)5
14. H2O hii ni fomula ya ……………… (a) Chumvi (b) maji (c) sukari aina ya
glukosi (d) komponenti (e) maziwa
15. C6 H12 O6 fomula hii ya sukari aina ya glukosi, ina maana kwamba
molekyuli moja ya sukari ina atomu … za kaboni (a)8 (b)12 (c)6 (d)24 (e)1
16. Kamilisha mlinganyo ufuatao wa pambano la kikemikali
ELEMENT ELEMENTI (a)kompaundi (b)Metali (c)elementi
(d)Atomu (e)maziwa
17. Maji ,kutu ,chumvi na gesi ya kaboni dioksidi hii ni mifano ya …….…
(a) kompaundi (b)Elementi (c)Molekyuli (d)radikali (e)Asidi
18. Kazi ni zao la ……… (a) uzito na uzani (b) kani na umbali (c) urefu na
upana (d) Msukumo na msuguano (e) uwezo na nishali
19. Unyafuzi au chirwa ni utapiamlo unaosababishwa na upungufu
wa…………. mwilini (a) Vitamini (b) kabohidrati (c) fati (d) protini (e) maji
20. Ukosefu wa vitamin B1 mwilini husababisha ugonjwa wa …………
(a)kiseyeye (b)matege (c)ukavumacho (d)beriberi (e)Moyo
21. Sayari kubwa kuliko zote ni ………..(a) Zebaki (b) Sumbula (c)pluto
(d) zuhura (e)sarateni
22. Sayari maarufu kwa jina la “nyota ya asubuhi “kutokana na kuonekana
iking’aasana angani hasa nyakati za alfajiri huitwa ………….. (a) Dunia
(b) Zuhura (c) Utaridi (d) sarateni (e) mekyuri
23. Mama mjamzito huhitaji kwa wingi vyakula vyenye virutubisho
vya……… (a) protini na vitamini (b) fati na vitamin (c) Kabohidrate na
chumvi chumvi za madini (d) fati na kabohidrati (e) vitamin na sukari
24. Taswira hufanyika kutokana na ……………. (a) Mwanga kushindwa
kupenya maada (b) kusharabiwa kwa mwanga (c) kuakisiwa kwa mwanga
(d) mwanga kuwa hafifu (e)mwanga kuwa mkali mno
25. Chunguza kwa makini taswira ifuatayo ya neno SAYANSI.

Je, taswira zenye muonekano huu ufanyika katika nini? (a) Lenzi
mbinuko (b) lenzi mbonyeo (c) uso wa kioo bapa (d) uso wa karatasi (e) uso

26. Katika mwili wa mwanamke baada ya gameti ya kike kurutubishwa


Mimba huhifadhiwa katika ………………. (a) Mirija ya folopia (b) seviksi
(c) uke (d) ovary (e)uterasi
27. Mchakato wa viumbehai kuongezeka idadi huitwa ………… (a).Balehe
(b) kukua (c) kuchanua (d) uzazi (e) kujamiiana
28. Virusi vya UKIMWI kwa kiasi kikubwa hushambulia seli zipi za damu?
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 47
(a) seli nyeupe za damu (b) seli nyekundu za damu (c)seli mundu(d)plazma
(e) chembel
29. Sehemu ya damu yenye nyukilia ni….. (a) ute wa damu (b) chembe
sahani (c)plazma (d) seli nyeupe za damu (e) seli nyekundu za dam
30. Homoni inayouandaa mwili wa binadamu kukabiliana na hatari iliyo
mbele yake ni …… (a) thairoksini (b) Adrenalini (c) parathormoni
(d) projesteroni (e) Estrojeni 31. Tezi ndani kuu huitwa ……………………….
(a) pituitari (b) adrenalini (c) parathairoidi (d) thairoidi (e) korodani
32. Homoni inayodhibiti ukuaji na mabadiliko katika mwili wa mwanamke
ni ……… (a) estojeni (b) testosterone (c) adrenalini (d) projestoroni
(e) homoni za pituitari
33. Samaki hupumua kwa kutumia ………… (a) ngozi (b)vitundu kwenye
mwili Tumboni (c) mapafu (d) mkia (e)matamvua
34. Kundi lipi la wanyama huweza kuishi nchi kavu na katika maji?
(a) ndege (b) samaki (c) reptilian (d) amfibia (e) mamalia
35. Nishati ipatikanayo kutokana na mjongeo wa elektroni huitwa ………
(a) mwanga (b) sauti (c) umeme (d) msuguano (d) mlipuko
36. Kutu ni matokeo ya chuma kukutana na…………(a) mwanga (b) sauti
(c) umeme (d) msuguano (d) maji na hewa
37. Chunguza kielelezo kifuatacho cha wenzo. Ikiwa kifaa hiki kitafanya
kazi ya kung’oa misumari katika ubao.Je, wakati huo kitawakilisha nyenzo
daraja lipi?

(a) Kwanza (b) pili (c) tatu (d) kwanza na la pili (e) tatu na la kwanza
38………….ni msukumo unaosababisha mjongeo wa kiolwa (a) nyutoni
(b) juli (c) kani(d) uzi (d) gurudumu
39. Dalili kubwa ya kuvunjika mfupa katika sehemu fulani ya Mwili ni
ipi?. (a)sehemu
hiyo hupinda (b) mfupa lazima utoke nje (c) maumivu makali, kuvimba
na sehemu hiyo, kushindwa kufanya kazi (d) damu huvuja ovyo (e) kuhisi
joto kali katika sehemu husika
40.Elimu inayohusu kutegemeana kwa viumbe katika mazingira huitwa ____
(a) saikolojia (b) ikolojia (c) metamosisi (d) epidemisi
41. Katika wenzo msawazo ifuatayo kokotoa thamani ya M

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 48
M Gm 20
Sm 4 Sm 2

42.Taja sehemu mbili za utumbo mwembamba. __________ na _________


43. Hatua ya ukuaji wa kipepeo yenye madhara makubwa sana kwa
mazingira ni __________________________________________________
44. Mshale wa dira huelekea upande wa:__________________________
45. Andika valensi ya kalisiamu _____________________________

JARIBIO LA 16
1. Kitendo cha mizizi kufyonza maji na madini kutoka katika udongo
huitwa____ (a) Uvukizaji (b) Upumuaji (c) Osimosis (d) difyusheni [ ]
2. Katika mfumo wa mifupa maungio hushikiliwa na ________________
(a) Ligamenti (b) gegedu (c) Kano (d) Nyuzi (e) Neva [ ]
3. Ipi kati ya ogani zifuatazo haipatikani katika mfumo wa mmeng’enyo wa
chakula [ ] (a) Koromeo (b) Utumbo mwembamba (c) Kongosho (d) Ini
(e) Figo
4. Ugonjwa wa kifua kikuu (TB) huathiri zaid ogani gani ya mwili?
(a) Mapafu (b) Figo (c) Ngozi (d) Pua (e) Utumbo [ ]
5. Chakula kinapofika mdomoni huchanganyikana na kimeng’enya
ambacho huvunja vunja vyakula vya __________________________
(a) Protini (b) Wanga (c) Vitamini (d) Mafuta (e) Chumvi [ ]
6. Kifaa ambacho hutumia kielekezi kumwelekeza mtumiaji wa tarakilishi kuamuru au
kuelekeza tendo Fulani analotaka kufanya huitwa: (A) kiteuzi (B) monita
(C) kibodi (D) kasha mfumo
7. Vifuatavyo ni visakuzi vya mtandao isipokuwa: (A) ruta (B) google chrome
(C) mozilla firefox (D) internet explorer
8. Kipimo cha Fahrenheit huanzia namba ngapi? [ ]
(a) O0F (b) 860 F (c) 2120F (d) 320F (e) 120F
9. Vimiminika vyenye uwezo wa kutanuka pindi joto linapoongezeka na
kusinyaa pindi jotolinapopungua hutumika katika kutengeneza ______ [ ]
(a) Haidromita (b) KIpima Joto (Themomita) (c) Kipima mvua
(d) Haigromita (e) Haigromita
10. Ni aina ipi ya vijidudu husababisha ugonjwa wa kipindupindu. [ ]
(a) Protozoa (b) bacteria (c) Amoeba (d) Plasimodiam (e) Virusi
11. Kemikali inayotumika kutibu maji ya kunywa huitwa ___________ [ ]
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 49
(a) Klorini (b) Kalisi (c) Kabondayoksaidi (d) Florine (e) Ayodini
12. Ni yapi kati ya maelezo yafuatayo NI KWELI kuhusu mimea jamii ya
kunde? [ ]
(a) Ina sehemu kuu mbuli (d) Huongeza rutuba katika udongo
(b) Ni mimea isiyo na maua (e) Mbegu zake husambazwa na maji
(c) Huzaliana kwa kugawanyika
13. Ni sehemu ipi ya damu ambayo haemoglobini kupatikana? [ ]
(a) Fibrinojeni (b) Chembe sahani (c) Plasma (d) Seli hai nyeupe za damu
(e) seli hai nyekundu za damu.
14. Unaweza kuwatambua wanyama wanaokula nyama kwa kuangalia [ ]
(a) Meno yao (b) macho yao (c) masikio yao (d) Sauti zao (e) Matumbo yao
15. Mwale wa mwanga unapotua kwenye uso angavu hugonga na kurudi
kitendo hiki Huitwa (a) Kusharabu (b) Kupenya (c) Kuakisi (d) Kuvunja
(e) Kupinda [ ]
16. Sehemu ya sikio la binadamu inayokusanya mawimbi ya sauti
inaitwa____________ [ ] (a) Neva ya sikio (b) Cochlea (c) Ngoma ya sikio
(d) Mrija (e) Pina
17. Dalili kuu ya ujauzito kwa binadamu ni____________________
(a) Kutapika (c) Kulala muda wote (d) Kukoma hedhi (b) Matiti kutanuka
(e) Kuhisi kichefuchefu.
18. Chakula kwa ajili ya watoto kinatakiwa kiwe na kiwango cha ______ ili
kusaidia kuimarisha meno na mifupa yao. [ ]
(a) Protini (b) Kabohaidreti (c) madini chumvi (d) Vitamini (e) Mafuta
19. Ni lenzi gani hutumika kukuza vitu? [ ] (a) Duara (b) Lenzi mbonyeo
(c) Lenzi mbinuko (d) Lenzi duara (e) Lenzi maalumu
20. Badiliko la maada linalopekelea badiliko la uzito wa maada huitwa. [ ]
(a) Badiliko la kiumbo (c) Badiliko rejeshi (d) Badiliko la haraka
(b) Badiliko la muda (e) Badiliko la kikemikali
21. kimeng’enya kinachobadili protini kuwa aside za amino huitwa ____
(a) amilasi (b) peptoni (c) peptaid d) ptylin (e) melatonin
22. Sababu ya hewa ya kabondayoksaidi kutumika kuzimia moto ni ___[ ]
(a) Husaidia vitu kuungua (b) Hairuhusu kuungua (c) Haina harufu
(d) Inaweza Kulipuka (e) Hubadili maji ya ndumu kuwa kama maziwa.
23. Wakati wa uchavushaji chavua husafiri kuelekea kwenye ________ [ ]
(a) Ovari kutoka kwenye ovyuli (d) Stigma kutokea kwenye antha
(b) Antha kutoka kwenye stigma (e) Staili kutokea sepali
(c) Stima kutokea kwenye petali
24. Karatasi nyekundu ya litmasi ikitumbukizwa kwenye …………..
hubadilika rangi kuwa bluu [ ] (a) Besi/nyongo (b) Chumvi (c) Pigmenti za
ini (d) Sukari (e) Asidi/tindikali

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 50
25. Maelezo yapi ni sahihi kuhusu Ampia? [ ] (a) Ni kifaa cha kupimia
mkondo ukinzani (b) Ni kifaa cha kupima nguvu ya umeme (c) Ni kizio cha
mkondo wa umeme (d) Hupimwa kwa kutumia viltimita (e) Ni kifaa cha
kupimia ukinzani
26. Ugumba kwa binadamu unaweza kusababishwa na _______ [ ] (a) Kula
kupita kiasi (b) Utapiamlo (c) kukosa vitamin C (d) Magonjwa ya zinaa
27. Vifuatavyo hupatikana katika seli ya mnyama na seli yam mea
ISIPOKUWA [ ] (a) Nyuklia (b) Chembeumbijani (c) Vakuli (d) Uteseli
28. Mzigo ulipandishwa mita 8 baada ya mkono wa jitahada kuvutwa mita
24 kuelekea chini, Uwiano wa mwendo dhahiri ni __________________ [ ]
(a) 8 (b) 4 (c) 2 (d) 10 (e) 3
29. 29. Transipiresheni katika mimea ni muhimu ili kusaidia ________ [ ]
(a) Kuupoza mmea (d) Kupunguza matumizi ya maji (b) Kuondoa kiasi
cha maji kisichohitajika (e) Kubeba chakula cha mmea (c) Kukua vizuri
30. Ni mlango upi wa fahamu utautumia kutofautisha joto na baridi [ ]
(a) Ngozi (b) Jicho (c) Sikio (d) Pua (e) Ulimi
31. Bwana Donald alitumia nguvu ya 30 N kubeba gunia la mchele umbali
wa mita 5. Kazi aliyofanya ni? (a) 4 Joule (b) 120% (c) 4 M (d)150 Joule [ ]
32. Ni mstari unaonesha pembe ya mstari ulioakisiwa? [ ]

33. Kuta za majengo ya mikutano na studio zimewekewa vitu laini ili


kuweza _______ (a) Kusharabu sauti (b) Kusambaza sauti (c) Kuakisi sauti
(d) Kuzuia Sauti (e) Kupindisha sauti [ ]
34. Ni gesi ipi huhitajika na mmea ili kuweza kutengeneza protini? [ ]
(a) Kabondaiyoksaid (b) Oksijeni (c) Nitrojeni (d) Haidrojeni (e) Salfu
35. Njia bora ya kujikinga na virusi vya ukimwi na ukimwi ni [ ]
(a) Kuepuka kuvaliana nguo (b) Kuhudhuria Kliniki (c) Kuepuka ngono
isiyo salama (d) Kula mlo kamili (e) Kuepuka kuongea na waathirika
36. Joto kutoka katika jua huweza kuufikia uso wa dunia kwa njia ya ____
(a) Mpitisho (b) Mgandamizo (c) Mvukizo (d) Mnururisho (e) Mvutano
37. Kati ya vifuatavyo kipi huathiri rangi ya mkojo? [ ]
(a) Maziwa (b) Damu (c) uzito wa mwili (d) msongo wa mawazo (e) dawa
38. Faida kuu ya uzazi wa mpango ni ___________ [ ] (a) Kuongeza idadi
ya watoto (b) Kuwapa watoto elimu (c) Kuwa na uwezo kutoa huduma
muhimu (d) Kupata uwezo wa kujenga nyumba za kisasa (e) Kuepuka
matatizo
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 51
39. Ni sehemu ipi ya ubongo huratibu kuona, kusikia na kunusa? [ ]
(a) Ubongo wa mbele (b) Uti wa mgongo (c) Ungwe mgongo (d) Medula
oblongata (e)Neva
40. Matumizi ya kondomu ni moja kati ya njia za uzazi za ………………..
(a) asili (b) kienyeji (c) kizembe (d) kisasa (e) kidini

SEHEMU B: ANDIKA JIBU


41. Aina mbili za nishati zinazotolewa na moto ni
(i) ……………………………
(ii) …………………………..
42. Mshipa unaotoa damu kwenye mapafu kupeleka moyoni unaitwa …….
43. ………………………. Ni tishu ambayo ipo katika hali ya kimiminika.
44. Tezi ya ovary huzalisha homoni ya ………………….. na ……….…………
45. Mche wa sumaku ukiufunga kamba na kuunin’giniza hewani ncha zake
zitaelekea upande wa …………………………… na ………..……………………

JARIBIO LA 17
1. Mshipa mkuu unaotoa damu kwenye mapafu kuelekea kwenye moyo
unaitwa ________ A. Vena kava B. Ateri ya palmonari C. Vena ya palmonari
D. Aorta E. Vena [ ]
2. Mbu jike aina ya anofelesi huambukiza ugonjwa wa_________________
A. Matende B. Malale C. Kichocho D. Malaria E. Kipindupindu [ ]
3. Joto husafiri katika maada ya yabisi kwa njia ya ______
A. Mnururisho B. Msafara C. Mpitisho D. Mitetemo D. Kusharabu [ ]
4. Sehemu ya ubongo wa binadamu inayo tawala matendo yote ya hiari
inaitwa ___ A. Ubongo wa mbele B. Ubongo wa nyuma C. Ubongo wa kati
D. Ugwe mgongo E. Aksoni [ ]
5. Hatua ya pili katika ukuaji wa Mende ni___________
A. Lava B. Tunutu C. Buu D. Mende kamili E. Yai [ ]
6. Ualbino ni matokeo ya ngozi kukosa jeni inayoitwa___________ [ ]
A. kiini (nyuklias) B. kromosomu C. jeni D. Melanini E. saitoplazim
7. Kwa wastani mwili wa binadamu una jumla ya mifupa__________
A. 200 B. 106 C. 306 D. 100 E. 206 [ ]
8. ____________ ni njia kamili ya umeme.
A. waya B. glopu C. amita D. sakiti E. waya wa ethi [ ]
9. Ipi ni sahihi kuhusu Virusi Vya Ukimwi?

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 52
A. Hushambulia seli hai nyekundu za damu B. Hushambulia
chembesahani C. Hushambulia seli hai nyeupe za damu D. Huimarisha
kinga ya mwili E. Hushambulia watu wazima tu [ ]
10. Yafuatayo ni mabadiliko ya kiumbo isipokuwa_____________
A. Kuyeyuka kwa mshumaa B. Maji kuwa barafu C. Kuyeyuka kwa
chumvi D. Chuma kupata kutu E. barafu kuwa maji (kimiminika) [ ]
11. Kifaa gani kati ya vifuatavyo unaweza kukitumia kutafutia sindano
iliyopotea kwenye kikapu cha unga? __ A. darudini B. hadubini
C. sumaku D. seismografu E. macho [ ]
12. Ifuatayo si mashine rahisi A. kisu B. kitasa C. opena D. Toroli
13. Mgonjwa anayaharisha anatakiwa kupewa huduma ya kwanza ifuatayo
A. Kumpa chakula cha kutosha B. Kumpeleka kwa mganga wa asili
C. Kumpa mchanganyiko wa maji, limau, sukari na chumvi
D. Kumpa vidonge vya maumivu E. Kumpeleka kwa daktari [ ]
14. Hatua ya tatu katika kuandika ripoti ya jaribio la kisayansi ni;
A. Njia B. Vifaa C. Kusudi D. Matokeo E. Hitimisho [ ]
15. Sehemu inayosafirisha mkojo kutoka kwenye kibofu kwenda nje ya
Mwili inaitwa: A. Mrija wa manii B. Ureta C. Urethra D. Mirija ya falopio
E. Vena ya renali [ ]
16. Eneo linaloathiriwa na kani ya sumaku katika mche wa sumaku
linaitwa___A. Ncha ya sumaku B. ncha ya kaskazini C. ncha ya kusini
D. Uga wa sumaku E. katikati ya sumaku [ ]
17. Ipi ni kazi ya homoni ya parathormoni_____ A. Kurekebisha kiasi cha
maji Mwilini B. Kurekebisha na kudhibiti matumizi ya madini ya kalisiam
mwilini C. Hurekebisha ukuaji wa uterasi D. Hurekebisha kiasi cha sukari
Mwilini E. Kuandaa mwili kuweza kukabiliani na hatari [ ]
18. Kabohaidreti huanza kumeng’enywa kikemikali katika_________ [ ]
A. Puru B. utumbo Mwembamba C. ini D. Utumbo mpana
E. Mdomo (kinywa)
19. Mama mjamzito anashauriwa kula vyakula aina ya________ ili
kuongeza damu Mwilini A. Protini B. Fati C. Chumvi chumvi na madini D.
Mboga za majani E. chipsi [ ]

20. Alama hii huwakilisha nini katika michoro ya sakiti za


umeme? A. Ukinzani B. Taa ya umeme C. seli D. Galvanometre E. soketi
21. Mbu aina ya culex hueneza ugonjwa wa _______________ A. kichocho
B. malaria C. malale D. matende E. anaemia D. E. [ ]
22. Zifuatazo ni sehemu zinazounda sehemu ya kike ya ua
A. Stigma, antha na ovary B. Antha, staili na stigma C.Filament, ovari
na ovyoli D. Ovari, staili na poleni E. Ovari, staili na stigma [ ]
23. Mahitaji muhimu kwa mbegu kuota ni ________
A. Maji, Udongo na Kabondayoksaidi B. Udongo,Maji na oksijeni
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 53
C. Maji, oksijeni na joto la kiasi D. Maji, mbolea na mbegu
E. Kabondayoksaid, maji na joto kali [ ]
24. Chunguza mlinganyo ufuatao wa kisayansi. Je herufi M imesimama
badala ya ___[ ]
BESI + ASIDI = CHUMVI+ M A. NaCl B. Co2 C. O2 D. H2O E. Mg
25. Badili 32OF kuwa sentigredi A. 189.6OC B. 896OF C. 0OC D. 32OC 3.2OC
26. Sehemu ya mbegu aina ya daikotiledoni inayohifadhi chakula cha mmea
mchanga Inaitwa A. Kikonyo B. Mizizi C. Embriyo D. Testa E. kotiledoni
27. Tafuta mzigo uliobebwa na mashine katika umbali wa Sm 900; Ikiwa
kazi iliyofanyika ni Joule 45 A. 20N B. KG 20 C. 50N D. KG 50 E. 5N
28. Katika mwili wa binadamu utungisho hufanyika katika sehemu
inayoitwa____ A. Ovari B. Ureta C. Mirija ya falopio D. Uterasi E. Uke [ ]
29. Ukosefu wa virutubisho vyenye vitamin A katika chakula
husababisha______ A. Matege B. Ukavu macho C. beriberi D. kwashakoo
30. Viumbehai vimeundwa kwa chembechembe ndogo sana ziitwazo:
A. atomi B. Testa C. poda D. spirako E. seli [ ]
31. Zifuatazo ni kazi za mifupa katika Mwili wa binadamu isipokuwa ____
A. Kulinda sehemu za ndani B. Kuwezesha Mwili kujongea C. Kusaidia
kuzalisha seli hai zadamu D. kuupa Mwili umbo lake E.Kusafirisha chakula
32. Tafuta manufaa ya kimakenika katika mashine iwapo mzigo wa N
750,utahitaji jitihada ya KG 15 A. 15 B. 5 C. 50N D. 50KG E. 0.5
33. Filamu katika kamera hufanya kazi sawa na ______katika jicho
A. Lenzi B. Misuli sihari C. retina D. konjaktira E. irisi [ ]
34. Kitendo cha mmea kupoteza maji yake kupitia stomata huitwa_______
A. osmosis B. Difyusheni C. Transipiresheni D. kusharabu
E. Fotosinthesis
35. Kundi la viumbe hai ambalo linaweza kujitengenezea chakula chake
ni__________ A. Simba B. Amfibia C. binadamu D. Wanyama E. mimea [ ]
36. Asilimia kubwa ya mwili wa binadamu ni___________
A. Damu B. maji C. misuli D. neva E. ogani [ ]
37. Yupi kati ya wanyama wafuatao hana uti wa mgongo
A. Nyoka B. samaki C. mnyoo D. binadamu E. mbwa [ ]
38. Mbung’o hueneza ugonjwa wa_____ [ ] A. kipindu pindu B. malaria
C. malale D. homa ya matumbo E. ukavu macho
39. Jani la mmea lifuatalo ni la mmea jamii ya___________

A. monokotiledoni B. daikotiledoni C. Mnazi D. ndizi E. Ngano [ ]


Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 54
40. Joto la jua hutufukia duniani kwa njia ya___________ [ ]
A. Mnururisho B. Ombwe C. Msafara D. Mpitisha E. Msafara na mpitisho

JAZA NAFASI ZA WAZI


41. Kitu chochote chenye uzito na kinachochukua nafasi hujulikana kwa
jina la____________________________________________________________
42 . Kizingiti cha mgando cha maji ni nyuzi _________________ sentigredi.
43. Badili 1000C kuwa farenhaiti ______________________________________
44. Matendo yote yasiyo ya hiari huratibiwa na sehemu ipi ya ubongo_____
45. Sehemu ya jicho la binadamu inayorekebisha ukubwa wa pupili
inaitwa_______________________________________________________________

JARIBIO LA 18
1. Hewa itumiwayo na seli za wanyama kuunguza chakula ili kupata
nishati huitwa………….. a)kabonidayoksaidi, b)Oksijeni, c)Ayoni,
d)Amonia. [ ]
2. Figo za binadamu zipo upande wa kulia na kushoto nyuma
ya………...a)mapafu, b)tumbo, c)ini, d)moyo. [ ]
3. Maji hutolewa nje ya mapafu yakiwa katika hali ya………….. a)gesi,
b)joto, c)mvuke, d)baridi. [ ]
4. Homoni husafirishwa na………kwenda sehemu husika za mwili.
A)maji, b)tezi, c)damu, d)seli. [ ]
5. Mlango unaounganisha uke na mji wa mimba huitwa… …a)seviksi,
b)vulva, c)uterasi, d)ovary. [ ]
6. Kimeng`enya cha amilesi hubadili wanga kuwa………… a) glaikojeni,
b)sukari, c)tindikali za amino, d)maltosi. [ ]
7. .huipa damu rangi nyekundu. a)nyongo, b)madini, c)haemoglobini,
d)ayani. [ ]
8. Mirija inayosafirisha maji na chumvichumvi katika mimea
huitwa…….. a) floemu, b)vinyweleo, c) mizizi, d)zailemu. [ ]
9. Kemikali ipatikanayo katika mmea wa tumbakuhuitwa………….
a)haidroklorini, b)nikotini, c)tindikali, d)kafeini. [ ]
10. Mbu anayeeneza ugonjwa wa homa ya manjano
huitwa……….a)anofelesi, b)kuleksi, c)anofelesi jike, d)aedesi. [ ]
11. Mwanga husafiri katika mstari ……………a)ulionyoka,
b)uliopinda, c)sambamba, d)angavu. [ ]
12. Kuna aina ……….za sakiti. a)tatu, b)mbili, c)nne, d)tano. [ ]

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 55
13. Nyenzo daraja la ……jitihada huwa katikati ya mzigo na
egemeo. a)kwanza, b)pili, c)tatu, d)nne. [ ]
14. Kipi si chanzo cha umeme kati ya hivi vifuatavyo? a)Upepo,
b)jua, c)Maporomoko ya maji, d) Glopu. [ ]
15. Rangi ya kwanza juu katika mpangilio wa rangi za jua katika
prizimu ni…….. a)nyekundu, b)bluu, c)hudhurungi, d)urujuani. [ ]
16. Ugonjwa wa unyafuzi husababishwa na upungufu wa
virutubisho vya………….a)wanga, b)protini, c)vitamin, d)mafuta.
17. Huduma ya kwanza hutolewa na…….a )mganga wa jadi, b)mtu
yeyote, c)hospitalini d)popote. [ ]
18. Kuna hatua ngapi za kufuata wakati wa kuandaa taarifa ya
jaribio la kisayansi? a)Nne, b)Tano, c)Sita, d)Nane. [ ]
19. ………….ni taarifa zinazokusanywa wakati wa kufaya jaribio la
kisayansi. a)Uchunguzi, b)Data, c)Jaribio, d)Uchambuzi. [ ]
20. Maada ambayo inaweza kupatikana katika hali zote za maada ni
ipi kati ya zifuatazo? a) Fe b) Ca c) Al d) H2O
21. Maada zipi kati ya zifuatazo ni radikali?. a) NH4 b) H2 c) Ag
d) Ca(Cl)2 [ ]
22. Kuna aina ngapi za uchavushaji? a)Mbili, b)Tatu, c)Nne, d)Tano.
23. Kitendo cha mmea kujitengenezea chakula huitwa………
a)usanisi nuru, b)hairdo pizini, c)fototropizini, d)stomata. [ ]
24. Maada ambazo huruhusu mwanga kupita upande mmoja tu
zinaitwa b………..a)angavu dufu b)andavi, c)kikinza, d)spectra. [ ]
25. ………..ni uwezo wa atomi kuungana kikemikali na atomi
nyingine. a)Valensi, b)Radikali, c)Kampaundi, d)Atomi.. [ ]
26. Watu waishio milimani wanashauriwa kula zaidi vyakula vya
……... a)vitamini, b)protini, c)wanga, d)fati. [ ]
27. Homoni ya Oestrojeni ni homoni ya … a)kike, b)watoto, c)kiume,
d)wazee. [ ]
28. Mirija ambayo husafirisha chakula kwenye mimea
huitwa………….a)zilemu, b)foelemu, c)stomata, d)jani. [ ]
29. …..ni hali ya damu kutoganda katika jeraha. a)Anemia, b)Seli
mundu, c)Himofilia, d)kiharusi. [ ]
30. Utando wa ngozi unaotenganisha kifua na na fumbatio (tumbo)
huitwa……..a)kiribahewa, b)broncha, c)bronchiole, d)kiwambo. [ ]
31. Kipepeo anapitia hatua ngapi za mabadiliko yake? …………..…
32. Mbegu zenye ghala mbili huitwa ……………………………..………
33. Ikiwa Masanja alinyanyua mzigo kwa umbali wa meta 2 kwa
kani ya 6 nyutoni. Je,Masanja alifanya kazi kwa kiasi gani? ……….
34. Pembe ya mwale mtuo ni sawa na pembe ya mwale ………………
35. Kuna aina ngapi za mashine? …………..….…………………….....
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 56
36. Njia inayotumika kubadili maada ya gesi kuwa kimiminika ni…
37. …. ni mlango wafahamu ambao hupokea vichocheo vya joto.
38. Sehemu ya ua inayovutia wadudu huitwa…………….…..…………
39. …………………….. ni madini yenye ukinzani mdogo kabisa na
ndiomaana hutumika kutengenezea kinga radi
40. Ni gesi gani inayo sharabiwa kwenye damu wakati wa
upumuaji? …..........................................................................................
41.‘‘Ncha mbili za sumaku zinazofanana hukwepana ila ncha mbili za sumaku
zisizofanana huvutana’’
Hii ni ………………………………………………………..…….. ya sumaku.
42. Kuna aina mbili za kinga ya mwili ambazo ni kinga ya
……………….………..……..……. na …………………………………….……
43. Taja vipimo viwili vya ukimwi……………….. na …………………
44. Amina alitumia kani ya nyutoni 20 kusogeza mzigo wenye uzito
wa kg 10. ikiwa kazi aliyofanya ni joule 60. Umbali utakuwa mita …..
45. Mwendokasi wa upepo hupimwa kwa kifaa kiitwach ……………

JARIBIO LA 19
1. Sauti iliyoakisiwa huitwa……………………….. [ ] (a) mazigazi (b) kivuli
(c) mwangwi (d) kelele (e) muziki
2. Kizio cha kani ni…….. [ ] (a) Kilogramu (b) Joule (c) Nyutoni (d) Meta
(e) Gramu
3. Ili damu ipate oksijeni katika mwili wa binadamu lazima ifike katika [ ]
(a) Ini (b) Figo (c) Moyo (d) Mapafu (e) Tumbo
4. Mtu mwenye upungufu wa virutubisho vya Kabohaidreti mwilini ni
rahisi Zaidi kupata ugonjwa gani? (a) Moyo na msukumo mkubwa wa
damu (b) kansa (c) Nyongea (d) kwashakoo (e) kuvia kwa ukuaji wa akili
5. Vinyesi na vitu vya Wanyama na mimea iliyooza [ ] (a) hufanya udongo
usifae kwa kilimo (b) vinakaribisha wadudu wengine wanoharibu mazao
(c) vinaongeza mbolea na mboji kwenye udongo (d) havina umuhimu
kwenye udongo (e) vinatumika kama chambo kwenye uvuvi
6. Ukiweka sarafu ya shilingi 100 katika beseni lenye maji, sarafu hiyo
inaonekana imepanda juu. Hali hiyo hutokea kwasababu…………..…. [ ]
(a) sarafu hiyo ni nyepesi (b) macho yana matatizo (c) mwanga umenyooka
(d) maji ni kidogo (e) mwali wa mwanga hupinda unapoingia kwenye maji
7. Mwanga na sauti vina tabia zinazofanana isipokuwa moja tu. Tabia hiyo
ni ipi? [ ] (a) kusambaa (b) kupinda (c) kuakisiwa (d) kusharabiwa (e)kupita
kwenye vakyumu
8. Kwanini chupa za soda na bia hazijazwi hadi pomoni? (a) kwaajili ya
nafasi ya gesi (b) kuruhusu kutanuka wakati wa hali ya hewa ya joto

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 57
(c) husaidia kufungua chupa kwa urahisi (d) ikijazwa huweza kumwagikia
mnywaji (e) kupunguza gharama
9. Volcano hai hutoa kimiminika kizito kiitwacho………………… [ ]
(a) kreta (b) magma (c) gesi (d) lava (e) volkano
10. Chanzo cha chakula kwa Wanyama ni………………… [ ]
(a) mimea na wanyama (b) wanyama (c) maziwa (d) maharage (e) mimea
11. kabali ni wenzo ambao hutumika ………………………. Vitu. (a) kupasua
(b) kubana (c) kusaga (d) kuinua (e) kushusha
12. Nishati ya joto kutoka katika jua huifikia ardhi kwa njia ya ……… [ ]
(a) mpitisho (b) msafara (c) mnururisho (d) kuvukiza (e) kuvushwa
13. Goita ni ugonjwa unaosababishwa na upungufu wa…………… [ ]
(a) ayodini (b) vitamini (c) chuma (d) kalisiamu (e) oksijeni
14. Kuna hatua ngapi katika metamofosisi isiyokamili? ………………… [ ]
(a) mbili (b) tatu (c) tano (d) nne (e) moja
15. Kipi kinatangulia VVU au UKIMWI? [ ] (a) UKIMWI (b) TB (c) VVU
(d) hakuna kinachotangulia (e) vyote kwa pamoja
16. Ipi kati ya alama zifuatazo huiwakilisha galvanometa? [ ]

(a (b) (c) (d) (e)


17. Tendo lipi kati ya matendo yafuatayo huongeza kinga ya mwili? [ ]
(a) kuvuta sigara (b) kunywa pombe (c) kula vyakula vya mafuta
(d) kufanya maoezi (e) kufanya kazi sana
18. Ipi kati ya zifuatazo ni mashine tata? ………………………….…… [ ]
(a) mtange (b) mkasi (c) cherehani (d) fagio (e) nyundo
19. Upungufu wa protini mwilini hupelekea kuleta ugonjwa wa……… [ ]
(a) Nyongea (b) Pelagra (c) Anemia (d) Goita (e) Unyafunzi
20. Katika mpangilio huu wa hali za maada ni herufi ipi inawakilisha
yabisi? [ ]

(a) (b) (c) (d) (e)


21. Ni sehemu ipi ya mfumo wa utoaji taka mwili haiendani na takamwili
inayotoa? [ ] (a) mapafu-oksijeni (b) figo-urea (c) Ngozi-Jasho (d) Ini-
Nyongo (e) Mapafu-kabonidaiyoksaidi
22. Chuma + Y + maji = Kutu. Herufi Y inawakilisha [ ] (a) Asidi (b) besi
(c) chumvi (d) oksijeni (e) kabonidaiyoksaidi
23. Hatua ipi ya ukuaji wa kipepeo ina faida kwa mimea? [ ]
(a) Pupa (b) Lava (c) Mdudu Kamili (d) Mayai (e)
24. Tezi ipi kati ya tezi zifuatazo hailandani na homoni inayozalisha [ ]
(a) Thairoidi-Thairoksini (b) Adrenali-Adrenalini (c) Korodani-
Projesteroni (d) Kongosho-Insulini (e) Pituitari-Homoni za ukuaji
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 58
25. Kokotoa thamani ya ‘K’ [ ]

(a) gramu 6 (b) gram 8.57 (c) gramu 84/7 (d) gramu 126/7 (e) gramu 12.86
26. Chunguza mlishano ufuatao. Nini kitatokea kama Simba watahama
kutoka kwenye hiyo mbuga? Nyasi Swala Simba [ ] (a) nyasi
zitaongezeka (b) nyasi zitapungua (c) swala watapungua (d) nyasi zitabaki
vilevile (e) Simba watapungua
27. Jina lingine la viribahewa ni………………… [ ]
(a) brachi (b) yurea (c) Alveoli (d) trakea (e) mapafu
28. Ipi kati ya zifuatazo ni simboli ya Potasiamu? [ ] (a) P (b) K (c) Pb
(d) Na (e) Ag
29. Chunguza mchoro ufuatao wa sumaku mche. Herufi A na B
zinawakilisha. [ ]

(a) Ncha ya kusini (b) Ncha ya kaskazini na kusini (c) Ncha ya kusini na
kusini (d) Ncha ya kaskazini na kaskazini (e) Ncha zinazofanana
30. Myeyuko wa sukari na chumvi ni huduma ya kwanza ya …………… [ ]
(a) kutetemeka (b) kuungua (c) kutapika na kuharisha (d) kizunguzungu
(e) kuzimia
31. Mkondo wa umeme wa ampia 0.8 unapita katika waya wenye ukinzani
wa ohm 24. Tafuta kani elektroni mwendo………..… [ ] (a) 19.2 V (b) 19V
(c) 30V (d) 24V (e) 192V
32. Vena pekee inayobeba damu yenye oksijeni huitwa [ ] (a) vena ya
palmonari (b) ateri ya palmonari (c) vena kava (d) aota (e) vena ya renali
33. ………………… ni kundi la wanyama ambao joto la miili yao hubadilika
kutokana na mazingira. [ ] ndege (b) homothemiki (c) poikilothemiki
(d) vetebrata (e) Mamali
34. Ili mbegu iote inahitaji……… [ ] (a) mwanga wa jua,hewa, oksijeni
(b)maji,hewa,joto (c) maji, hewa, haidrojeni
(d) mwanga,kabondayoksaidi,klorofili (e) joto, na hewa
35. Kifaa kinachotumika kupima jotoridi la mwili huitwa [ ]
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 59
(a) Barometa (b) Galvanometa (c)Themometa (d) Hadubini (e) Anemometa
36. Mabadiliko gani yatatokea kama mtu atapumulia kwenye uso wa kioo?
(a) kuganda (b) kuyeyuka (c) kuvukishwa (d) matonesho (e) kutanuka
37. Wakati mtu anasukuma toroli mikono yake na mishiko ya toroli
hufanya. [ ] (a) Egemeo (b) Mzigo (c) Jitihada (d) Nyenzo (e) Nishati
38. Vinundu vilivyo kwenye mimea jamii ya kunde vina bakteria ambao
husharabu na kubadili hewa gani angani? [ ]
(a) Naitrojeni (b) Yurea (c) Fosforasi (d) Haidrojeni (e) Salfeti ya amonia
39. Sehemu ya mbegu ambayo huhifadhi chakula cha mmea kwenye udongo
ni …..… [ ] (a)Embriyo (b) Testa (c) Kotiledoni (d) Epikapi (e) Kianza mche
40. Tunashauriwa kupanda miti kwa wingi sehemu zilizo kame ili: [ ]
(a) Kuzuia mmomonyoko wa udongo (b) kuleta kivuli (c) kupata kuni
(d) kupata mbao (e) kusaidia kuleta mvua

SEHEMU B: JAZA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI


41. Chakula kilichomeng’enywa husharabiwa katika utumbo mdogo na……

42. Mlay alitumia kani ya Nyutoni 10 kunyanyua mzigo kwa umbali wa


mita 5. Je, atakuwa amefanya kazi kiasi gani?……… ……… ………..……

43.Sehemu ya Ua inayovutia wadudu katika mmea na kusaidia katika


uchavushaji na uchukuaji wa poleni inaitwa………………………………..……

44. Kutokuganda kwa damu husababishwa na upungufu wa vitamini………

45. Tafuta jumla ya ukinzani katika mchoro ufuatao……………………………

JARIBIO LA 20
1. Zilizoorodheshwa hapa chini ni sehemu za jicho la binadamu isipokuwa_
(a) Siliari (b) Retina (c) Mboni (d) shata (e) irisi [ ]
2. Usambazaji wa chakula mwilini hufanywa na .________
(a) Damu (b) Maji (c) hewa (d) Misuli (e) neva [ ]
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 60
3. Kemikali inayotumika kutambua iwapo chakula Fulani ni cha wanga
ni_____(a) Besi (b) Alkoholi (c) Asidi (d) alkahali (e) Ayodini [ ]
4. Kipande cha chuma husafirisha joto kwa njia ya ____________ [ ]
(a) Kuakisi (b) mnururisho (c) mpitisho (d) mnururisho na msafara
(b) (e) msafara
5. Katika mwili wa mwanamke mayai ya uzazi hutengenezwa kwenye ____
(a) Foliko (b) ovari (c) Falopia (d) mji wa uzazi (e) tezi
6. Gurudumu kapi ni mashine __________ (a) Tata itumikayokupandisha
vitu juu. (b) imara iliyoshikishwa na gurudumu dogo (c) yenye meno
yanayoingiliana (d) rahisi itumikayo kupandisha vitu juu
(e) inayotumika kufunga maunzi pamoja.
7. Ni maada ipi kati ya maada zifuatazo zinaweza kuonekana katika hali
ya yabisi, kimiminika, na gesi. __________[ ]
(a) Chuma (b) hewa (c) maji (d) mshumaa (e) kipande cha ubao
8. Nini hutokea mwanga upitapo katika media tofauti___________[ ]
(a) Husafiri kwa kugawa vitu sehemu mbili (b) kusafiri katika mstari
mnyoofu (c) hupinda (d) husafiri ndani ya maji kwa kujikunja
(e) husafiri na kusababisha vitu kupinda
9. Mnyororo wa baiskeli hupitia gia mbili, gia iliyozungushwa na tairi la
nyuma ina meno 20. Na ile iliyozungushwa na pedeli ina meno 50.
Iwapo pedeli zitafanya mizunguko miwili, tairi la nyuma litazunguka
mara ______ (a) 5 (b) 4 (c) 3 (d) 1 (e) nyingi [ ]
10. Volkano hai hutoa kimiminika kizito katika uso wa dunia
kiitwacho_________________________________________
(a) Lava (b) Kreta (c) Gesi (d) Volkano (e) Maji [ ]
11. Kwa nini kwa kawaida mwanga unaonekana kwanza kabla ya
mngurumo wa radi ingawa vyote vinatoka pamoja? (a) mwanga una
mawimbi makubwa kuliko sauti
(b) mishipa ya fahamu ya macho inafanya kazi haraka kuliko mishipa
ya fahamu ya kusikia (c) mwendo kasi wa mwanga ni waharaka kuliko
wa sauti (d) Mwanga na sauti kwa kawaida husafiri wima (e) Mawimbi
ya sauti hayasafiri katika hewa [ ]
12. Vipi kati ya vitu vifuatavyo vinaweza kusababisha uchafuzi wa hewa?
(a) Maji machafu ya viwanda, spiriti na ujenzi wa biashara (b) moshi,
majivu na mbolea (c) moshi wa viwanda na matokeo ya kuungua kwa
petrol (d) misitu ya asili, viwanda na mbolea (e) mbolea, mboji na
maji machafu ya viwandani [ ]
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 61
13. Ni kiumbe kipi kati ya vifuatavyo huishi kwenye maji? (a) Inzi (b)
Buibui (c) Kaa (d) Panzi (e) Mende [ ]
14. Ukuaji wa mbu hupitia hatua kuu nne, mtiririko sahihi wa ukuaji
huo ni____________ (a) Yai, pupa, lava, mbu (b) pupa, yai, lava, mbu
(c) yai, lava, pupa, mbu (d) lava, yai, pupa, mbu (e) pupa, lava, yai, mbua
[ ]
15. Chunguza jani la mmea lililoonyeshwa kwenye kielelezo kisha jibu swali
linalofuata.

Jani hilo unaweza kulifananisha na jani la mmea upi kati aya


ifuatayo?
(a) Mpunga (b) mtama (c) kunde (d) mahindi (e) mnazi [ ]
16. Protini huanza kumeng’enywa kikemikali kwenye__________________
(a) mdomo (b) tumbo (c) utumbo mwembamba (d) utumbo mpana (e)
figo [ ]
17. Sehemu ya Ua inayovutia wadudu wanaokuja katika mmea na
kusaidia uchavushaji na uchukuaji wa poleni
inaitwa____________________________________________________
(a) Petali (b) Sepali (c) Stigima (d) Kikonyo (e) Pistili [ ]
18. Mgongo wa chura ni mfupi ili
kumwezesha_____________________________________________________
(a) Kukimbia (b) kulala (c) kupaa (d) kuruka na kutua (e) kugeuka [ ]
19. Ndugu chapakazi alitumia kani ya nyutoni 10 kunyanya mzigo.
Kwa umbali wa mita 5 Je , ndugu chapakazi alifanya kazi kiasi gani?
(a) Joule 100 (b) Nyutoni 20 (c) Joule 20 (d) Joule 50 (e) kg 10 [ ]
20. Kati ya mashine zifuatazo ipi ni mashine rahisi? (a) Baiskeli (b)
pikipiki (c) winchi (d) wenzo (e) gari [ ]
21. Sehemu kubwa ya bayogesi ni ___________
(a) Kabonidayoksaidi (b) Oksijeni (c) Naitrojeni (d) Gesi asili (e) mvuke
22. Uchunguzi wa kisayansi unaanza na __
(a) Maswali (b) uchunguzi (c) dhanio (d) udadisi (e) data [ ]
23. Katika jaribio la kisayansi data humanisha_______________ (a) Taarifa
ya mambo yanayojitokeza unapofanya jaribio (b) orodha ya vitu
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 62
utakavyovitumia kwenye jaribio (c) taarifa ya jaribio thibiti (d)
Mpangilio wa hatua kwa hatua namna ya kufanya jaribio (e)
mapendekezo ya hatua za kutatua tatizo [ ]
24. Nyuzi 212 za farein Haiti ni sawa na nyuzi___ za sentigredi (a) 75 (b)
108 (c) 176 (d) 40 (e) 100 [ ]
25. Ni mazingira yapi yanaufaa mmea ulioonyeshwa katika kielelezo
kifuatacho. [ ]

(a) Misitu minene (b) katika maji (c) misitu yenye nyasi nyingi (d)
jangwa (e) milima
26. Kwanini baadhi ya mimea huwa haipukutishi majani yake wakati wa
masika?
(a) Kuhifadhi maji (b) kuruhusu transpiresheni (c) kuhifadhi chakula
(d) kuhifadhi udongo (e) kurutubisha ardhi
27. Mchoro huu unaonyesha_______________________________________

(a). seli mfuatano (b) .seli rahisi (c). seli sambamba (d). vikinzani (e). taa
za umeme
28. Umeme unaozalishwa na betri (kurunzi) hutokana na nishati ya
______________
(a) Jua (b)kimakenika (c) sauti (d) sumaku (e) kikemikali [ ]
29. Ikiwa pembe ya mwale mtuo katika kioo bapa ni 600 tafuta thamani
ya pembe iliyoakisiwa (A) 900 (B) 400 (C) 300 (D) 600 (E) 450
[ ]
30. Kuyeyuka kwa barafu ni badiliko la aina ipi? [ ]
(a) Kikemikali (b) kiumbo (c) kimazingira (d) kibaolojia (e) kitiziolojia
31. Njia rahisi ya kurutubisha udongo ni _____
(a) Kuchanganya samadi na mbolea ya chumvi chumvi (b) kuchoma
miti yote inayokausha vyanzo vya maji (c) kuchoma majani na
mabua ya mahindi (d) kupunguza idadi ya ng’ombe wanaochungwa
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 63
(e )kulima mazao ya jamii ya kunde kwa mbadilishano [ ]
32. Vitu vipi kati ya vifuatavyo huweza kutenganishwa kwa sumaku?
(a) Unga wa chuma na mchanga (b) unga na vipande vya karatasi
(c) pini za plasiki na mchanga (d) unga wa kioo na mchanga
(e) mchanga na mchele [ ]
33. Mabadiliko ya hali ya hewa na maji ni vitu ambavyo
vinavyosaidia___________
(a) Kufanya uso wa ardhi uwe mzuri (b) wanyama wadumu mazingira
yao
(c) wanyama na mimea waishi (d) kuharakisha mmomonyiko wa ardhi
(e) kusawazisha uhusiano wa mlishano [ ]
34. Tafuta thamani ya X katika mchoro ufuatao:-
Sm 10 sm 8

x Gm 350

(A) gm 250 (b) gm 280 (c) gm 437.5 (d) gm 240


(e) gm 175 [ ]
35. Ateri kuu imegawanyika katika mishipa midogo midogo
iitwayo____________
(a) Venakava (b) bronchioli (c) valvu (d) kipilari (e) vena [ ]
36. Haemoglobini ni kampaundi inayopatikana ndani ya damu
katika______________________________________________
(a) Seli hai nyeupe (b) seli hai nyekundu (c) ute wa damu (d) uroto wa
njano katika mifupa (e) seli zinazoganisha damu [ ]
37. Nini kitatokea iwapo mbegu Y ya kiume itaungana na mbegu X ya
kike?
(a) Mapacha wasiofanana (b) mtoto wa kike (c) mapacha walioungana
(d) mtoto wa kiume (e) mapacha wanaofanana [ ]
38. Ni ubongo wa mnyama yupi kati ya wafuatao umeundwa kitaalamu
zaidi kuliko wengine? (a) Binadamu (b) farasi (c) sungura (d) sokwe
(e) tembo [ ]
39. Kutu ni matokeo ya kuwepo kwa pambano la kikemikali lifuatalo:-
Y + CHUMA + MAJI herufi “Y” inasimama badala ya ____________
(a) Oksijeni (b) Asidi (c) Naitrojeni (d) Unyevu (e)Kabonidayoksaidi [ ]
SEHEMU :B JAZA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI KWA SWALI LA
41- 45
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 64
40. Katika mchoro ufuatao wa metamofosisi herufi X inaitwa___________

41. Mchoro ufuatao unaonesha alama ya betri, je betri hiyo ina seli kavu
ngapi?______
+ -
_________________ ____________

42. Badili nyuzi 122 za farenheiti kuwa nyuzi za sentigredi


_________________________
43. Ogani ipi hutoa taka mwili aina ya kabonidayoksaidi na maji mwilini?
___________
44. Katika mchoro ufuatao herufi A inawakilisha …

45. ……………………………… ni simetali ambayo ni kipitisho cha meme.

JARIBIO LA 21
1. Upi kati ya magonjwa yafuatayo hudhoofisha na kuharibu kinga ya
mwili? A. UKIMWI B. Kuhara damu C. Kifua kikuu D. Seli
mundu
2. Mimea iotayo jangwani huwa na majani membamba, hali hii husaidia
………. A.Mmea kukua haraka B. Mmea kutengeneza chakula kingi
C. Kupata mwanga wa jua kwa urahisi D. Kuhifadhi maji
3.Wadudu hupumua kwa kutumia spirako, Je, mmea hutumia………………
A. Kovu B. Stomata C. Vinyweleo D. Kloroplasti
4. kuna aina ………… za maumbo ya sumaku. A. 1 B. 3 C. 5 D. 7
5. Ifuatayo ni simboli ya mekyuri….. A. Ag B. Mg C. Fe D. Au

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 65
6. Yafuatayo ni magonjwa yanayosababishwa na bakteria
isipokuwa………… A. surua B. Trikonoma C. Trakoma D. Kawende
7. Kipi kati ya vifuatavyo ni chanzo kikuu cha kuenea kwa VVU/ UKIMWI?
A. Kuchangia vitu vyenye ncha kali B. Kujamiiana
C. Uchaniaji wa damu D. Ajali
8. Moja kati ya yafuatayo si majanga ya asili yanayotokea katika mazingira
yetu A. Mafuriko B. Mlipuko wa mabomu C. Tetemeko la ardhi
D. Kimbunga
9. Katika mwili wa binadamu kuna jumla ya mifupa mingapi?
A. 206 B. 6000 C. 205 D. 204
10. Mende hupitia hatua ngapi za ukuaji? A. Mbili B. Tatu C. Nne
D. Tano
11. Kiasi cha kani ya msukumo wa umeme katika sakiti hupimwa kwa
kutumia A. Rektifaya B. Transifoma C. Voltimita D. Amita

12. Alama hii katika sakiti ya umeme inawakilisha nini?


A. Kikinza B. Fyuzi C. Waya wa ethi D. Gropu
13. Huduma ya kwanza kwa mtu anayeharisha na kutapika ni kumpatia
………… A. Sukari B. Maji ya sukari na chumvi C. Juisi ya azam
D. Maji
14. Chura hupumua kwa kutumia ogani gani anapokuwa kwenya maji?
A. Mapafu B. Matamvua C. Mapezi D. ngozi
15. Ualbino ni ulemavu unaotokana na ukosefu wa …………………………
kwenye ngozi. A. kaboni B. melanini C. seli nyekundu za damu
D. Chembe sahani
16. Kuchoma vitu angani kama vile mimea, mafuta n.k. huoneza gesi ya …
A. Oksijeni B. Haidrojeni C. Naitrojeni D. Kabonidayoksaidi
17. Idadi ya mbu inaweza kupungua kwa urahisi kwa ……
A. Kuua mbu wazima kwa dawa B. Kuharibu sehemu wanazotagia mayai
C. Kunywa dawa ya kuzuia homa D. Kutumia chandarua chenye dawa
18. Moja ya aina ya vyakula vifuatavyo hufaa kuliwa na mtu anayefanya
kazi ngumu. Aina hiyo ni …A. Mboga za majani B. Vitamini C. Wanga
D. Protini
19. Mmoja kati ya wanyama wafuatao huvuta hewa kwa kutumia mapafu
na ngozi naye ni …………… A. Chura B. Samaki C. Binadamu
D. kambale
20. Kundi lipi limeainisha wanyama wenye uti wa mgongo? A. Konokono,
mjusi na kenge B. Papasi, panzi na mbung`o C. Kuku, popo na bata
D. Chura, mamba na mchwa

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 66
21.Lipi kati ya mabadiliko yafuatayo ni badiliko la kiuombo? A. Maji
kuwa mvuke B. Maziwa kuchacha C. Kuchoma karatasi D. Pambano
la asidi na besi
22. Chanzo cha sauti ni…. A. Mitetemo B. Kelele C. Mkazo D. Hewa
23. Sifa mojawapo inayowatambulisha insekta ni……A. Mwili kugawanyika
sehemu tatu
B. Kutaga mayai C. Kuishi nchi kavu D. Kuruka kwa mbawa
24. Wakati wa mchana mimea yenye rangi ya kijani huongeza gesi gani
katika hewa? A. Haidrojeni B. Kabonidayoksaidi C. Naitrojeni
D. Oksijeni
25. Katika utengenezaji wa chakula cha mmea moja kati ya vitu vifuatavyo
havihitajiki. Kitu hicho ni A. Hewa ya ukaa B. Chumvichumvi
C. Umbijani D. Maji
26. Askaris husababisha ugonjwa gani kwa binadamu? A. Safura
B. Malale C. Polio D. Kipindupindu
27. Zifuatazo ni sifa za samadi isipokuwa moja. Sifa hiyo ni…. A. Kuruhusu
hewa kupita B. Kutunza unyevu C. Kuleta fukuto kwenye
udongo D. Kutumiwa na bakteria.
28 2 H2 + O2 ….H2O A. 2 B. 4 C. 1 D. 3
29. Mkondo wa umeme wa ampia 6.0 ukipita kwenye kikinza chenye omu
1.5, tofauti ya poteshali kati ya ncha za kikinza hicho ni volti……….
A. 9.0 B. 4.5 C. 4.0 D. 1.5
30. Katika uchunguzi wa kisayansi hatua ipi hutumuka kukubali au
kukataa dhanio A. Kukusanya data B. Kuandika hitimisho
C. Kufanya jaribio D. Kutafsiri data
31. Zifuatazo ni maada isipokuwa ……………… A. Hewa B. karatasi
C. Mwanga D. Chuma
32. Katika mlishano, SIMBA SWALA NYASI nini kitatokea
iwapo Simba watayahama mazingira haya? A.Nyasi zitaongezeka
B. Swala watakufa C. Nyasi zitapungua D. Swala watapungua
33. Ripoti ya jaribio la kisayansi huandikwa kwa mpangilio ufuatao:
A. Kusudi,njia, vifaa, matokeo,hitimisho B. Njia, vifaa,
matokeo,kusudi, hitimisho
C. Njia, vifaa, kusudi, hitimisho, matokeo D. Njia, vifaa,
kusudi,matokeo,hitimisho
34. Kifaa kinachotumika katika kuangalia seli za viumbe hai huitwa………
A. Darubini B. Periskopu C. Hadubini D. Kamera
35. Mlango wa fahamu unaotumiwa na binadamu kuhisi hali ya joto au
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 67
baridi huitwa….. A. Ulimi B. Sikio C. Jicho D. Ngozi
36. Wakati wa uchavushaji wa ua chavua husafirishwa kutoka kwenye
A. ovari kwenda kwenye ovyuli B. stigma kwenda kwenye kichavua
C. petali kwenda kwenye stigma D. kichavua kwenda kwenye stigma

37. Mwangwi ni kitendo cha ………………………………………………sauti


A. Kusharabiwa B. Kufifia C. Kusikika D. Kuakisiwa
38. Mshipa mkuu unaotoa damu kwenye moyo unaitwa……………..
A. Veini B. Aota C. Venakava D. Kepatiki
39. Homoni inayorekebisha uingiaji wa hewa ya oksijeni katika mfumo wa
upumuaji wa binadamu inaitwa…. A. Adrenali B. Insulini
C. Thairoksini D. Estrojeni
40. Paka aliyekuwa amefungiwa kwenye kisanduku kilichokuwa na
kipande cha samaki alikufa baada ya saa sabini na mbili. Ni kitu gani
kilisababisha paka huyo kufa?.................................................................
A. Alikula nyama iliyooz B. Alikosa hewa ya kabondayoksaidi
C. Alikosa hewa ya oksijeni D. Alikosa maji ya kutosha baada ya kula
nyama
JAZA NAFASI WAZI
41. Mtu anayevua samaki kwa kutumia ndoano ni mfano wa nyenzo darala
la …………………………………………………………………
42. Homoni ya kike inayohusika na kuongeza unene wa mji wa uzazi
(uterasi) baada ya mwanamke kushika mimba inaitwa ……………………
43. Tafuta manufaa ya kimakanika (M.K) ya mashine inayonyanyua mzigo
wa Kg 120 kwa jitihada ya Kg 30.
44. Muungano wa kikemikali kati ya gesi ya haidrojeni na oksijeni huunda
kampaundi iitwayo…………………………………………………………..………
45. andika simboli ya shaba. ……………………………………………………….

JARIBIO LA 22
1. Mmea mojawapo wenye uchavushaji pekee ni ________________________
(a)Mahindi (b) Karafuu (c) Ndizi (d) Papai (e) Korosho
2.Fueli zinazotumika kuzalisha nishati ni ___ (a) Dizeli, petroli, gesi asilia
(b) Diseli, gesi asilia na makaa ya mawe (c) Petroli, diseli na upepo
(d) Maji, gesi asilia na diseli (e) Petroli, makaa ya mawe na upepo
3. Ni aina ipi kati ya vitamini zifuatazo ambayo hufanya kazi ya
kugandisha damu kwenye jeraha _______ (a) B (b) E (c) D (d) C (e) K
4. Sehemu ya kike ya Ua inayobeba mbegu ni ________
(a) Ovari (b) Sepali (c) Staili (d) Stameni (e) Stigma
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 68
5. Moja kati ya makundi ya magonjwa yafuatayo ni ya kurithi. _______
(a) Marasimasi na athma (b) Selimundu na albino (c) Kisukari na
uvimbe (d) Polio na selimundu (e) Albino na nyongea
6. Zifuatazo ni mashine rahisi isipokuwa ____________
(a) Koleo (b) Mkasi (c) Shoka (d) Roda (e) Saa
7. Maisha ya kipepeo yana hatua nne, hatua ipi ni hatari kwa mimea? ___
(a) Tunutu (b) Lava (c) Yai (d) Buu (e) Kipepeo kamili
8. Wanga hutambulishwa kwa kutumia ___________ (a) Karatasi
(b) Myeyusho wa benedikti (c) Ayodini (d) Karatasi nyeupe (e) Asidi
9. Ipi kati ya zifuatazo ni aina ya mbegu zinazojisambaza zenyewe?
(a) Nazi na pamba (b) Mbaazi na kunde (c) Kunde na papai (d) Embe
na pera (e) Mbaazi na chungwa
10. Chombo kinachotumika kupima wingi wa umeme katika mkondo
huitwa ___________ (a) Ameta (b) Volti (c) Ampia (d) Ohm (e) Ometa
11. Sehemu kuu tatu za Pistili ni ______________ (a) Ovari, staili na
filament
(b) Stigma, staili na kichavua
(c) Ovari, stigma na filamenti
(d) Ovari, staili na stigma
(e) Staili, kichavua, na filament

12. Mpangilio wa kani za sumaku uliooneshwa hapo chini hutokea wakati


gani? _________

(a) Zinapokwepana (b) Zinapovutana (c) Zinapokaribiana


(d) Zinapoakisiana (e) A na B ni jibu sahihi
13. Mambo muhimu yanayosababisha mbegu kuota ni maji, hewa na _____
(a) Mbolea (b) Udongo (c) Mwanga (d) Joto (e) Mvua
14. Kupwa na kujaa kwa bahari husababishwa na kani ya uvutano kati ya
dunia na _____ (a) jua (b) mwezi (c) miamba (d) nyota
15. Kati ya wadudu wafuatao, mdudu yupi hapitii metamofosisi kamili? ___
(a) Inzi (b) Mbu (c) Panzi (d) Kipepeo (e) Nyuki
16. Ukosefu wa vitamin C mwilini husababisha ugonjwa gani? ________
(a) Beriberi (b) Uoni hafifu (c) Kiseyeye (d) Matege (e) Malaria

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 69
17. __________ ni moja ya wanyama wasio na uti wa mgongo?
(a) Nyoka (b) Mjusi (c) Popo (d) Chura (e) Konokono
18. Yafuatayo ni magonjwa yanayoweza kuambukizwa isipokua ________
(a) Pumu (b) Surua (c) Kifua kikuu (d) Kifadulo (e) Tetekuwanga
19. Mimea hutengeneza chakula chake katika ____________ (a) Nyuklia
(b) Kloroplasti (c) Ukuta wa seli (d) Vakyuli (e) Kiwambo cha seli
20. Je! Nini utakachokifanya ikiwa utaona nguo alizovaa rafiki yako
zinaungua kwa moto? (a) Kumpaka mafuta (b) Kumweka maji kwenye
jeraha (c) Kumfunika kwa blanketi au nguo nzito (d) Kumpulizia hewa ya
oksijeni (e) Kumvua nguo zilizokwisha ungua
21. Kipimio kinachotumika kuhakiki damu kama ina VVU au la ni ____
(a) Western blot (b) CD4 (c) Themomita (d) Elisa (e) Hadubini
22. Mbolea ya NPK ni mchanganyiko wa viashiria vya ______ (a) Nitrojeni,
salfa na fosforasi (b) Naitrojeni, fosforasi na kalsiamu (c) Fosforasi, salfa na
naitreti (d) Naitrojeni,potasiamu na kalsiamu (e) Naitrojeni, fosiforasi na
potasiamu
23. Badiliko lifuatalo si la kikemikali __________ (a) Kuoza kwa matunda
(b) Kuchacha kwa maziwa (c) Kuungua kwa karatasi
(d) Kuyeyuka kwa mshumaa (e) Chuma kupata kutu
24. _________ hubadili rangi nyekundu ya karatasi ya litmasi kuwa rangi ya
bluu. (a) Aluminiamu (b) Kloraidi (c) Asidi (d) Sodium (e) Besi
25. Y + O2 + maji= kutu. Y imesimama badala ya _______________________
(a) Shaba (b) Zinki (c) Kaboni (d) Chuma (e) Aluminiam
26. Zipi kati ya tabia zifuatazo zinachangia kuenea kwa VVU?
(a) Kushikana mikono na mgonjwa (b) Kula pamoja na mgonjwa mwenye
vvu (c) Kuchangia vifaa vyenye ncha kali na uasherati (d) Kuwekewa
damu salama (e) Kukaa na kucheza pamoja na mwenye vvu.
27. Mvulana mwenye uzito wa kilo 60 amekaa mita 2 kutoka kwenye
egemeo. Msichana amekaa upande wa pili mita 3 kutoka kwenye egemeo,
ili kusawazisha uzito kwenye bembea hiyo, tafuta uzito wa msichana.
(a) Kg. 120 (b) Kg. 60 (c) Kg. 40 (d) Kg. 180 (e) Kg. 90
28. Mtu anayeota moto hufikiwa na joto kwa njia ya ____________________
(a) Mnunurisho (b) Msafara (c) Myuko (d) Mpitisho (e) Myeyuko
29. Matendo ya hiari katika mwili wa binadamu hutawaliwa na ubongo wa..
(a) Kati (b) Mbele (c) Nyuma (d) Kati na nyuma (e) Ndani
30. Retina katika jicho la binadamu ni sawa na kifaa gani katika kamera? _
(a) Filamu (b) Pupili (c) Lenzi (d) Flashi (e) Kasha
31. Mtaimbo ni mfano wa nyenzo daraja la ngapi? _______________________
(a) Pili (b) Nne (c) Tatu (d) Kwanza (e) Tano
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 70
32. Ni kwa nini watu wanaoishi na VVU wanahitaji vyakula vyenye
virutubisho zaidi? __ (a) Wanahitaji kunenepa ili kuepuka unyanyapaa (b)
Wanahitaji kuimarisha kinga ya mwili (c) Wanapata njaa kila wakati (d)
Maisha yao ni mafupi, hivyo wanahitaji chakula cha kutosha (e) Ugonjwa
wao ni wa muda mrefu
33. Dunia inazunguka mizunguko mingapi _______ (a) 1 (b) 2 (c) 3 (d) 4
34. John alitumia Kani 980 kuvuta toroli lenye mzigo umbali wa mita 7.
Tafuta kiasi cha kazi iliyofanyika ___________
(a) Juli 6,760 (b) Juli 6,860 (c) Juli 973 (d) Juli 140 (e) Juli 987
35. ________ inawajibu wa kukusanya mawimbi ya sauti.
(a) Upepo (b) Pina (c) Ngoma ya sikio (d) Koklea (e) Spika
36. ‘Ni kweli kuwa mbegu ikikosa maji haioti’. Katika uchunguzi
wakisayansi, kauli hiyo inawakilisha _______________ (a)Dhanio
(b) Kubuni jaribio (c) Hitimisho (d) Kubaini tatizo (e) Kukusanya data
37. Mtu asiyeona mbali anashauriwa kutumia miwani yenye lenzi aina
gani? _____ (a) Bapa (b) Mbinuko (c) Mbonyeo (d) Duara (e) Prizim
38. Mfumo wa homoni unafahamika kama mfumo wa _________
(a) Eksikretori (b) Endokrini (c) Fahamu (d) Utoaji taka mwili
(e) Upumuaji
39. Mapacha wa kufanana wakiwa kwenye uterasi hushirikiana __________

(a)Mlango wa kizazi (b) Plasenta (c) Moyo (d) Chakula (e) Utumbo
40. zifuatazo ni ogani zinazohusika na utoaji wa taka mwili nazo ni ______
(a) Moyo, Macho na Pua (b) Kucha, Mapafu na Maini (c) Figo, Ngozi na
Mapafu (d) Maini, Pua na Kibofu (e) Makadi, Kibofu na Pua

SEHEMU B
41.Ikiwa umeme unaopita katika sakiti ni Ampia 5, kiasi cha ukinzani (R)
wa waya katika sakiti hiyo ni ohm ngapi kama kani elektroni mwendo ni
40V ? ___________
42. Mshipa Mkuu unaotoa damu kutoka kwenye moyo
kwendasehemu zote za mwili unaitwa? _____________
43. Kifaa kinachopima mwendokasi wa upepo
kinaitwa _____________
44. Sehemu ipi ya mfumo wa umeng’enyaji chakula
inahusika na umeng’enyaji wa protini kwa mara ya kwanza?
______________
45. Elimu ya mahusiano kati ya viumbe na mazingira
huitwa _______________

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 71
JARIBIO LA 23
1. Chakula kilichomeng’enywa husharabiwa mwilini kwenye A) utumbo mpana
B) utumbo mwembamba C) ini D) figo E) kongosho
2. Ogani zifuatazo hutumika na mfumo wa utoaji wa taka mwili A) ngozi, figo, ini,
mapafu B) ini, kongosho, nyongo, figo C) pua, kinywa, utumbo, moyo
D) bandama, mapafu, figo, ini E) mapafu, utumbo, figo
3. Ugonjwa unaotokana na mwili kukosa virutubisho vya kutosha vya protini
huitwa A) kiseyeye
B) matege C) pepopunda D) unyafuzi E) kiribatumbo
4. Sehemu ya kiume ya ua huitwa: A) stameni B) pistil C) stigma D) petali
E) sepali
5. Maji halisi huanza kuchemka kwa nyuzi za sentigredi ngapi? A) 500c B) 1000c
C) 1500c D) 2000c
6. Wanyama wanaonyonyesha na wenye kuzaa huitwa A) insekta B) viumbe
C) reptilia D) mamalia E) amfibia
7. Baada ya kurutubishwa, ovari kwa kawaida hubadilika kuwa A) mbegu
B) tunda C) ganda la mbegu D) ua E) gamba
8. Mlo wenye mchanganyiko wa protini, kabohaidreti, mafuta, vitamin na maji
huitwa A) chakula bora B) mchanganyiko bora C) chakula cha kisasa D) mlo
kamili
9. Kipi kati ya yafuatayo siyo muhimu katika uotaji wa mbegu? A) mwanga
B) maji C) hewa D) joto
10. Utamu uliopo katika ua unaofuatwa na nyuki huitwa A) asali B) sukari
C) nekta D) ulimbo E) mbelewele
11. Kitendo cha kusafiri kwa chavua kutoka kichavua hadi kwenye stigma
huitwa A) urutubishaji B) utungisho C) fotosinthesisi D) uchavushaji E) uzazi
12. Kuta za kumbi za mikutano na studio za redio huwekwa maada laini ili
A) kusharabu sauti B) kuakisi sauti C) kuongeza sauti D) kuchuja sauti
E) kuongeza mwangwi
13. Homoni inayoleta mabadiliko katika mwili wa msichana inaitwa A) ostrojeni
B) gamete C) insulin D) testosteroni E) adrenali
14. Panzi hupumua kwa kutumia A) pua B) vinyweleo C) mapafu D) spirako
E) nywele
15. Homoni ya insulin hutolewa na tezi ya A) pituitari B) adrenali
C) parathoidi D) kongosho E) ethirapi
16. Gesi inayotolewa katika mchakato wa fotosinthesis katika mimea ni
A) naitrojeni B) kabondayoksaidi C) haidrojeni D) mitheni E) oksijeni
17. Kifaa kitumikacho kuongeza au kupunguza nguvu ya umeme huitwa
A) transfoma B) jenereta C) sakiti D) amita E) koili
18. Polio ni ugonjwa unaolemaza viungo, ugonwa huu huenezwa na
A) bakteria B) minyoo C) basila D) virusi E) amiba
19. Zifuatazo ni sehemu za seli ya mnyama isipokuwa A) kiwambo cha seli
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 72
B) nyukliasi C) ukuta wa seli D) vakyuli E) saitoplazimu
20. Malaria huenezwa kwa kuumwa na mbu jike aina ya A) anofelesi
B) reptilia C) amfibia D) kuleksi E) mbung’o
21. Matokeo ya mwisho ya usanisi nuru (fotosinthesisi) ni A) maji na sukari
B) oksijeni na wanga C) maji na kabondayoksaidi D) asidi za amino
E) oksijeni na kabondayoksaidi
22. Tochi yenye kutumia seli mbili za kawaida (seli kavu) hutoa jumla ya
umeme wenye volti A) 1.5 B) 4 C) 2.0 D) 3. E) 4.5
23. Ni mdudu yupi kati ya wafuatao hapitii metamofosisi kamili? A) nzi
B) panzi C) kipepeo D) nyuki E) mbu
24. Elementi zimegawanyika katika makundi mawili ya A)mimea na
wanyama B) yabisi na gesi C) metali na simetali D) asidi na gesi
E) vimiminika na gesi
25. Vitundu vidogo katika jani la mimea huitwa A) stomaki B) stomata
C) stigima D) petali E) ovari
26. Ogani itumikayo kuhisi kiamshi cha mwanga huitwa A) sikio B) pua
C) jicho D) ulimi E)ngozi
27. Ni ugonjwa upi kati ya yafuatayo una chanjo? A) kaswende B) polio
C) kisukari D) nyongea E) kiseyeye
28. Chuma kupata kutu na kuungua kwa vitu ni matukio yanayofanana kwa
sababu A) oksijeni inatumika B) naitrojeni inatolewa
C) oksijeni inatolewa D) kabondayoksaidi inatumika E) ni badiliko la kiumbo
29. Mzunguko wa damu huanzia kwenye A) damu B) mishipa ya damu
C) moyo D) figo E) mapafu
30. Sauti husafiri kwa kasi zaidi katika maada gani? A) yabisi B) maji C) hewa
D) ombwe E) gesi
31. Ukiweka sarafu ya shilingi 500 katika beseni lenye maji, sarafu hiyo
inaonekana imepanda juu. Hali hiyo hutokea kwa sababu A) sarafu hiyo ni
nyepesi B) macho yana lensi mbonyeo C) mwanga husafiri katika mstari
ulionyooka D) maji ni kidogo E) mwale wa mwanga hupinda unapoingia katika
maji
32. Taka mwili zilizochujwa na figo husafirishwa kwenda kwenye kibofu kupitia
A) aorta B) urethra C) ureta D) vena ya venali
33. Mwili wa binadamu una jumla ya misuli A) 600 B) 206 C) 58 D) 200 E) 1000
34. Lipi ni badiliko la kiumbo kati ya mabadiliko haya? A) chuma kupata kutu
B) mshumaa kuyeyuka C) mafuta ya taa kuwaka D) kuchacha kwa maziwa
E) matunda kuoza
35. Nyongo hutengenezwa na ………mwilini. A) insulin B) ini C) glukosi
D) mapafu E) kongosho

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 73
36. Sayari iliyo karibu sana na jua ni A) zuhura B) pluto C) zebaki D) sumbula
E) dunia
37. Maji ni ainisho la chembe za hewa ya ….…. na …….. A) kaboni na naitrojeni
B) heimu na oksijeni C) haidrojeni na oskijeni D) naitrojeni na oksijeni
38. Wakati mtu anasukuma toroli, mikono yake na mishikio ya toroli inafanya
A) egemeo B) mzigo C) jitihada D) nyenzo
39. Kupwa na kujaa kwa maji baharini husababishwa na nguvu ya mvutano kati
ya mwezi na A) dunia B) jua C) nyota D) vimondo E) bahari
40. Kati ya viumbe wafuatao ni yupi hana uti wa mgongo? A) samaki B) nyoka
C) konokono D) mamba E) mjusi

JAZA NAFASI ZILIZO WAZI


41. Hili ni jani la mmea uliopo katika kundi la ……..………………………

+ -
42. Katika mchoro wa sakiti ya umeme, alama hii inawakilisha
……………………………………………………………………..…………………….
43. Chunguza mchoro huu. Lensi hii ni aina gani ya lenzi? A) …………….
lensi

44. Mkondo wa umeme (I) unaopita katika sakiti hii ni: ampia ngapi? .........
20V
I

40Ω

45. Mishumaa 5 iliyowashwa ilifunikwa kwa glasi zenye ukubwa tofauti.


Mshumaa gani utakuwa wa mwisho kuzimika?

A B C D E
D

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 74
JARIBIO LA 24
1. …….…ni kimeng’enya chenye uwezo wa kumeng’enya chakula chenye
asili ya mafuta na kuwa gliseroli na asidi ya mafuta (a) Lipasi
(b) Amylase (c) Taipsini (d) Peptoni (e) amplesi
2. Nini matokeo ya mwisho ya myeyuko wa chakula aina ya
protini?...........(a) Asidi za fati na glaiserini (b) Asidi za amino
(c) Sukari rahisi (d) Maltose (e)chumvi
3. Chakula kilichomeng’enywa husharabiwa tumboni kupitia vinyweleo
viitwavyo ……... (a) Haidrokloliki asidi (b) Vilasi (c) Peptoni
(d) Pepsini (e) vairasi
4. Kusharabu maji na madini yaliyotokana na mmeng’enyo wa chakula
ni moja ya kazi ya ………. (a) utumbo mdogo (b) utumbo mpana (c)
kongosho (d) puru (e) Ini
5. Mate huwa na kimenyenyo ambacho hubadilisha ……….kuwa ………..
rahisi (a) Fati, sukari (b) Wanga- protini (c) Sukari, fati (d) Wanga,
sukari (e) protini,wanga
6. Wekundu wa damu hupatikana kwenye rangi ya kampoundi iitwayo:
(a) chembe sahani (b) Plazima (c) Seli hai nyeupe (d) Haimogrobini
(e) mishipa
7. Viumbe hai vimeundwa kwa chembechembe ndogo ziitwazo………..
(a) Nyukliasi (b) Saitoplazimu (C) Seli (d) seli hai nyekundu (e)Atom
8. Katika mfumo wa mzunguko wa damu ateri zote hubeba damu yenye
oksijeni isipokuwa …………..(a) Vena (b) aota (c) Palmonari ateli
(d) Palmonari vena (e) Ateri za Kapilari
9. Kupatwa kwa jua hutokea wakati …………upo katikati ya magimba
mawili (a) Jua (b) Mwezi (c) dunia (d) sayari (e) Jupita
10. Myeyuko wa ………..hutumika kujaribia uwepo wa wanga katika
chakula (a) Zebaki (b) Asidi (c) Besi (d) Ayodini (e) insulini
11. Wanyama wanaokula nyama na majani huitwa ……….(a)Canvorasi
(b) Omivorasi (c) Hebivorasi (d) Optivorasi (e) Canvorasi na
Omnivorasi
12. Ugonjwa wa kiseyeye husababishwa na upungufu wa vitamin ………
(a) C (b) D (c) A (d) E (e) K
13. Sehemu ya sikio inayohusika na kukusanya mawimbi ya sauti
huitwa? ………. (a) akausitika (b) Koklea (c) Miatusi (d) Pina
14. Fyuzi hufungwa kwenye vifaa vitumiavyo umeme kama
ifungwavyo…..… kwenye nyumba ili kuepusha hitilafu ya umeme
mwingi. (a)Sakiti breka (b) waya wa ethi (c) volteji (d)Ampia (e) amita
15. Madini ya ………… huimarisha meno na mifupa (a) madini joto
(b) kalisiamu (c) ayodini (d) almasi (e) chuma
16. Mtu asiyeona vizuri vitu vilivyopo jirani, anashauriwa kuvaa miwani
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 75
yenye lenzi……(a) Lenzi mbonyeo (b) Lenzi mbinuko (c) Lenzi bapa
(d) Prizimu (e) Miwani.
17. Mchanga unaopatikana katika firigisi ya kuku husaidia ………....….
(a) kusharabu chakula (b) kuyeyusha chakula
(c) kuhifadhi nyongo (d) kuuwa vijidudu katika vyakula (e) Kukipa
kinyesi rangi yake.
18. Kifaa kinachobadilisha mkondo geu wa umeme kuwa mkondo
mnyoofu ni … (a) Redieta (b) Amita (c) Transista (d) Sakitibreka
(e)Rektifaya
19. Moja ya matendo yafuatayo hayaharibu usumaku ……….(a) Kuchoma
moto (b) kugongagonga (c) Kutumia umeme mkondo geu (d) Kutumia
mkondo mnyoofu wa umeme (e)kuweka pamoja na vifaa vya chuma.
20. Ogani ipi kati ya hizi haihusiani na mfumo wa mmeng’enyo wa
chakula?.........(a) figo (b) Ini (c) Utumbo (d) mapafu (e)Mdomo.
21. Kukosekana kwa chanikiwiti katika mmea huweza kusababisha …..
(a) Majani ya mmea kupukutisha (b) Majani ya mmea kukauka
(c) Mmea kukosa madini joto (d) Mmea kushindwa kusanisi chakula
(e) Mmea kudumaa.
22. Fototropizimu ni kitendo cha mmea kuota kuelekea kwenye ……….
(a) Maji (b) Kani ya mvutano (c) Mwanga (d) Kemikali (e)Gizani.
23. Sehemu ya chembe hai inayohusika na kutawala shughuli zote za
chembe hai huitwa…………(a) Saitoplazimu (b) Vakuoli
(c) Kloroplasti (d) Nyuklias (e) Seli
24. Ni kifaa gani hutumika kukuza taswira ya violwa vidogo sana?.........
(a) Periskopu (b) Prizimu (c) Lenzi (d) Kioo bapa (e) Hadubini
25. Mkondo wa umeme wenye ampia 0.8 umepita kwenye waya wenye
ukinzani wa Omu 24. Je nguvu ya umeme katika sakiti hiyo ni Volti
ngapi?.......... (a) 19.4 (b) 192.2 (c) 19.2 (d) 19.48 (e)19.22.
26. Kipi kati ya vifuatavyo hakipitishi mkondo wa umeme?.........(a) Zebaki
(b) Shaba (c) mpira (d) chuma (e)Waya.
27. Mfumo wa homoni hujulikana pia kama mfumo wa ……….
(a) endokrini (b) Respiresheni (c) Translokation (d) Haidrometa
(e)Transipilasheni.
28. Hatua wanazopitia wadudu katika ukuaji huitwa (a) ukuaji
(b) makuzi (c) metamofosisi (d) ubatilisho (e)kutaga matai
29. Ni muhimu kuweka kumbukumbu za jaribio lililofanyika kwa sababu
hutumika ……….(a) Kama rejea (b) Kuchora jedwali la matokeo
(c) Kurekebisha taarifa mbalimbali (d) Kutangaza umakini wa
aliyefanya jaribio (e)Kumtambulisha aliyeandaa jaribio.
30. Data za uchunguzi zilizochambuliwa huweza kuwasilishwa kwa njia
ya ………(a) Ripoti (b) Kutafsiri (c) Grafu (d) Kukokotoa
31. ipi kati ya jozi zifuatazo si sahihi kuhusu lenzi?
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 76
(a). Lenzi mbonyeo – hurekebisha kutokuona mbali
(b) Lenzi mbinuko – hutawanya miale ya mwanga
(c ) . Lenzi mbonyeo- hukusanya miale ya mwanga
(d). A,B,C na E ni majibu sahihi
(e) Lenzi mbinuko – hurekebisha kutoona mbali
32. Matumizi ya roda katika maisha ya kila siku ni ………(a) kunyanyua
vitu vizito (b) kufunga vitu (c) kuzibua vizibo vya vyupa
(d) kurahisisha kukata kuni (e)Kulimia
33. Ni Tezi ipi kati ya zifuatazo huratibu utendaji wa Tezi zingine zote
katika mwili wa binadamu?.......... (a) Kongosho (b) Thairoidi
(c) Pituitali (d) Adrenali (e)Ini
34. Tendo la mmea kusafirisha maji kutoka kwenye mizizi hadi kwenye
majani huitwa ……………. (a) Difyusheni (b) Respiresheni
(c) Transilokesheni (d) Osmosisi (E) Transipiresheni
35. Mtu mwenye tatizo la kutokuona mbali anashauriwa kuvaa miwani yenye
lenzi _______________________________________________________________
36. Gesi ya oksjeni huhitajika mwilini ili ___________________________________
37. Sehemu zinazoathirika zaidi katika mwili wa binadamu kutokana
nakunywa pombe
kupindukia ni figo na ________________________________________________
38. Myeyuko unaotumiwa kutambua chakula aina ya wanga ni _____________
39. Tunaweza kuhisi mitetemo ya sauti kwa kutumia ogani inayoitwa _______
40. Tishu iliyo katika hali ya kimiminiko mwilini ni _________________________
41. Ni mdudu yupi kati ya panzi na kipepeo anakua kwa metamophosisi iliyo
kamil?__________________________________________________________________
42. Chumba cha moyo kinachosukuma damu safi kwenda sehemu za mwili
kinaitwa ___________________________________________________________
43.Kibonde alitumia 40N kutupa jiwe. Ikiwa jiwe lilienda mita 20 je, kibonde
alifanya kazi kiasi gani? ________________________
44 Mimea hutumia matundu madogomadogo kupupua yaitwayo ______ wakati
panzi hutumia ___________

45. Alama hii inawakilisha nini? _______________________________


JARIBIO LA 25
1. Umuhimu wa vyakula vya kabohaidret mwilini ni …….… [ ] a) kujenga
mwili b) kulinda mwili c) kuleta nguvu d) kuongeza joto e) kuongeza mafuta
2. Kikohozi kikavu, homa, kutokwa jasho usiku na kukohoa damu ni dalili
za……….. [ ] a) kifua kikuu b) pepopunda c) kifadulo d) tetekuwanga
3. Michoro ifuatayo inawakilisha seli katika mwili wa binadamu ambazo
kazi zake ni… a) kuzuia na kukinga maradhi mwilini b) kusafirisha oksijeni

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 77
c) kugandisha damu d) kurekebisha joto la mwili e) kusafirisha
kabonidayoksaidi
4. Ni kiumbe yupi kati ya vifuatavyo huishi kwenye maji? [ ]
a) inzi b) buibui c) kaa d) panzi e) nyuki
5. Ukuaji wa mbu hupitia katika hatua kuu nne, mtiririko sahihi wa ukuaji
huu ni upi? a) yai, pupa, lava, mbu b) pupa, yai, lava, mbu
c) yai, lava, pupa, mbu d) pupa, lava, yai, mbu e) lava, yai, buu, mbu
6. Chanzo cha chakula kwa wanyama ni …….. [ ] a) mimea b) mimea na
wanyama c) mimea kwa habivora na nyama kwa kanivora d) maziwa
e) mimea na maji
7. Kuna uhusiano gani kati ya sumaku na umeme? [ ] a) zote ni nishati za
kikemikali b) zote ni sakiti za umeme c) palipo na umeme ni lazima
kuweko na sumaku d) kuliko na sumaku ni lazima kuweko na umeme e)
majibu yote ni sawa

8. Katika mchoro wa sakiti ya umeme alamahii


inawakilisha? [ ] a) seli kavu b) seli c) fyuzi d) ukinzani e) volti
9. Ni kundi lipi linawakisha mashine rahisi? [ ] a) nyundo, shoka, kisu,
mkasi b) mkasi, gari, toroli, msumeno c) shoka, skrubu, mkasi, cherehani
d) baiskeli, gari, cherehani na nyundo e) mkasi, cherehani, toroli
10. Ripoti ya jaribio la kisayansi huandikwa kwa mpangilio ufuatao [ ]
a) njia, vifaa, kusudi, matokeo, hitimisho b) kusudi, vifaa, njia, matokeo,
hitimisho c) njia, vifaa, kusudio, hitimisho, matokeo d) kusudi, njia, vifaa,
matokeo, hitimisho e) vifaa, lengo, hatua, matokeo, hitimisho
11. Tezi lililo katika ubongo linalofanya kazi ya kuchochea tezi nyingice
huitwa ….. [ ] a) kongosho b) gonadi c) thairodi d) adrenali e) pituitari
12. Ni upi kati ya mishipa ya damu hupeleka damu kwenye mapafu? [ ]
a) vena kava b) ateri ya palmonari c) ini d) mapafu e) aota
13. Chembe nyekundu za damu hutengenezwa katika sehemu gani ya
mwili? [ ] a) uroto wa mifupa mirefu b) moyo c) ini d) mapafu e) figo
14. Mayai ya kike hutengenezwa kwenye ……………………. [ ] a) korodani
b) mirija ya folopia c) uterasi d) kongosho e) ovari
15. Mwale wa mwanga ukipita kwenye ……… hutawanyika katika rangi
saba. [ ] a) lenzi mbinuko b) mche glasi c) glasi prizimu d) mche sumaku
e) kioo bapa
16. Tunashauriwa kupanda miti sehemu iliyo kame ili ……… [ ] a) kuzuia
mmomonyoko wa udongo b) kuleta kivuli c) kupata kuni d) kusaidia kuleta
mvua e) kuongeza mmomonyoko wa udongo
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 78
17. Kinyonga hujibadili rangi mara kwa mara ili hali hii humsaidia
katika….. [ ] a) kupata chakula b) kupumua c) kujilinda d) kuona maadui
e) kujipatia joto
18. Yupi kati ya wafuatao hana uti wa mgongo? [ ] a) samaki b) popo
c) binadamu d) kobe e) buibui
19. Ni nini kati ya vifuatavyo hupinda kunapotokea midia moja kwenda
midia nyingine? a) upinde wa mvua b) mistari sambamba c) mwale wa
mwanga [ ] d) fokasi za lensi e) rangi ya njano
20. Kizio cha kazi ni ………… [ ] a) kilogramu b) nyutoni c) tani d) joule
e) sentimeta
21. Nini kitatokea ikiwa ncha za sumaku za KASKAZINI na KASKAZINI
zitakaribiana? [ ] a) zitavutana b) zitakwepana c) zitavunjika d) hakuna
kitakachotokea e) zitatoa cheche
22. Dhana ya kuakisiwa kwa mwanga inajidhihirisha katika mojawapo ya
vifaa vifuatavyo? a) hadubini b) televisheni c) balbu d) miwani e) darubini
23. Kuwepo kwa viumbe hai, maji na hewa ni sifa ya sayansi ipi kati ya
zifuatazo? a) mirihi b) sumbula c) dunia d) zuhura e) jupita [ ]
24. Mboga za majani na matunda hutusaidia kutengeneza ….. a) chembe
hai nyekundu za damu b) chembe hai nyeupe za damu [ ] c) chembe sahani
d) plazma ya damu e) damu
25. Ugonjwa unaosababishwa na ukosefu wa madini ya chuma mwilini ni
……. [ ] a) matege b) kwashakoo c) rovu d) unyafuzi e) upungufu wa damu
26. Sehemu kuu tatu za mfumo wa damu ni .. [ ] a) damu, mishipa ya damu
na moyo b) ateri, vena na kapilari c) damu, moyo na mapafu d) moyo,
aota na ateri e) damu, mapafu na moyo
27. Mlishano wa chakula ulio sahihi ni …………………………………..… [ ]
(a) tai nyasi chui swala (b) nyasi tai chui swala
(c) nyasi swala chui tai (d) chui tai nyasi swala
(e)nyasi chui swala tai
28. Hatua za ukuaji wa mende zipo ngapi? [ ] a) mbili b) tatu c) nne
d) tano e) sita
29. Usambazaji wa chakula mwilini hufanywa na ………. [ ] a) damu
b) maji c) hewa d) misuli e) oksijeni
30. Mbungó husababisha ugonjwa uitwao …………… [ ] a) malaria
b) kichocho c) malale d) kipindupindu e) homa ya manjano
31. Watu wanaofanya mazoezi ya viungo wanapaswa kula chakula chenye
wingi wa ….. a) protini b) kabohaidreti c) vitamin D d) madini e) mafuta [ ]
32. utawezaje kumsaidia mtu aliyenaswa na umeme?
a) kupiga simu Tanesco b) kupiga simu zimamoto c) kumshika miguu na
kumvuta d) kumsukuma kwa mti mbichi e) kumsukuma kwa mti mkavu

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 79
33. Tafuta thamani ya x [ ] a) kg. 10 b) kg. 5 c) kg. 20 d) kg. 25 e) kg. 250

34. Kwa kutumia mashine, jitihada ya nyutoni 30 ilivuta umbali wa m. 15


ili kuinua mzigo wa nyutoni 120 kufikia umbali wa m. 3. Kokotoa ufanisi
wa mashine. [ ] a) 20% b) 60% c) 500% d) 30% e) 80%
35. Kani inayotuwezesha kutembea bila ya kuanguka huitwa ………… [ ]
a) umeme b) sumaku c) msuguano d) kani ya uvutano ya dunia e) kani
mnyanyuo
36. Kundi gani kati ya haya yafuatayo hutoa elimu na huduma ya kwanza?
[ ] a) msalaba mwekundu b) angaza c) wasamaria wema d) polisi e) nesi
37. Kazi kuu ya vinyweleo vya puani na umajimaji katika mfumo wa
upumuaji ni …… [ ]
a) kusaidia mbadilishano wa gesi b) kusafisha hewa c) kulinda pua
d) kufungua koromeo e) kuchafua hewa
38. Mkono wa binadamu ni mfano wa nyenzo daraja la …………….. [ ]
a) kwanza b) pili c) tatu d)nne e) tano
39. Ili mbegu iote inahitaji ……………………. [ ] a) udongo, maji,
unyevunyevu b) mbole, udongo na maji c) mbole, maji na hewa d) maji,
hewa na joto la wastani e) joto, unyevunyevu
40. Hewa ya Naitrojeni ni mojawapo ya virutubisho vinavyopatikana katika
mbolea ya NPK, virutubisho vingine ni ……. [ ] a) kashamu na fosiforasi
b) chokaa na kashamu c) fosiforasi na potasiamu d) kasham na
potasiamu e) potasiamu na sodiamu

SEHEMU B: JAZA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI


41. Miili ya wadudu imegawanyika katika sehemu kuu tatu. Taja mdudu
ambaye mwili wake umegawanyika katika sehemu kuu mbili ……………..
42. Tafuta R1 ………………………………………………………………………….

43. …………………........ huupa mwili umbo lake na kuuwezesha kujongea.


44. 41. Kuna aina mbili za uchavushaji ambazo ni ………… na ……………

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 80
45. Mfumo wa fahamu wa kati unaundwa na …………………. Na ……………

JARIBIO LA 26
1. Kitendo cha mmea kufyonza maji kutoka kwenye udongo kwa kutumia
mizizi huitwa ________________________________ [ ] (a)transipiresheni
(b) umande (c) osmosis (d) photosinthesis (e) phototropizimu
2. Viumbe wafuatao wapo katika kundi lipi la Wanyama? Nyoka, Kobe na
Kinyonga [ ] (a) Reptilia (b) Amfibia (c) Mamalia (d) Ndege (e)wadudu
3. Katika mchoro wa Ua ufuatao, ni sehemu ipi huvutia wadudu kwa ajili
ya uchavushaji? [ ] (a) 1 (b) 2 (c) 3 (d) 4 (e) 5
1 2 3

4 5
4. Seli ya mnyama na seli ya mmea hufanana katika _____________ [ ]
(a) ukuta wa seli (b) rangi ya kijani (c) nyukliasi (d) umbo maalumu
(e) rangi
5. Ni aina ipi ya chakula mmeng’enyo wake huanzia mdomoni _____ [ ]
(a) Matunda (b) protini (c) mafuta (d) vitamini (e) kabohaidreti
6. Mazoezi ni njia mojawapo ya kupunguza ______________________ [ ]
(a) kutapika (b) kuharisha (c) kuzimia (d) msukumo mkubwa wa damu
(e) Kifua Kikuu
7. Sehemu iliyooneshwa kwa herufi N kwenye mchoro ufuatao inaitwa: [ ]

(a) Dendriti (b)Aksoni/axon (c)Saitoplazimu (d)Nukliasi (e) Neva


8. Viungo vifuatavyo vinaunda mfumo wa fahamu isipokuwa _____ [ ]
(a) Ubongo (b) milango ya fahamu (c) neva za ugwe mgongo (d) misuli
(e) ngozi
9. Ateri zote husafirisha damu safi isipokuwa ______
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 81
(a) ateri ya renali (b) ateri ya palmonari (c) ateri ya koronari (d) ateri za
jugular (e) ateri ya mesentari
10. Katika upumuaji wa wanyama, mapafu hutoa takamwili iitwayo __ [ ]
(a) Kabonidayoksaidi (b) oksijeni (c) kabohaidreti (d)urea (e) chumvi za
ziada
11.Utungaji wa mimba hutokea ikiwa tendo lifuatalo litafanyika ____ [ ]
(a) mwanaume na mwanamke watajamiana (b)ikiwa mbegu za mwanaume
zinaingia kwenye uke (c) ikiwa mwanamke na mwanaume wataishi pamoja
(d) ikiwa mbegu za kiume zitaingia kwenye yai la mwanamke
(e) ikiwa mwanamke na mwanaume watalala pamoja
12.Viumbe hai wamegawanyika kwenye makundi makuu wawili ambayo ni _____
(a) wanyama na mimea (b) wadudu na Wanyama (c) viumbe na wanyama
(d) viumbe wenye uhai na viumbe wasio na uhai (e) binadamu na wanyama
13. Mifupa miwili inayotengeneza sehemu za muundi (ugoko) wa mguu ni
_________________ na ______________[ ]
(a) Fibula na Tibia (b) Humas na kraviko (c) Skapla na stenamu
(d) Nyundo na fuawe (e) Fupaja na radiasi
14. ________ ndiyo mlo uliojitosheleza kwa uwepo wa virutubisho vyote
vinavyohitajika na mwili [ ] (a) Pilau (b) mlo kamili (c) ugali (d) biriani
(e) soya
15.Moja kati ya magonjwa yafuatayo hauwezi kukingwa kwa chanjo______
(a) pumu (b) surua (c) kifua kikuuu (d) pepopunda (e) kifaduro
16.Huduma ya kwanza ifaayo kutolewa kwa mtu aliyekunywa sumu ni _[ ]
(a) Kumfanya aitapike (b) kumnywesha maziwa (c) kumnywesha sukari
(d) kumwahisha hospitali (e) Kumlaza chali
17.Anaemia ni ugonjwa unaoweza kuepukwa kwa kuongeza _____ katika
mlo [ ] (a) Nyama na Samaki (b) Nafaka na Maharagwe (c) Matunda na
mboga za majani (d) wali na njegele (e) maziwa na mkate
18.Watu walioathirika na virusi vya UKIMWI huhitaji yote yafuatayo
isipokuwa_____ [ ] (a) Upendo na msaada (b) Mlo kamili (c) Kutibu
magonjwa nyemelezi (d) kuwanyanyapaa (e) usafi
19. Iwapo swala wataongezeka katika mlishano huo nini kitatokea? [ ]
NYASI SWALA SIMBA (a) nyasi zitapungua (b) simba
watakufa (c) idadi ya simba haitabadilika (d) hakutakuwa na mabadiliko
katika upatikanaji wanyasi (e) majani yataongezeka
20. Badiliko la kikemikali ni badiliko la kudumu. Kipi kinabainisha
hilo?______ [ ] (a) Kuungua kwa karatasi (b) maji kuwa barafu (c) chaki
kusagika (d) Kuyeyuka kwa mshumaa (e) maji kuwa mvuke
21.Upi kati ya michoro ifuatayo unaonesha hali halisi ya kuakisiwa kwa
mwali wa mwanga?
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 82
(a) (b) (c) (d) (e)
22. urea, maji na chumvichumvi hutolewa kwa wingi wakati wa joto
kupitia______ [ ] (a) figo (b) kukojoa (c) mapafu (d) ini (e) ngozi
23. Kula chakula chenye wanga na mafuta kwa wingi na mara kwa mara
husababisha ______ [ ] (a) Kiriba tumbo (b) kuvimba tezi za shingo
(c) Afya njema (d) upungufu wa damu (e) kukosekana kwa magonjwa
24…………….. ni umeme mkubwa sana unaotokana na mgongano na
msuguano wa ______ [ ] (a) shoti ya umeme (b) jua (c) kimondo (d) radi
25.Vitu vipi kati ya vifuatavyo huweza kutenganishwa kwa sumaku?__ [ ]
(a) Unga wa ayani na mchanga (b) unga na vipande vya karatasi (c) pini za
plasiki na mchanga (d) unga wa kioo na mchanga (e) mchanga na mchele
26.Vitu muhimu katika uotaji wa mbegu ni _____________________
(a) maji, joto na hewa (b) Mwanga na rutuba (c) Mbolea na unyevu
(d) mwanga, hewa na udongo (e) maji na mbolea ya chumvi chumvi
27.Mahusiano kati ya viumbe hai na visivyo hai katika mazingira
hujulikana kama ______ [ ]
(a) Kutegemeana (b) Mlishano (c) ikolojia (d) mfumo (e) uwiano wa kiasili
28.Umeme wa ampia 0.6 umepita kwenye waya wenye ukinzani wa 6
Ohm.Nini volteji yake? [ ] (a) 36V (b) 10V (c) 0.6V (d) 3.6V (e) 1/6V
29. Zifuatazo ni mashine tata isipokuwa:- _________________ [ ]
(a) Cherehani (b) mkasi (c) Baiskeli (d) Gari ( e) Kikokotoo
30. ……………….. huhifadhi na kulinda ubongo
(a) mishipa (b) ubongo wa mbele (c) ubongo wa nyuma (d) fuvu (e) ngozi [ ]
31.Ni nani mwenye jukumu la kutoa huduma ya kwanza?_____________
(a) Madaktari (b) wauguzi (c) wakunga (d) mtu yeyote mwenye ujuzi wa
kufanya hivyo
(e) watumishi wa chama cha Msalaba mwekundu
32. Katika spektramu ya mwanga, rangi ya mwisho kupinda ni ______ [ ]
(a) urujuani (b) nyekundu(c) hudhurungi (d) kijani (e) njano
33.Usafirishaji wa chakula kilichoyeyushwa kwenye mwili wa binadamu
hufanywa na ________[ ] (a) hewa (b) maji (c) damu (d) neva (e) misuli
34.Ni hatua gani ya uchunguzi wa kisayansi hukanusha au kukubali
dhanio/bunio la utafiti? (a) Kugundua tatizo (b) kuandaa kufanya jaribio
(c) kukusanya data (d) kutafsiri data (e) kuandaa taarifa
35. ________ ni tishu ngumu zilizoundwa kwa madini ya fosforasi na kalisi.
(a) misuli (b) mishipa (c) mifupa (d) nywele (e) ngozi [ ]
36.Ateri kuu imegawanyika katika mishipa midogo midogo iitwayo___ [ ]
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 83
(a) Venakava (b) bronchiole (c) valvu (d) kapilari (e) vena
37.Nini hutokea mwanga upitapo katika media tofauti__________ [ ]
(a) Husafiri kwa kugawa vitu sehemu mbili (b) kusafiri katika mstali
mnyoofu (c) hupinda (d) husafiri ndani ya maji kwa kujikunja (e) husafiri
na kusababsiha vitu kupinda
38.Homoni zinazoandaa mwili kukabiliana na hatari huitwa _____ [ ]
(a) adrenalini (b) insulini (c) sailoksini (d) tezi (e) projestroni
39.Mmojawapo kati ya mimea ifuatayo ina tabia ya uchavushaji peke__ [ ]
(a) Papai (b) karafuu (c) mahindi (d) korosho (e) mgomba
40. Joto husafiri kwa njia ya mpitisho kwenye vitu vifuatavyo. [ ]
(a) maji na chuma (b) hewa na chuma(c) chuma na bati (d) bati na vakyumu
(e) hewa na maji

JAZA NAFASI ZILIZOACHWA WAZI


41.Chumba cha moyo wa binadamu kinachosukuma damu kwenda sehemu
zote za mwili huitwa___________________________________________________
42. Mpangilio wa ogani mbalimbali zinazofanya kazi moja kwa ushirikiano
hujulikana kama ______________________________________________________
43. Tishu nyumbufu ambazo hushikilia misuli na mifupa huitwa _________
44 ___________ ni nyuzinyuzi zinazounganisha mfupa mmoja na mwingine
45. Katika mchoro ufuatao, herufi C inajulikana kama __________

JARIOBIO LA 27
1. Viumbe hai vimeundwa kwa chembe hai ndogo ziitwazo:
A) ogani B) gesi C) saitroplazimu D) tishu E) seli
2. Wanyama wenye uti wa mgongo wamegawanyika katika makundi mangapi?
A) 2 B) 3 C) 5 D) 6 E) 4
3. Ugonjwa upi hauambukizi? A) polio B) kisukari C) surua D) donda koo E)malaria
4. Ukuaji wa mbu hupitia katika hatua nne. Mtiririko sahihi wa ukuaji huo ni
A) yai, buu, lava, mbu B) buu, yai, lava, mbu C) yai, lava, buu, mbu D) lava, yai,
buu, mbu E) mbu, lava, yai, buu
5. Ni homoni ipi inahusika na marekebisho ya madini ya kalsiamu katika mwili
A) adrenalini B) parathomoni C) thairoksini D) insulini E) thairoidi
6. Neno lipi la kisayansi husimama badala ya uwezo wa kufanya kazi A) nishati
B) nguvu C) momentamu D) joule E) kani
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 84
7. Kampaundi ni muunganiko wa ____ mbili au zaidi A) molekyuli B) nyutroni
C) atomi D) seli E) elementi
8. Takamwili zinazochujwa na figo husafirishwa kwenda kwenye kibofu kupitia
A) ureta B) aota C) urethra D) ateri ya palmonari E) vena kava
9. Kikohozi kikavu, homa, kutokwa na jasho usiku, kukohoa damu ni dalili za
A) pepo punda B) ndui C) T.B. D) homa ya matumbo E) athma
10. Viroboto wa panya hueneza ugonjwa wa A) tauni B) mafua C) malaria
D) mapunye E) dondakoo
11. Mkondo wa umeme kwenye sakiti hupimwa kwa kutumia chombo kiitwacho
A) voltimita B) ukinzani C) ampia D) nikotini E) amita
12. Watu waishio sehemu za baridi hushauriwa kula zaidi aina ipi ya chakula kwa
wingi? A) fati B) protini C) vitamin D) kabohaitredi E) wanga
13. Katika jaribio la kisayansi data humaanisha nini? A) taarifa ya mambo
yanayojitokeza B) taarifa ya jaribio thabiti C) mpangilio wa hatua jinsi ya
kufanya jaribio D) orodha ya vifaa utakavyotumia kwenye jaribio
E) mapendekezo ya hatua za kutatua tatizo
14. Mfumo wa fahamu umeundwa na milango ya fahamu, neva __________
na ubongo. A) ugwe mgongo B) nyukliasi C) nyuroni D) misuli E) medula
15. Ni magonjwa yapi husababishwa na ukosefu wa vitamin?
A) tetekuwanga ndui na polio B) matege, safura na kiseyeye
C) kifua kikuu na ukavumacho D) kiseyeye, beriberi na ukavumacho
E) kuhara, trakoma na malale
16. Kiwavi ni lava wa A) chura B) mende C) panzi D) kipepeo E) mbu
17. Moja ya magonjwa yafuatayo huweza kuzuiwa kwa chanjo, nao ni
A) pepopunda B) kisonono C) kipindupindu D) malaria E) hemofilia
18. Insekta ni jamii ya wadudu ambao miili yao imegawanyika katika
sehemu kuu A) mbili B) nne C) tano D) tatu E) nane
19. Chunguza mchoro huu wa samaki. Je ni sehemu ipi ya mwili
ambayo humsaidia kuhisi miguso na hatari mbalimbali majini?

20. Ili mbegu iote inahitaji A) kabondayoksaidi, maji na mwanga


B) hewa, udongo na maji C) joto, maji na mwanga D) maji, joto
na unyevu E) joto, hewa na unyevu
21. Taka mwili ya kabondayoksaidi hutolewa mwilini na A) ini
B) mapafu C) figo D) moyo E) kongosho
22. Kiasi cha mwanga kinachoingia ndani ya jicho hudhibitiwa na:
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 85
A) retina B) mboni C) lensi D) irisi E) neva za uoni
23. Nyuzi 30 za Sentigredi ni sawa na nyuzi ngapi za Farenhaiti? A) 58
B) 25 C) 86 D) 67 E) 32
24. Kitendo cha maji katika mimea kusafiri kutoka myeyusho hafifu
kwenda myeyusho mzito huitwa A) respiresheni B) osmosis
C) stomata D) spirako E) translokesheni
25. Sehemu mbili za stameni katika ua ni A) stigma na staili B) chavulio
na filamenti C) staili na pistili D) sepali na ovary E) kikonyo na staili
26. Chakula mwilini husafirishwa kwenda sehemu mbalimbali za mwili. Kazi ya
kusafirisha chakula hicho hufanya na A) mapafu B) mishipa C) ini D) utumbo
mwembamba E) damu
27. Elimu ya sayansi inayohusu hali ya afya bora inayotokana na ulaji na
matumizi bora ya chakula huitwa A) lishe B) usanisi C) mlo kamili
D) virutubisho E) mfumo wa chakula
28. Kwa kawaida mimea hukua kuelekea kwenye:
A) maji B) upepo C) mwanga D) rutuba E) shina
29. Kutu kwenye chuma ni mfano wa badiliko la A) kiumbo B) rangi
C) kikemikali D) kimiminika E) kisayansi
30. Maji safi yasiyo na mchanganyiko wa chumvi chumvi zozote ni yale:
A) yaliyovukizwa B) yaliyotoneshwa C) ya chemchem D)yaliyogandishwa
E) yaliyochemshwa na kuchujwa
31. Mwale wa mwanga ukipita katika media tofauti ……………. A) hupinda
B) hutawanyika katika rangi 7 C) huakisiwa D) hutawanyika E) Huzimika
32. Katika mchoro huu wa sakiti ya umeme herufi W ni A) waya B) betri
C) glopu D) swichi E) ampia

33. Sumu iliyopo katika sigara


inayosababisha matatizo kwa mtumiaji inaitwa A) bangi B) kafeni C) heroini
D) kilevi E) nikotini
34. Ugonjwa wa matende huenezwa na mbu jamii ya A) kuleksi B) protozoa
C) anofelesi D) plasmodiamu E) amoeba (amiba)
35. Inakadiriwa kwamba ukubwa wa moyo wa binadamu ni sawa na A) ngumi
yake B) roho yake C) jinsia yake D) umri wake E) kidole gumba
36. V.V.U vinapoingia mwilini hushambulia A) seli nyeupe B) seli nyekundu
C) plazima D) chembehai E) maradhi mengine
37. Mchakato wa kumeng’enya chakula mwilini huanzia A) tumboni B) kwenye
ini C) kinywani D) kwenye ulimi E) kwenye utumbo mwembamba
38. sehemu ya nje ya jino ambayo ni nyeupe inaitwa ……………………………………
(A) Enamali (B) dentini (C) mvungu (D) sementi (E) ufizi
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 86
39.Minyoo aina ya askari husababisha ugonjwa wa ……………………………………
(A) kichocho (B) polio (C) safura (D) malale (E) kifaduro
40. kusafirisha chakula kwenda sehemu mbalimbali za mwili na kuondoa uchafu
sehemu mbalimbali za mwili ni kazi ya …………………………… (A) chembechembe
nyekundu (B) chembe sahani (C) chembechembe nyeupe (D) plazma (E) maji
41. Kipi kinaanza kuota katika mbegu kati ya kianza mzizi na kianza shina? ……

42. Sehemu iliyoathiriwa na kani ya sumaku huitwa ………….………………………..

43.Wenzo una sehemu kuu ngapi? ………………………………………………………….

44.Kani inayotumika kusukuma mzigo inaitwa …………………………………………

45. …………………………………………………………….…. Ni uwezo wa kufanya kazi.

JARIOBIO LA 28
1.Fuvu la kichwa cha binadamu lina jumla ya mifupa mingapi?
(A) 206 (B) 600 (C) 22 (D) 58
2. Inasadikika kuwa ubongo wa binadamu una uzito wa ………………………
(A) kg 20 (B) gm 8 (C) tani 21/2 (D) Kg 11/2
3. Sehemu kubwa ya gesivunde huundwa na gesi gani? (A) Kaboni
dayoksaidi (B) methane (C) haidrojeni (D) oksijeni
4. ……………………………………………………………… huzalisha gametiume.
(A) ovari (B) korodani (C) tezidume (D) figo
5. Kuna aina ……………..……. Za mivunjiko (A) 2 (B) 3 (C) 4 (D) 5
6. Mlo kamili ni ule wenye ……………………………………………………………
(A) nyama (B) virutubisho vyote (C) matunda (D) protini
7.Panya hueneza ugonjwa wa (A) tauni (B) korona (C) matege (D) unyafuzi
8.Wakati wa usiku mimea huvuta hewa ya:
(A) oksijeni (B) kabonidayoksaidi (C) naitrojeni (D) CO2
9. Peter anakua taratibu, unafikiri ana upungufu wa vitamin gani?
(A) C (B) A (C)B (D) E
10. Mshipi wa ndowano na mfagio ni mfano wa nyenzo daraja la:
(A) kwanza (B) pili (C)nne (D) tatu
11. …… hulinda ua likiwa tumba. (A) sepali (B) petali (C) stigma (D) ovary
12.Unafikiri ni mzigo upi mzito kati ya A na B ?
(A) B (B) A (C) yote ni sawa (D) yote ni myepesi tu

Sm4 sm 8

A B
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 87
13. …………… ni sehemu ya seli ya mnyama inayoruhusu vitu kuingia na
kutoka. (A) nyuklia (B) saitoplazimu (C) kiwambo (D) kiinitete
14.Msumari wenye ngazi za mzunguko (hesi) hujulikana kama (A) bisibisi
(B) nati (C) skurubu (D)mtaimbo
15. Juma alitumia kani ya 10N kusukuma gogo. Ikiwa kazi aliyofanya ni
joule 20 je, mzigo umesogea umbali gani? (A) M 200 (B) J 2 (C) M 2
(D) J200
16. Kifua kikuu husababishwa na bacteria aina ya ….. (A) basili (B) kulex
(C) amiba (D) ephedrine sulfate
17. Muungano wa elementi zaidi ya moja kikemikali huitwa (A) radikali
(B) elementi (C) simetali (D) kampaundi
18. Sehemu ya nje ya chungwa inaitwa: …………………………..……………
(A) endokapi (B) mezokapi (C) kiinitete (D) epikapi
19. Sehemu ya ua ambayo hufanya kazi sawa na uke kwa wanyama
ni……………………… (A) ovary (B) filament (C) stigima (D) kichavua
19. Samaki hupumua kwa kutumia … (A)mapafu (B) ngozi (C) mapezi
(D)matamvua
20.Lenzi ambayo hukusanya miale ya mwanga ni lenzi aina ya (A) mbinuko
(B) mbonyeo (C) bapa (D) mche glasi
21. Ukubwa wa tetemeko la ardhi hupimwa kwa kifaa kiitwacho
(A) seismografu (B) rikta (C) darubini (D) anemometa
22. Sehemu ya kike ya ua huitwa: (A) staili (B) stigma (C) ovary (D) pistili
23. Tunashauriwa kuanika nguo nyeupe kwenye ………………………………
(A) kivuli (B) mwanga (C) joto (D) giza
24. Zifuatazo ni takamwili isipokuwa (A) jasho (B) mkojo (C) kinyesi
(D) cabonidaioksaidi
25. Vinyoyanyoya vilivyopo kwenye utumbo mwembamba ambavyo
husharabu chakula Vinaitwa: (A) virusi (B) viribachakula(C)vilasi(D) sungilo
26. Maji husharabiwa kwenye ………………………………... (A) tumbo
(B)utumbo mwembamba (C) koo (D) utumbo mpana
27. Yafuatayo ni majanga ya asili isipokuwa …………………………………..
(A) tetemeko la ardhi (B) kimbunga (C) mafuriko (D) vita
28. nyota kubwa ambayo hutoa mwanga na joto kwenye uso wa dunia ni
(A) kasopia (B) nyota ndogo ya Kaskazini (C) jua (D) nyota kuu ya Kaskazini
29. Chanjo ni ……………. (A) matibabu ya watoto (B) matibabu (C) kinga
dhidi ya maradhi (D) huduma ya kwanza

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 88
30. Neva zinazounganisha jicho na ubongo zinaitwa: …………………………
(A) mota (B) sensori (C) akustika (D) optiki
31. Joto la mwili wa ndege ni nyuzi joto za sentigredi 40 ambazo ni sawa na
nyuzi ngapi za farenheiti? (A) 2120F (B) 320F (C) 1040F (D) 1000F
32. Kani inayotuwezesha kutembea kwa miguu bila kuteleza na kuanguka ni
kani ya (A) uvutano (B) msuguano (C) mburuto (D) mnyanyuo
33.Ili ndege iweze kuruka angani ni lazima kani msukumo iishinde kani
mburuto na kani mnyanyuo iishinde kani ……………………………………….
(A) uvutano (B) msuguano (C) mburuto (D) mtiririko
34. Uzani hupimwa katika vipimo vya (A) km (B) kg (C) m (D) Nyutoni
35. Soma kwa makini kielelezo kifuatacho kisha jibu swali linalofuata

X X X Y
YY

X Y
X X
X

XY

Mtoto aliyezaliwa hapo ni …………………………………………………….…..


(A) Albino (B) muathirika wa anaemia (C) wa kike (D)wa kiume
36. Homini inayohusika na kusisimua uterasi ipanuke baada ya mimba
kutunga ni (A) projesteroni (B) testosteroni (C) oestrojeni (D) adrenalini
37. Sehemu kubwa ya mwili wa binadamu ni (A) damu (B) maji (C) mifupa
(D) misuli
38. Taswira ya herufi V A kwenye kioo bapa inaonekanaje?
(A) (B) (C) (D)
39. Ili mawimbi ya sauti yaweze kufikia ngoma ya sikio hukusanya na.... (a)koklea
(b)pina (c)sikio la nje (d)viferejividogo
40. Zingatia mlishano huu:-
SIMBA-SWALA-NYASI (katika mbuga za wanyama).Iwapo simba wote
watahama katika mazingira haya nini kitatokea? (A) nyasi zitapungua (B) swala
watakufa (c) nyasi zitaongezeka (d) swala watafuata simba

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 89
SEHUMU B: JAZA NAFASI ZA WAZI
41. Taja aina kuu mbili za roda. ……………………… na …………………….
42. SELI TISHU OGANI …………………………… KIUMBE
43. Mirija myembamba inayosafirisha maji na virutubisho katika mmea
Huitwa ……………………………………………………………………………….
44. Vitu huenda juu na kurudi chini kutokana na kani ya …………………….
45. Maji ya bahari yakikupwa upande wa …...…… hujaa upande wa…………

JARIBIO LA 29
SEHEMU A: ANDIKA HERUFI YA JIBU SAHIHI
1. Zifuatazo ni sifa za viumbe hai isipokuwa:
(A) kuona (B) kujongea (C) kuzaliana (D) kuitikia vichocheo
2. Ifuatayo ni seti ya mimea isiyotoa maua.
(A) mbani, mvinje na kangaga (B) mbani mwembe na mhindi (C) mnazi, mhindi
na ukoka (D) katani, mnazi na mchungwa
3. Zifuatazo ni sehemu za mmea isipokuwa: (A) matawi (B) shina (C) majani
(D) mizizi
4. Yafuatayo ni makundi ya wanyama wasio na uti wa mgongo isipokuwa:
(A) reptilia (B) minyoo (C) konokono na ngisi (D) athropoda
5. Wafuatao ni wanyama katika kundi la athropoda.
(A) kaa, panzi, buibui, tandu na jongoo (B) minyoo, panzi, na popo
(C) chura, mjusi na mamba (D) kenge, mjusi na mamba
6. Yafuatayo ni makundi ya wanyama wenye uti wa mgongo isipokuwa:
(A) athropoda (B) amfibia (C) samaki (D) reptilia
7. _______________ ni kiumbe ambaye hutaga mayai majini hata kama yeye anaishi
nchi kavu. (A) chura (B) mjusi (C) mamba (D) bata
8. ___________________ ni kiumbe ambaye huishi majini lakini hutaga mayai yake
nchi kavu. (A) mamba (B) kasa (C) kenge (D) samaki
9. _______________________________ ni mamalia ambaye hana tezi za jasho
(A) nyangumi (B) mbwa (C) kuku (D) kinyonga
10.Ufuatao ni mmea ambao unatoa mbegu lakini hautoi maua.
(A) mvinje (B) mhindi (C) mpera (D) mtama
11.Kabohaidreti hutengenezwa katika sehemu ipi ya jani la mmea? (A) ndani ya seli
zenye klorofil (B) kwenye kikonyo (C) kwenye vena (D) kwenye mipaka ya jani
12.Sehemu inayosharabu nishati ya mwanga katika jani ni:
(A) umbijani (B) mishipa (C) kikonyo (D) stomata

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 90
13. Ni aina gani ya mchavusho ambayo chavua husafirishwa kutoka kwenye chavulio
za ua la mmea mmoja kwenda kwenye stigma za mmea mwingine? (A) mchavusho
tambuko (B) mchavusho pweke (C) mchavusho asili (D) mchavusho kisasa
14.Zifuatazo ni sifa za taswira kwenye kioo mbinuko isipokuwa:
(A) hugeuzwa juu chini chini juu (B) taswira ni ndogo kuliko kiolwa (C) huwa
wima (D) hugeuzwa upande wa kulia kuwa upande wa kushoto wa kiolwa
15.Mstari unaounganisha pointi C na F na kufika katikati ya kioo mbonyeo huitwa:
(A) mwale mkuu (P) (B) Fokasi (F) (C) mwale mtuo (D) kitovu cha mbonyeo (C)

16.Ifuatayo ni sumaku katika umbo gani?

(A) sumaku kwatofarasi (B) sumaku mche (C) sumaku duara (D) sumaku mche duara
17. Yafuatayo ni matumizi ya sumaku isipokuwa: (A) kutengenezea madini
(B) kutengenezea dira (C) kutengenezea kengele ya umeme (D) kutenganisha vitu
18. _________ ni kifaa cha tarakilishi ambacho huhifadhi na kulinda vifaa vyote vya
kielektroniki. (A) kasha mfumo (B) monita (C) kibodi (D) kichakato kikuu
19. ______ ni kifaa ambacho hupokea na kuchakata kazi zote zinazoingia kwenye
tarakilishi. (A) Kichakato kikuu (KIKU) (B) monita (C) kibodi (D) kasha mfumo
20. Kifaa ambacho hutumia kielekezi kumwelekeza mtumiaji wa tarakilishi kuamuru
au kuelekeza tendo Fulani analotaka kufanya huitwa: (A) kiteuzi (B) monita
(C) kibodi (D) kasha mfumo
21.__________ hutumika kuonyesha kazi inayofanyika au taarifa iliyomo ndani ya
tarakilishi. (A) skirini /monita (B) kiteuzi (C) kibodi (D) kasha mfumo
22.____________ ni kifaa ambacho hutumika kuingiza data au taarifa kwenye
tarakilishi katika mfumo ya herufi, tarakimu au alama. (A) kibodi (B) monita
(C) kiteuzi (D) kasha mfumo
23.__________ ni vifaa muhimu vinavyotumika kuingiza data kwenye tarakilishi.
(A) vitumi ingizi (B) programu endeshi (C) programu tumizi (D) vitumi toleo
24.Vifuatavyo ni vitumi ingizi kwenye tarakilishi isipokuwa:
(A) kipaza sauti (B) kiteuzi (C) maikrofoni (D) kibodo
25.Vifaa vinavyotoa taarifa kutoka kwenye tarakilishi huitwa: (A) vitumi toleo
(B) kiteuzi (C) maikrofoni (D) kibodo

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 91
26. Kifuatacho ni moja kati ya vitumi toleo kwenye tarakilishi. (A) kipaza sauti
(B) kiteuzi (C) maikrofoni (D) kibodo
27.Tarakilishi imeundwa kwa sehemu kuu mbili ambazo ni: (A) maunzi na programu
(B) program endeshi na programu tumizi (C) kiteuzi na kibodo (D) kiteuzi na
skrini
28.Sehemu za tarakilishi ambazo hushikika na kuonekana huitwa: (A) maunzi (B)
maunzi na programu (C) programu (D) vitumi toleo
29.Sehemu za tarakilishi ambazo haziwezi kushikika wala kuonekana huitwa:
(A) programu (B) maunzi na programu (C) maunzi (D) vitumi toleo
30.Kichakato kikuu, monita, kiteuzi, printa na kipaza sauti ni mifano ya: (A) maunzi
(B) maunzi na programu (C) programu (D) vitumi toleo
31. _______ ni mkusanyiko wa maelekezo ya kuviongoza vifaa vya tarakilishi vifanye
kazi na kutoa matokeo kulingana na maelekezo: (A) programu (B) maunzi
(C) kiteuzi na kibodo (D) kiteuzi na skrini
32. _______ ni seti ya maelekezo ambayo hutumika katika tarakilishi ili kufanya
shughuli mbalimbali. (A) programu (B) maunzi (C) kichakato kikuu (D) kiteuzi na
skrini
33.___________________________ hudhibiti utendaji wa kazi zote ndani ya
tarakilishi na kutawala kazi zinazofanywa na vifaa vilivyounganishwa kwenye
tarakilishi. (A) program endeshi (B) program tumizi (C) programu (D)
maunzi
34. ____________________ humsaidia mtumiaji wa tarakilishi kufanya shughuli
zake. (A) program tumizi (B) programu endeshi (C) kipaza sauti (D) injini
pekuzi
35.________________ ni kifaa ambacho huzuia umeme unaoweza kuleta madhara na
pia huhifadhi nguvu za umeme kwa muda fulani ili kumsaidia mtumiaji wa
tarakilishi kukamilisha kazi zake na kuzihifadhi pale umeme unapokata.
(A) kidhibiti umeme (B) fyuzi (C) sakiti breka (D) kinga radi
36. _______ ni programu ya kuzuia, kulinda na kukinga tarakilishi na taarifa zake
dhidi ya virusi. (A) kinga virusi (B) virusi (C) programu endeshi (D) programu tumizi
37._______________________________ ni programu ambazo hutengenezwa na watu
wasio na nia njema kwa lengo la kuvuruga, kudukua, na kuharibu kazi au taarifa.
(A) virusi (B) programu tumizi (C) program endeshi (D) kinga virusi
38.Data inapoingizwa katika seli huonekana sehemu gani nyingine? (A) mwamba wa
kanuni (B) programu tumizi (C) program endeshi (D) kinga virusi
39. = SUM(A5:A10) ina maana gani katika programu jedwali?
(A) jumlisha namba kuanzia seli A5 hadi A10 au A5 + A6 + A7 + A8 + A9 + A10
(B) kutoa namba kuanzzia seli A5 hadi A10 au A5 - A6 - A7 - A8 - A9 - A10
(C) kutafuta wastani wa A5 hadi A10
(D) kulinganisha namba kuanzia A5 hadi A10
40.Kanuni ya kukokotoa wastani wa namba zilizoandikwa katika seli A3 hadi F3 ni
ipi? (A) =AVERAGE(A3 :F3 (B) =AVERAGE(A3 +F3 (C)
=AVERAGE(A3 - F3 (D) =SUM(A3 :F3
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 92
SEHEMUB: JAZA NAFASI ZA WAZI
41.Taja aina mbili za program za tarakilishi.
i. ________________________________ ii ________________________________
42.Taja aina mbili za uyeyushaji mweneo
i. ________________________________ ii ________________________________
43.Taja matumizi mawili ya hewa ya CO2
i. ________________________________ ii ________________________________
44.Taja kanuni mbili za Ohm
i. ________________________________ ii ________________________________

45.Taja sehemu kuu za wenzo. ___________________________________________

JARIBIO LA 30
SEHEMU A: ANDIKA HERUFI YA JIBU SAHIHI
1. Zifuatazo ni aina za data zinazoweza kuingia katika mkekakazi.
(A) matini, tarehe, namba na sarafu (B) matini, tarehe na wastani (C) matini,
tarehe na maunzi (D) matini, tarehe na mkwaju
2. Kanuni inafanya kazi gani kwenye mkekakazi? (A) kuelekeza ukokotoaji wa data
na kutoa jibu sahihi (B) kuhifadhi data (C) kuongeza data (D) kulinda data
3. Sehemu ya mkekakazi ambayo huingizwa data huitwa: (A) seli amilifu
(B) seli mchakato (C) seli yakinifu (D) seli butu
4. Tarakilishi, ruta, madaraja, swichi na nyaya ni vitumi vinavyounda ___________
(A) mtandao (B) tarakilishi (C) programu (D) barua pepe
5. ______________________ ni mtandao mkubwa wa mawasiliano unaotumia
tarakilishi kuunganisha watu, mashirika, makampuni na serikali duniani kote.
(A) intaneti (B) mtandao janibu (C) mtandao mpana (D) barua pepe
6. Vifuatavyo ni visakuzi vya mtandao isipokuwa: (A) ruta (B) google chrome
(C) mozilla firefox (D) internet explorer
7. Kielelezo kifuatacho kinawakilisha vitu gani? (A) visakuzi vya mtandao
(B) vitumi vya mtandao (C) aina za mtandao (D) injini pekuzzi

8. Yafuatayo ni makundi ya injini pekuzi kwenye intaneti isipokuwa: (A) injini ya gari
(B) injini pekuzi mtambazi (C) injini saraka (D) injini pekuzi mseto

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 93
9. Kidhibiti umeme na kinga virusi ni vifaa vinavyolinda tarakilishi isipatwe na
madhara. Kipi kati ya hivyo ni program? (A) kinga virusi (B) kidhibiti umeme
(C) programu endeshi (D) programu tumizi
10.Wenzo, mteremko, kabari, gurudumu na ekseli, roda na skurubu ni makundi ya nini?
(A) mashine rahisi (B) mashine (C) mashine tata (D) hakuna jibu
11.Mkasi na mkokoteni ni baadhi ya mashine rahisi katika kundi la: (A) wenzo
(B) roda (C) kabari (D) mteremko
12.Meno, patasi, shoka, kisu na kipande cha mti ni baadhi ya mashine rahisi katika
kundi la: (A) kabari (B) roda (C) wenzo (D) mteremko
13. ___________ ni mashine rahisi ambayo hugeuka au kujizungusha kwenye sehemu
iitwayo egemeo. (A) wenzo (B) roda (C) kabari (D) mteremko
14.Lishe bora, usafi wa mazingira, kutumia maji safi na salama, kupumzika na kulala
na kufanya mazoezi ya viungo ni: (A) kanini za afya (B) maisha ya mjini
(C) maisha ya kijijini (D) utandawazi
15.Ni aina ipi ya udongo haupitishi majji kwa urahisi?
(A) mfinyanzi (B) tifutifu (C) kichanga (D) tofari
16.Hapa Tanzania udongo wa tifutifu hupatikana zaidi mikoa ya: (A) Arusha,
Kilimanjaro, Mbeya na Iringa (B) Tanga na Pwani (C) Tanga na Iringa (D) Tanga
na Mtwara
17._______________________________________ hutokana na rasilimali za asili.
(A) nishati jadilifu (B) nishati ya kimakanika (C) nishati tuli (D) umeme
18.Vifuatavyo ni vyanzo vya nishati jadilifu isipokuwa: (A) umeme (B) jua (C) upepo
(D) maporomoko ya maji
19.________________________________ ni hali ya maada kuhama kutoka sehemu
moja kwenda sehemu nyingine inayotofautiana ukolevu. (A) uyeyushaji mweneo
(B) osmosisi (C) difyusheni (D) metamofosisi
20.Kitendo cha harufu kutoka sehemu inayozalishwa na kusambaa sehemu kusikokuwa
na harufu huitwa: (A) difyusheni (B) osmosisi (C) uchafuzi wa hewa (D) usanisi nuru
21.Mwalimu alijipulizia manukato kwenye sweta lake na kuingia darasana akaenda
kusimama ubaoni. Ghafla harufu ya manukato ilitapakaa darasa zima. Je, unafikiri
ni kitendo gani kimefanyika kusambaza harufu? (A) difyusheni (B) osmosisi
(C) uchafuzi wa hewa (D) usanisi nuru
22.Kitendo cha maji kusafiri kutoka sehemu yenye myeyuko hafifu kwenda kwenye
myeyuko mzito huitwa: (A) osmosisi (B) difyusheni (C) uchafuzi wa hewa
(D) mwendokasi
23.Mizizi ya mmea hufyonza maji kutoka ardhini kwa njia ya : ________________
(A) osmosisi (B) difyusheni (C) usanisi nuru (D) uchavushaji

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 94
24.Myeyuko mweneo ambao molekyuli za maada husambaa kutoka ukolevu hafifu
kwenda ukolevu mkubwa huitwa: (A) osmosisi (B) difyusheni (C) usanisi nuru
(D) uchavushaji
25.Zifuatazo ni baadhi ya huduma za afya kwa watoto isipokuwa: (A) kupata elimu
bora (B) vipimo (C) ushauri wa kitaalamu (D) chanjo na dawa
26.Ni ipi kati ya sehemu zifuatazo imeunda sehemu kubwa ya damu? (A) plazima
(B) seli nyeupe za damu (C) seli nyekundu za damu (D) chembe sahani
27.Himoglobini ni muhimu sana katika kutengeneza _________________________
(A) seli nyekundu za damu (B) seli nyeupe za damu (C) plazima (D) chembe
sahani

28.Zifuatazzo ni sehemu kuu zinazounda mfumo wa mzunguko wa damu isipokuwa:


(A) ubongo (B) damu (C) mishipa ya damu (D) moyo
29.Kirutubisho cha aina ya ___________ husaidia katika ukuaji wa maua kwa mmea.
(A) fosforasi (B) calisiamu (C) naitrojeni (D) potasi
30.Kirutubisho cha aina ya ___________ husaidia katika ukuaji wa mizizi kwa mmea.
(B) potasi (B) calisiamu (C) naitrojeni (D) fosforasi
31.Kirutubisho cha aina ya ___________ husaidia katika ukuaji wa majani kwa mmea.
(C) naitrojeni (B) calisiamu (C) potasi (D) fosforasi
32.Maji na virutubisho husafirishwa kutoka kwenye mizizi ya mmea hadi kwenye
majani kupitia mirija ya: (A) zailemu (B) floemu (C) falopia (D) urethra
33.Kipi kati ya vifuatavyo humeng’enya kinyesi kwenye mtambo wa gesivunde?
(A) minyoo, inzi na bakteria (B) hewa ya kabonidayoksaidi (C) joto (D) umeme
34.Sehemu kubwa ya gesivunde huundwa na gesi gani?
(A) methani (B) O2 (C) kabonidayoksaidi (D) naitrojeni
35.Kuzuia au kukataza, onyo au tahadhari, lazima au amri na dharura ni aina ya alama
za: (A) usalama (B) ishara (C) kufikirika (D) uandishi
36.Alama za usalama za kuzuia au kukataza zinakuwa na rangi_________________
(A) nyekundu (B) njano (C) bluu (D) kijani
37.Alama ipi kati ya zifuatazo ni alama ya onyo au tahadhari?

(A) (B) (C) (D)


38.Alama ifuatayo ina maana gani? (A) hairuhusiwi kutumia simu (B) zima mashine
(C) simu ya dharura (D) tunatengeneza simu

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 95
39.Kipi kati ya vifuatavyo ni kizio sahihi cha density? (A) g/sm3 (B) kg/ sm3
(C) g/sm2 (D) sm3/g
40.Chautundu alimimina mafuta ya kula kwenye ndoo iliyokaribia kujaa maji. Mafuta
hayo yakaonekana kuelea juu ya maji. Hii ni kwa sababu: (A) densiti ya maji ni
kubwa kuliko densiti ya mafuta (B) densiti ya mafuta ni kubwa kuliko densiti ya
maji (C) maji yalikuwa ni mengi (D) mafuta yalikuwa ni machache

SEHEMUB: JAZA NAFASI ZA WAZI


41.Taja aina mbili za mtandao
ii. ________________________________ ii ________________________________

42.Kitu chochote kinachoelea kinaweza kufanywa kizame kwa kuzidisha _____bila


kubadili ujazo wake.

43. Taja aina ya mvunjiko inayoonyeshwa katika kielelezo kifuatacho: ____________

`
44. Tafuta densiti ya kipande cha chuma chenye tungamo ya kg2 na ujazo wa sm31500
45. Densiti ya kipande cha ubao ni g/sm31.5. ikiwa ujazo wa kipande hicho cha mbao
ni sm3 300, tafuta tungamo lake.

JARIBIO LA 31
SEHEMU A: ANDIKA HERUFI YA JIBU SAHIHI
1. Density ya maji ni (A) g/sm3 1 (B) g/sm3 0.5 (C) sm3 /g 1 (D) sm3 /g 1
2. Kuelea au kuzama kwa vitu kwenye maji hutegemea vitu vifuatavyo isipokuwa:
(A) wepesi wa kitu (B) density ya kitu (C) umbo la kitu (D) uhusiano wa
kanielezi na kani ya uvutano
3. Kama densiti ya kitu ni ndogo kuliko ya maji nini kitatokea ukikidondosha kitu
hicho kwenye maji? (A) kitaelea (B) kitazama (C) kitazama na kuelea
(D) kitazama au kuelea
4. Kifaa ambacho hunasa na kusambaza mawimbi sumakuumeme kwenye vifaa vya
mawasiliano kama redio na runinga huitwa: (A) antena (B) spika (C) maikrifoni
(D) dikoda
5. Waya, kipenyo, safu, akisi na kidoa ni aina za: (A) antena (B) runinga (C) redio
(D) ving’amuzi

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 96
6. Katika kunasa mawimbi ya utabiri wa hali ya hewa, ipi ni antenna bora zaidi kati ya
hizi zifuatazo? (A) antena mchirizo akisi (B) antenna ya Yagi-Uda (C) antenna
kidoa (D) antenna kitanzi
7. Ipi kati ya antenna zifuatazo ina uwezo wa kujikinga na na kelele kwa ufanisi?
(A) antenna kitanzi (B) antenna ya Yagi-Uda (C) antenna kidoa (D) antenna
mchirizo akisi
8. Ipi ni tungo sahihi kuhusu vitumi vya mawasiliano ambavyo havijaunganishwa kwa
waya? (A) haviwezi kuwasiliana bila antena (B) vinaweza kuwasiliana bila antena
(C) haviwezi kuwasiliana bila antena kitanzi (D) vinaweza kuwasiliana kwa
antenna ya upande mmoja tu
9. Antenna kidoa hutumika zaidi kwenye mojawapo ya jozi za vifaa vifuatavyo:
(A) simu ya mkononi na kwenye ndege (B) antenna na madishi (C) redio za
kupokelea matangazo na meli (D) runinga na simu za mkononi
10.Ipi kati ya malighafi zifuatazo inaleta ufanisi katika matumizi ya antenna kwa
sababu ya uwezzo wake wa kupitisha umeme? (A) shaba (B) aluminiamu
(C) chuma (D) uraniamu
11.Nishati katika mashine ya kusaga nafaka husafirishwa kutoka kwenye mota hadi
kwenye kinu kwa kutumia (A) mkanda (B) gurudumu na ekseli (C) waya
(D) nyenzo
12.Mota katika blenda hubadilisha nishati ya umeme kuwa nishati ya:
(A) makanika (B) mwanga (C) joto (D) joto na mwanga
13.Moto unaotokana na kuungua kwa vitu yabisi kama kuni, karatasi na nyasi ni moto
daraja la: (A) A (B) C (C) D (D) B
14.Vifuatavyo ni vifaa vya kuzimia moto daraja la A isipokuwa: (A) rangi ya mafuta
(B) maji (C) mchanga (D) blanketi maalumu
15.Moto unaotokana na vimiminika vinavyowaka na kulipuka kama mafuta ya petroli,
dizeli na rangi za mafuta ni moto daraja la: (A) B (B) A (C) D (D) C
16.Moto daraja B huweza kuzimwa kwa kutumia: (A) gesi ya kabonidayoksaidi au
poda kava (B) maji (C) hewa ya oksijeni (D) mafuta
17.Butani, propani na methani ni gesi zinazowaka ambazo hutoa moto daraja la :
(A) C (B) A (C) D (D) B
18.Moto daraja C huweza kuzimwa kwa kutumia: : (A) gesi ya kabonidayoksaidi au
poda kava (B) maji (C) hewa ya oksijeni (D) mafuta
19.Moto unaotokana na kuwaka kwa metali kama maginesiamu, potasi na vitu vyenye
asili ya chuma ni moto daraja la: (A) D (B) A (C) F (D) B
20.Moto daraja D huzimwa kwa kutumia: (A) poda kava (B) gesi ya kabonidayoksaidi
au poda kava (C) hewa ya oksijeni (D) gesi ya kabonidayoksaidi na maji
21.Hitilafu ya umeme hutoa moto daraja: (A) F (B) A (C) D (D) B
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 97
22.Moto unaotokana na umeme, daraja F huzimwa kwa kutumia vitu vifuatavyo
isipokuwa: (A) gesi ya oksijeni (B) gesi ya kabonidayoksaidi (C) poda kava
(D) mchanga mkavu
23.Damu huchukua oksijeni na kutoa kabonidaiyoksaidi kupitia …… [a] viribahewa
[b] kuta za mapafu [c] koromeo [d] kapilari [e] pua
24.Madini yapi ni magumu zaidi ya mengine kati ya yafuatayo?...................... [a] almasi
[b] dhahabu [c] chuma [d] makaa [e] ulanga
25.Nishati ambayo huweza kupenya katika baadhi ya vitu kama maji, glasi na hewa ni:
[a] mwanga [b] umeme [c] upinde [d] sauti [e] ngurumo
26.Kuna aina ngapi za uchavushaji? …… [a] mbili [b] nne [c] tano [d] tatu [e] sita
27.Mojawapo ya huduma muhimu ya kumpa mtu anayeungua moto ni .....…..…
[a] kumfunika blangeti [b] kumfunika na nyasi [c] kumwagia asali [d] kumwagia
maji [e] kumpaka asali
28.Vimelea vinavyoharibu chembea hai nyeupe za damu ni ……………………..
[a] VVU [b] bacteria [c] plasm [d] amiba [e] kuvu
29.Mchanganyiko wa gesi mbalimbali kwa pamoja huitwa … [a] hewa [b] haidrojeni
[c] oksijeni [d] naitrojeni [e] maada
30.Lipi kati ya yafuatayo sio badiliko la kikemikali?……..… [a] kuyeyuka kwa sukari
[b] kuchacha kwa maziwa [c] kuungua kwa mkaa [d] kuoza kwa taka [e] chuma
kupata kutu
31.Ni kifaa gani hutumika kukuza taswira ya violowa anuwai?
[a] hadubini [b] darubini [c] periskopi [d] prizimu [e] lenzi
32.Ugonjwa unaoambukizwa na bacteria na huwapata watoto wadogo wenye chini ya
miaka miwili ………. [a] pepopunda [b] kifaduro [c] surua [e] tetekuwanga
33.Sehemu tupu iliyopo katika chupa ya chai ambayo huzuia kupitishwa kwa joto
huitwa………….. [a] vakyumu [b] mpitisho [c] mnururisho [d] uwazi [e] silva
34.Mtoto aliyetumboni mwa mama hupata hewa na chakula kupitia kwenye [a] plasenta
[b] seviksi [c] ovary [d] ureta [e] uterasi
35.Atomi mbili za haidrojeni zikiungana kikemikali na atomi moja ya oksejini,
kompaundi inayotengenezwa huitwa………………………………………..…
[a] maji [b] gesi [c] aside [d] chumvi [e] besi
36.Wakati wa usiku mimea huvuta hewa ya ………………….. [a] oksijeni [b] nitrojeni
[c] kabonidaiyoksaidi [d] sodiamu [e] haidrojeni
37.Ni kundi lipi la wanyama wenye uti wa mgongo lina damu ya joto zaidi?
[a] ndege [b] mamalia [c] samaki na chura [d] chura [e] nyoka
38.Kizingiti mgando cha maji ni nyuzi ngapi za sentigredi?
[a] 0 [b] 100 [c] 42 [d] -100 [e] 32
39.Mahitaji mbalimbali yanayotolewa kwa jamii ili kujenga afya huitwa ………………
[a] huduma za afya [b] huduma za kwanza [c] msaada wa haraka [d] uzazi wa
mpango [e] mazoezi ya viungo
Chunguza mchoro ufuatao kisha jibu swali.

A D

Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 98
B ’’’’’’’’’’’’’’ c

40.Herufi B inawakilisha nini? ……………………………………………………...


[a] chumvi [b] kiazi [c] kopo [d] osmososi [e] difyusheni

SEHEMU B: JAZA NAFASI WAZI


Wanafunzi wa darasa la saba walifanya jaribio la kupima uzito wa jiwe hewani na
kisha kwenye maji kama inavyoonekana hapo chini. Tazama kwa makini jaribio hilo
kisha jibu maswali yanayofuata.

41.Eleza kanuni ya Archimedes. ___________________________________________


42.Uzito wa jiwe hewani ni newtio ngapi? __________________________________
43.Uzito wa jiwe ndani ya maji ni newton ngapi? ____________________________
44.Uzito wa maji kwenge chupa ya plastiki ni newton ngapi? ___________________
45.Kanielezi ni newton ngapi? ___________________________________________
UHUSIANO ULIOPO KATI YA SEHEMU ZA JICHO NA KAMERA

SEHEMU KAZI
KAMERA JICHO
Lenzi Lenzi Kupinda mwanga na kufanya taswira
Diaframu Irisi Kurekebisha ukubwa wa shata/mboni
Apecha Mboni Kuingiza mwanga
Filamu Retina Kupokea taswira
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma 99
Kirekebisha fokasi Misuli ya siliari Kurekebisha umbali kati ya lenzi na
filamu/retina
Kasha jeusi Koroidi Kusharabu mwanga usiharibu
filamutaswira inayofanyika katika retina
Shata Kope Kufunga na kufungua

Shule ya Msingi Chechemea iliandaa mahitaji ya vifaa vya kieletroniki vinavyohitajika pamoja na gharama
zake kama inavyoonekana katika mkekakazi ufuatao:

Chunguza mkekakazi huo na kisha jibu maswali yafuatayo:


(a) Kifaa chenye jina la “tarakilishi” kipo katika seli gani?

(b) Je, utatumia fomula gani kupata jumla ya gharama za vifaa vyote?

MAJIBU
Galaxy Library, 0764 968 345/0784 678 250 bunduki76said@gmail.com. Karibu kwetu ukue kitaaluma
100

You might also like